Msaada juu ya kaka yangu, nifanyeje?

Msaada juu ya kaka yangu, nifanyeje?

Ulitaka akuchukue wewe?? Mmelelewa vibaya sana nyie tena usikute na wewe unaleta hapo nyumbani wanaume hivyo ngona droo,unakaaje na lizee nyumbanikwako??? Mwambie akapange asee,ma house girl hapo wamepona kweli??
 
Una wivu hadi kwa kaka ako duu,tatizo huna cha kufanya tafuta cha kufanya tu
Wivu upi mkuu maana ni kakaangu wadamu sema hii tabia ndo imenishinda. Nafanya kazi mkuu
 
Nilisha jaribu kumwambia akasema for security purposes maana nilikua mimi na namsaidizi ndo tukakubalina tuishi pamoja
Mmmh aisee vipi huyo Sugar Mummy?? ulishamueleza bro kuwa huyo mwanamke hafai kuwepo hapo?? na mumeo hili suala lote anazungumziaje kama ulishawahi kumdodosea?
 
jitu kubwa hivyo halafu hana kwake!!!
Aaaaa we mwambie tu kiutu uzima, kuwa mama anakuja siku fulani na unahisi kabisa kuwa hali itachafuka kwa sababu hii na hii...., so kama vipi jiongeze anza kufanya maandalizi mapema ya kumuweka huyu jimama sehemu nyingine hata kama ni kwa muda tu ambao mama atakuwepo.... yakikushinda mwambie mumeo akusaidie kumchana, kana naye hawezi basi hata ndugu mwingine wa kiume ambaye mko naye karibu na ambaye ni muelewa
 
Wivu upi mkuu maana ni kakaangu wadamu sema hii tabia ndo imenishinda. Nafanya kazi mkuu
Kama mtu kakupita miaka 10 na ni mtu mzima na haoni umuhimu wa kuacha hiyo tabia basi huna cha kufanya ndo maisha aliyochagua...kama unaona na undugu umekushinda vinja undugu vin ginevyo muache na maisha yake au mfukuze kwako
 
37/40 mbona wanaMatch tuu. Ww kula maish na mumeo mwache blaza nae Ale Vyake
 
Mi ninge mfukuza na mawe, 35y.o kwa shemeji na bado una mkosea adabu kuleta mademu ndani, hata kama ni uzungu huo umezidi dada
 
Huyo mama kubwa anajua kuwa hapo sii kwa ben ten???? Maana Unaweza kuta Kakako kamwambia ndo kwake. Mtimue huyoo unayemuita kaka, yaaani na uzee wooote alala kwa shemeji????

Nimekwambia Mtimue aondoke, akafanyie huo ufuska kwake hukooo, hilo nalo lakushinda kweeeli????
 
Naomba tu ushauri jinsi yakumwambia aondoke bila ugonvi. Pia nilitaka kumwambia mme wangu mamaangu kaniomba nisimwambie ndo kasema anakuja kuongea nae. Ndi kinachomleta maza. Kama kweli mtu unamweshim nduguyo huwezi mfukuza kama mbwa nitumie njia gani yayeye kuondoka bila kuleta shida kwenye famila.
 
Back
Top Bottom