Nucky Thompson
JF-Expert Member
- Sep 20, 2016
- 1,817
- 4,058
Wakuu habari, juzi nilileta uzi kuhusu line yangu kufungiwa
Kabla ya yote kwanza niwajibu waliokuwa wakilaumu au kushangaa mtu kuweka milioni 10 kwenye M pesa wakisema benki ndio salama
Benki unaweza kuweka na hela zako zikipotea vilevile, kama mnakumbuka kuna benki kama 3 zilifungwa kipindi cha Magufuli kutokana na benki hizo kufilisika na waliokuwa na fedha humo kuzipata ikawa ni mtihani,
So ishu inategemea umeweka hela benki gani au mtandao gani, kama benki haina afya au mtandao hauna afya hela inapotea
Nirudi kwenye mrejesho, kuna jamaa alinipa namba ya dada anayefanya kazi TCRA makao makuu, akanionyesha ushirikiano vizuri na kunipa namba ya mkuu wa kitengo kinachohusika na malalamiko ya wateja
Baada ya kuwasiliana na mkuu huyo wa kitengo akaniambia nirudi Vodacom na kama line yangu haitafunguliwa siku hiyo basi nimpigie nikiwa hapohapo
Nikaenda Vodacom asubuhi wakaniambia leo lazima niondoke na line yangu ikiwa inafanya kazi maana usumbufu ulikuwa umezidi
Nikasubiri mpaka saa tisa, najaribu kupiga bado haikubali. Jamaa akaniambia nichomoe line kwenye simu niwape wakaondoka nayo, siku zote hizo line nilikuwa sijawapa ile line bali nawatajia namba tu
Jamaa kurudi akaniambia lin iliyokuwa kwenye simu yangu wameiangalia na wameona haikuwa ile niliyowatajia na line hiyo inaonyesha niliifunga tarehe 12 mwezi wa pili,
Aisee nilishikwa na hisia tatu tofauti kwa wakati mmoja mshangao , furaha na kukosa pozi
Ni kweli kuwa tarehe 12 nilienda Vodacom na kufuta line moja ya Vodacom niliokuwa naitumia kwenye device ya intaneti,
Lakini kumbe ile line niliyoifuta niliichanganya na line iliyokuwa na hela sababu zote zinafanana muonekano
Sababu niliiweka kwenye simu na ikawa inasoma mnara vizuri, nikaona ipo sawa hadi nilipojaribu kupiga simu zikawa haziendi
nikamwaambia a renew ile line iliyokuwa na hela sababu nilikuwa sina uhakika na nilipoiweka
Jamaa akawa ananiuliza ilikuwaje nikachanganya line na kuwahangaisha kiasi kile, nikawapa pole ambayo hata hakuitikia.
Nikahakiki salio na kuchukua line yangu na kuondoka
Nimewajibika kuleta huu mrejesho sababu nilichangia kwa kiasi flani watu kukosa imani na Vodacom kwa sababu yangu
Pia soma: Vodacom wamefungia line yangu ikiwa na milioni 10 kwenye M-PESA
Kabla ya yote kwanza niwajibu waliokuwa wakilaumu au kushangaa mtu kuweka milioni 10 kwenye M pesa wakisema benki ndio salama
Benki unaweza kuweka na hela zako zikipotea vilevile, kama mnakumbuka kuna benki kama 3 zilifungwa kipindi cha Magufuli kutokana na benki hizo kufilisika na waliokuwa na fedha humo kuzipata ikawa ni mtihani,
So ishu inategemea umeweka hela benki gani au mtandao gani, kama benki haina afya au mtandao hauna afya hela inapotea
Nirudi kwenye mrejesho, kuna jamaa alinipa namba ya dada anayefanya kazi TCRA makao makuu, akanionyesha ushirikiano vizuri na kunipa namba ya mkuu wa kitengo kinachohusika na malalamiko ya wateja
Baada ya kuwasiliana na mkuu huyo wa kitengo akaniambia nirudi Vodacom na kama line yangu haitafunguliwa siku hiyo basi nimpigie nikiwa hapohapo
Nikaenda Vodacom asubuhi wakaniambia leo lazima niondoke na line yangu ikiwa inafanya kazi maana usumbufu ulikuwa umezidi
Nikasubiri mpaka saa tisa, najaribu kupiga bado haikubali. Jamaa akaniambia nichomoe line kwenye simu niwape wakaondoka nayo, siku zote hizo line nilikuwa sijawapa ile line bali nawatajia namba tu
Jamaa kurudi akaniambia lin iliyokuwa kwenye simu yangu wameiangalia na wameona haikuwa ile niliyowatajia na line hiyo inaonyesha niliifunga tarehe 12 mwezi wa pili,
Aisee nilishikwa na hisia tatu tofauti kwa wakati mmoja mshangao , furaha na kukosa pozi
Ni kweli kuwa tarehe 12 nilienda Vodacom na kufuta line moja ya Vodacom niliokuwa naitumia kwenye device ya intaneti,
Lakini kumbe ile line niliyoifuta niliichanganya na line iliyokuwa na hela sababu zote zinafanana muonekano
Sababu niliiweka kwenye simu na ikawa inasoma mnara vizuri, nikaona ipo sawa hadi nilipojaribu kupiga simu zikawa haziendi
nikamwaambia a renew ile line iliyokuwa na hela sababu nilikuwa sina uhakika na nilipoiweka
Jamaa akawa ananiuliza ilikuwaje nikachanganya line na kuwahangaisha kiasi kile, nikawapa pole ambayo hata hakuitikia.
Nikahakiki salio na kuchukua line yangu na kuondoka
Nimewajibika kuleta huu mrejesho sababu nilichangia kwa kiasi flani watu kukosa imani na Vodacom kwa sababu yangu
Pia soma: Vodacom wamefungia line yangu ikiwa na milioni 10 kwenye M-PESA