Ndagullachrles
Senior Member
- Jun 20, 2023
- 104
- 116
Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Vodacom imepuuza amri ya Mahakama ya Mwanzo mjini Moshi ilyowataka kurudisha pesa za mteja wao anayedaiwa kitapeliwa na mtandao wa mataperi.
Mahakama hiyo chini ya mheshimiwa P.S Claudia ambaye ni hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo,aliamuru kiasi cha shilingi Milioni 2.5 zilizokuwa zomezuiliwa kwenye namba ya wakala 098505 yenye jina la Emmanuel Alphonce Msele kurudishwa kwenye namba ya M-Pesa 0763475327 kwa jina la Waziri Idd Kachikao.
"Kwa sababu hiyo basi mahaakama hii inayakubali maombi ya mdai mhukumiwa kwa hukumu ya mahakama kutekelezwa kwa pesa hizo kurudishwa kwa mdai mhukumiwa".
"Hivyo namuamuru meneja wa Kampuni ya Vodacom Moshi kurudisha pesa kiqsi cha sh. 2.500.000 zilizokuwa zomezuiliwa kwenye namba ya uwakala 098505 yenye jina la Emmanuel Alphonce Msele".
"Pesa hizo zirudishwe kwa mdai mhukumiwa kwa malipo kufanyoka kwenye kwa namba ya M-Pesa 0763475327 kwa jina la Waziri Idd Kachikao"
Iko hivi:
Januari 11/2023 Kachakio alifanya makubaliano ya kufanya biashara ya mapazia pic 125 kwa bei ya 25,000 kwa kila pazia na kufanya hesabu kiwa 2,500,000.
Baada ya makubaliano hayo,Emmanuel aliomba awekewe pesa kwa wakala mkuu aitwaye Kachaina Ltd,fedha hizo zikawekww na baada ya muda Emmanuel akakiri kupokea fedha hizo.
Emmanuel aliahidi mzigo utamfikia mhusika januari 16/2023 lakini siku hiyo mzigo haukufika na ndipo jamaa alipoamua kuzuia fedha hizo.
Katika uamuzi wa awali kwenye shauri la madia namba 191/2023,mahakama ya mwanzo Moshi mjini kupitia kwa Mheshimiwa L.L Mushi ,iliamuliwa mdai kurejeshewa fedha zake lakini hamuzi huo haukutekelezwa kabla ya Mdai kukazia hukumu.
Mpakq Sasa Vodacom wameshindwa kutii amri hiyo ya Mahakama huku wahusika wakitupiana mpira ni nani arejeshe fedha hizo kati ya Vodacom Moshi na Vodacom Makao makuu.
Acha tusubirie tuone hatima ya jambo hili.
Mahakama hiyo chini ya mheshimiwa P.S Claudia ambaye ni hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo,aliamuru kiasi cha shilingi Milioni 2.5 zilizokuwa zomezuiliwa kwenye namba ya wakala 098505 yenye jina la Emmanuel Alphonce Msele kurudishwa kwenye namba ya M-Pesa 0763475327 kwa jina la Waziri Idd Kachikao.
"Kwa sababu hiyo basi mahaakama hii inayakubali maombi ya mdai mhukumiwa kwa hukumu ya mahakama kutekelezwa kwa pesa hizo kurudishwa kwa mdai mhukumiwa".
"Hivyo namuamuru meneja wa Kampuni ya Vodacom Moshi kurudisha pesa kiqsi cha sh. 2.500.000 zilizokuwa zomezuiliwa kwenye namba ya uwakala 098505 yenye jina la Emmanuel Alphonce Msele".
"Pesa hizo zirudishwe kwa mdai mhukumiwa kwa malipo kufanyoka kwenye kwa namba ya M-Pesa 0763475327 kwa jina la Waziri Idd Kachikao"
Iko hivi:
Januari 11/2023 Kachakio alifanya makubaliano ya kufanya biashara ya mapazia pic 125 kwa bei ya 25,000 kwa kila pazia na kufanya hesabu kiwa 2,500,000.
Baada ya makubaliano hayo,Emmanuel aliomba awekewe pesa kwa wakala mkuu aitwaye Kachaina Ltd,fedha hizo zikawekww na baada ya muda Emmanuel akakiri kupokea fedha hizo.
Emmanuel aliahidi mzigo utamfikia mhusika januari 16/2023 lakini siku hiyo mzigo haukufika na ndipo jamaa alipoamua kuzuia fedha hizo.
Katika uamuzi wa awali kwenye shauri la madia namba 191/2023,mahakama ya mwanzo Moshi mjini kupitia kwa Mheshimiwa L.L Mushi ,iliamuliwa mdai kurejeshewa fedha zake lakini hamuzi huo haukutekelezwa kabla ya Mdai kukazia hukumu.
Mpakq Sasa Vodacom wameshindwa kutii amri hiyo ya Mahakama huku wahusika wakitupiana mpira ni nani arejeshe fedha hizo kati ya Vodacom Moshi na Vodacom Makao makuu.
Acha tusubirie tuone hatima ya jambo hili.