MREJESHO; Wa Kaka yangu aliyechanganyikiwa

MREJESHO; Wa Kaka yangu aliyechanganyikiwa

Nimekwambia mkiingia kichwa kichwa mtapukutishwa ukoo mzima kuweni makini kuweni makini tena, mganga anawaset muingie kwenye mfumo anachosimulia ni story za chama cha wachawi akiwapa masharti mkafanya ndivyo sivyo mtajuta baadae kuweni makini kuna mtego atawapa mkinasa mmeisha na anajua hamuwezi kua makini kiasi hicho kwa hio lazima mnase

Hawajui waganga walivyo wajanja.

Watamfanyia practical za chemistry ambazo hajawai kuziona.. yeye atajua dawa zinafanya miujiza ndio maana anaona maajabu ya kichawi. Kumbe chemical reactions tu
 
Yeye kagoma kututajia kabisa amesema tu mwanamke mmoja na wanaume wawili, yaani hapo katuacha na maswali sasa
Si kama napinga no,yeah watu wapo kazini kutesa wenzao,


Pambaneni kumtibia nduguyo,hayo mambo yakujua ni nani kafanya ni uchonganishi,,,maana wachawi wanajivika sura.na hao waganga ni matapeli.
 
Kuna dawa nimeambiwa nitumie for 7days atanipa after hapo ndiyo tutapewa kinga kwa pamoja na kingine alisema mimi kuna Chale nimechanjwa na hao wanachama kwenye paji la uso hapa sasa kila ninapoenda wanakuwa wananiona hao watu wabaya
Usiende kupewa kinga! utaweza mambo ya ku renew kila baada ya muda fulani Inakuja kua kama ni utumwa mtakuja kuingia kwenye mikataba ambayo kuja kutoka inakua too rate!

Tafuta usaidizi wa kiroho wa Mungu utapona na Mungu atakusaidia! Unaweza mcheki Prophet James Nyakia, Mwenge mpakani anaona nani kakufanyia, lengo lake e.t.c. Nimeshuhudia watu wenye kesi kama yako na huyo braza wako wengi wakipona na kurejea kwenye hali za kawaida na maisha yao kubadilika kabisa. Jaribu kumfatilia Roho ikikusukuma unaweza kumwona.

Waganga wanaweza wavuruga na mambo yenu yakaenda kombo kabisa, mtaibiwa nyota, mtajikuta siku majanga hayaishi ndani na mtapoteza hela nyingi sana mkianza hizo safari za waganga huwa haziishi ukishafungua huo mlango.
 
Hata Mm naona pia.
Komradhi Jiran, ila haya ni mawazo yangu.

Ulisema kuwa alishawah ugua tena huko nyuma, na pia kama nakumbuka alikuwa pia na bodaboda nyingne.
Ulisema pia kuwa anavuta Ganja.

Na hapa katkat wakat hana pikpik alikuwa yuko vizur.

Mm nadhan alivyopata pikpik akawa na kipato alienda vuta ganja iliyochanganywa na madawa ya kulevya, na ikaharibu ubongo wake.
Kipind hayuko vizur alikuwa anavuta ya kawaida ila alivyopata ajira akawa sasa anavuta zenye madawa ambazo ni kali zaidi.

Ndugu yenu hajarogwa.
Ww pia hujarogwa achana na hizo dawa alizokupa mganga.

Mkiendelea kumtegemea huyo mtaalam huko mbele atawagombanisha na pia atawala hela.
Hi idirect kwa huyo binti
 
Asante mkuu, kwahiyo unanishauri hata hiyo dawa nisiende kuoga?
Wewe ushajaa kwenye mfumo na ushasetiwa, usifanye tofauti na aalivyokwambia ndio maana nakwambia huo ni mtego, sasa ukifanya tofauti unajitengenezea matatizo mengine just do it n relax then angalia nini kinafuata, ukishamaliza jitakase kwa namna yako ila usifanye kinyume na alivyokwambia utalipia gharama mara 2
 
Asante mkuu, kwahiyo unanishauri hata hiyo dawa nisiende kuoga?
Usitumie achana nayo. Na ukiona shida pokea wakiondoka tupa. Na usionyeshe kuwa hutumii.

Lakini jambo la muhimu ni kukaa mbali nao ila watatafuta mbinu ya kukutisha zaidi ili usiharibu ugali wao.
 
Hata Mm naona pia.
Komradhi Jiran, ila haya ni mawazo yangu.

Ulisema kuwa alishawah ugua tena huko nyuma, na pia kama nakumbuka alikuwa pia na bodaboda nyingne.
Ulisema pia kuwa anavuta Ganja.

Na hapa katkat wakat hana pikpik alikuwa yuko vizur.

Mm nadhan alivyopata pikpik akawa na kipato alienda vuta ganja iliyochanganywa na madawa ya kulevya, na ikaharibu ubongo wake.
Kipind hayuko vizur alikuwa anavuta ya kawaida ila alivyopata ajira akawa sasa anavuta zenye madawa ambazo ni kali zaidi.

Ndugu yenu hajarogwa.
Ww pia hujarogwa achana na hizo dawa alizokupa mganga.

Mkiendelea kumtegemea huyo mtaalam huko mbele atawagombanisha na pia atawala hela.
Huamini kwenye ushirikina? Nadhani hujawahi kukutana na watu waliorogwa, hata mimi sina imani sana lakini kwa hili nimeogopa mno, je vip kama ni kweli haya mambo yakawa yakishirikina yakatoka kwa ndugu yangu yakahamia kwangu, na mimi mtasema navuta bangi au iliyochanganyika na madawa?
 
Hawajui waganga walivyo wajanja.

Watamfanyia practical za chemistry ambazo hajawai kuziona.. yeye atajua dawa zinafanya miujiza ndio maana anaona maajabu ya kichawi. Kumbe chemical reactions tu
Sio vitu vya kukimbilia ndio maana nikamuuliza yeye anamjua huyo kaka yake nje ndani au anamjua juu juu tu?
 
Sina hiyo nia na wala sitoi namba ya mtaalamu, na pia sina namba yake kabisa
Wadau kuweni makini kuna dalili za kutapeliwa hapa ni hivi matapeli huwa wanatunga story wanapost kwenye mitandao ya kijamii story kama hii .....wanajua kuna watu wataenda kuomba number ya mganga .....
 
Huamini kwenye ushirikina? Nadhani hujawahi kukutana na watu waliorogwa, hata mimi sina imani sana lakini kwa hili nimeogopa mno, je vip kama ni kweli haya mambo yakawa yakishirikina yakatoka kwa ndugu yangu yakahamia kwangu, na mimi mtasema navuta bangi au iliyochanganyika na madawa?
Nina amin kwenye ushirikina . Uchawi upo.

Ila sababu hasa ya Kaka ako kuanza kuumwa ndio inanitafakarisha.

Kwann akiwa hana hela haumwi?.
Akipata ajira ndio anaumwa!

Umesema pia kwenu hakuna historia ya vifo vyenye utata. Then kwenu hakuna ndugu wa karibu mchawi.
Maana ndugu huanza kuua damu zao kwanza, ndio masharti yao.
Hawez toa kafara mtu wa mbaki
 
Wewe ushajaa kwenye mfumo na ushasetiwa, usifanye tofauti na aalivyokwambia ndio maana nakwambia huo ni mtego, sasa ukifanya tofauti unajitengenezea matatizo mengine just do it n relax then angalia nini kinafuata, ukishamaliza jitakase kwa namna yako ila usifanye kinyume na alivyokwambia utalipia gharama mara 2
Sasa kuliko kwenda kufanya hiyo dawa si ni heri nikajitakase kanisani, kwanini niende huko then baadae nianze kuhangaika kwenda kujitakasa
 
Wadau kuweni makini kuna dalili za kutapeliwa hapa ni hivi matapeli huwa wanatunga story wanapost kwenye mitandao ya kijamii story kama hii .....wanajua kuna watu wataenda kuomba number ya mganga .....
Sikia mkuu mimi sipo kwaajili hiyo hiki ninachokisema ni kitu kipo serious kabisa
 
Nina amin kwenye ushirikina . Uchawi upo.

Ila sababu hasa ya Kaka ako kuanza kuumwa ndio inanitafakarisha.

Kwann akiwa hana hela haumwi?.
Akipata ajira ndio anaumwa!

Umesema pia kwenu hakuna historia ya vifo vyenye utata. Then kwenu hakuna ndugu wa karibu mchawi.
Maana ndugu huanza kuua damu zao kwanza, ndio masharti yao.
Hawez toa kafara mtu wa mbaki
Kuna huyo mama yetu mdogo nasikia ana hayo mambo ya uchawi, kuna dada yetu mmoja aliwahi kulalamika kuwa huyo mama mdogo anataka kumuulia mtoto wake binafsi sijawahi kufanyiwa uchawi na huyo mamdogo labda kama ananifanyia lakini mimi sielewi kuwa nafanyiwa, kwasasa yupo mkoani nasikia alikimbia huku Dar kwasababu ya uchawi
 
Back
Top Bottom