Son of Gamba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2012
- 4,358
- 6,078
Wiki nzima timu ya Simba walilinda uwanja wa Taifa (Kwa Mkapa) kabla ya mechi yao na Raja Casablanca iliyofanyika jana jioni.
Matokeo yake Simba wamechapwa mabao 3 kwa sufuri hapo hapo kwenye uwanja walioulinda kwa wiki nzima huku wakifanya ushirikina na imani za kishenzi za Kiswahili.
Ifike mahali sasa Watanzania tufahamu na kukubali kuwa mchezo wa mpira wa miguu sio uchawi, wala matokeo ya mchezo hayaamuliwi kwa uchawi au ushirikina.
Tena tufahamu wazi kabisa matokeo ya mpira hayawezi kuamuliwa kwa mporojo za wasemaji wa vilabu vyetu. Raja Casablanca hawana msemaji wa clabu, lakini wameichapa kichapo Simba yenye msemaji.
Mpira wa miguu sio siasa. Wanasiasa wana haki ya kushabikia mpira lakini hawana uwezo wowote wa kufanya matokeo yakawa upande wa timu zao. Ifike mahali Rais aache porojo za kuahidi zawadi kwa timu itakaposhinda, badala yake, yeye na Serikali yake waweke mikakati endelevu ya kitaalamu kuinua kiwango cha soka hapa nchini.
Mfalme wa Morocco hakuahidi zawadi yoyote kwa Raja Casablanca lakini wameipiga Simba kipigo cha mbwa koko hapa hapa nyumbani.
Ningependa sana kuona Serikali ya Tanzania inaingilia kati na kusimamia kwa dhati kuondolewa kwa dhana potofu na imani potofu za kichawi kwenye michezo yetu. Itungwe sheria kali sana itakayowaadhibu wale wote watakaofanya mambo ya kishirikina kwenye michezo.
Kama uchawi ungekuwa na uwezo wa kuleta matokeo chanya viwanjani basi nchi kama Nigeria na Tanzania zingekuwa zinashikilia kombe la dunia miaka yote.
Mpira wa miguu ni sayansi, ni utaalamu unaohitaji uwekezaji mkubwa wa pesa na mikakati endelevu ya kitaalamu na ya muda mrefu. Wenzetu Ulaya wanafanya hivyo na matokeo yake yanaonekana.
Watanzania tubadilike, hatujachelewa bado. Simba na Yanga badilikeni, achaneni na imani za kishenzi kwenye mpira.
Matokeo yake Simba wamechapwa mabao 3 kwa sufuri hapo hapo kwenye uwanja walioulinda kwa wiki nzima huku wakifanya ushirikina na imani za kishenzi za Kiswahili.
Ifike mahali sasa Watanzania tufahamu na kukubali kuwa mchezo wa mpira wa miguu sio uchawi, wala matokeo ya mchezo hayaamuliwi kwa uchawi au ushirikina.
Tena tufahamu wazi kabisa matokeo ya mpira hayawezi kuamuliwa kwa mporojo za wasemaji wa vilabu vyetu. Raja Casablanca hawana msemaji wa clabu, lakini wameichapa kichapo Simba yenye msemaji.
Mpira wa miguu sio siasa. Wanasiasa wana haki ya kushabikia mpira lakini hawana uwezo wowote wa kufanya matokeo yakawa upande wa timu zao. Ifike mahali Rais aache porojo za kuahidi zawadi kwa timu itakaposhinda, badala yake, yeye na Serikali yake waweke mikakati endelevu ya kitaalamu kuinua kiwango cha soka hapa nchini.
Mfalme wa Morocco hakuahidi zawadi yoyote kwa Raja Casablanca lakini wameipiga Simba kipigo cha mbwa koko hapa hapa nyumbani.
Ningependa sana kuona Serikali ya Tanzania inaingilia kati na kusimamia kwa dhati kuondolewa kwa dhana potofu na imani potofu za kichawi kwenye michezo yetu. Itungwe sheria kali sana itakayowaadhibu wale wote watakaofanya mambo ya kishirikina kwenye michezo.
Kama uchawi ungekuwa na uwezo wa kuleta matokeo chanya viwanjani basi nchi kama Nigeria na Tanzania zingekuwa zinashikilia kombe la dunia miaka yote.
Mpira wa miguu ni sayansi, ni utaalamu unaohitaji uwekezaji mkubwa wa pesa na mikakati endelevu ya kitaalamu na ya muda mrefu. Wenzetu Ulaya wanafanya hivyo na matokeo yake yanaonekana.
Watanzania tubadilike, hatujachelewa bado. Simba na Yanga badilikeni, achaneni na imani za kishenzi kwenye mpira.