Mkuu we mtu wa miaka 38 kwanini mnamuita mzee? Ana uzee gani huyo mwalimu?
Pili, ulitaka huyo Anita akae tu hata kumpa 15 ya mafuta humpi? Ujue saa ingine hawa viumbe tunawaonea bure kabisa, wewe ni mpenzi wake tena mchumba unasema kabisa unataka mafuta na pedi nani amnunulie?
Narudia tena kusema, ukizaliwa mwanaume fanya yote pambana uwezavyo ila kaa ujue watoto wako na mpenzi wako ni jukumu lako kuwalea! Hii haijalishi huyo dada ana hela au hana! Sasa wewe kabinti ka miaka 21 unataka kasikuombe matumizi kweli? Na bila haya unakapanda kila ukisikia ugwadu
Endelea kuwaza kuwa mapenzi sio pesa alafu utaona mwisho wake. Kwanza sio ishu ya mapenzi ni pesa ila ni ishu ya mwanaume kumuhudumia mpenzi wake fullstop