Mnazionaje huduma za Azam tv?

Mnazionaje huduma za Azam tv?

Wewe ukiwapigia wanakutajia account namba yako,angalia namba ya customer care kwenye kipeperushi au kwenye website yao. system>>system info utaona namba ya card yako ambayo utawatajia wakikuuliza,au njia rahisi subiri ikikaribia kuisha airtime yako wanakutumia msg yenye ac namba yako
 
huwez kufananisha azam tv na dstv sawa bt kwa maisha ya wa Tanzania weng watamudu gharama za azam na sio dstv maana malipo ya dstv kwa mwezi wengne ndo mshahara wetu huobkwa mwezi
 
Nijuavyo AZAM TV wanatumia satellite hivyo wanapatikana popote pale hata kijijini ilimradi pawepo nishati ya umeme, kwa kitendo hicho kinafanya coverage yao kuwa kubwa zaidi kuliko wale wa ving'amuzi ambao wanapatikana katika baadhi ya maeneo.

Ninafikiri kama StarTv Akijiunga na AZAM TV, STARTV atakuwa ameongeza maeneo ya kuwafikia watu wengi zaidi hivyo STARTV atafaidika zaidi kwa kupata Matangazo kwani anawafikia wengi. kwa kukataa kwao (STARTV) kujiunga na AZAMTV Sijui kina maana gani kibiashara labda tuwaombe wenzetu wenye uelewa wa kutosha katika masuala ya habari.
 
Najiunga nao soon. Issue itakuwa kuhama DSTv cz nishaizoea kinoma
 
Kweli nimeamini itv an eatv ni mpango Mzima yaani wote mnafurahia kuiona kupitia azam duh makubwa! Ndo mana taarifa ya Habari saa 2 usiku yani kila kona ukikatiza ni itv Ok Hongera ipp media
 
Ukitaka dstv sawa,ukitaka azam tv sawa,na watu hatulipii unaugeuza ungo tu kidogo na kuband unakula channeli hatari.
 
Back
Top Bottom