WBS Channel ya Uganda huwa inaonesha mechi moja ya Uingereza kila jumamosi na NBS huwa inaonesha Champions League mechi ya jumatano. Unaweza kuziona hizo mechi hapo juu kwa ku add satellite na kuziona kupitia MBC3/RODRIGUEZ TV ya Mauritius.
Mkuu umesema ukweli kabisa! Tatizo watu wengi tuna muangalia azam km kampuni kubwa na kudhani anaweza kufanya chochote kionekane. Mchakato wa matangazo ya mpira kusini mwa jangwa la sahara karibu ligi zote kubwa amepewa dstv kwa kushida zabuni,hiyo ndio pia sababu ya abudhabi sport kupoteza haki ya kuonyesha EPL kwa aljazeera msimu huu na miwili ijayo. Kwa sasa TV za afrika ukiondoa dstv wamepewa mechi moja ya jumamosi ya EPL na uefa moja ya jumatano, ndio maana utakuta ATN,WBS na MBC wanaonyesha mechi zinazofanana.