Mnawafahamu waliompachika Dkt. Salim Ahmed Salim jina la Hezbollah katika kugombea Madaraka?

Hapa inazungumzwa historia ya mambo na vijimambo vya zamani,

sio Malalamiko Mkuu!
Sahihi baba!!.
Kila kitu kina udadavuzi wa haki ya ki-Historia.
ni kuitendea haki historia!! ilikuwepo, ipo na itakuwepo nisheria vizazi na vizazi.

Bado ni mulemule tu. Yangekuwa malalamiko kamwe usingevumilia.
 
Mtandao wa Jakaya ulitumika kumuangusha Dr Gharib Bilal mwaka 2000 kwny NEC ya Bara na kumuibua Karume aliekuwa wa pili kutoka mwisho kwny kura za NEC ya Znz


Jk akajigeuza akiwa Waziri wa Mambo ya nje nakumbuka akajigeuza Kampen Manager wa Aman Karume hadi nakumbuka alionekana kwny Magazeti akimfungulia Mlango wa Gari Karume wakati anaingia Dodoma Chimwaga kwny kura kuashiria ndio Mgombea wake hivyo Wanamtandao wote wampe kura na ndicho kilichotokea

Ilipofika 2005 ikawa sasa zamu ya Karume kulipa fadhila kwa kuhakikisha Salim kwanza hapati kura za Wa Znz wenzie lakin pia aoneshwe yeye ni Hizbu na Mpinga Mapinduzi na baya zaid akapakaziwa alikuwa kwny mpango uliofanikiwa wa April 7,1972 pale Kisiwandui
Hakika Mzee wa Msoga Mungu anamuona, hakuishia hapo. Hali ya Lowassa ni dhofu sana kwa sasa hasa na hatimaye Magufuli hatuko naye katika huu ulimwengu wa walio hai
 
Genge lilio ongoza kumpiga vita Salim mwaka 1985 liliongozwa na Getrude Mongela..
Mongela alikuwa anafata maagizo ya 'taaasis' Fulani ya kidini
Iliyosema waunguja ndo moderate muslim so bora Mwinyi.. wapemba hawaaminiki ..wengi extremists..

Salim kusoma Misri pia kulimuongezea maadui...kuna mtu mmoja hapa Maarufu sana
Aliwahi kujaribu kum link Salim na Muslim Brotherhood'..

So fitina dhidi ya Salim ziko deep sana
Makini sana brother lakini unaonaje huyu jamaa kwa mwenendo wake angekuwa Rais wa nchi tungetarajia nini kiuchumi?
 
Jana wakati inasimuliwa historia ya maisha ya Mzee Ali Hassan Mwinyi kwenye maisha yake ya uongozi na Professor Mukandala kipengele hiki alikizungumzia,ni kinani hao tuwafahamu kwa mlio na kumbukumbu mpaka ilipelekea Mzee Mwinyi atengeneze nafasi ya naibu waziri mkuu na nafasi hizo na ile ya wizara ya ulinzi kukabidhiwa Dr Salim?

Kwangu mimi nakumbuka nikiwa na utimamu wa kufuatilia siasa nchini hali hii ilijitokeza pia wakati hayati Mzee Mkapa anamaliza muda wake ,fimbo hii pia ilitumika kumchapiaDr Salim tena kwenye kinyang'anyiro cha awamu ya nne
Cha kustaajabisha Dr Salim sikuwahi kwenye maisha yangu kumskia akilalamika sehemu yoyote ile ,bali alibaki kimya kwenye kigoda cha Mwalimu,bila ya kuwa na nongwa .nionavyo Maisha ya Mzee Mwinyi na Dr Salim ni kama yanashabihiana kwa namna moja ama nyingine
Nakumbuka alishawahi lalamika baada ya kinyang'anyiro cha kumpata Mgombea wa CCM mwaka 2005 kuisha, hakulalamika sana ila alitoa ya moyoni. Mimi nilimkubali sana huyu Dr. Salim Ahamed Salim. Mungu atamlipa kwa wale waliommaliza kisiasa kwa kumuita Hezbollah.

Baada ya Serikali ya yule wa awamu ya nne sikumuona akipata hata uteuzi, ila akina Mwandosya, Dr. Kigoda waliupata Uwaziri.
 
Hakika Mzee wa Msoga mungu anamuona ,hakuishia hapo ,hali ya Lowassa ni dhofu sana kwa sasa hasa na hatimaye Magufuli hatuko naye katika huu ulimwengu wa walio hai
Mfumo wa Ulinzi dhidi ya Makombora kule Msoga ni mkali sana …naambiwa 'ukirusha kombora' halitunguliwi bali linarudishwa lilipotoka kwa kasi zaidi

Huenda 'uranium' inayorutubisha vinu vya Nuclear kule Mwandiga kwa kina Zitto ndiyo hiyo hiyo inayochakatwa kule Msoga
 
Nakumbuka alishawahi lalamika baada ya kinyang'anyiro cha kumpata Mgombea wa CCM mwaka 2005 kuisha, hakulalamika sana ila alitoa ya moyoni. Mimi nilimkubali sana huyu Dr. Salim Ahamed Salim. Mungu atamlipa kwa wale waliommaliza kisiasa kwa kumuita Hezbollah.

Baada ya Serikali ya yule wa awamu ya nne sikumuona akipata hata uteuzi, ila akina Mwandosya, Dr. Kigoda waliupata Uwaziri.
Sio Hezbollah Ni hizbu

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Nakumbuka alishawahi lalamika baada ya kinyang'anyiro cha kumpata Mgombea wa CCM mwaka 2005 kuisha, hakulalamika sana ila alitoa ya moyoni. Mimi nilimkubali sana huyu Dr. Salim Ahamed Salim. Mungu atamlipa kwa wale waliommaliza kisiasa kwa kumuita Hezbollah.

Baada ya Serikali ya yule wa awamu ya nne sikumuona akipata hata uteuzi, ila akina Mwandosya, Dr. Kigoda waliupata Uwaziri.
Walimnyong'onyeza sana, halafu eti aliwahi tamka kiana mwendazake anammaliza mzee wa niguse ninuke, kumbe wale wale tu
 
Back
Top Bottom