Mnawachukia wazungu ila mnatumia teknolojia yao na elimu yao na mnapenda maisha yao na mnakimbilia Ulaya na Marekani kwa wingi

Binadamu tunaishi kwa kutegemeana Mungu ndo alivyo iumba dunia na hakuna atakaye weza kubadilisha.

Hao wazungu unao wasema na wao wanatumia tarakimu zilizo buniwa na waarabu yaani 0 to 9 kwenye elimu yao kama wangekuwa na akili nyingi wangebuni za kwao.

Alafu unacho takiwa kujua ni kuwa kila jamii hapa duniani ina mchango wake kwenye ukuaji wa teknolojia na sio wazungu tu, ukienda kwenye makampuni makubwa ya kiteknolojia duniani yana wataalamu kutoka jamii mchanganyiko duniani na sio wazungu tu.

Alafu hiyo hoja ya kusema sijui watu wanapenda kukimbilia Ulaya na Marekani mbona huwa ni hoja ya kipumbavu sana.

Kwani hakuna raia wa Marekani na Ulaya walioko kwenye nchi za watu wengine? Ya kwamba wao wana haki ya kwenda kuishi kwenye nchi za wengine ila sisi tukienda kwao tunaonekana tuna shida sana sio?

Hapa duniani kila binadamu ana haki ya kwenda sehemu yeyote kutokana na mahitaji yake la msingi afuate taratibu tu.

Hiyo dhana yenu ya kusema eti kila mtu hapa duniani anatamani kuishi Marekani ni dhana ya kipumbavu na kitumwa kwa sababu hapa duniani hakuna taifa lisilo kuwa na raia wa kigeni kwenye ardhi yake,

Mfano Tz ni nchi maskini ambayo haiwezi hata kuwahudumia raia wake lakini ina mamilioni ya raia wa kigeni wanao ishi hapa nchini wakiwemo hao raia wa Marekani na Ulaya.
Mkuu basi vijana wote wa bara la afrika na uarabuni na asia ya kati ni watumwa kwa asilimia 97%.
Maana wote ndoto zao ni kuishi ilaya au marekani.
 
Mkuu basi vijana wote wa bara la afrika na uarabuni na asia ya kati ni watumwa kwa asilimia 97%.
Maana wote ndoto zao ni kuishi ilaya au marekani.
Sina ndoto yakuishi huko mimi acheni generalization, hivi unajua taxable pay ya marekani au uingereza🤣🤣🤣. Tunakariri sana, cost of living ni very high na living under credits ni bonge la deni. Vijana wasomi🤣🤣, aisee.
 
Mnajua mnajichanganya bila kujua,tarakimu zimebuniwa na jamii nyingi duniani.
Kuna waajemi wa iran ya leo,kuna wagiriki na kuna waturuki wa kale na kuna wachina na kuna wajapani na kuna wakorea na kuna wahindi na kuna watamil na kuna wazungu wa uitaliano na kuna wamsiri wa kale na kuna wanubi na kuna wahabeshi na kuna wathailand na kuna wahindi wekundu.
Na baadhi ya hizi tarakimu zinatumika duniani kama lugha na namba rasmi za nchi huska.
Sasa nyinyi mnakariri waarabu tu na tarakimu.
SWALI :: ni waarabu wa eneo gani walibuni hizo tarakimu mnazozibishania???
Jibuni kisomi afu niwasaidie ufafanuzi kisomi
Wagunduzi wa mwanzo wa tarakimu, hasa katika muktadha wa hesabu na uhandisi, wanaweza kutambuliwa kama ifuatavyo:

1. Babylonia: Watu wa zamani wa Babylonia walikuwa miongoni mwa wachunguzi wa kwanza wa tarakimu. Walitumia mfumo wa tarakimu ya hexagesimal (msingi 60), ambao una athari katika vipimo vingi vya wakati na pembe hadi leo.

2. Kigiriki: Pythagoras na wafuasi wake walikuwa miongoni mwa Wagiriki wa zamani waliotumia tarakimu katika muktadha wa nadharia ya hisabati.

3. India: Uhindu ulikuwa mahali pa maendeleo makubwa ya tarakimu na mfumo wa namba ya sifuri. Sulemani na Brahmagupta ni baadhi ya wanahisabati wa Kihindu ambao walisaidia kuendeleza mfumo huu.

4. Arabi: Baada ya kuvuna maarifa kutoka Uhindi, dunia ya Kiislamu ilichangia sana katika maendeleo ya tarakimu. Al-Khwarizmi, ambaye jina lake lina athari kubwa katika neno "algorithm," alikuwa mchango muhimu.

5. Ulaya: Tarakimu na mfumo wa namba za Kiarabu zililetwa Ulaya na mawasiliano kati ya Waarabu na Wazungu. Hii ilisaidia kuleta mapinduzi katika hesabu na uhandisi wa Magharibi.

Hawa ni baadhi tu ya watu na tamaduni zilizochangia katika maendeleo ya tarakimu na mfumo wa namba tunazotumia leo. Inapaswa kusemwa kuwa mchakato wa maendeleo ya tarakimu ulikuwa wa muda mrefu na uliathiriwa na tamaduni nyingi tofauti.
 
Back
Top Bottom