Mnara wa Babeli na historia ya kutisha

Mnara wa Babeli na historia ya kutisha

Kwani Mungu anaishi wapi? (Geographical Location). Je wangetakiwa kupanda huu mile ngapi? Hali ya hewa (baridi, upepo, hewa ya kuvuta vingewatosha? Je huko juu kwa kuzingatia nguvu ya mvutano wa vitu (Gravitation, G) na nguvu ya kuvutwa duniani (gravity, g) ukuta ungejengeka? Maana kuna mahali ambapo vitu vinagoma kushikana. Dunia IPO kwenye universe hii yenye sayari kadhaa, kama Mungu yupo universe zingine huko? na je, kama Mungu hana makazi ya kuonekana physically.

Binafsi nafikiri hata wangeachwa wasingeweza kukifikia kiti cha enzi cha Mungu.
 
kwahiyo uliishia hapo
Sio uliishia ndio ulijengwa kwa staili hiyo na ilimalizika kabisa ingawa ujenzi ulitumia zaidi ya mwaka...... Na kazi ilikuwa masaa 24 kwenye simulizi moja inasema kuna mama mjamzito alitaka kuzaa walikataa kumruhusu hadi muda wa kujifungua ulipofika walichofanya walimzalisha alafu yule mtoto akafungwa kwenye kifua alafu yule maza akaambiwa aendelee kupiga kazi hakuna cha kupumzika wala nni dah hatari sana

Ila wanasema haukumalizika sababu dhamira yao haikufika Mwisho ya kutengeneza geti la kufika mbinguni na kumfikia Mungu ili wammalize na ndio maana kuna nembo moja maarufu inaonyesha mnara wa babeli ila juu haujakamilika

largeeye.gif
 
Kwani Mungu anaishi wapi? (Geographical Location). Je wangetakiwa kupanda huu mile ngapi? Hali ya hewa (baridi, upepo, hewa ya kuvuta vingewatosha? Je huko juu kwa kuzingatia nguvu ya mvutano wa vitu (Gravitation, G) na nguvu ya kuvutwa duniani (gravity, g) ukuta ungejengeka? Maana kuna mahali ambapo vitu vinagoma kushikana. Dunia IPO kwenye universe hii yenye sayari kadhaa, kama Mungu yupo universe zingine huko? na je, kama Mungu hana makazi ya kuonekana physically.

Binafsi nafikiri hata wangeachwa wasingeweza kukifikia kiti cha enzi cha Mungu.
Mkuu walijenga GETI la kufika mbinguni ila sio mnara physical zaidi walijenga tu pyramid kubwa sana la kufanyia matambiko ndio ukaitwa mnara ila kazi yao kubwa ilikuwa kumfikia Mungu kiroho sio kimwili kama ingekuwa hivo ina maana NASA wangeshakuwa wamefika mbinguni kitambo sana kutumia rocket zao
 
sasa we unafikiri huko juu ana kaa nani?
Mungu ana damu? anakaa mbinguni? Mbinguni ni wapi (galaxy ipi), kweli Mungu aliogopa wajenzi wa mnara kuwa watamfikia mpaka akawachanganyia Lugha? wangefikaje huko kwa kujenga tu? Hadithi hizi zitawatoka lini? Leo tu kwenda kwenye mwezi (jirani kabisa) ni shughuli pevu,ingekuwa mnara kweli? huko juuu wangepumuaje? hata mawinguni wasingefika!!!!
 
Kuna wakati biblia inaacha maswali mengi kuliko majibu. Ukiwa mtu wa facts lazima utaona kuna tatizo mahala!

Anyway, tusubiri majibu mkuu!
Tatizo kubwa sana, na hakika hakuna mwanadamu anayeweza kutoa suluhisho kwa hili. Biblia imejaa masimulizi ya kimapokeo, mengi ya kutunga ili kuonyesha ukuu wa huyo waliyemwita Mungu wao. Haiwezekani Mungu asumbuke na watu amabo huo mnara usingefika hata km 10 achilia mbali km 5 tu kutoka usawa wa bahari
 
Zitto Junior naomba nisaidie kunijuza hiyo mishale waliyokuwa wanamrushia Mungu na kurudi ikiwa na damu ilikuwa ikimlenga nani??? na ilimchoma nani??? na kama ilimchoma mtu au malaika nini ilikuwa madhara yake??
hiyo mishale itakua kweli ya kiroho,we mshale upite kuanzia dunia mpaka Jupiter huko na kuendelea siyo mchezo hiyo nguvu iliyotumika
 
Aisee watu wa zamani walikuwa advanced balaa...yaani nilivyokuwa na makosa huwa nawaza hata Mungu nitaenda kumuangaliaje siku akinitwaa ila wao waliamua wamfuate yeye wakamuuwe!!!hapana aisee hawa walikuwa mazombie sio watu.
Walikuwa na akili za kitope, lucifer alishindwa tena walikuwa wako karibu, lakini akaishia kutupwa huku duniani, wao ndio wangeweza wapi?
 
Mkuu walijenga GETI la kufika mbinguni ila sio mnara physical zaidi walijenga tu pyramid kubwa sana la kufanyia matambiko ndio ukaitwa mnara ila kazi yao kubwa ilikuwa kumfikia Mungu kiroho sio kimwili kama ingekuwa hivo ina maana NASA wangeshakuwa wamefika mbinguni kitambo sana kutumia rocket zao
aahhaahaaaa
 
Dah walikuwa na akili mkubwa we jiulize hata majengo yao yamedumu zaidi ya miaka 10,000 si mchezo kabisa au angalia hata pyramids zile zimejengwa kwa sayansi kubwa sana ambayo kwa miaka ile hakuna machine kma za sasa unajiuliza waliwezaje !!!! Walikuwa na akili kubwa pia kuishi miaka mingi kuliwasaidia sababu wanafanya utafiti na wanasayansi wanacombine akili kwa muda mrefu yaani mfano Newton na enstein na hawakings wangeishi miaka 1000 unategemea nini hapo?? Lazma wangegundua mambo mazito zaidi

Kuhusu CERN wenyewe wanadai wanatumia sayansi kufanikisha hayo ila hawa kina nimrod uchawi wa voodooo ulihusika kidogo maana Mungu ni Roho hivyo kma unataka upambane naye lazima uwe kiroho sio kimwili kma hao CERN
Mkuu hata hizi program za CERN kuna mambo mazito nyuma ya pazia
 
Ila ukweli ukijifunza kwa undani kuhusu babeli siyo mnara ni nguvu ya kiroho ilitumika kumfikia Mungu na jamaa walifanikiwa kwa kiasi kikubwa Mungu angeacha kuwatawanya mwezi mmoja wangemfikia.
Maana hakuna mnara wa kufika kwa Mungu hapa inabaki ni nadharia lakini ukweli ni mlango wa kiroho
 
Wakuu, mimi nilijua gharika iliangamiza watu wote duniani isipokua Nuhu na wenzie waliokua kwenye safina.

Sasa huyu Nimrod na wenzake walitokea wapi?

Pia mleta mada anasema Nimrod na wenzie walitaka kujenga mnara mrefu ili wajifanyie jina kwa majirani zao.

Hao majirani zao nao walitoka wapi?

Je, ni kweli kwamba gharika haikuangamiza dunia nzima?
Ni kizazi cha nuhu
 
Gharika la Nuhu halikuwa kwa dunia nzima kama bible imavyosema ilikuwa ni kwa sehem husika ya ebeo lile kwa nuhu hakutumwa kwa ajili ya ulimwengu mzima ila ni kwa watu wa eneo lile hata kisayans leo haisapot hicho kitu dunia nzima ku floot maji.!
 
Ila mimi bado najiuliza huko mbinguni ni wapi ki location yaani? Ni huko tunapotazama jua ama? Au ni nje ya ulimwenguu huu labda..

Maana Yesu Kristo alipokua akipaa kwenda mbinguni alipaa kwenda juu uelekeo wa jua kwa mujibu wa maandiko. Lakini zama hizi sayansi imeweza kutoka nje ya dunia na kuona umbali wa ma bilion ya km mbele, sasa hio mishale ya nimrodi ilirushwa kwa style ya namna gani mpaka kufika huko aliko Mungu?

Sambamba na hilo ikiwa wana sayansi wameweza kuona umbali ambao ukitaka kwenda itakuchukua miaka bilion kufika tena kwa speed ya mwanga, na mpaka hapo mbingu hawajaiona huenda iko mbele zaidi. Sasa Yesu aliepaa tuchukue alikua na speed ya mwanga mara 1000 huenda mpaka leo hajafika bado, zingatia mwanga husafiri km 300000 kwa sekunde?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom