Mbunge SIMAI SAID ametukumbusha mambo ya Mnara wa Babeli

Mbunge SIMAI SAID ametukumbusha mambo ya Mnara wa Babeli

feyzal

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2016
Posts
8,963
Reaction score
18,535
Wakuu habari ya wakati huu.

Awali ya yote naomba moderator msiunganishe huu uzi na nyuzi zingine huu unajitegemea.

Ukisoma kitabu cha biblia ambacho ni kitabu takatifu kwa waumini wa dini ya kikristo ipo stori inayozungumzia namna utawala wa mfalme nimrodi baada ya kufanya dhambi nyingi mwishowe wakata kujengea mnala ambao utawapeleka mbinguni wakampige Mungu. Lakini kwa ukuu wa Mungu akafanya lugha gonga dhahiri shahiri ili lengo lisifanikiwe hapo ndipo lugha za mataifa zikazaliwa ,watu wakatengana kutokana na lugha zao na kazi ile ikafia pale.

Hiki ndo kile kile kinachotokea pale bungeni baada ya madhambi mengi ya wabunge hawa wasiochaguliwa na wananchi sasa M/Mungu mtukufu ameleta lugha gongana na ameamua kumtumia Huyu mbunge kuvuruga bunge hili lisilo la wananchi na kwa mara ya kwanza Mbunge ameongea jambo lakini hakuna aliyepiga makofi.

Ukiangalia vizuri maneno ya msemaji na confidence yake walayi anaongea unaona kabisa jambo hili alipewa script kwanza alikua hajiamini anatetemeka(tone yake) lakini M/Mungu mtukufu jambo zuri zaidi alimfanya mtu huyu aongee bila kumficha huyo mtu aliyemuita Yuda.

Soma pia: Mbunge Simai: Serikalini kuna Yuda, huko nyuma amewahi kutajwa ni mzigo, amewaumiza watu wengi

Hii ni nukuu ya meneno yake “Rais Samia anaongoza Nchi kwa upendo lakini ndani ya Serikali kuna (YUDA) huyu Yuda anazunguka makanisani kutafuta huruma ya wananchi, anatuaminisha kwamba Rais Magufuli alimpenda sana, kama Magufuli alimpenda kwa nini alimtupa huko Nje, Sisi tunajua watu waliopendwa na Magufuli” - SIMAI SAID, Mbunge Kupitia Baraza la Wakalishi ZANZIBAR.

Binafsi huu nauona kama ushindi kwa watu hawa kuanza kugombana hasa viongozi wa kubwa zaidi ,huu ni sehemu ya ushindi mdogo kuelekea mafanikio.

Nawasilisha
 
Wakuu habari ya wakati huu.

Awali ya yote naomba moderator msiunganishe huu uzi na nyuzi zingine huu unajitegemea.

Ukisoma kitabu cha biblia ambacho ni kitabu takatifu kwa waumini wa dini ya kikristo ipo stori inayozungumzia namna utawala wa mfalme nimrodi baada ya kufanya dhambi nyingi mwishowe wakata kujengea mnala ambao utawapeleka mbinguni wakampige Mungu. Lakini kwa ukuu wa Mungu akafanya lugha gonga dhahiri shahiri ili lengo lisifanikiwe hapo ndipo lugha za mataifa zikazaliwa ,watu wakatengana kutokana na lugha zao na kazi ile ikafia pale.

Hiki ndo kile kile kinachotokea pale bungeni baada ya madhambi mengi ya wabunge hawa wasiochaguliwa na wananchi sasa M/Mungu mtukufu ameleta lugha gongana na ameamua kumtumia Huyu mbunge kuvuruga bunge hili lisilo la wananchi na kwa mara ya kwanza Mbunge ameongea jambo lakini hakuna aliyepiga makofi.

Ukiangalia vizuri maneno ya msemaji na confidence yake walayi anaongea unaona kabisa jambo hili alipewa script kwanza alikua hajiamini anatetemeka(tone yake) lakini M/Mungu mtukufu jambo zuri zaidi alimfanya mtu huyu aongee bila kumficha huyo mtu aliyemuita Yuda.

Hii ni nukuu ya meneno yake “Rais Samia anaongoza Nchi kwa upendo lakini ndani ya Serikali kuna (YUDA) huyu Yuda anazunguka makanisani kutafuta huruma ya wananchi, anatuaminisha kwamba Rais Magufuli alimpenda sana, kama Magufuli alimpenda kwa nini alimtupa huko Nje, Sisi tunajua watu waliopendwa na Magufuli” - SIMAI SAID, Mbunge Kupitia Baraza la Wakalishi ZANZIBAR.

Binafsi huu nauona kama ushindi kwa watu hawa kuanza kugombana hasa viongozi wa kubwa zaidi ,huu ni sehemu ya ushindi mdogo kuelekea mafanikio.

Nawasilisha
Mmh,mnara wa Babeli
 
Huyo mbunge Yale ni maneno ya kambi siyo ya kwake na timing imekuwa perfect Sana hivyo hiyo ni message kamili kabisa...kambi iloyomtuma wamejipanga na wanajua juu chini namna ya kucheza na mfumo, hata akiwa ni mbuzi wa kafara lakini SMS imetumwa.....ngoja tuone, na unajua nini kitacho amsha hisia za watu kushindwa kufanya maamuzi sahihi kuhusiana na Jambo la Aina hii?, ni IMANI na UKANDA
 
Ila Bible!!! Eti lugha za mataifa hapo ndio zilipo Anza kuzaliwa

Wakati kiswahili tangu kizaliwe hakuna miaka 1000

😄😄😄

So or kiswahili sio lugha ya kimataifa!?
 
Kwanini amwite Dr Nchimbi YUDA?
Kwanza Nchimbi hajawahi kumuita Samia Mh Dakatari Samia yeye husema Rais Samia. Fuatailia hotuba zake inaonekana kabisa hawana connection na ile 29 october imeua kabisa ukaribu.

NB:CCM ni wale wale
 
Kwanza Nchimbi hajawahi kumuita Samia Mh Dakatari Samia yeye husema Rais Samia. Fuatailia hotuba zake inaonekana kabisa hawana connection na ile 29 october imeua kabisa ukaribu.

NB:CCM ni wale wale
Ukoo wa panya ,wote wezi.
 
Back
Top Bottom