MMU hot talk

MMU hot talk

Mimi mshuwa alianza ubepari kitambo tu, Tv nyumbani ilikuwepo ila station ilikuwa ni Tv Zanzibar peke yake Tanganyika hatukuwa hata na kituo kimoja, kwahiyo home kulikuwa kumejaa Library ya mikanda ya vhs kibao.

Sheikh Yahya naye hakuwa nyuma alijizolea ujiko kwa wapenzi wa kuangalia mpira.

Hahahahah sisi TV kwa mara ya kwanza ilitinga home mwaka 1994. ilikuwa inch 14 black and white. kwa mbele tulikuwa tunaweka kioo cha rangi ili tufaidi tofauti ya rangi!!!

Hahahahha nakumbuka wkt ITV ndo wanaanza tangazo pendwa lilikuwa SALAMA CONDOM CHAGUO LA KISASA.
 
Leo ndio nimejua kumbe tunachat mababu hapa wakati mwingine mnasound kama viserengeti boy
 
Hahahahah sisi TV kwa mara ya kwanza ilitinga home mwaka 1994. ilikuwa inch 14 black and white. kwa mbele tulikuwa tunaweka kioo cha rangi ili tufaidi tofauti ya rangi!!!

Hahahahha nakumbuka wkt ITV ndo wanaanza tangazo pendwa lilikuwa SALAMA CONDOM CHAGUO LA KISASA.

Nadhani World Cup iliyofanyika Marekani mwaka 1994 ilimfanya mshuwa wako kunuwa tv ambapo tournament ile Romario na Bebeto wa Brazil walishine vilivyo bila kumsahau Robert Bagio.

Je tamthilia ya Tausi ya kina Mzee Mombasa mliiwahi au mlikutia vituko vya Masakuu na Otorong'ongo tu?

Hapo zamani mambo yalikuwa poa kinyume kabisa na sasa.
 
Ila mimi nakujua komredi. Lazima tulishagongana kwenye UDA au kuchungulia Sikinde wakipiga pale SILENT INN Mwenge. Hatujawahi gongana NEW CHOX cinema au kwenye CHAI MAHARAGE?

Hahahaha acha nami nijifanye najua watu bhana inaweza ninenepeshea CV yangu hapa JF intelijensi.

Komredi hata mi nahisi nakujua sana wewe:usa2:!

Ila kuhusu Silent Inn umenikumbusha mbali sana aisee. Nakumbuka ilipofunguliwa ile mwaka 1983 nilikuwa napenda sana kwenda kula pilau pale. Halafu Jumamosi na Jumapili nilikuwa naenda kuangalia ngoma za Muungano Cultural Troupe na ile mijoka yao.

Fast forward mwaka 1987 nikaanza kazi ya ubaunsa hapo hapo Silent (kitaani tulikuwa tunaiita Sailentini). Mwaka huo huo wakaja Tabu Ley na Mbilia Bel wakapiga bonge moja la show hapo na mi ndo nilikuwa kama head baunsa.

Fast Forward miaka kumi baadaye (1997), akaja tajiri mmoja wa Kihaya (jina nimemsahau) akapanunua (kama sikosei) halafu akapafanyia bonge moja la ukarabati na baadaye ndo ile bendi ya Diamond Sound ikaanza kupiga muziki pale. Ila wakati huu nilikuwa nishakuja kubeba maboksi baada ya kuona ubaunsa haulipi bongo. Lakini kila niliporudi likizo Silent ndo kilikuwa kiwanja changu.

Kuhusu New Chox pale, mi nahisi lazima tuliwahi kugongana hapo hususan kwenye moja ya zile movie za Emanuelle. Unazikumbuka hizo Komredi? Enzi hizo matangazo ya movie yanawekwa magazetini na mimi nilikuwa napenda sana movie za X. Na kwa jinsi wewe Komredi unavyopenda kuwakagua mabinti humu basi sina shaka lolote kabisa kuwa tumewahi kugongana hapo New Chox, Avalon, Empire, Empress, na hata Drive-In pale.

Halafu Chai Maharage nimezipanda sana mimi. Ruti la Mwenge-Ubungo zilikuwa kibao tu. Kuna wakati fulani hivi nilikuwa napenda sana kwenda kupata supu ya utumbo kwenye ule mgahawa wa Tarakea (pale Mwenge barabara ya Sam Nujoma karibu na yale maduka ya vifaa vya ujenzi). Huu mgahawa mpaka leo bado upo aisee na juzi juzi tu hapa nilienda nikapata mbuzi katoliki hapo. Kuna shori mmoja hivi anaitwa Manka nilikuwa namfukuziaga kipindi fulani.

Komredi leo umenikumbusha mbali sana aisee. Ila ndo hivyo bana...nami nakujua sana wewe. Hahahahaaaaa.
 
Nadhani World Cup iliyofanyika Marekani mwaka 1994 ilimfanya mshuwa wako kunuwa tv ambapo tournament ile Romario na Bebeto wa Brazil walishine vilivyo bila kumsahau Robert Bagio.

Je tamthilia ya Tausi ya kina Mzee Mombasa mliiwahi au mlikutia vituko vya Masakuu na Otorong'ongo tu?

Hapo zamani mambo yalikuwa poa kinyume kabisa na sasa.
Yeah inawezekana.... kina Romario na crying baby Bebeto. Ile Brazil ilikuwa mwisho wa maarifa. AFCON nawakumbuka enzi hizo kina Roger Mila, Kunde, Makanaky.... et el

Kudadadeki. Tausi ndege wanguuuu.... hii makitu ilichangia sana mimi kuwahi kurudi home. jamaa walikuwa creative. mpaka sasa sijaona tamthilia iliyofikia level hiyo. Hata kina Bishanga walijitahidi sana enzi hizo.

Kuna nyingine ilikuwa inaitwa Egoli ya Sauzi wacha kabisa. sio huu uchafu usioisha wa Isidingo.
 
Nadhani World Cup iliyofanyika Marekani mwaka 1994 ilimfanya mshuwa wako kunuwa tv ambapo tournament ile Romario na Bebeto wa Brazil walishine vilivyo bila kumsahau Robert Bagio.

Ebana eeh ile World Cup ilikuwa bab kubwa.

Romario na Bebeto walikuwa ni moto wa kuotea mbali. Kipa alikuwa Taffarel. Bila kuwasahau akina Ricardo Rocha, Mauro Silva, Dunga, Branco, Rai, Aldair, Cafu, Marcio Santos, Ronaldo (akiwa na miaka 18 tu) na wengineo.

Nakumbuka kwenye mechi yao dhidi ya Uholanzi Bebeto alipofunga goli akaenda pembeni kushangilia na wenzake kwa staili ya kumbeba mtoto mchanga.

Baadaye nikaja kujua kumbe siku ile Bebeto na mkewe walikuwa wamepata mtoto wa kiume ambaye naye sasa hivi anacheza soka ya kulipwa huko Brazil.

Icheki hiyo clip hapa.....

 
Last edited by a moderator:
Yeah inawezekana.... kina Romario na crying baby Bebeto. Ile Brazil ilikuwa mwisho wa maarifa. AFCON nawakumbuka enzi hizo kina Roger Mila, Kunde, Makanaky.... et el

Kudadadeki. Tausi ndege wanguuuu.... hii makitu ilichangia sana mimi kuwahi kurudi home. jamaa walikuwa creative. mpaka sasa sijaona tamthilia iliyofikia level hiyo. Hata kina Bishanga walijitahidi sana enzi hizo.

Kuna nyingine ilikuwa inaitwa Egoli ya Sauzi wacha kabisa. sio huu uchafu usioisha wa Isidingo.

Komredi itabidi nasi tuanzishe #TeamVibabuVyaJF ili tuwe na nguvu pindi tunaponyanyapaliwa humu na hivi vitoto vya dotcom.
 
Komredi hata mi nahisi nakujua sana wewe:usa2:!

Ila kuhusu Silent Inn umenikumbusha mbali sana aisee. Nakumbuka ilipofunguliwa ile mwaka 1983 nilikuwa napenda sana kwenda kula pilau pale. Halafu Jumamosi na Jumapili nilikuwa naenda kuangalia ngoma za Muungano Cultural Troupe na ile mijoka yao.

Fast forward mwaka 1987 nikaanza kazi ya ubaunsa hapo hapo Silent (kitaani tulikuwa tunaiita Sailentini). Mwaka huo huo wakaja Tabu Ley na Mbilia Bel wakapiga bonge moja la show hapo na mi ndo nilikuwa kama head baunsa.

Fast Forward miaka kumi baadaye (1997), akaja tajiri mmoja wa Kihaya (jina nimemsahau) akapanunua (kama sikosei) halafu akapafanyia bonge moja la ukarabati na baadaye ndo ile bendi ya Diamond Sound ikaanza kupiga muziki pale. Ila wakati huu nilikuwa nishakuja kubeba maboksi baada ya kuona ubaunsa haulipi bongo. Lakini kila niliporudi likizo Silent ndo kilikuwa kiwanja changu.

Kuhusu New Chox pale, mi nahisi lazima tuliwahi kugongana hapo hususan kwenye moja ya zile movie za Emanuelle. Unazikumbuka hizo Komredi? Enzi hizo matangazo ya movie yanawekwa magazetini na mimi nilikuwa napenda sana movie za X. Na kwa jinsi wewe Komredi unavyopenda kuwakagua mabinti humu basi sina shaka lolote kabisa kuwa tumewahi kugongana hapo New Chox, Avalon, Empire, Empress, na hata Drive-In pale.

Halafu Chai Maharage nimezipanda sana mimi. Ruti la Mwenge-Ubungo zilikuwa kibao tu. Kuna wakati fulani hivi nilikuwa napenda sana kwenda kupata supu ya utumbo kwenye ule mgahawa wa Tarakea (pale Mwenge barabara ya Sam Nujoma karibu na yale maduka ya vifaa vya ujenzi). Huu mgahawa mpaka leo bado upo aisee na juzi juzi tu hapa nilienda nikapata mbuzi katoliki hapo. Kuna shori mmoja hivi anaitwa Manka nilikuwa namfukuziaga kipindi fulani.

Komredi leo umenikumbusha mbali sana aisee. Ila ndo hivyo bana...nami nakujua sana wewe. Hahahahaaaaa.

Comrade.....hahahahhaa.... umenikubusha black na Yellow Emannuelle. Wakati huo tunawahi gazeti la mfanyakazi tuone Drive-in kuna movie gani... kama vipi tunachepukia Empire, avalon au Empress. Madogo hawajui uwanja wa basketball na drive-in cinema tulikuwa tunajichanganya sana pale kabla mmarekani hajapachukua.

Comrade hatujawahi kukutana Railway Gerezani kuangalia ngumi enzi hizo sijui kina Titus Simba wanatamba? Hatujawahi kukutana uwanja wa Taifa enzi za kina Peter Tino?

Ndo nshakuambia mi nakujua sana tu LOL
 
Yeah inawezekana.... kina Romario na crying baby Bebeto. Ile Brazil ilikuwa mwisho wa maarifa. AFCON nawakumbuka enzi hizo kina Roger Mila, Kunde, Makanaky.... et el

Kudadadeki. Tausi ndege wanguuuu.... hii makitu ilichangia sana mimi kuwahi kurudi home. jamaa walikuwa creative. mpaka sasa sijaona tamthilia iliyofikia level hiyo. Hata kina Bishanga walijitahidi sana enzi hizo.

Kuna nyingine ilikuwa inaitwa Egoli ya Sauzi wacha kabisa. sio huu uchafu usioisha wa Isidingo.
Nyani Ngabu yule Muhaya anaitwa Joseph Rwegasira ila baadaye akaingia dili za ulokole na New Silent inn ikageuzwa kuwa hekalu la bwana na siyo pambio la shetani tena.

Mkuu Asprin binafsi nimeshiriki kama crew kwenye Cape film industry tangu mwaka 1995 na nimeshiriki location za endemol siyo nia yangu kujiexpose hapa ila tu Isidingo imesimama sana ila hujaielewa maudhui yake

Egoli maana yake ni Johannesburg au The City of gold.

Mkuu naishia hapo wadogo zetu siku wanapita sana humu wakikusoma tu mwandiko wakautambuwa itakuwa haijakaa vizuri.
 
Last edited by a moderator:
Ebana eeh ile World Cup ilikuwa bab kubwa.

Romario na Bebeto walikuwa ni moto wa kuotea mbali. Kipa alikuwa Taffarel. Bila kuwasahau akina Ricardo Rocha, Mauro Silva, Dunga, Branco, Rai, Aldair, Cafu, Marcio Santos, Ronaldo (akiwa na miaka 18 tu) na wengineo.

Nakumbuka kwenye mechi yao dhidi ya Uholanzi Bebeto alipofunga goli akaenda pembeni kushangilia na wenzake kwa staili ya kumbeba mtoto mchanga.

Baadaye nikaja kujua kumbe siku ile Bebeto na mkewe walikuwa wamepata mtoto wa kiume ambaye naye sasa hivi anacheza soka ya kulipwa huko Brazil.

Icheki hiyo clip hapa.....



Hii ndio mechi Baggio alikosa penalt kwenye fainali?
 
Last edited by a moderator:
Komredi itabidi nasi tuanzishe #TeamVibabuVyaJF ili tuwe na nguvu pindi tunaponyanyapaliwa humu na hivi vitoto vya dotcom.

Yeah inawezekana.... kina Romario na crying baby Bebeto. Ile Brazil ilikuwa mwisho wa maarifa. AFCON nawakumbuka enzi hizo kina Roger Mila, Kunde, Makanaky.... et el

Kudadadeki. Tausi ndege wanguuuu.... hii makitu ilichangia sana mimi kuwahi kurudi home. jamaa walikuwa creative. mpaka sasa sijaona tamthilia iliyofikia level hiyo. Hata kina Bishanga walijitahidi sana enzi hizo.

Kuna nyingine ilikuwa inaitwa Egoli ya Sauzi wacha kabisa. sio huu uchafu usioisha wa Isidingo.

Hahahah..shkamooni
 
Comrade hatujawahi kukutana Railway Gerezani kuangalia ngumi enzi hizo sijui kina Titus Simba wanatamba? Hatujawahi kukutana uwanja wa Taifa enzi za kina Peter Tino?

Ah pale Relwe Gerezani mbona nilikuwa naenda sana. Enzi za kina Stanley "Ninja" Mabesi na yule Mzambia Charles Libondo. Pale mi nilikuwa mwenyeji sana.

Ndo nshakuambia mi nakujua sana tu LOL

Halafu unajua Dar kipindi hicho ilikuwa ndogo sana ukilinganisha na sasa. Nazimiss sana enzi hizo aisee na najua tushapishana sana kwenye hivyo viwanja. Hahahaaa
 
Hii ndio mechi Baggio alikosa penalt kwenye fainali?

Hapana. Hii ilikuwa ni robo fainali kati ya Brazil na Uholanzi.

Halafu unalikumbuka goli la Rashid Yekini dhidi ya Bulgaria?

Jamaa abaada ya kufunga akaenda akazishika nyavu kwa hisia sana.

Cheki hapa.....

 
Last edited by a moderator:
Ebana eeh ile World Cup ilikuwa bab kubwa.

Romario na Bebeto walikuwa ni moto wa kuotea mbali. Kipa alikuwa Taffarel. Bila kuwasahau akina Ricardo Rocha, Mauro Silva, Dunga, Branco, Rai, Aldair, Cafu, Marcio Santos, Ronaldo (akiwa na miaka 18 tu) na wengineo.

Nakumbuka kwenye mechi yao dhidi ya Uholanzi Bebeto alipofunga goli akaenda pembeni kushangilia na wenzake kwa staili ya kumbeba mtoto mchanga.

Baadaye nikaja kujua kumbe siku ile Bebeto na mkewe walikuwa wamepata mtoto wa kiume ambaye naye sasa hivi anacheza soka ya kulipwa huko Brazil.

Icheki hiyo clip hapa.....



Rais wa wabeba box kwenye ubora wake, kweli nimeamini asiyekujuwa hakuthamini, sikuwahi kujuwa hapo kabla kama eneo hili unaweza kulichambuwa kwa viwango vya juu kama vya Dr Rick Abdalla.

Hii style ya Bebeto siku moja Mohamed Hussein Mmachinga aliiga uwanja wa Taifa, siku moja nilienda nyumbani kwa Method Mogela fundi R.I.P nilikumta Mohamed Hussein naye yupo pale nikamwambia kaka ulichemka.
 
Last edited by a moderator:
Yeah inawezekana.... kina Romario na crying baby Bebeto. Ile Brazil ilikuwa mwisho wa maarifa. AFCON nawakumbuka enzi hizo kina Roger Mila, Kunde, Makanaky.... et el

Kudadadeki. Tausi ndege wanguuuu.... hii makitu ilichangia sana mimi kuwahi kurudi home. jamaa walikuwa creative. mpaka sasa sijaona tamthilia iliyofikia level hiyo. Hata kina Bishanga walijitahidi sana enzi hizo.

Kuna nyingine ilikuwa inaitwa Egoli ya Sauzi wacha kabisa. sio huu uchafu usioisha wa Isidingo.
Umesahau sunset beach na the bold and the bautfull ......!
 
Back
Top Bottom