Mwanakijiji,Hivi kweli Hussein Mwinyi ana standinding ya kuwa Waziri wakati si mbunge? Labda kama miye nimesahau katika chaguzi zote za nyuma sikumbuki kuona mawaziri wakiendelea na shughuli za uwaziri baada ya Bunge kuvunjwa, naomba nikumbushwe. Inawezekana kabisa nimekosea kabisa katika uelewa wangu kwa sababu toka zamani tulijua Bunge likivunjwa hakuna mawaziri, na shughuli zinafanywa na Makatibu. Why now tunafanya vinginevyo kuna mabadiliko yaliyopita ambayo hatukuyajua?
AG alishalitolea ufafanuzi hili. Kama ufafanuzi ule hautoshi hilo litakuwa ni suala jingine ambalo linahitaji marekebisho ya Katiba yetu ya JMT. Wenzetu Kenya wameliona hili kwenye Katiba yao mpya. Mawaziri wao sasa hawatatokana na Wabunge na idadi ya wizara imetajwa kabisa kwenye katiba yao mpya. Teuzi zote za Rais wao zitathibitishwa na Bunge. Wana Katiba nzuri sana sasa kuliko hata ile ya South Africa.