Mmepoteza Ubunge kwanini bado ninyi mawaziri?

you guys give the poor girl a break.
"Poor girl"? Unacheza wewe. Tunachambua wagombea watakaoenda kuchukua nchi, nchi letu linaenda na maji kwa sababu tunachagua majinamizi tusiyoyajua kutuongoza, unasema "poor girl"? Kizazi chetu tunaanzisha utamaduni mpya wa kuchambua wagombea kama karanga, tuwajue ndani na nje kabla ya.

mlijuaje kama ulikuwa muda au tarakishi za chadema? hana lunch break? hana internet yake binafsi? hana likizo na kutumia kufanya hicho alichokifanya?
Ndio maana kuna maneno "au muda wake." Kutumia muda wako kuanjia wanaume mitandaoni ambao tayari wana wanawake zao hilo ni kashfa. Ushawahi kuona mwenendo wa wakina Zitto na Slaa na Mnyika wanapokuwa mtandaoni, adabu na heshima mwanzo mwisho. Huyu dada Mtema anaaibisha chama.

alipofanya hivyo alikuwa gender sensitive na si regia mtema na wala alikuwa hajatangaza nia ya kugombea ubunge bado... mhukumuni kwa aliyoyafanya baada ya kutangaza nia
Ndio maana mpaka leo Sophia Simba ana sifa mbaya ya kashfa za ngono kabla ya uwaziri (amekiri alitembea na wame za watu, kina Meya Kitwana Kondo, mpaka akapata mimba). Na hata baada ya kutangaza nia, Mtema bado yumo humu anasema yeye ni mtu wa "kujiachia mzima mzima." Mgombea ubunge kweli?

(japo kuwa sidhani kama inaweza kumsaidia sana kwa kuwa haonyeshi mabadiliko ya kabla na baada)
Angalia sasa, wewe mwenyewe unampiga madongo. Tumwambieni ukweli jamani, huyu dada anachemka.
 
Mawaziri wako kwenye muhimili wa serikali...japo bunge limevunjwa, serikali siku zote inaendelea kufanya kazi
 
Mawaziri wako kwenye muhimili wa serikali...japo bunge limevunjwa, serikali siku zote inaendelea kufanya kazi

mmh.. haya... kama wapo wabunge basi wapo na mawaziri kwa sababu tukikubali kuwa kiufundi kwamba mtu akishateuliwa waziri anaweza kupoteza Ubunge na akabakia kuwa Waziri. Fikiria kwamba mtu kateuliwa kuwa Waziri halafu akaamua kuacha Ubunge je ataendelea kuwa Waziri kwa sababu alipoteuliwa alikuwa ni Mbunge?
 
Kwa kweli kuna ulazima wa hii katiba kuandikwa upya maana yaelekea hata sisi wenyewe hatuielewi vizuri na ndio maana kunakuwa na tafsiri mbalimbali.

Mambo kama haya ya uwaziri na ubunge yalitakiwa yawe ya kueleweka moja kwa moja bila hata tafsiri.

Nyani, umegusa mtima, tano za haraka kwanza!
Wale mnaoelewa vifungu vya katiba naomba msaada wenu tafadhali. Kwa vile mawaziri watabaki kuwa hivyo, je ni mpaka Rais mteule atakapotangazwa? au ni mpaka Rais mteule atakapoapishwa? au ni mpaka Rais atakapounda baraza la mawaziri jipya? je katiba imesema nini kuhusu lini ni ukomo wao! Kwavile Rais anapochaguliwa anatangaza baraza la mawaziri, je kuna siku anavunja lile la zamani na je anatakiwa kutangaza au ni kimya kimya?
Kama Rais mteule akiwa Dr Slaa, katika kipindi cha kuelekea kutangaza baraza lake la mawaziri, je hawa wa sasa wataendelea kuwa mawaziri hadi baraza jipya litakapotangazwa?.
 
mmh.. haya... kama wapo wabunge basi wapo na mawaziri kwa sababu tukikubali kuwa kiufundi kwamba mtu akishateuliwa waziri anaweza kupoteza Ubunge na akabakia kuwa Waziri. Fikiria kwamba mtu kateuliwa kuwa Waziri halafu akaamua kuacha Ubunge je ataendelea kuwa Waziri kwa sababu alipoteuliwa alikuwa ni Mbunge?

The whole shebang ya kuteua wabunge kuwa mawaziri ni so that rais aweze kuteua watu waliopata ridhaa ya wananchi. Asiweze kutuletea mchizi yeyote tu (which is neatly defeated by his special seats, what a reasoning)

Hata kama bunge limevunjwa, mawaziri walioteuliwa kutoka bunge lililopita bado wanakuwa ni watu waliopewa ridhaa na wananchi, na kunakuwa hakuna wengine wapya waliopewa ridhaa mpya zaidi, kwa hiyo wanaendelea kuwa mawaziri mpaka hapo ridhaa mpya ya wananchi itakapotolewa.

Kama kuna criticism basi mi naona swala kubwa zaidi ya hili ni waziri kuwa mbunge, which may raise a conflict of interest between the executive and the legislature.

Mtu unapelekwa bungeni kutetea wananchi wa jimbo lako, halafu unapewa kazi ya serikali kuitetea serikali kuu, wapi na wapi.
 
mmh.. haya... kama wapo wabunge basi wapo na mawaziri kwa sababu tukikubali kuwa kiufundi kwamba mtu akishateuliwa waziri anaweza kupoteza Ubunge na akabakia kuwa Waziri. Fikiria kwamba mtu kateuliwa kuwa Waziri halafu akaamua kuacha Ubunge je ataendelea kuwa Waziri kwa sababu alipoteuliwa alikuwa ni Mbunge?

Mfano ulioutoa wa mbunge kuacha ubunge kwa sababu zingine zozote na sio kwa sababu za uchaguzi, hapo anaweza kubaki kuwa waziri kama Raisi anaweza kumteua katika vile viti maalumu, la sivyo hawezi kuingia bungeni na hivyo hawezi kuwa waziri. Lakini nafikiri ubunge unaoungelea sasa hivi ni katika hiki kipindi cha uchaguzi (transition period), kabla ya kuundwa kwa bunge jipya. Serikali bado wako kazini, kwa hiyo ni haki yao hawa wakuu kuitwa mawaziri, kwa sababu kiutendaji bado ni mawaziri...hivi hii Wizara ya katiba na sheria hawana website? Nimejaribu kutafuta sijaiona, Maana hivi vitu vingene ni bora vingewekwa wazi...
 
Kuwa mbunge ni SIFA YA LAZIMA: Katiba inasema mawaziri wote ni lazima watokane na wabunge. Period.



Kuna mazingira ya Kikatiba ambapo Rais anaweza kuteua mtu ambaye si mbunge kuwa Waziri (lakini lazima awe mtu aliyekuwa Mbunge katika Bunge lililopita). Mazingira hayo yameanisha katika ibara ya 90. Kwamba Jamhuri iko vitani au kuna jambo ambalo linalazimu Rais aunde serikali. Sasa hivi hakuna na nilazima Rais "ateue" siyo wao "waendelee" kuwa mawaziri kana kwamba hawakupoteza ubunge wao.



Ndio lakini katika mazingira fulani si kwamba anaendelea kuwa Waziri wakati Bunge limevunjwa.




"Hivi leo" hawezi kwa sababu hakuna mazingira ya kuteua mtu kuwa Waziri bila kuwa Mbunge. Na unaposema kuteua maana yake, si kwamba waliokuwepo wanaendelea kuwa mawaziri.



Kuna mazingira ya Rais kuteua watu nje ya Bunge na mazingira hayo hayapo kwa sasa.

Kuna vitu vilivyosemwa katika katiba, na vitu anavyosema Mwanakijiji.

Katiba ilivyosema ni kwamba, sifa ya kuteuliwa kuwa waziri ni ubunge, pia mawaziri hawakomi kuwa mawaziri kwa bunge kuvunjwa, pia rais anaweza kumteua mtu ambaye hakuwa waziri, lakini alikuwa mbunge katika bunge lililovunjwa, kuwa waziri baada ya bunge kuvunjwa na kabla ya bunge jipya kuapishwa.

Ni vitu vilivyowekwa wazi katika katiba, sasa kama hukubali exceptions na qualifications hizi na unataka katiba irekebishwe nitakuelewa.

Lakini ukijifanya kukomaa shingo, kwamba mtu akikwambia statement a, na kutoa exception b, kwamba useme ukishatoa statement a huwezi kutoa exception b, utakuwa ume fail somo la logic. Hata misahafu ina qualifications, itakuwa hiyo katiba ?

Nikiwambia natengeneza Non Euclidean Geometry kwamba pembe zinapimwa kwa nyuzi, lakini pembetatu zote zina nyuzi zaidi ya 180, huwezi kuanza kupinga eti hakuna pembetatu iliyo na nyuzi zaidi ya 180, utakuwa unapingana na axioms za Non Euclidean Geometry.

Vivyo hivyo, katiba ni axiomatic, huwezi kupinga axioms zilizo katika katiba. Kama huzikubali zibadilishe, lakini zikiwemo tu katika katiba ni valid mpaka utakapozibadilisha.
 
Mimi nina kawaida ya kusoma kwanza kabla ya kutoa hoja. Mwanakijiji ungesoma katiba ya nchi yaani URT usingekuwa na hoja hii au ungekuwa nayo wakati Rais mtarajiwa Dr. Slaa anapofanya mchakato wa kubadili katiba yetu ndani ya siku 90 baada ya kuapishwa kwake! Ibara ya 57 (1) na (2) zinaongelea au kujibu hoja hii. Mfano, 57 (2) inasema "kiti cha waziri au naibu waziri kitakuwa wazi litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo: a. ..., b. ikiwa mwenye madaraka hayo atakoma kuwa mbunge kwa sababu yoyote isiyohusika na kuvunjwa kwa bunge, c. ..., d. ... e. ... f. ukiwadia wakati wa Rais mteule kushika madaraka ya Rais basi mara tu kabla Rais mteule hajashika madaraka hayo, g. ..." Source: The Tanzania National Website


Hawa jamaa yaani mawaziri wataendelea kushika nyadhifa hizo mpaka siku jamaa anaapishwa. Swali kwa katiba, je kampeni zao zitatenganishwa vipi na shughuli za kiserikali? Je, watatumia magari na fedha za serikali kuchanganya kampeni na serikali? Mimi naona ni ngumu kidogo!!
 
Jaji anabakia kuwa cheo tu, sasa hivi Werema hafanyi kazi yake ya Ujaji tena kwani ni Mwanasheria Mkuu. HIvyo amebakia na title tu ya "jaji" kama tunavyowaita kina Jaji Kisanga n.k si kwa sababu ni mtumishi wa mahakama. Kumbuka mojawapo ya masharti ya kuweza kuwa AG ni kuwa awe ni mtu ambaye anaweza kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.



sidhani kama kuna tatizo labda kwa watu wengine, lakini kwangu ni title ya heshima na usomi wake tu siyo kazi yake ya sasa. Anapozungumza anazungumza kama Mwanasheria Mkuu. .

Naomba nami niongezee kuwa title ya "jaji" inabakia hata akistaafu na ndio maana hadi leo tunao akina Judge Robert Kisanga ( alikuwa Jaji kabla ya kutumikia kwenye Tume ya haki za binadamu kama mwenyekiti), na wengineo kama Jaji Lewis Makame - mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, etc. bado wakiendelea kuitwa cheo hicho japo hawasikilizi na kuamua mashauri.Hata wakifa bado wataendelea kuitwa " jaji" fulani na ndio maana kuna hata Jengo la LHRC lina jina la Justice Lugakingira.Title itakoma tu kama jaji alifukuzwa kupitia due process.

Kuna situations ambapo jaji ame staafu na kuamua kuingia katika legal practice kama wakili, hapa hawezi kuitwa tena jaji maana amehamia upande mwingine ( bar) ilhali alikuwa kwenye (bench) as a judge na hapa wanakuwa uso kwa uso na jaji au hakimu katika kusikilizwa kwenye shauri..Mifano ni akina Advocate Mkate, Advocate Mrosso, Advocate Chua, Advocate Chipeta N.K.Wakiendelea kuitwa "jaji" italeta confusion huko mahakamani, itaondosha dhana ya usawa mbele ya sheria na pia siyo sahihi kufuatana na utendeji kimahakama.

Werema anabakia kuitwa title hiyo hata baada ya kuingia kwenye mhimili wa Executive baada ya kuacha kutumikia nafasi ya Ujaji Judiciary.Hakuna any harm kuendelea kuitwa title yake ya "Jaji" maana hasikilizi na kuamua shauri bali yeye kama AG anatoa mwongozo kuhusu maswala ya Sheria kama mshauri mkuu wa serikali wa sheria.

Nimeona nichukue fursa iliyojitokeza kutoa mwanga kidogo kwenye hili.
 
Pia lazima kutakuwa na maana ya hawa jamaa kuendelea kuwa mawaziri. Mfano, kukiwa na burning issue ambayo inataka maamuzi ya baraza la mawaziri itakuwaje? Yaani Raisi akae na makatibu wakuu kinyume na katiba? Ni sawa na kusema Rais avue madaraka yake wakati wa kampeni halafu nani ashikilie nchi - Chief Justice?
 
Kiranga:

a. Wabunge wanapoteza Ubunge wao vipi?

b. Ni sifa gani zinamfanya mtu awe Waziri?

Mwanakijiji na Kiranga;

Ukisoma"statutory law"yetu utagundua kabisa mgogoro wa kikatiba wa wazi uliopo kwenye provision ya"Bunge na Mawaziri",Katiba inasema wazi kabisa kuwa ili kuwa Waziri lzm uwe Mbunge na kwa hiyo basi kama leo kuna "test case"kuhusu kipengele hicho na mie ningeitwa mahakamani kama "amicus curiae" na kwenye "per curiam opinion"yangu ningesema wazi kabisa kuwa HUWEZI KUWA WAZIRI KAMA BUNGE LIMEVUNJWA,kwa hapo ningekubaliana na Mwanakijiji!

Kiranga,naungana na wewe kwenye matatizo ya " Strict Constriction" kwa hawa wanasheria wetu ambapo hata Mwanasheria Mkuu katoa majibu rahisi sana kuhusu mkanganyiko huo mkubwa kwenye katiba yetu.Kama TZ ingekuwa na vyombo hili vya kisheria visivyo chini ya serikali ndiyo wakati wao huu kwenda mahakamani na kuanzisha"legal brief"ili kila Waziri avuliwe nafasi hiyo pindi Bunge likivunjwa!

Fikiria mkanganyiko wa Uchaguzi wa ubunge jimbo la Nyamagana;Waziri wa Mambo ya Ndani Lau Masha kamuwekea pingamizi Mbunge Mteule wa CHADEMA kama sio raia na pingamizi lake limepita.Hata kama kweli pingamizi lake lina msingi watu tunaweza fikiria kuwa katumia madaraka yake vibaya kwa sababu tu kuwa ni wizara anayoiongoza ndiyo inahusika na uhalali wa uraia wa Mtz!


Regina,yachukulie maneno ya Mwana JF Kiranga kama changamoto kwako na wala usiyachukulie maneno yake kivingine.Ni wakati wako sasa hasa kama ukishinda Ubunge uyafanyie kazi matatizo haya ya kikatiba kwa kuomba "judicial Review",ingawaje sina imani yangu kwa Mahakama chini ya Mzee Jaji Ramadhani kidogo imepungua hasa kufuatia hukumu "isiyoeleweka" ya Mgombea Huru.

Regina,ukishinda ubunge nenda mahakamani haraka kafungue "Writ of Mandamus"ili kumuamuru Mahakama imuambie Mwanasheria Mkuu wa Serikali atangaze wazi kuwa Bunge likivunjwa Mawaziri warasimu nafasi zao kwa Makatibu wakuu!
 
Solution nzuri tu ni kuondoa ulazima wa mawaziri kuwa wabunge, mawaziri watoke nje ya bunge lakini wawe confirmed na bunge. Simple and clear.

Unaondoa / punguza significantly conflicts of interests za legislature / executive, electioneering, favoritism, backdoor dealings etc na hapo hapo unabakisha ukweli kwamba mawaziri watapata consent ya watu by proxy.

Plus unakuwa na abigger pool to choose from.
 
Kama mpk sasa wanadhan wana madaraka hayo,kuna uwezekano hata baada ya uchaguz wakaondoka na hayo ma'V8.Yaan washafny madaraka kama kijiwen-muda wa kukaa ukiisha kila mtu anachkua kiti alichokalia anaenda nacho nyumbani kwao
 
Naomba nami niongezee kuwa title ya "jaji" inabakia hata akistaafu na ndio maana hadi leo tunao akina Judge Robert Kisanga ( alikuwa Jaji kabla ya kutumikia kwenye Tume ya haki za binadamu kama mwenyekiti), na wengineo kama Jaji Lewis Makame - mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, etc. bado wakiendelea kuitwa cheo hicho japo hawasikilizi na kuamua mashauri.Hata wakifa bado wataendelea kuitwa " jaji" fulani na ndio maana kuna hata Jengo la LHRC lina jina la Justice Lugakingira.Title itakoma tu kama jaji alifukuzwa kupitia due process.

Kuna situations ambapo jaji ame staafu na kuamua kuingia katika legal practice kama wakili, hapa hawezi kuitwa tena jaji maana amehamia upande mwingine ( bar) ilhali alikuwa kwenye (bench) as a judge na hapa wanakuwa uso kwa uso na jaji au hakimu katika kusikilizwa kwenye shauri..Mifano ni akina Advocate Mkate, Advocate Mrosso, Advocate Chua, Advocate Chipeta N.K.Wakiendelea kuitwa "jaji" italeta confusion huko mahakamani, itaondosha dhana ya usawa mbele ya sheria na pia siyo sahihi kufuatana na utendeji kimahakama.

Werema anabakia kuitwa title hiyo hata baada ya kuingia kwenye mhimili wa Executive baada ya kuacha kutumikia nafasi ya Ujaji Judiciary.Hakuna any harm kuendelea kuitwa title yake ya "Jaji" maana hasikilizi na kuamua shauri bali yeye kama AG anatoa mwongozo kuhusu maswala ya Sheria kama mshauri mkuu wa serikali wa sheria.

Nimeona nichukue fursa iliyojitokeza kutoa mwanga kidogo kwenye hili.

Kuna umuhimu wa kuitwa Jaji Mstaafu, maana wanatengeneza confusion kama hii kwa kumuita A.G Jaji.
 
Kuna umuhimu wa kuitwa Jaji Mstaafu, maana wanatengeneza confusion kama hii kwa kumuita A.G Jaji.


Ndio hivyo. Hii pia italeta confusion maana technically speaking hajastaafu.

Kuondosha confusion ingewezekana kutofautsha inapokuja kumnukuu Werema kwa mfano, kinachotakiwa ni kwa mwandishi kusema "....Judge Werema ( as he then was)......" lakini hili nalo litafinyika nadra maana muktadha mara nyingi hautatoa fursa hiyo.Matokeo yake inatumika "Judge" (Werema) the AG, kama title ya "Mr." au "honorable" ..
 
So far.... katika hii thread nimefurahia sehemu ambayo Tindikali na Kiranga wanajibizana! Halafu mtu wa aina hii ndio unakuta anakosoa wanasiasa eti ni matapeli.... mh... kazi ipo!!!!
 
Kiranga
Mengi yapi asiyiayelewa dada wa watu
siasa, sheria, kilimo, biashara, michezo utamaduni, kazi, katiba. jaribu kumsaidia wapi apige msasa zaidi maaana binafsi naona dada yetu ana kiu ya kujua mengi.

Regia usikate wale kukatishwa tamaa hizo ni constructive criticism. Unaweza kujaribu kuiga mbinu hii. Google it kabla. Nadani part ya exposure anayosema kiranga itapata dawa.


Mtazamaji thank you for the comment.Mimi wala sikati sikatishwi tamaa na huyu jamaa.nafahamu kwamba namzidi kiuwezo kwa mbali sana,yeye kazi yake ni kubishana na watu tu kila siku na hasa watu tuliomzidi akili.Nimekuwa nikijuliza kwanini ananifuata kiasi hiki lakini sijapata bado jibu.Kutofahamu kipengele kimoja cha katiba haimaniishi kuwa huijui katiba.Maendeleo hayaletwi na kuijua Katiba yote,ingekuwa hivyo basi kina Mwanakijiji wangebadilisha hii nchi,kila siku wanasoma na kuandika lakini bado tuko pale pale.Maendeleo yanaletwa kwa vitendo sio kukaaa kwenye kompyuta masaa 24 na kubishana na watu.Ninafuraha kwamba mimi ni sehemu ya mabadiliko katika nyanja zote,ya kuandika na kufanya kwa vitendo.Wengine watabaki kuwa waongeaji tu.
 
Hivi kweli Hussein Mwinyi ana standinding ya kuwa Waziri wakati si mbunge? Labda kama miye nimesahau katika chaguzi zote za nyuma sikumbuki kuona mawaziri wakiendelea na shughuli za uwaziri baada ya Bunge kuvunjwa, naomba nikumbushwe. Inawezekana kabisa nimekosea kabisa katika uelewa wangu kwa sababu toka zamani tulijua Bunge likivunjwa hakuna mawaziri, na shughuli zinafanywa na Makatibu. Why now tunafanya vinginevyo kuna mabadiliko yaliyopita ambayo hatukuyajua?
 
Mtazamaji thank you for the comment.
Mimi wala sikati sikatishwi tamaa na huyu jamaa.nafahamu kwamba namzidi kiuwezo kwa mbali sana,yeye kazi yake ni kubishana na watu tu kila siku na hasa watu tuliomzidi akili.Nimekuwa nikijuliza kwanini ananifuata kiasi hiki lakini sijapata bado jibu.

Kutofahamu kipengele kimoja cha katiba haimaniishi kuwa huijui katiba.Maendeleo hayaletwi na kuijua Katiba yote,ingekuwa hivyo basi kina Mwanakijiji wangebadilisha hii nchi,kila siku wanasoma na kuandika lakini bado tuko pale pale.Maendeleo yanaletwa kwa vitendo sio kukaaa kwenye kompyuta masaa 24 na kubishana na watu.Ninafuraha kwamba mimi ni sehemu ya mabadiliko katika nyanja zote,ya kuandika na kufanya kwa vitendo.Wengine watabaki kuwa waongeaji tu.


hebu Ms Mtema tufafanulie kidogo ulijuaje kama umemzidi akili ( au japo jibu la general la watu wanajuaje kuwa wamemzidi fulani akili)
 
Back
Top Bottom