Japo swala lenyewe lipo wazi mno (Mwanakijiji hupenda kutengezea mada zenye tafrani za bandia labda akipungukiwa mada za makala) niseme ni Wanasheria wachache sana wana ufasihi wa udadavuzi wa maswala ya Kikatiba na sheria kama ulivyofanya hapo, ahsante.
Hebu fikiria, Mahakama Kuu ilikubaliana na hoja inayosema "Katiba inavunja Katiba." Na Wanasheria wote wenye vipasa sauti mjini wakasema hukumu ya Mahakama ya Rufaa imekosewa. Eti wangependa jaji aweze kufuta kipengele cha Katiba asichokipenda.
Ila niongeze moja ambalo unaweza kuwa unakosea, maana mimi na wewe hatulegezeani wala hatudekezani kwenye udadavuzi: si sahihi kusema kuna kitu kilifanya Mahakama ya Rufaa "isiamue kesi na kuirudisha Bungeni." Waliamua kesi. Ilitangua uamuzi wa Mahakama za chini. Na hawakurudisha kitu Bungeni, kesi haikutoka Bungeni. Walichokisema kuhusu Bunge ni mazungumzo baada ya habari muhimu, wanaita kisheria "dicta," hakitusaidii chochote kiamri, hawakuliamuru Bunge chochote, walishauri tu. Walisema wanasikitishwa na sheria ya mgombea huru, lakini hawana nguvu ya kuandika upya Katiba. Na walikua sawa.
Na wewe uko sawa sawia unaposema kwenye Katiba yetu hakuna kipengele kizito kuliko chenzake.