Mmepoteza Ubunge kwanini bado ninyi mawaziri?

Sijui kipindi hiki hawa mawaziri utaona plate number za magari yao zimebadilishwa na zinatumia STK na sio zile plate number za mawaziri

Je kisheria katika kipinid hiki kuna vitu hawawezi kufanyia maamuzi? Je Kuna stahili zao zinapunguzwa? Wataaalam nielimisheni
 
Mkuu haukupaswa kukiri kutofahamu hili, angalia usije ukawakatisha tamaa wafuasi wako.

Mi nishasema hapo hamna kitu, watu wananiona mbishi. Mbona kuna mengi tu tushaona hapa kwamba huyu bibie hana uwezo kabisa kabla hata ya hili ?

Kuna watu wanafikiri kwamba, excessive humility, actually humility iliyo bordeline na pure ignorance, ni virtue.

Tunataka watu wanaoenda bungeni wawe wanajua mambo yanavyoenda, kwa sababu watu wanaojua mambo yanavyoenda - hususan mambo basic kama haya- ndio wanaoweza kutoa mchango wa kubadilisha mambo makubwa, kama kubadilisha katiba.

Sasa wewe Regia hata katiba huijui, utaweza kutaka kuibadilisha ili iwe nzuri zaidi ?
 
Sijui kipindi hiki hawa mawaziri utaona plate number za magari yao zimebadilishwa na zinatumia STK na sio zile plate number za mawaziri

Je kisheria katika kipinid hiki kuna vitu hawawezi kufanyia maamuzi? Je Kuna stahili zao zinapunguzwa? Wataaalam nielimisheni

Ukifuatilia mfululizo na kusoma vifungu vya katiba utaona mawaziri wanaendelea kuwa mawaziri na wana nguvu zote za kiwaziri mpaka baraza jipya la mawaziri litakapotangazwa na kuapishwa rasmi.

Watu wameweka vifungu vya katiba na kuvielezea, sasa unataka kuelimishwa zaidi vipi mkuu wangu ?
 
Ukifuatilia mfululizo na kusoma vifungu vya katiba utaona mawaziri wanaendelea kuwa mawaziri na wana nguvu zote za kiwaziri mpaka baraza jipya la mawaziri litakapotangazwa na kuapishwa rasmi.

hakuna kifungu hata kimoja kinachoonesha hilo ndugu yangu; kama mawaziri wanatokana na wabunge, na wabunge wanakoma Bunge linapovunjwa au kwa sababu nyingine yoyote; basi mawaziri hawawezi kuwepo kama hawapo wabunge. Mtu pekee ambaye anaendelea kuwa na madaraka yake hadi kuapishwa ni Rais wa Jamhuri ya muungano na makamu wake. Hadi atakapoapishwa rais mwingine.

Kama kuna haja ya kuwepo Waziri baada ya Bunge kuvunjwa basi Rais anateua na kumwapisha mtu ambaye hakuwa aliwahi kuwa mbunge katika Bunge lililopita na hilo ni katika mazingira kama ya wakati wa vita (wa mujibu wa ibara ya 90). Hii ni kwa mara ya kwanza (katika kumbukumbu yangu) ambapo mawaziri wameendelea kutumia nyadhifa zao za uwaziri wakati Bunge limevunjwa. Nitakuwa tayari kusahihishwa.



Watu wameweka vifungu vya katiba na kuvielezea, sasa unataka kuelimishwa zaidi vipi mkuu wangu ?[/QUOTE]
 
Sijui kipindi hiki hawa mawaziri utaona plate number za magari yao zimebadilishwa na zinatumia STK na sio zile plate number za mawaziri

Kwa sababu si mawaziri

Je kisheria katika kipinid hiki kuna vitu hawawezi kufanyia maamuzi? Je Kuna stahili zao zinapunguzwa? Wataaalam nielimisheni

hakuna jambo lolote wanaloweza kufanya wakiwa ni mawaziri ni kinyume na katiba.. tngekuwa na able opposition ingefunguliwa mara moja kesi ya Kikatiba kwani hawa jamaa wanatumia madaraka wasiyokuwa nayo unless kama tumetangaziwa kuwa Jamhuri iko vitani na Rais kawateua kutekeleza mambo fulani. Nje ya hapo wanatuibia huku tunawaangalia. Matokeo yake Masha anafikiria bado ana cloud na mambo ya ndani na Ngeleja anafikiria kuwa yeye bado ni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje.

Kwa sababu kama siyo wabunge wameweza vipi kuwa Mawaziri?
 
Kwa sababu si mawaziri



hakuna jambo lolote wanaloweza kufanya wakiwa ni mawaziri ni kinyume na katiba.. tngekuwa na able opposition ingefunguliwa mara moja kesi ya Kikatiba kwani hawa jamaa wanatumia madaraka wasiyokuwa nayo unless kama tumetangaziwa kuwa Jamhuri iko vitani na Rais kawateua kutekeleza mambo fulani. Nje ya hapo wanatuibia huku tunawaangalia. Matokeo yake Masha anafikiria bado ana cloud na mambo ya ndani na Ngeleja anafikiria kuwa yeye bado ni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje.

Kwa sababu kama siyo wabunge wameweza vipi kuwa Mawaziri?

Mazee nimeweka vifungu vya katiba vinavyoonyesha kwamba kuvunjwa kwa bunge sio msingi wa uwaziri kuisha, kama unavyo vingine vinavyosema tofauti, kwamba kuvunjwa kwa bunge ni msingi wa uwaziri kuisha tuwekee hapa tuelimike zaidi.

Ngeleja kawa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje kuanzia lini ? Afikiri yeye Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje kwa sababu gani ?

Katiba imesema wazi kuhusu grounds za Waziri kuacha kuwa waziri

(b) ikiwa mwenye madaraka hayo atakoma kuwa Mbunge kwa sababu yoyote isiyohusika na kuvunjwa kwa Bunge;

Meaning kwamba Waziri haachi kuwa Waziri kwa sababu ya kuvunjwa kwa bunge.

Sasa tuonyeshe unaposema wewe basi tujue argument yako ina ammunition gani.
 
Dada kuna wengine tuishasema usiyoelewa mbona mengi sana tu na unahitaji exposure zaidi.
Kiranga
Mengi yapi asiyiayelewa dada wa watu
siasa, sheria, kilimo, biashara, michezo utamaduni, kazi, katiba. jaribu kumsaidia wapi apige msasa zaidi maaana binafsi naona dada yetu ana kiu ya kujua mengi.

Regia usikate wale kukatishwa tamaa hizo ni constructive criticism. Unaweza kujaribu kuiga mbinu hii. Google it kabla. Nadani part ya exposure anayosema kiranga itapata dawa.
 
Na hata waingereza tunaofuta na kuiga iga mfumo wao wa sheria na utawala nadhani mawaziri wao bado wanakuwa na mamlaka fulani hata bunge linapovunjwa kwa ajili ya uchaguzi. Ila mamlaka wanayokuwa nayo ni minimal na kuna baadhi ya maamuzi hawawezi kufanya katika katika kipindi hicho cha kampeni na uchaguzi.
 
Sababu ingine ya mawaziri kutopaswa kuwa wabunge.

Yaani vitu vyepesi vyepesi tu lakini tuna vi complicate wenyewe.

Wabunge wanaweza kufanya kampeni wakati bunge likiwa kwenye recess huku baraza la mawaziri likiendelea kuwepo na kufanya kama kawaida hadi hapo litakapoundwa jingine na mawaziri wapya kuapishwa. Simple as that.
 
Tanzania hatuna katiba, ila tulicho nacho ni bunch la viraka vipya juu ya vya zamani. Katiba yetu haina tofauti na gari ambalo body yake ni model ya Moris, engene korolla, gearbox bedford, site mirror Kiberenge na tyres Toroli. Halafu uanze kushangaa kwamba pamoja na kwamba gari inatembea kwenye lami bado inatetemeka. Mtu yeyote anaetetea hoja kwa kutegemea utetezi wa vifungu vya katiba ya tanzania sioni namna ya kumthibitisha. Kuna chama kimoja kimetamba ikiwa kitapewa ridhaa ya kuunda serikali ndani ya miezi minne wataanza mchakato wa kuunda katiba mpya. Chama hicho sii kingine ni chadema. Hivyo basi sote tukiunge mkono kwa kura zetu kiweze kutukomboa na mtesi wetu katiba. Wajameni acheni kulia lia ndani ya gari bovu ccm, shukuni huko na kwa pamoja tuagize gari mpya model ya 2010, Chadema with new consitusion!
 
Ukifuatilia mfululizo na kusoma vifungu vya katiba utaona mawaziri wanaendelea kuwa mawaziri na wana nguvu zote za kiwaziri mpaka baraza jipya la mawaziri litakapotangazwa na kuapishwa rasmi.

Watu wameweka vifungu vya katiba na kuvielezea, sasa unataka kuelimishwa zaidi vipi mkuu wangu ?

Msingi wa swali langu unatokana na Observation kwa nini Plate number za magari yao zinabadilishwa?
 
Are you serious unaposema Jaji si sehemu ya mahakama ?

Hapana sikusema hivyo, rudia ndugu yangu nilichosema.

Hahaha, unajua Tanzania tuna mambo ya ajabu sana. Hapa kuna a very big potential conflict of interest.

Hivi imekuwaje Kikwete akamteua Jaji, mtetezi wa judiciary, aende kuwa A.G, mtetezi wa executive ? This is a big no no.

Jaji anabakia kuwa cheo tu, sasa hivi Werema hafanyi kazi yake ya Ujaji tena kwani ni Mwanasheria Mkuu. HIvyo amebakia na title tu ya "jaji" kama tunavyowaita kina Jaji Kisanga n.k si kwa sababu ni mtumishi wa mahakama. Kumbuka mojawapo ya masharti ya kuweza kuwa AG ni kuwa awe ni mtu ambaye anaweza kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Na huyu Jaji naye kakubali appointment tu, sasa anapoongea na kuitwa A.G Jaji Werema watu wanakuwa wanajiuliza anaongea kama nani ?

sidhani kama kuna tatizo labda kwa watu wengine, lakini kwangu ni title ya heshima na usomi wake tu siyo kazi yake ya sasa. Anapozungumza anazungumza kama Mwanasheria Mkuu.


Kuna wakati Jaji Edward Mwesiumo alikuwa Mbunge, Jaji na Naibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani. Mtu mmoja huyo huyo yupo katika legislature, executive na judiciary. Ingekuja showdown kati ya mihimili hii mitatu sijui ange resolve vipi conflicts of interest.

Kumbuka kuwa Ujaji mtu akishakuwa Jaji ni Jaji hadi anastaafu. Hivyo hata baada ya kustaafu bado unaweza kumwita Jaji.



Wabunge wa bunge lililovunjwa, kabla ya kuchaguliwa bunge jipya, hata wale ambao hawakuwa mawaziri wanaweza kuteuliwa kushika nafasi ya uwaziri, implying kwamba uwaziri unaweza kushikwa by virtue ya mtu kuwa mbunge katika bunge lililovunjwa in the interim before a new parliament is elected.

Ndiyo inawezekana on certain condition (soma ibara ya 90) not under normal circumstances.


Tunachoshindwa kuelewa, au kukataa kukubali, ni kwamba hawa watu waliokosa ridhaa ya kuwakilisha wananchi wamekosa ridhaa hii kwa bunge lifuatalo, na ingawa bunge lililopita limekwishavunjwa, rais ana uwezo hata wa kuwateua watu ambao hawakuwa mawaziri kushika uwaziri kwa nguvu yao ya kwamba walikuwa wabunge katika bunge lililopita mpaka hapo bunge jipya litakapoapishwa.

very true.. lakini anatakiwa kuwateua tena na kuwaapisha na pili only wakati kuna mazingira maalum ambayo yako kwenye Ibara ya 90 a.k.a Tanzania iko vitani. Nje ya hapo hakuna mawaziri.


Ukisema katiba ina walakini unaweza kuwa na point, lakini ukisema Mawaziri hawa hawafai kuwa mawaziri kwa sababu si wabunge, na kwamba kuna violation ya katiba, utashangaza watu kwa sababu katiba yenyewe imetoa provision wabunge wa bunge liliopita walio mawaziri kuendelea kuwa mawaziri, na hata kumpa uwezo rais kuteua mawaziri wapya miongoni mwao, in the interim.


of course nimekubali toka mwanzo kuwa waliokuwa wabunge wanaweza kuteuliwa tena kuwa Mawaziri lakini siyo kuendelea kuwa mawaziri kutokana na mandate yao iliyoisha wakati Bunge limevunjwa. Hadi hivi sasa Kikwete hajateua mawaziri wengine (labda kama sijasikia na hatujatangaziwa) lakini pili hakuna mazingira ya kuwarrant Rais kuteua mawaziri wakati tunaenda kwenye kampeni. Haijawahi kutokea Bunge kuvunjwa na mawaziri wakaendelea kuwa mawaziri.
 
Sababu ingine ya mwaziri kutopaswa kuwa wabunge.

Yaani vitu vyepesi vyepesi tu lakini tuna vi complicate wenyewe.

Wabunge wanaweza kufanya kampeni wakati bunge likiwa kwenye recess huku baraza la mawaziri likiendelea kuwepo na kufanya kama kawaida hadi hapo litakapoundwa jingine na mawaziri wapya kuapishwa. Simple as that.

sasa hivi Bunge halipo kwenye recess. Bunge limevunjwa, hakuna Spika, hakuna wabunge hakuna mawaziri.
 
Oh wait....ningependa kujua kama hao wabunge walio mawaziri bado wanaendelea kulipwa mishahara yao....
 
Mazee nimeweka vifungu vya katiba vinavyoonyesha kwamba kuvunjwa kwa bunge sio msingi wa uwaziri kuisha, kama unavyo vingine vinavyosema tofauti, kwamba kuvunjwa kwa bunge ni msingi wa uwaziri kuisha tuwekee hapa tuelimike zaidi.

Ngeleja kawa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje kuanzia lini ? Afikiri yeye Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje kwa sababu gani ?

Katiba imesema wazi kuhusu grounds za Waziri kuacha kuwa waziri



Meaning kwamba Waziri haachi kuwa Waziri kwa sababu ya kuvunjwa kwa bunge.

Sasa tuonyeshe unaposema wewe basi tujue argument yako ina ammunition gani.


Kiranga:

a. Wabunge wanapoteza Ubunge wao vipi?

b. Ni sifa gani zinamfanya mtu awe Waziri?
 
sasa hivi Bunge halipo kwenye recess. Bunge limevunjwa, hakuna Spika, hakuna wabunge hakuna mawaziri.

Whatever the case hoja yangu bado iko pale pale kuwa hakuna ulazima wa mawaziri kuwa wabunge na pindi bunge livunjwapo basi hata uwaziri wao unakoma.

Kwa hiyo kama hakuna mawaziri ina maana basi hata serikali kwa namna fulani haipo, si ndio? Kwa hiyo tupo tupo tunaeleaelea...
 
Kianga
Mengi yapi asiyiayelewa dada wa watu
siasa, sheria, kilimo, biashara, michezo utamaduni, kazi, katiba. jaribu kumsaidia wapi apige msasa zaidi maaana binafsi naona dada yetu ana kiu ya kujua mengi.

Regia usikate wale kukatishwa tamaa hizo ni constructive criticism. Unaweza kujaribu kuiga mbinu hii. Google it kabla. Nadani part ya exposure anayosema kiranga itapata dawa.

Huyu dada kaanza kutangaza anagombea ubunge bila kutaja jimbo wala jina lake, akawa anataka kuleta biashara za kutuuzia mbuzi aliye katika gunia, watu makini tukakataa na kumweleza kwamba ukishasema unagombea ubunge huna budi kutangaza jina lako na jimbo, kama hutaki kutangaza, usiseme chochote.

Akabisha kama mtu ambaye haelewi the very basic principles of public service, kwamba ukishataka kazi ya kuwahudumia watu katika siasa, huna privilege ya kutaka kutojulikana, ukitaka kufanya hivyo wengine tutafikiri una jambo unaficha au hujiamini, au vyote.

Nikashikia bango hili, mpaka akakubali kujitaja. Alivyojitaja akawa anataka kuchukua credit kwamba kajitaja, kama vile kajitaja kwa kutaka mwenyewe na si kwa preessure ya watu. Nikamwambia ukishalazimishwa kufanya kitu huwezi kuchukua credit, umelazimishwa. Akatuonyesha tena asivyo organized, akasema kaamua kutaja jina lake mwenyewe bila kulazimishwa, na alijitaja siyo kwa pressure yangu, bali kwa kuambiwa na watu fulani waliomshawishi (contradicting her first position). Hata hivyo akaendeleza usiri wake na kukataa waliomshawishi katika PM hapa JF ni kina nani, na hivyo kutufanya wengine tuhisi hakuna mshawishi kwenye PM wala nini, ni utunzi wa hadithi za ku "save face" tu. Usiri siri unatupa watu sababu ku suspect uongo ongo.

Alipojitaja akajionyesha kwamba hata anapoamua kufanya jambo zuri, hawezi kulifanya vizuri - hata mazuri nayo yanaweza kufanywa vizuri au vibaya- akaenda kututajia historia ya maisha yake yote mpaka vitu ambavyo havina relevancy katika uchaguzi huu, ikawa anajitaja kama anatafuta mtu wa kumuoa wazae watoto. Akajionyesha hana kiasi na hajui proportion, wala hana priority, anapokuwa msiri anaficha kila kitu hata jina humjui, anapoamua kujitaja anakutajia mpaka vitu vya ndani kabisa ambavyo hatuhitaji kuvijua, too much informatiopn. Anajionyesha asivyokuwa na exposure.

Listi inaweza kuwa ndefu, lakini kama unaona namuonea na chochote atakachofanya nitaona makosa, hili linatokana na ukweli kwamba chochote atakachofanya anafanya kwa makosa. Juzi kaja hapa kajionyesha tena kwamba hana tact, akitaka kujionyesha muwazi katoa mambo yao ya ndani kabisa chamani, na kuanzisha confrontation na mwanachama mwenzake Kitila Mkumbo basically akimuita Kitila muongo anayepotosha mambo hapa JF, bila ya kuwa na sababu ya msingi ya kusababisha confrontation hii. Bahati nzuri Kitila kauchuna, maana angeamua kujibizana na huyu wangewapa faida watu. Regia akajidai uwazi hapa na kusema huo ndio msimamo wake, baadaye akafuta maneno yake na kujionyesha hana msimamo. Flip flopping, tena hata bila kueleza kwamba kabadili mawazo.

Kwa kifupi ndiye mtu wa aina hii, incoherent, msiri msiri, mnyemela nyemela etc. Wanasema King Midas kila alichogusa kiligeuka dhahabu, huyu dada kila anachoguza kinageuka kinyesi.

Ndiye mbunge mtarajiwa huyu ? Hata watu kama kina Tundu Lissu na Mnyika washaanza kumshtukia na kum diss by her own admission aliyopost hapa JF.
 
Back
Top Bottom