Mmepoteza Ubunge kwanini bado ninyi mawaziri?

Mmepoteza Ubunge kwanini bado ninyi mawaziri?

Ningekuonyesha, lakini tatizo sitaki ku compromise privacy yangu. Halafu si muhimu sana kujionyesha.
Umechomoa tego hilo, mtu anakwambia "ni bora ungeonyesha mifano badala ya kulaumu tu," nitakuonyeshaje mifano wakati hapa hatujuani? Na hata kama tungejuana, si vizuri kujisifia.

Mtu kama wewe angekuwa msemaji kwenye serikali huko mbona Watanzania wengi wangejifunza kuwasiliana. Sijui tutafika huko katika uzao wetu? Hahahahahahaaa
 
Asante sana Malafyale,nimekupata.
Kuhusu Mwanakijiji naomba nieleweke sikumaanisha ambavyo imeeleweka na wengi humu.Namheshimu Mwanakijiji kuliko mtu mwingine yeyote ndani ya JF,natambua mchango wake katika taifa hili hata kwangu pia as an individual,namuomba radhi kama nayeye atakuwa amenielewa vibaya.Hata Ilani yangu ya Jimboni imekuwa polished na yeye.

Mwanakijiji kama na wewe umenielewa vibaya na kukwazika kwa hili ninaomba unisamehe sana.

Naanza kuona machungu ya kutumia jina halisi wakati huo ukiwa na maadui ambao siwafahamu wala sijui niliwatengenezaje.Nachelea kutolitumia tena jina hili na hii itakuwa ni post yangu ya mwisho kwani kama mwanadamu mwenye moyo,mwili na nafsi nakwazika ninaposhambuliwa bila sababu za msingi na hasa watu wenyewe siwajui ni kina nani.
Kila pande inamwona mwenzake ana makosa hivyo sio rahisi kufikia muafaka.Niko kwenye kipindi kinachohitaji uvumilivu wa hali ya juu lakini kama mwanadamu nashindwa.

Kwaheri friends.
Kwa heri Kiranga na timu yako Tindikali na Gaijin napenda kuwaambia kuwa Jimbo ninashinda na mjengoni nitakwenda,hii ni ndoto yangu na lazima itimie.

Malafyale nitakutafuta.

Aluta Continua

Regia Mtema
Mgombea Ubunge-Kilombero(CHADEMA)

Usijali dada nyumako tuko wengi, tunakuombea na pia tunakusaidia hata katika kampeni mpaka kieleweke. Jipe moyo mjengoni ukiingia haya ya hapa jf yatakuwa madogo so chukulia hii kama changamoto kwako ili by the time unatinga kumjengo ushapata mazoezi ya kutosha. Endelea kutumia jina lako ili uweze kukomaa katika siasa...Ili upate mazoezi ya kujua wapi uongee na nini, jinsi ya ku-react na hasa jinsi ya ku-control feelings zako.

Napenda ushupavu wako na comitment....Nilikuona kwenye uwanja wa mapambano ukiwa na gari lako jeusi...Kaza mwendo dada shujaa ni yule mwenye makovu mengi mgongoni mwake lakini mwenye tabasamu la ushindi usoni mwake...
 
Umechomoa tego hilo, mtu anakwambia "ni bora ungeonyesha mifano badala ya kulaumu tu," nitakuonyeshaje mifano wakati hapa hatujuani? Na hata kama tungejuana, si vizuri kujisifia.

Mtu kama wewe angekuwa msemaji kwenye serikali huko mbona Watanzania wengi wangejifunza kuwasiliana. Sijui tutafika huko katika uzao wetu? Hahahahahahaaa

Bonge la tego,

Hapo mtu ukiweka mbele mi ego na kutaka sifa unakwenda kichwa kichwa, nimefanya hiki wapi na hiki wapi.

Watu wanachukua data tu aaah kuumbe ndiye huyu.

Ndiyo maana sehemu nyingine hata ikiwa tempting vipi unauchuna tu.
 
Bonge la tego,

Hapo mtu ukiweka mbele mi ego na kutaka sifa unakwenda kichwa kichwa, nimefanya hiki wapi na hiki wapi.

Watu wanachukua data tu aaah kuumbe ndiye huyu.

Ndiyo maana sehemu nyingine hata ikiwa tempting vipi unauchuna tu.

Kwani una nini cha kuficha bana? Wakikujua wewe ni nani ubaya uko wapi?
 
Bonge la tego,

Hapo mtu ukiweka mbele mi ego na kutaka sifa unakwenda kichwa kichwa, nimefanya hiki wapi na hiki wapi.

Watu wanachukua data tu aaah kuumbe ndiye huyu.

Ndiyo maana sehemu nyingine hata ikiwa tempting vipi unauchuna tu.
Hahhahahahhahaaaaa

Ushanielewa?
 
Mimi nilishayaona haya matatizo ya communication, pamoja na mengine mengi ya attitude na exposure, kitambo tu hapa.

Watu wakaniona nataka kumzibia, sasa naona baadhi ya watu wanaelewa ninachosema.

Kiranga nimeona sehemu ya tatizo
assume dada regia anakubali amechemsha na anakuomba ushauri diplomatically . Ebu jaribu kumpa ushauri wa way foward. Afanyeje asinase kwenye hii mitego tena na kuchemsha vitu vidogo vidogo . Exposure ataipaaje? Attitude yake airekebishe vipi.
Maana kazi aliyonayo ni kubwa anahitaji msaada wa mawazo na ushauri kamaa wagombea wengine wowote wale.
 
Kiranga nimeona sehemu ya tatizo
assume dada regia anakubali amechemsha na anakuomba ushauri diplomatically . Ebu jaribu kumpa ushauri wa way foward. Afanyeje asinase kwenye hii mitego tena na kuchemsha vitu vidogo vidogo . Exposure ataipaaje? Attitude yake airekebishe vipi.
Maana kazi aliyonayo ni kubwa anahitaji msaada wa mawazo na ushauri kamaa wagombea wengine wowote wale.

Amesema hivyo ? Sijaona aliposema hivyo.
 
Tecnically wabunge bado wanaendelea kuwa wabunge mpaka uchaguzi mpya ufanyike.

Ukiwapotezea uwaziri wabunge kabla ya uchaguzi mpya utatengeneza leadership vacuum (as if we didn't have one already).
Hiyo red nimeipenda
 
Mtazamaji thank you for the comment.Mimi wala sikati sikatishwi tamaa na huyu jamaa.nafahamu kwamba namzidi kiuwezo kwa mbali sana,yeye kazi yake ni kubishana na watu tu kila siku na hasa watu tuliomzidi akili.Nimekuwa nikijuliza kwanini ananifuata kiasi hiki lakini sijapata bado jibu.Kutofahamu kipengele kimoja cha katiba haimaniishi kuwa huijui katiba.Maendeleo hayaletwi na kuijua Katiba yote,ingekuwa hivyo basi kina Mwanakijiji wangebadilisha hii nchi,kila siku wanasoma na kuandika lakini bado tuko pale pale.Maendeleo yanaletwa kwa vitendo sio kukaaa kwenye kompyuta masaa 24 na kubishana na watu.Ninafuraha kwamba mimi ni sehemu ya mabadiliko katika nyanja zote,ya kuandika na kufanya kwa vitendo.Wengine watabaki kuwa waongeaji tu.

Dada Regia..please jitahidi sana kuchunga kauli zako vinginevyo utamfanya Kiranga aonekane nabii.
 
Dada Regia..please jitahidi sana kuchunga kauli zako vinginevyo utamfanya Kiranga aonekane nabii.

Mazee Butola,

Mwambie huyu dada wenye uwezo hawajipigii ngoma kujisema kwamba wana uwezo, watu wanawajua na kuwasema kwamba wana uwezo.

Ukimuona mtu anajipigia ngoma sana kwamba "mimi najua sana" uanze kupata mashaka na kujua kwake, maana kujua kwake kunahitaji matangazo ya biashara.

Na kauli hizo ulizonukuu zinadhihirisha maneno yangu - huhitaji kuwa nabii by the way kuona haya- kwamba huyu dada ana kiburi, badala ya kuomba watu wampigie kura anasema ana hakika ataingia bungeni. Sehemu yenye kutaka kutuonyesha anajua mambo, kama kujibu maswali kiufundi, anakimbia (kaulizwa atafanya nini akiwa mbunge mpaka sasa hajajibu). Sehemu ya kuonyesha unyenyekevu na uerevu kwa kutojifanya mjuaji, anajifanya "ana uwezo sana".

Angekuwa ana uwezo sana angelia kwa maswali madogo ya JF? Angejiexpose kwa kukosa tact na kutukana "wabeba box" waliomuunga mkono ? Angemkashifu Mwanakijiji aliyemuandikia hotuba zake ? Angejiingiza katika kashfa zisizo na kichwa wala mguu za kuwatusi rejareja wanachama wenzake wa CHADEMA kina Mnyika, Kitila Mkumbo na Tundu Lissu?

Watanzania tunapenda watu wenye akili na kujiamini, lakini hatupendi hubris na kujidai. Hatupendi mgombea anayetuambia "mimi nimeshashinda uchaguzi, naingia bungeni/ ikulu" kabla ya siku ya uchaguzi. Hii ndiyo sababu moja Mrema alikosa urais 1995. Ukiwa na hubris ya kusema "naingia bungeni" essentially unawaambia wananchi "sihitaji kura zenu".

Mgombea akisema 'naamini wananchi wana imani nami na watanichagua tena" nitamuona ana jiamini, akisema "nitaingia bungeni tu" naona ego na hubris, red flags tayari. Huyu dada ana raise red flags.

Mgombea anaomba kura mpaka siku ya uchaguzi, hata kama anajiamini vipi.
 
Kiranga,

Unachokifanya hapa bodini dhidi ya Regia ni "BULLYING".


You should know better; please stop it.
 
Kiranga,

Unachokifanya hapa bodini dhidi ya Regia ni "BULLYING".


You should know better; please stop it.

Unaweza kufafanua bullying iko wapi? Kila kitu kina source, mostly mwenyewe Regia. Kama unabisha sema Kiranga umefanya bullying hapa, nikuonyeshe nimepata wapi hayo mawazo.

Moja ya matatizo yetu makubwa kama jamii na nchi ni kwamba hatutaki kuambiana ukweli, hatutaki ukweli hasa kama hatuupendi.Wengi wetu najua ni wakereketwa wa mageuzi, na tungependa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani viongeze wabunge, na hata kushinda urais. Hata mimi pia ningependa hili, lakini hili halimaanishi nikubali mtu asiye uwezo anapita mbele ya macho yangu kutaka kuingia bungeni, nitasema ukweli dhidi ya CCM, na nitatumia kanuni hizo hizo kuusema upinzani.

Upinzani una uungu gani mpaka uwe juu ya kukosolewa ?

Kwangu mimi, JF ni soko la mawazo, na kila mtu yuko huru kutoa mawazo yake, na kila kitu ili kiheshimiwe inabidi kiwe na source ya kukiback, sasa niambie hiyo bullying iko wapi na kitu gani kikufanyacho unione mimi ni bully tu na sio whistleblower anayesema kweli.

Ili kuendelea tunahitaji ushindani, sio ushindani kati ya CCM na upinzani tu, bali hata katika upinzani kuwe na mawazo tofauti yanayoruhusiwa kushindana. Kanuni hii hii inayotufanya tupende upinzani kati ya CCM na CHADEMA itufanye tupende kuona ushindani wa mawazo kati ya watanzania na upinzani, upinzani na upinzani, na CHADEMA na CHADEMA. Upinzani/ ushindani huu si mbaya, ni kitu tunachohitaji ili kuendelea. Maendeleo si kucheza lelemama, maendeleo yanataka kuumiza vichwa, yanataka ukiweka claim kwamba "Kiranga ni bully" uje na supporting evidence, hii na hii na hii, watu watakuelewa.Ama sivyo utaonekana mpambe wa Regia tu asiyependa watu waseme ukweli.

Ushindani huu wa kuwabana wapinzani na kutaka wafanye vizuri zaidi unaweza kuzaa mambo ya manufaa kwa taifa letu kiujumla kama mambo tunayosema hapa yatatiliwa maanani na watu tunaowasema na vyama vyao.

Hata mfalme wa Roma, Marcus Aurelius, alipokuwa akiranda mitaa ya Roma na kuamkuliwa kwa salamu zote zimfaazo mfalme mwenye bashasha zote kutoka kwa waja wake - nyingine bila shaka za kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa-, alikodi mtumwa mmoja kutembea nyuma yake karibu kabisa naye.Kazi ya mtumwa huyu ilikuwa ni moja tu, kumnong'oneza mfalme kwa karibu na kumwambia "Respica te, hominem te memento" ("Look behind you, remember you are only a man") na "Memento mori" ("Remember (that you are) mortal").

Regia na CHADEMA ni miungu gani hawa mpaka wasionyeshwe wanapofanya vibaya ? Miungu wapya hawa wameshushwa kwa msahafu gani huo ambao sijauona miye ? Analects? Torat? Quran? Baghavad-Gita ? Rig-Veda ? Dhammapada ? Talmud ? Tripitaka? The Bible ? The Egyptian Book of The Dead ? Zhuan Falun? The Book of Mormons? Kebra Negast ? The Communist Manifesto ? Mbona sikuyaona habari hizi kote huko ?

Mimi hapa kazi yangu ni kama huyu mtumwa wa Marcus Aurelius - tena bila malipo- CHADEMA wanapopandishwa kichwa na wafuasi wao wasioangalia hali halisi, mimi nawakumbusha mortality yao, nawaonyesha ninachofikiri si sawa, tena nawaonyesha hakuna chama chenye monopoly ya JF, nawaonyesha kwamba ingawa tunapenda mageuzi, kuna watu tunaheshimu kanuni na hatuwezi ku suspend kanuni eti kwa sababu tu huyu ni mgombea wa CHADEMA, kama tunakemea mediocrity CCM tutakuwa watovu wa uungwana na wengi wa hiyana kama hatutatanabahi ubaya wa kutokemea mediocrity CHADEMA. Hata kama tunaipenda CHADEMA, tunaipenda Tanzania zaidi.

Na tunaheshimu ukweli usiobadilika kwa kumuangalia mtu. Hatuwezi kuwa na double standards, eti set moja ya standards kwa CCM na kina Sophia Simba, na nyingine tofauti kwa CHADEMA na kina Regia Mtema, huu utakuwa unafiki.

Again, hebu nioneshe nimekuwa bully katika kipande gani nikuonyeshe kwamba siongei kufurahisha baraza tu, nikupe vielelezo, vingi sana kutoka kwa Regia mwenyewe.
 
Naanza kuona machungu ya kutumia jina halisi wakati huo ukiwa na maadui ambao siwafahamu wala sijui niliwatengenezaje.Nachelea kutolitumia tena jina hili na hii itakuwa ni post yangu ya mwisho kwani kama mwanadamu mwenye moyo,mwili na nafsi nakwazika ninaposhambuliwa bila sababu za msingi na hasa watu wenyewe siwajui ni kina nani.
Kila pande inamwona mwenzake ana makosa hivyo sio rahisi kufikia muafaka.Niko kwenye kipindi kinachohitaji uvumilivu wa hali ya juu lakini kama mwanadamu nashindwa.

Ms Mtema

tuko katika kipindi ambacho tungependa kujua misimamo ya wagombea wetu katika masuala mbali mbali. Usitunyime fursa hiyo

hao maadui usiowafahamu badala ya kuwaepuka kwa kuondoka hapa ungewachukulia kama sample ya watu wa aina hiyo ambao utaweza kukutana nao jimboni na sehemu nyingine kwenye siasa.


if you want peace, prepare for war
 
Back
Top Bottom