Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

kama hawa wakina abood basi kampuni ifutiwe leseni..

mh sidhani!sio rahisi!hili basi linawapeleka wajumbe wa mkutano mkuu wa chama kule dodoma na wanafika salama kabisa!ni ajali tu na dereva atatiwa nguvuni kwa mahojiano.
Alafu msipende kufuatilia biashara za mbunge na mchangiaji wa chama chetu magamba.
 
Poleni sana wote walipatwa na majeruhi, mungu yupo nanyi atawasaidia mpone haraka muendelee na majukumu yenu
 
Kiukweli mabasi mengi yanayobeba abiria ni chakavu, haiwezekani gari inatembea km 1,000 x 365 x 10yrs. Ajali ya sumry na aboud pia uchakavu unahusika. tunajua tumeongeza speed, governor, tukaweka mikanda na sasa tunweka car track lakini kuwe na ukomo wa gari kuwa barabarani either kwa miaka au mileage.

kama ma VX ni miaka mitano basi zisizidi jamani basi nyingi zilinunuliwa mwanzoni wa 2000, manake mlima nyoka si mchezo
 
Nakiri ajali zimekuwa nyingi sana sasa, lakini basi hili la Abood sijui ni mara ngapi limepata ajali ndani ya miezi 12 iliyopita. muda umefika sasa kwamba kila kampuni ya mabasi iwekewe record ya ajali inapotekea ajali zinajirudia rudia kama hawa wakina abood basi kampuni ifutiwe leseni. haya makampuni yamepewa leseni za kufikisha watu salama huko wanakoenda na sio kuuwa.

madereva wanachoka. Ni jukumu la serikali kuhakikisha wako wawili na mmoja wao asiwe kwenye bus hilo ila akae kama iringa ili awe kapumzika vya kutosha. Tukumbuke driver anapaswa kuwa fit kiakili na kimwili. Uzembe ni wa serikali kwa watu wake kujihusisha na rushwa ili hali sheria zipo wazi. RTO wa KIBAHA alishasukumwa tajiri basi nikiwa ndani ya busi lile miaka ya 2003 na sikuona tumesimamishwa popote hadi mwanza. Pia last 2 years nilikuwa natoka mwanza kufika nzega akaingia trafic kwa maana bus liende mwendo wa kawaida. Kilichotokea mwendo ulikuwa uleule na yeye akiwamo na b4 igunga tukabinuka watu wakafa na kuumia akiwemo trafick na dereva kufa. Alisinzia kwa kuwa alifika usiku wa manane mwanza tokea arusha na akatakiwa kugeuza bila kulala. Imagine.
 
Natamani biashara ya usafiri wa mabasi ufutiwe leseni turudi kwenye treni kama ilivyokuwa miaka ya nyuma, usafiri wa treni miaka ya nyuma ilikuwa ya uhakika kweli.
 
kuna swala mnaongea hamgusii yanayojiri katika hiyo nchi ya kufikirika
1.ulevi
2.ushirikina
3.uwongo
4.wizi
5.udalali
6.utumiaji madawa
7.uzinzi
8.njaa
9.uadilifu zero
10.kukata tamaa
11.short cut
12.wivu
13.usanii
14.ufisadi
15.kutokujali
16.ujanja kuwahi
17.
.
.
.
haya mambo yote niliyotaja watanzania wengi wanafanya wakiongozwa na rais wao,sasa uozo unaozalishwa hapo ndio matokeo ya hizo ajali na visa vya mauaji ya polisi na ufisadi kila siku
 
ndugu Bujibuji hujazungumzia pia ubovu wa barabara zetu, mathalani mlima nyoka pale lami kuna sehemu imejikusanya na ku form kama tuta hivi na pia mashimo (holes) kama lile lililomwangusha Dr Mwakyembe kipindi kile kwenye mteremko wa Ihemi. might also be the cause. unajua wahusika wetu hawa (Meneja Tanroads) mikoa, binafsi wananishangaza sana, hawana kawaida kutembelea barabara kuona deadly/dangerous damages zinazotokea kwa road na kushughulikia haraka matokeo yake wanaacha yanakuwa makubwa kiasi ya kusababisha ajali. Mfano ni kulika kwa barabara ya iringa - moro sehemu ya Iyovi kutokana na mvua.
 
Mungu awape tahfifu majeruhi wapone haraka tuje tuendelee kuijenga Tanzania yetu.
 
Hizi ajali ni sababu ya uzembe wa madereva, uchakavu wa vyombo vya usafiri, na tabia sugu ya trafiki ya kuendekeza rushwa.
Uswahilini wanamsingizia Rama mla watu kuwa eti ndiye chanzo cha ajali zote hapa nchini
Tatizo mi madereva kuendesha basi bila kujali kuwa ndani kuna wanadamu ambao uhai wao hauwezi kurudishwa ukishapotea. Bara ni mbaya hilo ni kweli na kila mtanzania anajua hili hivyo ni wajibu wa kila mtu kuwa makini hasa madereva wa mabasi. Pia kama nilivyosema awali abiria ni lazima watambue kuwa dereva anatakiwa kuhakikisha usalama wao na kama wanaona hafanyi hivyo wana haki ya kumtoa gamba. We live only once and therefore we should not allow anyone to temper around with this golden opportunity or if you wish, call it a prevelage from the Almighty God.
 
Marekani!!!!

Kama vibao vyako havisemi hii ndiyo speed limit, hiki hapa chini kinasema na kuna kingine hicho cha digital kinachokuonyesha mwendo kasi wako. Ku google vitu nusu nusu hakuhusiki.

radar-speed-sign.jpg
 
Sio lazima kibao kisema "hii namba ni kikomo cha mwendokasi - kilomita 50 kwa saa!"

Siyo lazima lakini ni bora kibao kiseme "SPEED LIMIT 30" kuliko kiseme "30".

btkm-speed-limit-sign.jpg


Vibao vyote hivyo havisemi "speed limiti ndio hii." Sasa usikandye kitu tu kwa sababu kiko Bongo kumbe ni vitu vina exist kimataifa. Na kama hujui kwamba polisi Bongo wanatumia radar speed detection basi unakuwa commentator wasiwasi, kwa lugha ya kiungwana, wa masuala ya udhibiti wa mwendokasi kwa sababu uko out of touch.
Hicho hapo juu kinasema "SPEED LIMIT 30". Na hao mapolisi wenu kama wanatumia "radar speed detection" (lol) basi nina mashaka hata kama zinafanya kazi.

Halafu "speed limiti" ndiyo nini?
 
wouldn't say out of your mind, out of touch, rather. Speed limit zipo karibu kila mahala along the major highways. Na kuna traffic officers all along, from Dar to Mwanza, for example, njiani nii wazee kwa kwenda mbele, na nimeshakuwa pulled over any number of times. Na speed limit sio moja Tanzania nzima, inategemea na eneo.

Kama unaruka na Precession Air mwanzo mwisho obviously u wouldn't be privvy to these things. Na ni moja ya drawbacks za wataalam wa JF, wengi, kama si majority, ni out of touch.

Mheshimiwa Taso, ewe uliye in "touch", hebu naomba maana ya hayo maneno niliyoyawekea rangi nyekundu hususan hilo la "privvy".
 
Pole kwa majeruhi...mh ilikuwa moro sasa mzimu wa ajali unahamia mbeya
 
jinamizi la ajali limehama kutoka morogoro na kwenda mbeya
 
mi nahisi ziraili amehamia mbeya kwa sasa. kabla ya kwenda mbeya ameichakaza sana morogoro, amemsamehe tu abood kwakua ni mwenyeji wa moro na akakumbuka ameshatoa roho za kutosha morogoro majuzi tu.
 
Back
Top Bottom