Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Ingekuwa nafuhu kwa kila ajari pakitokea vifo basi dreva awe wa kwanza kukatika make huwa wanajiona kama maroboti wasio na roho na nyama
 
Hamjamsikia mkuro badala ya kusema serikali inaondoa vp tatizo la msongamano, inataja adhabu mpya uendeshaji magari. Watanzania tumechimbiwa kaburi na ccm:grouphug:
 
Tatizo kubwa la madereva huwa hawafikirii maisha ya watu bali masilahi mbele.
Pia abiria ndo chanzo kikubwa cha ajali, kwani umchochea dereva kuongeza mwendo. Mwisho wake tena wanakuwa wa kwanza kumlaumu dereva. Mungu amlaze mahali pema peponi.:amen:
 
Dereva wa gari ndogo alikua anatoa watu kenye sherehe huko Kibada akawa anataka kushusha mtu hapo maeneo ya Kibaoni, akaanza kuingia kushoto, kuhamaki dereva wa Canter alikuwa yuko speed sana na (alionekana kuwa kalewa sana yani chicha baya) alikuwa akitokea feri kwenda kibada huku akiyumba yumba kama anataka kumkwepa dereva wa gari ndogo, sijuio ni mawenge au ni nini! huku akija upande wa saloon hiyo.

Kuonaa kuona vile derva wa gari ndogo akahamia kulia ili amkwepe ndipo wakagona uso kwa uso gari ndogo ikageuka ilikotoka, na canter ikaenda kugonga mti.

Hakuna aliyefariki eneo la tukio. Dereva wa gari ndogo ni mzima na ndiye aliyetoa maaelezo mengi katika habari hii, abiria wake wamejeruhiwa wanatoka damu na ni kama wameumia ndani kwa ndani.

Dereva wa canter ambaye hakua na abiria ameumia kichwani lakini alikuwa akiongea mwanzo mwisho huku akiwa chicha baya.

DSC08340.JPG DSC08340.JPG DSC08341.JPG DSC08342.JPG DSC08343.JPG DSC08344.JPG DSC08345.JPG DSC08347.JPG DSC08351.JPG
 
Ninawapa pole majeruhi na kuwatakia afya njema. Ni muhimu wakafanye uchunguzi wa kina juu ya maumivu ya ndani
 
I hope wote watakuwa salama.

Mkuu hongera sana kwa kutoa taarifa vizuri na kutuwekea picha inaweza kusaidia ndugu,jamaa na marafiki kutambua hizo gari.
 
Hivi huu udereva wa Bongo ni wa kivipi? Hizi DL wanazipataje watu kama hawa? Hawajali maisha. Yaani ni upumbavu mtupu.
 
kwa mtindo huu ajali zitateketeza wengi sana..yani bongo unaweza kutoka home asubuhi usijue kama utarudi nyumbani salama jioni kwa aina hii ya udereva..Agrrr!
 
Aiseee...pole kwa majeruhi!Afadhali hamna aliyepoteza maisha!
 
Hapo sasa kwa mujibu wa hotuba ya waziri sijui faini inaanzia Tsh 50000 au itakuwa laki 3? Kazi kweli!
Hapa sasa tatizo sijui serikali au wananchi, maana kila mtu anasehem yake. Unaendesha gari umelewa, unategemea nini? Pia kutokujali usalama wa watumia barabara wengine ni tatizo. Lakini kuna haja ya kuangalia mfumo wetu kuanzia utoaji wa leseni, vyombo vinavyosimamia usafiri na wasafiri na miundombinu. Maana hata faini inaweza isiwe suluhisho kwenye hili kama mamlaka zinapwaya.
 
kwa mtindo huu ajali zitateketeza wengi sana..yani bongo unaweza kutoka home asubuhi usijue kama utarudi nyumbani salama jioni kwa aina hii ya udereva..Agrrr!

Ingekuwa inawezekana ni bora kutembea kwa miguu tu..yaani ukipanda gari ni roho juu juu tu..
 
Barabara zetu zinatisha BJ! We acha tu!

tena ikichangiwa na madereva wabovu yani kama hii mtu njwii lakini kashika usukani kama siyo kujitakia kifo na kutaka kusababisha vifo vya wngine ni nini??!!..yaani huwa nahuzunika sana mana hizi ajali zinamaliza wengi na nyingi zingeweza kuzuilika!!
Huyo dereva wa cantel alitakiwa akamatwe, anyanganywe leseni na hata faini..sema dola yenyewe haipo serious kwenye hili suala, kuthibiti ni ngumu mno..
 
Ingekuwa inawezekana ni bora kutembea kwa miguu tu..yaani ukipanda gari ni roho juu juu tu..

Acha tu kaka mpendwa..yani mtu unakuwa na presha safari nzima..mana unaweza kuendesha kiuangalifu ukagongwa na gari lingine..kuendesha gari siyo kuendesha moja tu,aah!..
kutembea kwa miguu yenyewe inabidi uwe mwangalifu, hukawii kuchotwa hata kama uko mbalii na barabara..yani ni vurugu vurugu..!
 
Duuh! aisee madereva wa bongo sio ulevi nomaaaaa!!
DONT DRINK AND DRIVE
 
Imetokea maeneo ya Iramba,limegonga nyumba baada ya tair kupasuka na kuacha njia,hauna alokufa
sosi:radio one
 
Back
Top Bottom