Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Nimeona jina la legendary player Zamoyoni Mogella.. kwa vile jina hilo ni very distinct sijui kama ni yule yule au la kwani umri sidhani atakuwa na miaka 36...
 
Daladala lililohusika lilikuwa limefungiwa tangu 2007. Lilikuwa likifanya kazi usiku tu
__________________
Mkuu kana kwamb hilo alitoshi, TAA ZA ILE GARI ZA MBELE ZOTE ZIMEKUTWA HAZIFANYI KAZI
R.I.P DEREVA,ULICHOFANYA SIO UBINADAMU MMEFUNGIWA ,UNAIBA RTE USIKU TUU BASI HATA TAA JAMANI!!!!
HAYA KOMBE SIJUI ATASEMA NINI,,,AKA KAMDUDU RUSHWA AKA JAMANI
 
Kuna taarifa mbaya toka huko mbeya, kwa bahati lori limekata trailer ikarudi nyuma ikawaponda wanakijiji na mpaka sasa hivi kuna maiti 30, wanasema ni along tunduma -mbeya highway

mwenye taarifa azilete.

Rest in peace our dear citizen

mwikimbi
 
Kuna taarifa mbaya toka huko mbeya, kwa bahati mbaya lori limekata trailer ikarudi nyuma ikawaponda wanakijiji na mpaka sasa hivi kuna maiti 30, wanasema ni along tunduma -mbeya highway

mwenye taarifa azilete.

Rest in peace our dear citizen

mwikimbi
 
Jamani, not again! Mungu awaonee huruma, na kupumzisha roho za marehemu wote pema peponi; Amin
 
Ajali huwa ni bahati mbaya ila Tanzania zimezidi na zinamaliza watu kwakweli. Masikini hao watu mpaka inasikitisha. Wapumzike kwa amani!
 
da! yaani sijui kama tutafika maana kila kukicha jambo ni lile lile na wananchi wanazidi kumalizika jamani. Mungu awalaze mahala pema.
 
Mungu wangu! Imetokea sehemu gani? Mungu awasaidie walioumia na pole kwa familia za waliopoteza maisha na wale walioumia.
 
Labda kuna kalaana fulani hivi.!

Tatizo kubwa ni poor road infrastructure mkuu maana kama ni speed Tz bado speed zetu ni zakawaida. Hatuna hata 2X2 dual carriage way moja mkoani wala traffic litght mkoani, wala security lamp barabara za mikoani, shida tupu. Anyway Mungu azilaze pema roho za marehemu
 
Basi la Morning Star lenye nambari za usajili T674ADY limepata ajali ambapo watu saba wamekufa na wengine 20 kujeruhiwa. Basi hilo lilikuwa likitoka Dar kwenda Mloka na limepata ajali saa nane mchana. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani Absolam Mwakyoma amethibitisha.
 
Mara nyingi zinapotokea ajali. Jamii imekuwa na tendency ya kumlaumu dereva pekee kwa mwendo mkali. Hivi kati ya dereva, wamiliki wa mabasi na magari na abiria ni kundi lipi linapenda mwendo mkali kuliko jingine? Kwanini dereva akiendesha kwa mwendo wa Km 80/h kama inavyotakiwa na sheria wamiliki wa magari humwadhibu dereva kwa kumtimua kibarua na abiria huhama na kukimbilia ktk mabasi yanayokwenda kasi zaidi? Pengine our society needs to travel faster more than our laws and infrastracture can bear. Naomba mawazo yenu wana JF
 
Traffic police kwa kushindwa kusimamia sheria za barabara ambazo huvunjwa na madereva wengi sana, kushindwa kuhakikisha madereva wote wana leseni halali, kushindwa kuhakikisha magari ambayo hayastahili kuwa barabarani basi hayaingii barabarani wakati wowote. Mwaka 2006 pale mbuyuni karibu na Kanisa la St Peters kulikuwa na lori kama saa mbili au saa tatu usiku halikuwa na taa za mbele wala za nyuma lakini njemba ilikuwa inaendesha bila wasi wasi wowote. Nilikasirika sana kwa kweli maana wakati wowote lingeweza kusababisha ajali na mtu au watu kupoteza maisha yao kwa sababu ambazo zingeweza kabisa kuzuilika. Wanachojali Traffic police ni kuchangamkia rushwa na kuangalia pembeni juku sheria zikiwa ni machinjio makubwa ya Watanzania.
 
Mara nyingi zinapotokea ajali. Jamii imekuwa na tendency ya kumlaumu dereva pekee kwa mwendo mkali. Hivi kati ya dereva, wamiliki wa mabasi na magari na abiria ni kundi lipi linapenda mwendo mkali kuliko jingine? Kwanini dereva akiendesha kwa mwendo wa Km 80/h kama inavyotakiwa na sheria wamiliki wa magari humwadhibu dereva kwa kumtimua kibarua na abiria huhama na kukimbilia ktk mabasi yanayokwenda kasi zaidi? Pengine our society needs to travel faster more than our laws and infrastracture can bear. Naomba mawazo yenu wana JF

Makundi yote uliyoyataja hapo juu yanahusika kwa njia moja ama nyingine, pamoja na hao tunao waita Trafic.

Sheria ni sheria tu... imewekwa pale ili ISIFUNJWE. Kama suhala la jamii kutaka kusafiri kwa mwendo kasi, Basi watambue si kwenye chombo kinacho itwa BUS, or Motorcar. Kwani hata huko kwenye nchi zilizokwisha endelea sheria za barabarani na haswa kwa mabasi ya abiria ni 80 km kwa saa.

Hao Askari wa barabarani, wanapaswa kuwa makini na kuwacha tabia zao za kuomba rushwa. Wakiwa makini kwa kuwaadhibu waendesha mabasi ya abiria, bila kuingiza tamaa zao, basi ajali nyingi za barabarani zitapunua sana.
Tz ina safari ndefu sana ya kusafisha idara zake za serikali na haswa zile zinazo uhusiana moja kwa moja na raiya.
Sheria hipo pale na lazima ifuwatwe...!
 
Mara nyingi zinapotokea ajali. Jamii imekuwa na tendency ya kumlaumu dereva pekee kwa mwendo mkali. Hivi kati ya dereva, wamiliki wa mabasi na magari na abiria ni kundi lipi linapenda mwendo mkali kuliko jingine? Kwanini dereva akiendesha kwa mwendo wa Km 80/h kama inavyotakiwa na sheria wamiliki wa magari humwadhibu dereva kwa kumtimua kibarua na abiria huhama na kukimbilia ktk mabasi yanayokwenda kasi zaidi? Pengine our society needs to travel faster more than our laws and infrastracture can bear. Naomba mawazo yenu wana JF

dereva anatakiwa awaendeshe abiria na sio abiria kumwendesha dereva. Dereva aendeshe gari kulingana na hali ya barabara na pia kurekebisha makosa ya wengine-udereva wa kujihami.
 
opaque-albums-op-pics-picture477-trafic.jpg
 
Back
Top Bottom