Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Ni kweli sheria inataka mabasi ya abiria kutembea kwa maximum speed ya 80 Kms/h but the reality is yanatembea more than that na makundi yote ya jamii yanafurahia suala hilo. Mabasi kutoka nchi zingine za SADC yameandikwa maximum speed kati ya 100 na 120 Kms/h. Hivyo zipo nchi maximum speed kwa passengers buses ni kubwa kuliko sisi. Inawezekana sheria zetu zimepitwa na wakati sana kiasi cha jamii kuwa na urge of travelling faster than the law can provide.

Tazama wakati waheshimiwa wabunge na mawaziri wanapokwenda to and fro Dodoma magari yao yanatembe between 140 to 180 Kms/h hata katika sehemu zinazotakiwa kwenda 50 Kms/h.

Kama watunga sheria nao hawazingatii sheria tunatakiwa kufanya nini.Niliwahi kuzungumza na RTO wa mkoa mmoja akakiri kuwa akiendesha kwa 80Kms/h kwa muda mrefu atalala usingizi barabarni kwa kuwa it is too boring.

Je kuendelea kujidanganya kwa kumsukumia lawama zote dereva ndio suluhisho sahihi la tatizo hili ambalo chanzo chake ni sisi wenyewe?
 
Uzembe wa madereva (uendeshaje wao ni wa sifa na wengine hawana mafunzo yoyote ya uendeshaje), kila dereva anajifanya anajua kuendesha kuliko mwingine, barabara ndogo na mbovu. Pia magari yetu mengi haswa daladala, malori na mabasi kwa kweli hayastaili kuwa njiani. Wamiliki wanafikiria tu kukusanya pesa na hawajali kuyafanyia service mara kwa mara..yaani ukiangalia hali ya matairi (mfano) inasikitisha kuona watu wanaendesha malori au mabasi na matairi vipara!!
 
Habari zilizotufikia sasa hivi zinasema kuja ajali imetokea dodoma , ni basi lilitokuwa linatokea dare s salaam , mpaka sasa watu 6 wameripotiwa kufa eneo la ajali na majeruhi ni zaidi ya 15 tutaendelea kuhabarishana jinsi habari zinazozidi kuja
 
Du asante mkuu, tunasubiri info zaidi!!

Hizi ajali ama kweli zitatumaliza watz, inabidi tumwombe JK aweke njia nne nako kama ambavyo wanaweka chalinze mpaka tanga!!
 
Du asante mkuu, tunasubiri info zaidi!!

Hizi ajali ama kweli zitatumaliza watz, inabidi tumwombe JK aweke njia nne nako kama ambavyo wanaweka chalinze mpaka tanga!!

Hicho kijembe mkuu, mbona ajali ya Chenge na bajaji haikuwa kwenye highways!
 
so baad, why ajali zinafuatana kwa kipindi fulani then zinapotea?au kuna science hapo? ee mungu tuepushie hayo!!
 
Inasikitisha sana. Sitaki kutabiri chanzo cha ajali. Lakini MWENDO MKALI unachangia kwa zaid ya 90% ya ajali za barabarani.

Tunapokuwa na barabara nzuri, madereva wengi wanakuwa excited!
 
ajli nyingi chanzo chake ni uzembe wa aina mbalimbali, lakini ukiangalia hizi ajali za safari ndefu maranyingi ni sababu ya fatigue, hao madereva wanakuwa wamechoka sana na labda hata huwa awapatagi usingizi wa kutosha,
kwa hiyo hiyo solution yakuweka barabara nne inaqweza isisaidie sana kama mutaratibu mahususi wa uendeshaji usiposimamiwa vizuri
 
Hizi ajali zitaendelea kutokea kwasababu madereva wetu hawana discipline, sio wastaarabu barabarani hata kidogo. Wao kilamara aliyembele yake ni 'mjinga' na yeye ndio 'mjanja' wa barabara na mji. Angalia tui jinsi madereva wa taxi, daladala hata wengine wa magari binafsi wanavyoendesha mjini. Mie nadhani tunahitaji kufundisha watoto wetu subira na civility popote pale iwe barabarani, kwenye queue etc. Wao ndio madereva wa kesho wa magari, daladala hata basi.
 
Habari zilizotufikia sasa hivi zinasema kuja ajali imetokea dodoma , ni basi lilitokuwa linatokea dare s salaam , mpaka sasa watu 6 wameripotiwa kufa eneo la ajali na majeruhi ni zaidi ya 15 tutaendelea kuhabarishana jinsi habari zinazozidi kuja


Habari haijakamilika, Bus Gani? Eneo gani ajali imetokea? Mungu awaponye majeruhi na wafiwa poleni sana!
 
Ajali nyingi hapa nchini zinasababishwa na uzembe. Uzembe mwingi hutokea kwa driver kutaka ku-overtake bila kuwa makini. Ila pia sababu nyingine ni wembamba wa barabara zetu. Highway inakuwa nyembamba kuliko hata barabara za mjini (Dar), unategemea nini?
 
Habari haijakamilika, Bus Gani? Eneo gani ajali imetokea? Mungu awaponye majeruhi na wafiwa poleni sana!
Taarifa zinazoletwa na SHY zifanyieni uhakiki mara mbilimbili; huyu member mara nyingine ni controversial.
 
Jamani ajali inamaliza nguvu kazi ya nchi yetu,hatua zichukuliwe kuwadhibiti madereva wazembe.
 
Mh. Mudhihir ana matatizo ya kuwasilisha hisia zake kwa jamii, na wakati anapojaribu anakuwa mkali kama mbogo sijui mwajiri wake haoni umuhimu wa kumpeleka chuo cha chama kigamboni apate mafunzo zaidi ya utunzi wa mashairi na taarabu ?
 
alipata kweli ajali wala sio alikatwa mkono kwa kufumaniwa,idea ya kuukata mkono ilitolewa na madaktari wa MOI baaada ya kuona umeharibika kiasi amabacho usingeweza kutibiwa.na pia baada ya ajali alipelekwa hospitali ya nyangao iliyopo lindi,na alikuwa anaendesha yeye mwenyewe,sasa hayo ya kufumaniwa na kukatwa mkono sijui yantokea wapi wakati mkono haukukatika siki ya ajali
 
Kutoka kwa NEWTON MALLE:

YAH. AJALI ZINAKUWA WIMBO

Ndugu Mhariri

Naomba nipate nafasi ya kutoa maoni yangu machache kuhusu somo la hapo juu.

Ni muda mrefu sasa tunasikia jinsi ajali mbalimbali zinavyotokea kila siku na kuua watu wengi bila kuwepo na tahadhari au jitihada zozote za uokoaji. Pia ajali zingine ambazo hazihusishi vyombo vya usafiri kama vile ajali za migodini na juzi tu , ajali ya mlipuko wa mabomu kule mbagala.

Ni wazi kuwa nyingi ya ajali hizi zinaweza kuepukika kwa wahusika kuchukua tahadhari au kuwa makini na kazi zao na zaidi mamlaka zinazohusika kusimamia kwa makini masharti yanayoambatana na shughuli hizi.

Ni mara nyingi utaona mamlaka zinazohusika hukaa kimya na kufumbia macho swala la vyombo vya usafiri aidha kwa kutokujua majukumu yao au kwa uzembe huku kukiwa na upungufu mkubwa unaohatarisha usalama wa abiria na mali.

Mara itokeapo ajali ndipo wanakurupuka kama wametoka usingizini na kujifanya kuuliza maswali mengi ambayo ni wao wenyewe wanapaswa kuyajibu kimsingi. Na pia mikakati mingi hupangwa ili kuzuia ajali zisitokee tena lakini mikakati hii hubakia kwenye maandishi bila kutekelezwa au hutekelezwa kwa mida mfupi na kuachwa. Pamaoja na kwamba maswali yaulizwayo ni maswali ya msingi, lakini yanaulizwa wakati msiba mkubwa tayari umeshatokea na kuua watu wengi.

Ni hivi majuzi baada ya ajali kubwa iliyotokea Singida na kuua watu wengi yalijitokeza mambo mengi ambayo baadhi yake yalinishitua kwa sababu mie binafsi sikuwa nayafahamu na nahisi watanzania wenzangu pia walikuwa hawayafahamu. Kulikuwa na swala la milango ya dharura, uchakavu wa magurudumu, kujaza abiria kupita uwezo wa chombo na kubeba mizigo mingi na hatarishi ndani ya mabasi, jambo ambalo wengi tunalifahamu. Lakini cha ajabu ni kwamba kuna mkubwa mmoja wa mamlaka zinazohusika na vyombo vya usafiri alikurupuka na kusema kupitia vyombo vya habari bila hat woga kuwa mengi ya mabasi ya abiria yameundwa kwa kutumia “ CHASIS ZA MALORI”. Na akatoa miezi sita yarekebishwe.

Kwa kweli jambo hili lilinihudhunisha sana kwa sababu kumbe mheshimiwa huyu alikuwa analijua tatizo hilo, lakini bado akawa anaruhusu mabasi hayo yapewe leseni za kusafirishia abiria?

Ni kwa nini hakuweza kuchukua hatua mapema ili kuzuia ajali kama swala hilo ni tatizo?

Ajabu nyingine ni kwamba mheshimiwa huyu alitoa amri kuwa mabasi yote yakaguliwe na yale yatayokutwa na chesis za malori yarekebishwe ndani ya miezi sita.

Namuuliza huyu mheshimiwa, je ni mabasi mangapi ambayo ameshayagundua na kurekebishwa hadi leo?

Je ni mabasi mangapi yametimiza masharti ya kuweka milango ya dharura au vizima moto?

Sheria zote zinazotawala vyombo vya usafiri na usafirishaji nchi kavu na baharini zimewekwa bayana lakini bado utashangaa kuona kuwa gari inakaguliwa na kupewa kibali cha kufanya kazi huku likiwa halijatimiza masharti yote.

Mfano mzuri kachunguze magari ya abiria ya Dar es salaam yajulikanayo kama daladala ndipo utaelewa nasema nini. Magari mengine hayana viti au viti vimechakaa hadi vyuma vimejitokeza nje, mengine hayana vioo, mvua zinanyesha ndani ya basi, magurudumu ni cahakavu, lakini yako barabarani.

Juzi ilitokea ajali ya meli huko bandarini Zanzibar na kuua watu kadhaa. Lakini pia pamoja na wenye meli kutokuwa na vifaa vya kujiokoa lakini pia walishindwa kutaja idadi ya abiria waliokuwepo kwenye meli hiyo. Ilishangaza kuwa pale bandarini hakukuwa na vifaa wala timu yoyote ya uokoaji na hakuna jitihada za kitaifa zilizochukuliwa kujaribu kuokoa maafa hayo tangu ilipozama saa nne usiku hadi ilipofika saa tisa za usiku. J e, meli hiyo ingezama katikati ya bahari hali ingekuwaje?

Ni ajali zaidi ya moja ambazo tayari zimeukumba mgodi wa miererani na kuua wachimbaji wengi. Mara ya kwanza yaliongelewa mengi san yakihusu mikakati ambayo inabidi ichukuliwe ili kuepusha ajali ingine kama hiyo. Lakini cha ajabu hakuna kilichofanyika na ajali iliyofuata ikaua wachimbaji kadhaa. Na zaidi ya hapo viongozi na wenye migodi waliendelea kuongea maneno mengi ya kuzuia ajali. Nauliza je, kwa nini wanapoona mvua zinaanza wasitoe taarifa kwa wachimbaji walioko chini ya ardhi ili watoke? Pili ni kwa nini baada ya ajali ya kwanza wasichukue hatua za kuweka matuta au mifereji itakayolengesha maji maeneo mengine ambako hakuna mashimo ya migodi?

Mie sijawahi kufika huko miererani lakini hizi ni hatua za awali na chache sana ambazo zinaweza kuokoa ndugu zetu.

Je, kweli tuna uchungu na ndugu zetu waliopata na kufa au kuumia kwenye ajali hizi?

Baada ya muda kama siku moja hivi alijitokeza mheshimiwa kama kawaida akasema kuwa meli hiyo ilikuwa mbovu tangu siku za nyuma. Je, ni kwa nini iliruhusiwa kufanya safari na huku ikijulikana kuwa ni mbovu? Na pia ndipo ilipotangazwa kuwa meli zingine zote zisimamishe safari zikaguliwe.

Je, KUMBE HUWA HAZIKAGULIWI?

Ndugu Mtangazaji nafikiri utaona jinsi mambo yanavyofanywa kiholela utafikiri wanafanya mchezo wa kuigiza. Mie nafikiri na ni kwamba inatia hasira sana hadi utake kumpiga mtu. Ndio maana yule mkuu wa Wilaya alichukua hatua ya kuwatia bakora wale waalimu kule bukoba. Aliudhika na ndio maana akaamua kama anawaadhibu watoto. Alitenda sawa kabisa.

Jambo lingine ambalo ni la hatari ni kwamba mabasi yaendayo mikoani kutokea miji mingine mikuu hupakia mizigo ndani ya mabasi ambayo kwa kisheria hairuhusiwi kwenye mabasi ya abiria kama mabati, nondo, saruji, mbao na maboksi ya vitu vingine, ikiwa ni pamoja na kuzidisha abiria kupita kiasi.

Pindi polisi wa usalama barabarani wanapolikamata basi hupewa chochote kwa wale waroho wa pesa au hutozwa faini na mabasi huruhusiwa kuendelea na safari hivyohivyo.

Hii ina maana kuwa pato la serikali linalopatikana toka vyombo vya usafiri ni pato haramu kwa sababu kuwacha basi liendelee na safari wakati gurudumu limechoka, au kujaza abiria kupita uwezo au kupakia mizigo ya hatari ndani ya basi ni sawa na kusema kuwa wanaruhusu ajali ziendelee na serikali ipate mapato yatokanayo na ajali hizo. Na Serikali inaweka bageti kutokana na mapato hayo haramu.

Ni wakati sasa umefika kwa wahusika kuona umuhimu wa kusimamia vyema vyombo hivi ili kuepukana kabisa na ajali za kila siku. Tujaribu kwenda na wakati badala ya kukaa kama watu wasiojua huku tukisubiri kuzika watu wetu.

  1. Kusimamia matengenezo ya mabasi na kufanya ukaguzi wa kina kabla hayajapewa kibali cha kazi.
  2. Kuweka milango ya dharura (hakuna hata basi moja lenye milango ya dharura isipokuwa yale ya Scania super andar)
    • Kuweka vizima moto upande wa nyuma nje ya gari.
    • Kuweka sehemu ya kujishika abiria,
  3. Mabasi yasiruhusiwe kupakia ndani yake vifaa vya ujenzi na mizigo mingine.
  4. Endapo gari itakutanika na kosa la kupakia mizigo, mwenye basi atozwe faini na mizigo ishushwe hapohapo.
  5. Endapo basi litapakia abiria zaidi, mwenye basi atozwe faini na abiria aliyesimama ashushwe hapo hapo na arudishiwe nauli yake.
  6. Iwapo magurudumu yameisha, mwenye basi atozwe faini, gari lisimamishwe safari hapohapo hadi atakapoletewa gurudumu jipya.
  7. Kudhibiti mwendo wa mabasi.
  8. Najua sasa bajeti ya serikali itakuwa na upungufu wa mapato ndio maana nashauri hayo makosa hapo juu yaende sambamba na faini.
  9. Wakuu wa mamlaka husika wachukuliwe hatua kwa kushindwa kuwa wabunifu na kusimamia kikamilifu masawla ambayo yako kwenye himaya yao.
Ni matumaini yangu kuwa mamlaka zizohusika kama SUMATRA na POLISI wa usalama barabarani pamoja na wizara zinazohusika watalitilia mkazo jambo hili. Nina hakika kuwa haya ni machache sana. Kuna mengi mengine ambayo yanatakiwa yfanyiwe marekebisho.

Wenu katika ujenzi wa Taifa.

Mwananchi.

NEWTON MALLE
0784 3333 22
Mwanza.

 
Back
Top Bottom