Mlipuko watokea Darajani Zanzibar. Mmoja auawa

Mlipuko watokea Darajani Zanzibar. Mmoja auawa

Status
Not open for further replies.
Taarifa zilizopo ni kuwa Bomu limelipuliwa (hand thrown Grenade) baada ya mhadhara wa ndani ya msikiti huko Unguja na Ndg yetu kijana Muhammad mkombolaguha amefariki dunia, sheikh Abulfadh'li Qassim mlengwa wa shambulio amejeruhiwa mkono na mguu na yu wapata matibabu hospitalini na hali yake sio mbaya sana.

Aliyefariki ni mwanafunzi wa sheikh ktk Markaz iliyopo Tanga, Abulfadh'li ni miongoni mwa masheikh wanaowindwa sana na wanaharakati, mashia na makhawarij wanaopinga msimamo wake ulio sahihi wa kukataza maandamano, kupinga jihad bila ya shurutwi za kisheria, kupinga kukufurisha watu bila ya sababu za kisharia, kutukana na kulaani viongozi waliokabidhiwa mamlaka. Ni sheikh pekee na wa aina yake hapa Tz alie na low profile lakini akigusa mioyo na kubadilisha misimamo mingi ya kijazba na iliyokosa usuluub na ilm ya kisheria.

Allaah amponye sheikh na ampokee Marehemu wetu ktk pepo yake tukufu firdaous. Inna lillaah wainna ilaih rajioun.

Hayo ndio machache yaliyotufikia kutoka Znz kupitia mitandao ya kijamii
Duuh! Nimeshaelewa, kumbe na wao kwa wao?:israel:
 
hivi ikitokea muungano ukavunjika, usalama wa kidini baina ya waislamu na wakristo utakuwaje?

najua tu kwa hypothesis, hili tukio litahisiwa kuhusiana na mauaji ya viongozi wa kikristo na uchomaji wa makanisa.

mkuu ni kweli usemayo lakini laiti wangejaaliwa kumsikia kassim mafuta wale wenye jazba na vurgu za kidini labda wangetulia kwa kuwa ni mmoja wa masheikh wachache hapa Afrika mashariki wanaouelezea uislam katika sura yake halisi, kinyume na wengi wanaohamasisha watu kufanya machafuko.
mwenyeezi mungu amnusuru yeye pamoja na wote waliosimama katika haki inshaallah.
 
nimsika kwa mbaali magazeti ya leo.
_kama ilivyo ada wahusika hawajulikani
 
hizi taarifa zakweli?

Webo, ni vema ukajiridhisha kwa kupata taarifa yeye uhakika kwanza kabla ya kuanzisha thread mkuu...wanasema kama hujafanya utafiti, huna haki ya kuzungumza! Pls elewa humu ndani wengi wetu tunapategemea sana kwa kupata taarifa za kina ambazo hazijawa manipulated!!!
 
Sometimes huwa nafikiria labda ni utoto but nadhani Watanzania tuna tatizo. Issues zinazohusu maisha na uhai wa Wananchi zikifika hapa jukwaani watu wanajadili kishabiki, matusi, kulaumu watu na mamlaka hata kama hazihusiki... there is a problem somewhere.
Mi nadhani kama ni minyukano ya kisiasa au kidini zipo topics muafaka nyingi tu za kufanya hivyo.
Tuwe wepesi kuwapuuza watu wanaotaka kupotosha mada za kijamii kama hizi kwa kutojibizana nao. But only matured can pick this

UsiwTetee machogo wacha wamalizane.
 
Jamani mnaumia kichwa burena DrWHO.

Huyu DrWHO anaishi UK kama mkimbizi ama mla mapesa yetu .Kama anabisha aseme halafu mimi nitatoa nyeti zaidi akiendelea kukataa .Je hukai UK wewe ? Ndiyo maana hana uchungu na lolote .

Kutumia masaburi?
 
Nakumbuka Mashekhe walizunguka Tanzania nzima kuhamasisha jihadi. Sasa mbona Jihad imewageukia? naona vijana wamekolea sasa maana juzi wameua shekhe pale Mombasa. Hizo ndio faida za kufundisha vijana chuki, lakini poleni
 
Kilichofanya huyu Shekhe akoswe kuuawa ni kuhubiri maneno haya

[SUP]43 [/SUP]“Mmesikia kuwa watu zamani walikuwa wakisema, ‘Umpende jirani yako na umchukie adui yako.’ [SUP]44 [/SUP]Lakini mimi ninawaambia, wapendeni maadui zenu na waombeeni wanaowatesa, [SUP]45 [/SUP]ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake watu waovu na watu wema; na pia huleta mvua kwa wenye haki na wasio haki. [SUP]46 [/SUP]Kama mkiwapenda wanaowapenda tu, mtapata thawabu gani? Hata wenye dhambi hufanyiana hivyo. [SUP]47 [/SUP]Na kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, mnafanya nini zaidi ya wengine? Hata watu wa mataifa wasiomjua Mungu, hufanya hivyo. [SUP]48 [/SUP]Kwa hiyo inawapasa ninyi muwe wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.”
 
Kikubwa ni ukosefu wa elimu na umasikini. Katika mazingira kama hayo ni rahisi vijana bila kujali dini wala itikadi kurubuniwa na watu wenye maslahi yao ya kihalifu
 
Zenji 99% wafuasi wa S.A.W. Na hiyo ilisemwa na mtoto wa mkulima bungeni. Sasa na wao pia Ismail ndugu yao na bible ilisema mikono yake itakuwa juu ya wenzake. Wacha wauane wamezidi ubaguzi. Lakini jihad inaruhusu.

Mkuu, Sheikh aliye uwawa ni Mtanganyika, viongozi wa dini wanaohubiri utengamano hasa kwa kipindi hiki tunachoshuhudia mpasuko wa kidini. Viongozi wa aina hii yafaa wapewe ulinzi.
 
Mi niko Unguja hizo taarifa ni kweli na ilitokea jana kama saa mbili hivi. Hadi sasa imeshathibitika amefariki mtu mmoja na kuna majeruhi zaidi ya watatu
 
Wanataka kuitia kwenye makosa zanzibar tu, kwa nini wakafanye haya matukio zanzibar wasimfanyie huko kwao
 
Webo, ni vema ukajiridhisha kwa kupata taarifa yeye uhakika kwanza kabla ya kuanzisha thread mkuu...wanasema kama hujafanya utafiti, huna haki ya kuzungumza! Pls elewa humu ndani wengi wetu tunapategemea sana kwa kupata taarifa za kina ambazo hazijawa manipulated!!!
Habari ni ya kweli ila ni jana na humu kuna uzi unaoongelea hilo,
 
Mola wetu iepushe jamii nzima ya waja wako na majanga haya yanayotafuta kuivuruga amani na utulivu. Wajalie wanaokuamini wasidhulumike haslani. Amen! Jamani nyie mnaokatisha maisha ya wenzenu acheni woga, jitokoze mzungumze ili kuweka sawa pale mnapodhani panakwenda visivyo . Kumbukeni Mola anawaona!


(QUOTE=Zanzibar Spices;9801120]Habari zilizopo ni kwamba, mabomu yametupwa na watu wasiojulikana eneo la Darajani, Zanzibar na kuua mtu mmoja mpaka sasa na wengine 4 ni majeruhi.

Habari za awali ni kwamba waliotupiwa mabomu hayo ni baadhi ya viongozi wa dini ambao walikuwa wametoka msikitini kutoa mawaidha na wakati wanatoka na kuingia kwenye gari lao ndipo mtu asiyejulikana alitupa bomu hilo (inasemekana ni zaidi ya moja).

Habari kamili nikipata zaidi nitawajuza.

========
More:[/QUOTE]
 
Mola wetu iepushe jamii nzima ya waja wako na majanga haya yanayotafuta kuivuruga amani na utulivu. Wajalie wanaokuamini wasidhulumike haslani. Amen! Jamani nyie mnaokatisha maisha ya wenzenu acheni woga, jitokoze mzungumze ili kuweka sawa pale mnapodhani panakwenda visivyo . Kumbukeni Mola anawaona! (QUOTE=Zanzibar Spices;9801120]Habari zilizopo ni kwamba, mabomu yametupwa na watu wasiojulikana eneo la Darajani, Zanzibar na kuua mtu mmoja mpaka sasa na wengine 4 ni majeruhi.

Habari za awali ni kwamba waliotupiwa mabomu hayo ni baadhi ya viongozi wa dini ambao walikuwa wametoka msikitini kutoa mawaidha na wakati wanatoka na kuingia kwenye gari lao ndipo mtu asiyejulikana alitupa bomu hilo (inasemekana ni zaidi ya moja).

Habari kamili nikipata zaidi nitawajuza.

========
More:[/QUOTE]
 
What goes around comes around!!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom