Mlipuko watokea Darajani Zanzibar. Mmoja auawa

Mlipuko watokea Darajani Zanzibar. Mmoja auawa

Status
Not open for further replies.

Governor of Bettors-GB

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2013
Posts
10,878
Reaction score
10,099
Habari zilizopo ni kwamba, mabomu yametupwa na watu wasiojulikana eneo la Darajani, Zanzibar na kuua mtu mmoja mpaka sasa na wengine 4 ni majeruhi.

Habari za awali ni kwamba waliotupiwa mabomu hayo ni baadhi ya viongozi wa dini ambao walikuwa wametoka msikitini kutoa mawaidha na wakati wanatoka na kuingia kwenye gari lao ndipo mtu asiyejulikana alitupa bomu hilo (inasemekana ni zaidi ya moja).

Habari kamili nikipata zaidi nitawajuza.

========
More:
Taarifa zilizopo ni kuwa Bomu limelipuliwa (hand thrown Grenade) baada ya mhadhara wa ndani ya msikiti huko Unguja na Ndg yetu kijana Muhammad mkombolaguha amefariki dunia, sheikh Abulfadh'li Qassim mlengwa wa shambulio amejeruhiwa mkono na mguu na yu wapata matibabu hospitalini na hali yake sio mbaya sana.

Aliyefariki ni mwanafunzi wa sheikh ktk Markaz iliyopo Tanga, Abulfadh'li ni miongoni mwa masheikh wanaowindwa sana na wanaharakati, mashia na makhawarij wanaopinga msimamo wake ulio sahihi wa kukataza maandamano, kupinga jihad bila ya shurutwi za kisheria, kupinga kukufurisha watu bila ya sababu za kisharia, kutukana na kulaani viongozi waliokabidhiwa mamlaka. Ni sheikh pekee na wa aina yake hapa Tz alie na low profile lakini akigusa mioyo na kubadilisha misimamo mingi ya kijazba na iliyokosa usuluub na ilm ya kisheria.

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Kuna tetesi ya ndege kuanguka airport Zanzibar, taarifa kamili tafadhali. Poleni sana
 
hivi ikitokea muungano ukavunjika, usalama wa kidini baina ya waislamu na wakristo utakuwaje?

najua tu kwa hypothesis, hili tukio litahisiwa kuhusiana na mauaji ya viongozi wa kikristo na uchomaji wa makanisa.
 
Mkuu ni kweli hicho kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu kimetupwa na watu waliokuwa kwenye gari ambayo haikuwa na namba za usajili?
 
Nafikir polis wmeshindwa kuthubit masuala haya ya mabomu.

Wanasuburi hadi taarifa za kiinterejisia zipatikane ndo wachukue hatua wkt huo wanachi tumeshalipuliwa na kufa.
 
Hii taarifa ni ya kweli na sheikh aliyerushiwa bomu anaitwa Sheikh qasim mafuta kutoka Pongwe Tanga na kijana aliye fariki anaitwa Abutwalha,lakini Sheikh qasim anaendelea na matibabu.
 
Last edited by a moderator:
Taarifa zilizopo ni kuwa Bomu limelipuliwa (hand thrown Grenade) baada ya mhadhara wa ndani ya msikiti huko Unguja na Ndg yetu kijana Muhammad mkombolaguha amefariki dunia, sheikh Abulfadh'li Qassim mlengwa wa shambulio amejeruhiwa mkono na mguu na yu wapata matibabu hospitalini na hali yake sio mbaya sana.

Aliyefariki ni mwanafunzi wa sheikh ktk Markaz iliyopo Tanga, Abulfadh'li ni miongoni mwa masheikh wanaowindwa sana na wanaharakati, mashia na makhawarij wanaopinga msimamo wake ulio sahihi wa kukataza maandamano, kupinga jihad bila ya shurutwi za kisheria, kupinga kukufurisha watu bila ya sababu za kisharia, kutukana na kulaani viongozi waliokabidhiwa mamlaka. Ni sheikh pekee na wa aina yake hapa Tz alie na low profile lakini akigusa mioyo na kubadilisha misimamo mingi ya kijazba na iliyokosa usuluub na ilm ya kisheria.

Allaah amponye sheikh na ampokee Marehemu wetu ktk pepo yake tukufu firdaous. Inna lillaah wainna ilaih rajioun.

Hayo ndio machache yaliyotufikia kutoka Znz kupitia mitandao ya kijamii
 
Habari zolizotufikia hivi ni kwamba mtu asiyejuilikana amerusha bomu na kumuuwa muhadhir mmoja kutoka Tanga ambae yupo Zanzibar kwa ajili ya Jitimai.Kwa mujibu wa Kamanda wa mkoa waMjini Magharibi wahadhiri hao walikua wanatoka msikitini Darajani katika sala ya Isha wakati wanaelekea katika magari yao ndio yakaawakuta maswahibu hayo.Wahadhiri wengine saba wamejeruhiwa wapo hospital ya Alrahma kwa matibabu.
 
Muungano bado upo, sarakasi; ukivunjika itakuwaje? Na bado. Waumini wa muungano tunasema utadumu tu ili kuwalinda ndugu zetu wazanzibari wasio na hatia. Kina jusa ni wa kupuuzwa.
Walofanya ni wenye grenade ambao zipo chini ya muungano sio jussa sio uamsho
Ni wauaji walosema jeshi litachukua nchi
Haya ni mambo ya lukuvi na genge lake ambao alisema kanisani kuwa watafanya liwalo na liwe lakini znz hatuitoi
 
Kwa kweli ni tukio la kusikitisha sana!

Kwa muda wa miezi kadhaa kule Mombasa zimekuwepo taarifa za uwongo,upotoshaji na ufitini zikidai kuwa Sheikh Qaism Mafuta anapokea hela kutoka kwa Mayahudi.

Weledi waligundua kuwa hii ilikuwa ni njia ya kutaka "kuihalalisha" damu yake! na kweli ndiyo kile kile kinachotokea sasa.

Mombasa tayari wameshamkata kata mapanga Sheikh Bahero na kwa Tanzania ndiyo haya tunayoyaona sasa.

...ila bado siamini kama ni Waislamu wanaofanya haya.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom