PakaJimmy
JF-Expert Member
- Apr 29, 2009
- 16,202
- 8,781
Kitu kama bomu kimelipuka Hapa Arusha maeneo ya MTK Bar Mianzini na kusababisha mshindo mkubwa sana.
Taarifa zinasema baadhi ya watu wameumia.
========
UPDATES:
- Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha amethibitisha kutokea kwa mlipuko wa bomu Arusha Night Park, hakuna vifo, idadi ya majeruhi haijajulikana bado.
Eneo ambalo mlipuko huo ulitokea.
Taarifa zinasema baadhi ya watu wameumia.
========
UPDATES:
- Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha amethibitisha kutokea kwa mlipuko wa bomu Arusha Night Park, hakuna vifo, idadi ya majeruhi haijajulikana bado.
Mlipuko mkubwa umetokea leo majira ya saa 1.30 usiku katika baa maarufu ya Arusha night park "Matak0 bar" iliyopo eneo la Mianzini mjini Arusha.
Taarifa za awali zinaeleza kuwa mlipuko huo unatokana na bomu lililotengwa katika eneo la bar hiyo na kujeruhi watu zaidi ya 20 waliokuwa wakiangalia mchezo wampira wa miguu ligi kuu ya England kati ya Chelsea na Swansea.
Majeruhi wamekimbizwa katika hospitali ya dk. Mohamed na Mount Meru. Mashuhuda wanaeleza kuwa kuna baadhi ya majeruhi wamekatika viungo kama miguu nakadhalika.
Hili ni tukio la tatu mjini arusha bomu kurushwa na kutegwa katika maeneo ya mikusanyiko ya watu na hadi sasa Polisi hawajawahi kukamata wahusika wa matukio yote matatu.
Eneo ambalo mlipuko huo ulitokea.