Mkuu wa nchi lazima awe mkali na aogopwe. Asipoogopwa kila kitu kitakwenda mrama. Hata hayati Julius Nyerere aliogopwa na alikuwa mkali

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,086
6,568
Mkuu wa nchi ambae ndio ndio custodian wa mali za taifa la watanzania kudai kuwa hawezi kufokea mtumishi wa umma ni kushangaza umma wa watanzania.

Kwamba watumishi wa umma wakiharibu atawabembeleza?

Nimekaa na wazee wengi waliofanya kazi na hayati Julius Nyerere wanasema wazi kuwa Mwalimu alikuwa mkali sana.

Ilitokea akikuita kwake Msasani au Ikulu ilikuwa lazima upate wasiwasi na woga mkuu.

Wengine aliwaita kuwapongeza lakini hawakuamini walichoitiwa wapo pia aliowafokea hadharani au hata kifichoni.

Kwamba mkuu wa nchi unafanya kazi kwa kuonea aibu wateule wako? Kwamba utakuwa unawabembeleza?

Mbona hii sio sawa? Mkuu wa kaya lazima uwe mkali ili nidhamu ipatikane kuanzia juu mpaka chini.

Hatusemi ufokee watu kama watoto wako. Bali uwe na maamuzi na maelekezo yenye kuonyesha kuwa kuna kiongozi mwenye mamlaka aisiyetaka mzaha na anataka watu wafanye kazi.

Mfano, tulitegemea umkaripie January Makamba maana mradi wa JNHP unaweweseka kama vile hauna manufaa kwa wanaCcM wenzake.
 
Mkuu wa nchi amabae ndio ndio custodian wa mali za taifa la watanzania kudai kuwa hawezi kufokea mtumishi wa umma ni kushangaza umma wa watanzania. Kwamba watumishi wa umma wakiharibu atawabembeleza...
Bi tozo yeye anasema hana hulka ya kufokafoka kwa sababu ana watu wanaoamua kwa niaba yake.

tofauti na hayati JPM, yeye alijua wazi ukiwaacha baadhi ya watu wafanye wapendavyo nchi ingeenda mlama.

Kama ilivyo hivi sasa, mfumuko wa bei, hakuna anayeudhibiti!

Watu wanafanya wanavyoona inafaa.
 
Upo sahihi sana. mimi nampenda sana mama samia ktk utendaji wake ila la hili la nidhamu ya moyoni kwa watumishi wa umma mama aliangalie vizuri.

Kuchelewa kazini, kutokatoka hovyo kuzurula, kwenda kucheza kamali wakati wa kazi na vijiwe vya mpira vinashusha sana nidhamu ya kazi ktk secta zote.

Utakuta 80% ya watumishi wa umma wanastahili kufukuzwa kazi kila siku kwa utovu wa nidhamu.

utakuta wizara zote za serikali zina cheo kiitwacho ofisi supevisor maajabu yake ofisi supevisor hafuatilii watoro kazini, wacheza kamali, wafanyao ngono maofisini wala kuwabana wachelewaji.

Hwa maO.S, utakuta siku zote ni father X-mass tuu na hupenda kununua stationary tuu!matokeo yake katika wizara zote za serikali huwezi kumtuka mfanyakazi aitwae workaholic(yaani yule aketie kitini na kujituma kazini mpaka anaambiwa nenda nyumbani kinguvu}

mimi binafsi namuomba sana mama awe mkali sana na avae ndita muda wote maana tupo katika kipindi cha heated economy la sivyo wajanja watamuangusha kisawasawa..
 
Mkuu wa nchi amabae ndio ndio custodian wa mali za taifa la watanzania kudai kuwa hawezi kufokea mtumishi wa umma ni kushangaza umma wa watanzania. Kwamba watumishi wa umma wakiharibu atawabembeleza...
Amerika Waamerika hawamuogopi President wanamuheshimu vivyo hivyo nchi lukuki duniani watu wao President ni mwananchi mwenzao tu wanampa ile heshima tu ya kiongozi. Huku Afrika kuna raia kama wewe mleta sledi mnatutaka tuishi kama tupo kwenye zama za Anno Donimo (AD) enzi za akina Kayafa, Herode, Pilato, Koreshi huko Guba ya Uajemi, maFirauni aka maFarao wa Sinai nk
 
Hakuna Mtanzania anayependa kufanya kazi bila kusukumwa. Ndio maana sasa hivi ubora wa huduma za umma umeshuka sana. Tunapewa majibu ya hovyo na hatuna cha kuwafanya.
Binadamu wote tumeumbwa kupenda shortcuts. Hiyo ni kwa binadamu wote duniani, siyo kwa watanzania tu.

Ndiyo maana tukaletewa kitu kinaitwa sheria kutuzuia kufuata shortcut na magereza kwa ajili ya kutuadabisha tunapotaka kufuata shortcuts.

Ukimwambia mtu achague kati ya kufanya kazi ili apate hela au kukaa tu ila hela itakuja yenyewe, atachagua kukaa.
 
Binadamu wote tumeumbwa kupenda shortcuts. Hiyo ni kwa binadamu wote duniani, siyo kwa watanzania tu. Ndiyo maana tukaletewa kitu kinaitwa sheria kutuzuia kufuata shortcut na magereza kwa ajili ya kutuadabisha tunapotaka kufuata shortcuts. Ukimwambia mtu achague kati ya kufanya kazi ili apate hela au kukaa tu ila hela itakuja yenyewe, atachagua kukaa.
Na hii ndio sababu tunahitaji kusimamiwa kama alivyokuwa anafanya Magufuli.
 
Na hii ndio sababu tunahitaji kusimamiwa kama alivyokuwa anafanya Magufuli.
Kuongoza maana yake ni kusimamia; hakuna uongozi bila usiamamizi.

Ndiyo maana nilishangaa sana kauli iliyotolewa na rais kwamba watu walikuwa na nidhamu ya woga kwa sababu ya kusimamiwa.

Who cares iwapo nidhamu hiyo ni ya woga au ni ya halali ilimradi shughuli za serikali zinakwenda inavyotakiwa?
 
Back
Top Bottom