Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,274
- 9,717
Ndugu zangu Watanzania,
Baada ya hapo jana Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hasssan kipenzi cha watanzania mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge kuongoza watanzania katika mazishi ya waziri Mkuu mstaafu hayati Edward lowassa,hii leo anafanya kazi nyingine tena ya kimataifa kuwaongoza makumi ya viongozi mbalimbali kutoka barani Afrika katika uzinduzi wa Sanamu ya Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius kambarage Nyerere Addis Ababa Ethiopia.
Sanamu hiyo inakuja kama sehemu ya kutambua mchango mkubwa sana wa Mwalimu Nyerere na Tanzania katika ukombozi wa bara la Afrika.huwezi ukaiandika vyema historia ya bara la Afrika pasipo kuitaja kwa uzito na kuizungumzia kwa heshima kubwa nchi ya Tanzania. Ni Tanzania ndio iliyoongoza ukombozi wa nchi nyingi sana barani Afrika kutoka katika makucha ya wakoloni hususani nchi za kusini mwa Afrika. lakini pia Tanzania imewahi kutoa katibu mkuu wa OAU iliyokuwepo awali kabla ya hii ya sasa.
huyu si mwingine bali ni Salimu Ahmed Salim kuanzia mwaka 1989-2001,ambaye kama siyo kura ya VETO ya marekani alikuwa anakwenda kuwa mtanzania wa kwanza kuwa katibu mkuu wa umoja wa Mataifa yaani UN.kwa kuwa alikuwa amekidhi kila kitu na kila sifa na uwezo wa kutosha, lakini kutokana na itikadi na siasa za ujamaa na ubepari ambazo zilikuwa zimeota mizizi na kutawala kwa wakati huo ikawapa hofu Marekani walioamua kumpiga vita asitwae kiti hicho.
Kwa hiyo leo Rais wetu mchapa kazi ametua huko kwa kishindo na kwa kujivunia historia ya kutukuka na mchango wa kipekee wa baba yetu wa Taifa na Taifa letu kwa ujumla .lakini pia ikumbukwe ya kuwa hata lugha yetu ya Taifa yaani kiswahili ni miongoni mwa lugha zinazotambulika katika umoja huo, lugha ambayo baba wa Taifa aliitumia kwa nguvu zake zote kuliunganisha Pamoja Taifa letu na kujenga umoja wa kitaifa.
Rai yangu ni kuwa tumuenzi baba wa Taifa kwa kufanya yale mazuri yote aliyokuwa anayahubiri,tupinge vita rushwa,wizi,ufisadi,ubaguzi na unyonyaji wa aina yoyote ile. Ni lazima viongozi wetu wamuenzi kwa kudumisha uadilifu na uzalendo na siyo kuogopa kimvuli chake na sauti yake kwa yale aliyokuwa akiyakemea. Ni lazima viongozi wetu wawajali ,kuwapigania ,kuwatetea na kuwasemea watanzania wanyonge wasio na Sauti.ni lazima kila mmoja ajiulize ataifanyia nini Tanzania na siyo Tanzania itamfanyia nini yeye binafsi.
Ni lazima kila kiongozi ajuwe cheo ni dhamana.na kwamba mali ,pesa na vyeo vyote ni vya kupita tu. Ni lazima viongozi wetu wajuwe ni bora jina zuri kuliko mali na utajiri wote wa Dunia.na kwamba kitakachokumbukwa kutoka kwao na kukufanya uendelee kuishi hapa Duniani hata kama umetangulia mbele za haki ni matendo yako mema kwa watu,utu wako,kugusa kwako maisha ya watu,kutenda kwako haki kwa watu wote pamoja na mengine mengi kama haya.ukitenda mabaya ukiwa madarakani basi tambua yakuwa utakufa siku hiyo hiyo utakayotoka madarakani hata kama utakuwa bado upo hai maana watu watakusahau kabisa katika mawazo na akili zao kama umewahi kuwa kiongozi wao, kwa kuwa hukugusa maisha yao kwa namna yoyote ile ukiwa kiongozi.
Baada ya hapo jana Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hasssan kipenzi cha watanzania mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita, nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge kuongoza watanzania katika mazishi ya waziri Mkuu mstaafu hayati Edward lowassa,hii leo anafanya kazi nyingine tena ya kimataifa kuwaongoza makumi ya viongozi mbalimbali kutoka barani Afrika katika uzinduzi wa Sanamu ya Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius kambarage Nyerere Addis Ababa Ethiopia.
Sanamu hiyo inakuja kama sehemu ya kutambua mchango mkubwa sana wa Mwalimu Nyerere na Tanzania katika ukombozi wa bara la Afrika.huwezi ukaiandika vyema historia ya bara la Afrika pasipo kuitaja kwa uzito na kuizungumzia kwa heshima kubwa nchi ya Tanzania. Ni Tanzania ndio iliyoongoza ukombozi wa nchi nyingi sana barani Afrika kutoka katika makucha ya wakoloni hususani nchi za kusini mwa Afrika. lakini pia Tanzania imewahi kutoa katibu mkuu wa OAU iliyokuwepo awali kabla ya hii ya sasa.
huyu si mwingine bali ni Salimu Ahmed Salim kuanzia mwaka 1989-2001,ambaye kama siyo kura ya VETO ya marekani alikuwa anakwenda kuwa mtanzania wa kwanza kuwa katibu mkuu wa umoja wa Mataifa yaani UN.kwa kuwa alikuwa amekidhi kila kitu na kila sifa na uwezo wa kutosha, lakini kutokana na itikadi na siasa za ujamaa na ubepari ambazo zilikuwa zimeota mizizi na kutawala kwa wakati huo ikawapa hofu Marekani walioamua kumpiga vita asitwae kiti hicho.
Kwa hiyo leo Rais wetu mchapa kazi ametua huko kwa kishindo na kwa kujivunia historia ya kutukuka na mchango wa kipekee wa baba yetu wa Taifa na Taifa letu kwa ujumla .lakini pia ikumbukwe ya kuwa hata lugha yetu ya Taifa yaani kiswahili ni miongoni mwa lugha zinazotambulika katika umoja huo, lugha ambayo baba wa Taifa aliitumia kwa nguvu zake zote kuliunganisha Pamoja Taifa letu na kujenga umoja wa kitaifa.
Rai yangu ni kuwa tumuenzi baba wa Taifa kwa kufanya yale mazuri yote aliyokuwa anayahubiri,tupinge vita rushwa,wizi,ufisadi,ubaguzi na unyonyaji wa aina yoyote ile. Ni lazima viongozi wetu wamuenzi kwa kudumisha uadilifu na uzalendo na siyo kuogopa kimvuli chake na sauti yake kwa yale aliyokuwa akiyakemea. Ni lazima viongozi wetu wawajali ,kuwapigania ,kuwatetea na kuwasemea watanzania wanyonge wasio na Sauti.ni lazima kila mmoja ajiulize ataifanyia nini Tanzania na siyo Tanzania itamfanyia nini yeye binafsi.
Ni lazima kila kiongozi ajuwe cheo ni dhamana.na kwamba mali ,pesa na vyeo vyote ni vya kupita tu. Ni lazima viongozi wetu wajuwe ni bora jina zuri kuliko mali na utajiri wote wa Dunia.na kwamba kitakachokumbukwa kutoka kwao na kukufanya uendelee kuishi hapa Duniani hata kama umetangulia mbele za haki ni matendo yako mema kwa watu,utu wako,kugusa kwako maisha ya watu,kutenda kwako haki kwa watu wote pamoja na mengine mengi kama haya.ukitenda mabaya ukiwa madarakani basi tambua yakuwa utakufa siku hiyo hiyo utakayotoka madarakani hata kama utakuwa bado upo hai maana watu watakusahau kabisa katika mawazo na akili zao kama umewahi kuwa kiongozi wao, kwa kuwa hukugusa maisha yao kwa namna yoyote ile ukiwa kiongozi.