DOKEZO Mkuu wa mkoa wa Dar, wadhibiti wanaotaka kujigawia soko la Mbagala Zakhiem kinyume na utaratibu uliopangwa na Manispaa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,673
22,264
Ujenzi wa uboreshaji soko la Mbagala Zakhiem umekamilika na wafanyabiashara wa soko hilo walitegemea warejeshwe kwenye soko hilo kulingana na utaratibu waliopewa kabla ya ujenzi, kinachoendelea hivi sasa ni wamejitokeza viongozi wanaotaka kuvuruga utaratibu wa kuwarejesha wahusika ili wajigawie wao! Watu hawa hujitokeza kwenye kila miradi ya masoko inapokamilika.

Wafanyabiashara wa soko hilo kabla ya kupisha ujenzi walichukuliwa taarifa zao na kupewa namba za vizimba vipya kulingana na walivyokuwa awali, ila sasa wamejitokeza watu wanaotaka kuvuruga ahadi ya utaratibu wa awali ambao usingeleta taharuki wala vurugu na wanasababisha kuchelewa kuwarudisha wafanyabiashara walipewa namba za vizimba vipya hivyo kulikosesha mapato jiji.

Kama ulivyoweza kuwadhibiti watu hao waroho kwenye masoko ya Mwenge na la ndizi ndiyo matarajio ya wafanyabiashara wa soko la Mbagala Zakhiem.
 
Aisee hawa wafanyabiashara Bora wapatiwe Tu vizimba vyao ili waondoke pale barabarani....
Wafanyabiashara wanapanga bidhaa zao ndani ya barabara na kusababisha foleni Kwa kifupi itafaa Sana kama hili soko likifunguliwa mapema ingawa kuna tetesi zinadai kuwa litafunguliwa siku moja na mwendokasi
 
Huyo alivujisha kashindwa kusema akina nani wanacheza mfumo?
Hakuna mtu anayeweza kuthubutu kumtaja mtu jina kwa kuhofia yeye kutajwa kuwa amevujisha siri, ila mjue soko limekwama bila sababu za msingi huku kukiwa hakuna shughuri yoyote ikiendelea sokoni.
 
Aisee hawa wafanyabiashara Bora wapatiwe Tu vizimba vyao ili waondoke pale barabarani....
Wafanyabiashara wanapanga bidhaa zao ndani ya barabara na kusababisha foleni Kwa kifupi itafaa Sana kama hili soko likifunguliwa mapema ingawa kuna tetesi zinadai kuwa litafunguliwa siku moja na mwendokasi
Hiyo mwendokasi inapigwa viraka juu ya viraka!
 
Soko la Mbagala Zakhiem limemalizika kukarabatiwa, soko hili lilikuwa na wafanyabiashara ambao kabla ya kuanza ukarabati walichukuliwa taarifa zao ili baada ya ukarabati wapewe nafasi zao kama walivyokuwa mwanzo.

Baada ya kuchukuliwa taarifa walipigwa picha kwenye fremu zao na kupewa namba zao kulingana na walivyokuwa, lakini hivi sasa kumekuwa na njama za kutaka kuwaweka watu wapya kupitia "viongozi" njama ambazo wafanyabiashara wa awali hawahakuwa tayari kuzivumilia, hivyo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam unaombwa uzuie mtafaruku huu unaokwenda kimyakimya unaoweza kutokea Mbagala Zakhiem wiki ijayo Jumatatu.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam jana tarehe 28/08 alisimamisha ufunguaji wa soko hilo lililokarabatiwa baada ya kujiridhisha uovu kwenye kugawa vizimba, ameamuru iundwe tume kuchunguza tuhuma na kutoa orodha ya wafanyabiashara wa awali wanaotakiwa kurudi sokoni.
 
Soko la Mbagala Zakhiem limemalizika kukarabatiwa, soko hili lilikuwa na wafanyabiashara ambao kabla ya kuanza ukarabati walichukuliwa taarifa zao ili baada ya ukarabati wapewe nafasi zao kama walivyokuwa mwanzo.

Baada ya kuchukuliwa taarifa walipigwa picha kwenye fremu zao na kupewa namba zao kulingana na walivyokuwa, lakini hivi sasa kumekuwa na njama za kutaka kuwaweka watu wapya kupitia "viongozi" njama ambazo wafanyabiashara wa awali hawahakuwa tayari kuzivumilia, hivyo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam unaombwa uzuie mtafaruku huu unaokwenda kimyakimya unaoweza kutokea Mbagala Zakhiem wiki ijayo Jumatatu.
Hao viongozi ni viongozi gani? Wasoko hilo, serikali au Chama? Kuwa muwazi kama umeamua kuzungumza zungumza yote.
 
Hao viongozi ni viongozi gani? Wasoko hilo, serikali au Chama? Kuwa muwazi kama umeamua kuzungumza zungumza yote.
Miradi yote chama huwa mbele, ameliona hilo ndiyo sababu kawazuia na kuwatska waliochukua hela za watu wazitapike!
 
Back
Top Bottom