Kuna kikundi cha watu wamejivika ngozi kama waislamu zaidi ya waislamu wengine. Hawa ni propagandists wa ccm wanaojaribu kila liwezekanalo kuichafua chadema ili kionekane kinawabagua waislamu. Sina haja ya kuwataja hapa. Wanajulikana. Wengine hudai si wanachama wa chama chochote cha siasa ila tu wanaichukia chadema kwa sababu haiwapendi waislamu. To add salt to the wound, wanadai chadema ni chama cha wakristo. Ni kikundi cha aina hii ambacho hudai cuf ni chama cha waislamu. Hiyo propaganda ilifanya kazi vilivyo miaka hiyo cuf ilipokuwa na nguvu. Na leo tena ninaposikia kiongozi wa cuf anasema kwa wanasingiziwa kwamba ni chama cha waislamu, basi anawaomba waislamu wote wajiunge nacho....naishiwa nguvu.
Bahati mbaya zaidi ni kwamba mambo ya imani haya kwa watu wa nchi zetu hizi ni very sentimental and influential katika maisha ya kila siku. Katika jazba na hamaki za kujibu mashambulizi yaliyoandaliwa kiufundi, watu wengi hujikuta wamewarushia kombora waislamu/wakristo wote, jambo ambalo ni kosa kubwa na lenye madhara sana.
Bado naamini majority ya waislamu ni watu wenye uelewa na uvumilivu kama history inavyoonyesha. Ila hiki kikundi kisipodhibitiwa, huko mbele ni kiza tena kinene.