MATESLAA
JF-Expert Member
- Aug 11, 2011
- 1,246
- 74
Wakuu,
Nimeshuka hapa kituo cha Jangwani naelekea moja kwa moja mpaka kiwanjani, napishana na defender ikiwa na askari watatu...
Nitazidi kuwapa update
PICHA kwa hisani ya Blog ya Mjengwa:
Nimeshuka hapa kituo cha Jangwani naelekea moja kwa moja mpaka kiwanjani, napishana na defender ikiwa na askari watatu...
Nitazidi kuwapa update
Kuna mtu anazungumza sasa hivi anasema zamani CUF ilikuwa na kaulimbiu ya 'Jino kwa jino' na sasa ni Mchaka Mchaka hadi 2015 Prof. Lipumba atakapoingia Ikulu.
Anasema CDM kwa kushirikiana na CCM wametumia vyombo vya habari kuwa CUF ni CCM B
Mzungumzaji anasema vijana wa CUF wako tayari kwa lolote na wakati wowote
Anasema wamejipanda kuondoa CCM madarakani na wenzao wa vidole Viwili ambao majuzi wametuhumiwa kula rushwa bungeni
Kambaya ndie anazungumza kwa sasa. Anasema CUF ndio waanzilishi wa viwanja wa Jangwani. Anadai CHADEMA wamepageuza kwa kupaita Chadema Square
Anadai kuwa CHADEMA ilimfuata Kikwete 2005 agombee kupitia CHADEMA endapo asingepitishwa na CCM
Sasa CUF wako jangwani na wanawachana wau wa CDM ati hawana hazina ya viongozi kwa hoja kuwa kila mwaka wa uchaguzi ukifika wanaenda kuomba watu wa CCM wagombee kama ilivykuwa kwenye ishu ya kumuomba JK agombee urais kama asingechaguliwa ndani ya CCM.
Pia wanasema CDM wao hawana hazina ya viongozi maana Mwenyekiti wao hana elimu zaidi ya kujua elimu ya biashara ya kupiga disko.
Wanasema CDM ni sawa na CUF maana hata kada tajiri wa CCM anawasaidia CDM badala ya CUF.
Hajj Duni anawapa pole watanzania kwa mauji ya Mwangosi, anasema hivyo ni vita vya muda mrefu.
Anaendelea kwa kusema hakuanza kufa muandishi huyo bali walianza kufa CUF kwa makundi.
Wanaimba wimbo wao unasema "CCM ikifa, mimi siwezi kulia; nitaitupa Kagera iwe chakula cha mamba"
Prof. Lipumba anasogea kwenye mic anacheka cheka kisha anaanza kwa kusema:
"Wanaumeeeeee!!! Wanawakeeeee!!!!! CCM kwisha kwisha ndembe ndembe kifo cha mende"
Huyu ni Makamu Mwenyekiti wa CUF taifa, amewataka waislamu wote kujiunga na CUF, kwa vile CCM na CDM haviwataki.
Je, hajathibitisha madai ya siku nyingi kuwa CUF ni chama cha kidini?
PICHA kwa hisani ya Blog ya Mjengwa: