Mkutano wa CUF katika viwanja vya Jangwani

CUF yenyewe ina hazina ya viongozi?? mbona basi wamefunga ndoa na ccm? kwa nn wasingesubiri washinde zanzibar waunde serikali bila ndoa na magamba? Lipumba ana degree 3 fine zimesaidiaje taifa hili maskini??si hata bungeni hoja yoyote ya ccm inaungwa mkono na cuf kwa nn isiitwe ccm B?
 




Duh..ama kweli JF kuna mambo! Yaani badala ya kujibu hoja za Ritz we unakimbilia kuwapatanisha Chadema na Waislam kwa kutumia picha hii?


Tatizo ambalo ni kama kansa kwa Wabongo ni kwamba mtu akiwa ni Mwislamu au Mkristu na hapendi chama fulani cha siasa au msimamo fulani wa kisiasa (ambayo ni haki yake ya kikatiba) basi anajiaminisha kuwa kila Mwislamu au kila Mkristu (na mara nyingi huwa anasahau kuwa kuna Watanzania wengi tu hawana habari na Uislamu wala Ukristu ) anafikiri kama yeye!!!! Hili ni tatizo kubwa sana na liko dhahiri hapa jamvini JF. Ushauri mdogo kwa wana JF, wewe toa maoni/mtazamo/hoja zako kama wewe binafsi. Ondokeni na propoganda zenu zisizokuwa na miguu wala kichwa.
 
Mkutano tata sana huu.
Mwenye chama Maalim yupo USA inasemekana akitafuta kiti cha Zanzibar UN.
Chama kina sera ya serikali 3, mwenye chama anataka mkataba.

Inachangaya kidogo! Anyway kila la kheri
 
Wakuu,

Nimeshuka hapa kituo cha Jangwani naelekea moja kwa moja mpaka kiwanjani, napishana na defender ikiwa na askari watatu...

Nitazidi kuwapa update












PICHA kwa hisani ya Blog ya Mjengwa:

attachment.php

attachment.php

attachment.php

attachment.php




Jana nilikuwa na safari ya kwenda mikoa ya Kusini mwa Tanzania ,nilondoka Dar mida ya saa 6 mchana .Maeneo ya kutoka Mkuranga nilikutana na FUSO za kutosha zimebeba watu zikiwapeleka kwenye mkutano.Sasa najiuliza CUF haina wafuasi Dar mpaka itumie gharama ya kuzomba watu umbali wa zaidi ya km 50!!!! tena mkoa wa jirani!!!
 
kaka si kweli kuwa cdm haipatani na waislamu na haya yaliletwa na ccm na watu wajinga wachache wameyashika unakumbuka jumbe za cm 2015? Tuwe waangalifu mwingine atakuuliza swala la kejer kuwa kwann mikutano ya kaf tunawaona waislamu tu? Kitu hichi mm na kataa c kweli wapo wakritu kafu vile vile wapo waislamu cdm haya yote ni matunda ya ccm

Heri ambao wamekuelewa, naamini wengi watatafakari. Iwe ni CDM, CUF au yeyote ukianza kumbeza mwanachama wa chama kingine kwa mtazamo wa kidini huo sio udini bali ni u.pu.m.bavu tu, haijalisha una digrii ngapi jua tu wewe unahitaji kuelimishwa na kukombolewa kifikra.

Hivi inakuwaje kunakuwepo na watanzania wachache wanaamini uongo saaaaana, lakini hawataki kutumia akili zao walizojaliwa na Mwenyezi Mungu tena bure kuchanganua mambo, wanakubali tu kula kila kitu pumba, maaragwe, tope, n.k. Hivi kweli macho yenu na akili zenu hazioni waislamu na wakristo wakiunga mkono vyama vyao mbalimbali wanavyo vipenda, CDM, CUF, NCCR, TLP, CCM, n.k. nani anawaloga akili zenu nyie vipofu mnaanza kugeukia umbea wa watu wazembe wa fikra na wasiotaka kujibidiisha kuleta mawazo mapya yenye changamoto mpya, BADILIKENI acha kuwa wazembe wa kufikiri.

Hebu tuelimike, tusiwe ma-boya ya kueleaelea tu kila kona na kulishwa matapishi, tujaribu kutumia busara na akili zetu vizuri kwa kufanya mijadala yenye maana na kuleta hoja zenye kutupeleka mbele sio huu upuuzi wa dini, dini, dini, dini,.....hata na shetani ana dini zake nyingi tu kwani unafikiri kubeza dini ya mwenzio ndio kunakufanya uwe muumini mzuri au uwe karibu na Mungu. Unaweza ukafaanya yote hayo na bado Jehanam ukaenda tu haijalishi ni Mwislamu au Mkristo au nani.
 
TBC mkutano wa CUF wanaonyesha live ila wa CDM hata kwenye taarifa ya habari hawaweki mpaka Nchimbi awazungumzie CDM kuwa wamesababisha mauaji ndo utawasikia. Hiki chombo kinaendeshwa kwa kodi zetu iweje kinakuwa na ubaguzi?
 
Kuna kikundi cha watu wamejivika ngozi kama waislamu zaidi ya waislamu wengine. Hawa ni propagandists wa ccm wanaojaribu kila liwezekanalo kuichafua chadema ili kionekane kinawabagua waislamu. Sina haja ya kuwataja hapa. Wanajulikana. Wengine hudai si wanachama wa chama chochote cha siasa ila tu wanaichukia chadema kwa sababu haiwapendi waislamu. To add salt to the wound, wanadai chadema ni chama cha wakristo. Ni kikundi cha aina hii ambacho hudai cuf ni chama cha waislamu. Hiyo propaganda ilifanya kazi vilivyo miaka hiyo cuf ilipokuwa na nguvu. Na leo tena ninaposikia kiongozi wa cuf anasema kwa wanasingiziwa kwamba ni chama cha waislamu, basi anawaomba waislamu wote wajiunge nacho....naishiwa nguvu.

Bahati mbaya zaidi ni kwamba mambo ya imani haya kwa watu wa nchi zetu hizi ni very sentimental and influential katika maisha ya kila siku. Katika jazba na hamaki za kujibu mashambulizi yaliyoandaliwa kiufundi, watu wengi hujikuta wamewarushia kombora waislamu/wakristo wote, jambo ambalo ni kosa kubwa na lenye madhara sana.

Bado naamini majority ya waislamu ni watu wenye uelewa na uvumilivu kama history inavyoonyesha. Ila hiki kikundi kisipodhibitiwa, huko mbele ni kiza tena kinene.
waislam wanao uelewa kupitia wafuasi wa cdm hapa jf wanajua mbivu na mbichi...
 
kwani nawe vipi? Umetumwa kunakiri kila lisemwalo? mbona CDM wakifanya mkutano hutumi dondoo za maneno ya akina slaa, mbowe, mnyika, lissu nk.? Kuwa na akili endelevu, hiyo ndo siasa mbona CDM wanadai CUF ccm b?:director:
:flypig::loco::director:
 
waislam wanao uelewa........................................................
Nimejaribu kufuatilia ili kuthibitisha kauli yako kama ni kweli, nakakuta ina ukweli mkubwa usio na shaka baada ya kuangalia kidogo tu kwenye safu ya juu bila kwenda huko chini kwa akina Prof. Safari na wengineo ambao ni waislamu wenye uelewa mkubwa wa mambo, tuzidi kuelemishana wako tu na wakristo maboya wengi tu wanatusumbua kwa uelewa mdogo au kutokutaka kujieleimisha mambo ya kweli.....!!
 

Attachments

  • CHADEMA.png
    CHADEMA.png
    90.9 KB · Views: 39
ITV mbona wanaonesha wa CDM? TBC in biashara CDM wakilipia wataoneshwa pia-acha mawazo mgando?
 
serikali za umoja wa kitaifa ndo suluku za serikali zetu huki afrika,si kukosa viongozi-inasaidia kuwafanya viongozi wasiwe miunguwatu-kama cdm hawana utamaduni huo basi ujue haina tofauti na ccm ikiwa madarakani
 
Hawa jamaa ni sura zile zile zilizovamia Mambo ya Ndani juzi Ijumaa ........... Si mnakumbuka Lipumba alitoa mchango wa kuhamasisha watu kususia sensa!!????
 
Kama tunataka mageuzi ya kweli, basi vita kati ya CDM na KAFU lazima ife kwanza

Mkuu, uko sahihi kabisa, lakini kwa uzoefu wangu sijawahi kusikia CDM kutangaza vita dhidi ya CUF ila kinyume chake.
CUF kama CCM, wakiwa katika majukwaa ya siasa, adui yao mkubwa ni CDM.

Kwa CCM, haishangazi, ila inashangaza zaidi unapoona CUF kuipiga vita CDM wakati chenyewe nacho ni chama cha upinzani. Hii inanikumbusha siasa za Zimbabwe kabla ya uhuru.
 
Back
Top Bottom