Mke wangu kapata kazi Mkoani!

Mke wangu kapata kazi Mkoani!

Mkuu Hawa watu akishakuwa na kazi na kuweza kupata mkopo wa kununua gari usitegemee atakuwa chini yako Tena.
Yaani kama ni maisha wewe kula Bata tu.
Maana dharau kama zote!!
Hakuna anachofanya kama mama ndani ya nyumba
Kila kitu anafanya hg.
Ila wewe anataka uwajibike kama baba.
Sahii kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rejea Uzi wangu
"Hakuna ndoa ya mume na mke kuishi sehemu tofauti"
Ukitaka kuthibitisha hili wewe kaa miezi 6 tu. Utanipa jibu.
Wewe mwenyewe ndiye utaanza kugonga nje na yeye huko atagongwa nje then.
Then hatari zaidi ni kwamba amepata kazi ambayo ataweza kujisimamia.
All in all hapo hakuna ndoa.
Chukua screen shot hii post.
Aiseee
 
Meeen, I like this…

Ni kwamba mpaka naleta huu uzi, tuliongea akasema kama naweza kumruhusu aende kufanya kazi au la, so anasubiri uamzi kutoka kwangu, ndio nilikuwa naangalia possibilities hapa, ndoa haijafika miaka hiyo miaka 10. Nikalileta huku nikiamini kuna watu wanaweza kuwa na experience na hivo vitu.
Bro asiende kama kila kitu anapata utanishukuru baadae
 
Aiiiiiiiii just say it again, kwamba anapata kila kitu kwako?abeeee!! Unamdanganya nani? Tuseme vyakula vipo mnakula nakushiba na vile tumbo halinga kioo hatutaki kujua mnakulaga nini.

Sema hapa hapa kama kweli unampa kila kitu.
1. Akisema anaomba 40000 za kusuka unampa bila masimango kuwa anapenda vya bei kali?

2: nguo unamnunulia nzuri nae anajihisi fresh?
3. Kwao wakitaka msaada unatoa bila kumrushia vijembe?

4: tuseme mama yake ana shida unatoaga bila kuvuta mdomo na kushinda bar unaangalia mpira ila asikuombe?

5: sikukuu za pasaka Christmas au eid uwa unampa pesa za kutuma kwao hata kama hajakuomba? Yaani unamwambia hii làki moja tuma kwenu wanunuwe ka nyama?

6: tuseme mdogo wake kamwamba ada unamchangia kwa moyo safi bila kinyongo?

7.tofauti na mahali ulotoaga wakati ule kuna siku unatumaga hata vijizawadi kwao?

8: je kuna wakati unampa vimatumizi pembeni hata amnunulie kijizawadi mama yako bila wewe kujua? Maana mama mkwe huyu ndo aliye mzalia mme so anastahili ampe vijizawadi ma vitenge na mazagazagq mengine.

Kama haya yote unafanya basi mzuie asiende kama hufanyi pambana na hali yako, haya ndo yalimfanya akaombe kazi.

Na kama ungekuwa na hela miaka mitano anasota kwako ungelikuwa ushamfunguliaga hata kijiduka.

N.b nipo hapa msibani kwa queen eliza nasoma comments

Rip queen.
Hili nalo neno..🤔
 
Mwache tu aende maana kama siyo mwaminifu hata akiwa karibu na wewe haisaidii kitu.
 
duh hatari. basi sasa brother aamue kile atakacho amua kama mwanaume. then anaye amuliwa akiamua kufanyia nyumbani itakuwa rahisi zaidi kumsuspend au hatua nyingine kama hizo.
Bora apigwe kwako utajua kirahis utamuacha unafanya maisha yako, alafu kuna kitu hamuelewi vidume wa JF ,Issue hapa sio kupigwa,issue ni Reciprocation haipo ,sasa minimum requirements tu ya relationship inakua haipo zaid ya phone calls na txt msg,utaishi kweny r.ship kwa calls tu?

Alafu nikwambie hiyo ni form ya oneitis,Mwanaume unakua hauna options,unaji internalize na idea ya soulmate , ndio mana case za kijinga haziishi MMU simply kwasababu mna entertain vitu vinavyo kuharibu ww mwenyew,uliskia wapi kua Long distance relationship ni relationship? Mbona haijameet hata minimum requirements ya r.ship?

Thomas Rollo ameongea hili kweny The Rational Male mbona liko wazi.
 
Meeen, I like this…

Ni kwamba mpaka naleta huu uzi, tuliongea akasema kama naweza kumruhusu aende kufanya kazi au la, so anasubiri uamzi kutoka kwangu, ndio nilikuwa naangalia possibilities hapa, ndoa haijafika miaka hiyo miaka 10. Nikalileta huku nikiamini kuna watu wanaweza kuwa na experience na hivo vitu.
Nakushauri asiende, narudia Tena asiende, suala sio umalaya suala ni namna ya kutenganisha family, waza kuhusu Watoto zaidi. Asiende. Speaking from experience
 
Habarini wana jamvi!

Ebhana wife kapata kazi Mkoa wa Kagera na kazi ni nzuri, amekaa muda mrefu bila kazi takriban 5 yrs. Lakini kwa sasa ana mtoto mdogo, binafsi si kwamba sipendi akafanye kazi ila naona kama ni mbali sana na nyumbani, Kagera to Dsm ni parefu mno.

Naomba maoni yenu aende ama atulie tu, kwa sasa ni mama wa nyumbani na yuko desperate kweli kupata kazi.

Funguka Mdau, Hapa matusi si pahala pake.

Mwache akafanye kazi kwa faida yake, yako na watoto wenu
Kama yupo desperate hujamtosheleza
 
Japokuwa sijui yalivyo huko kwenye ndoa, ila ningekuwa Mimi ningemtafutia mtaji na kumfungulia biashara hapahapa dar. Umbali kati yenu unaleta majaribu ya kuchepuka, pili mnatakiwa mshirikiane kumlea mtoto sio baba mashariki mama magharibi.. Najua unampenda mkeo bro ndo mana ukamuoa Ila kama hutaki kumpoteza usiluhusu akafanye kazi mbali, hata kama huwezi kumfungulia biashara pambana apate kazi hapahapa bongo.
 
Angalia kama unaweza kuulipa huo mshahara anaoupata mwisho wa mwezi, basi mwache akae tu.

Ila kama huwezi na unaona umuhimu wa hio kazi unauona,

let her go to work...

Halafu kama wasiwasi wako ni kuchapiwa, kumbuka hata hapo ulipo bado kuna nafasi ya kuchapiwa.

kama tatizo ni distance, angalia namna ya kuhamia BK kule mkaishi kwa kula ndizi na senene.

mwisho kabisa,
mkeo akienda huko atachukua.miezi 6 tu akirudi atakua analoanisha godoro balaa😂😂😂
Vyakula vya wahaya vinatengeneza maji mengi sana mwilini

Angekuwa anayeweza ya kumlipa mshahara wala mwanamke asingeacha familia yake akatamani kwenda bukoba

Kama ni Kuchapiwa atachapiwa sana tuu.... anapokua kazini yeye akamwacha mke akiwa desperate nyumbani 😅😅😅
 
Huu Uzi ufutwe, hauna msaada wowote kwa muomba ushauri Wala kwa jamii. Umejaa mawazo potofu na ya kubomoa jamii na familia kuliko kujenga. Zaidi sana, watu wanatoa mawazo mepesi kwa mambo mazito, wanashusha hadhi na utukufu wa ndoa kwa kulinganisha na umalaya na tamaa za kimwili. Watu wanajitoa ufahamu mradi waonekane tu wanaongea Ila ukweli wanaujua na kuuficha makusudi, wengine hawajui lolote kuhusu ndoa na maisha ya familia lkn ndio wanaojitokeza kuwa washauri wakubwa wa ndoa. Wengine maisha hayo yalishawashinda, hukai kwa mke Wala mume hata kwa mwezi mmoja kwa tabia zako mbaya, Leo hii unataka kutoa ushauri jinsi ya mwenzako atakavyodumu kwenye ndoa milele. Na sisi wanandoa tupunguze mitandao tunajianika sana hadi kwa mashetani, namna ya kuishi na kutatua changamoto zetu itokee ndani ya ndoa yenyewe, kutafuta suluhu ya matatizo ya ndoa nje ya ndoa ni "kutoka nje ya ndoa" kitu ambacho ni dhambi kubwa katika ndoa. Tatizo la kijana kutafuta mke mitandaoni, kuchumbia mitandaoni, mahari kwa mtandao, ndoa kwa mitandao, mtoto akizaliwa wa kwanza kujua ni mtandao, chakula Cha mke mtandao ndo unaambiwa ni kizuri au kibaya, hizi ndoa za mitandaoni kila kitu mitandao Mimi nilivyofundishwa mafundisho ya ndoa na katekista wangu "ni ndoa batili tangu mwanzo" hivyo hata zikivunjika ni sawa na "hazikuwahi kuwepo".
 
Huu Uzi ufutwe, hauna msaada wowote kwa muomba ushauri Wala kwa jamii. Umejaa mawazo potofu na ya kubomoa jamii na familia kuliko kujenga. Zaidi sana, watu wanatoa mawazo mepesi kwa mambo mazito, wanashusha hadhi na utukufu wa ndoa kwa kulinganisha na umalaya na tamaa za kimwili. Watu wanajitoa ufahamu mradi waonekane tu wanaongea Ila ukweli wanaujua na kuuficha makusudi, wengine hawajui lolote kuhusu ndoa na maisha ya familia lkn ndio wanaojitokeza kuwa washauri wakubwa wa ndoa. Wengine maisha hayo yalishawashinda, hukai kwa mke Wala mume hata kwa mwezi mmoja kwa tabia zako mbaya, Leo hii unataka kutoa ushauri jinsi ya mwenzako atakavyodumu kwenye ndoa milele. Na sisi wanandoa tupunguze mitandao tunajianika sana hadi kwa mashetani, namna ya kuishi na kutatua changamoto zetu itokee ndani ya ndoa yenyewe, kutafuta suluhu ya matatizo ya ndoa nje ya ndoa ni "kutoka nje ya ndoa" kitu ambacho ni dhambi kubwa katika ndoa. Tatizo la kijana kutafuta mke mitandaoni, kuchumbia mitandaoni, mahari kwa mtandao, ndoa kwa mitandao, mtoto akizaliwa wa kwanza kujua ni mtandao, chakula Cha mke mtandao ndo unaambiwa ni kizuri au kibaya, hizi ndoa za mitandaoni kila kitu mitandao Mimi nilivyofundishwa mafundisho ya ndoa na katekista wangu "ni ndoa batili tangu mwanzo" hivyo hata zikivunjika ni sawa na "hazikuwahi kuwepo".

Ndoa haina utukufu, ila ndoa njema na ndoa sahihi inampa Mungu utukufu
Tumsifu Yesu Kristo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom