Mke wangu anaishi maisha ya ki-tamthilia, yananitesa haswa

Adolph Jr

JF-Expert Member
Nov 5, 2016
5,558
8,631
Ni muda tena napokea taarifa kutoka kwa familia hii ya rafiki yangu kuhusu mkewe ila nimeshindwa kumshauri hebu, tusaidiane pamoja wana JF....

Mke wangu nimeshindwa kumuelewa yaani maisha yake kama vile yananitatiza nikimueleza anasema ni wajibu wangu iko hivi...

Nimejiwekea utaratibu kila mwisho wa mwezi ninaenda dukani kwa mangi na kununua mahitaji yote muhimu ya nyumbani kwa mwezi unaofuatia, nazungumzia chakula na vitu vingine vidogo vidogo pamoja na kumpatia pesa za matumizi mwezi mzima.

Ila tatizo limeanzia pale ambapo mwanamke anapojaribu kuishi maisha ya kufuatilia tamthilia za mapenzi haswa za hawa Azam.

Yaani kuna tamthilia ya Azam TV (siifahamu jina) nahisi ni ya ki-spania, kuna mdada anaitwa Maria de pazi yaani yale maisha anayoishi ndiyo mke wangu anaishi kuanzia kazi hadi hisia kwanini.

Huyo Maria de poz alianzisha biashara ya kuuza keki, maandazi, skonzi na vitafunwa vingine mke wangu akaiga (hilo siyo tatizo) ila shida kila kitu anachotumia ni cha bajeti ya ndani ya nyumba.

Siku huyo Maria de pozi akiumizwa huko kwenye ma-tamthilia tambua na yeye kuwa na huzuni siku nzima yaani ole wako umuagize kitu utasikia "Si uchukue mwenyewe nyie wanaume ni wale wale tu.

Siyo kwa tamthilia moja bali hujirudia mara kwa mara siyo kwamba sipendi mke wangu kufanya kazi ila kila ninayomuamzishia inakufa zaidi ya tatu hadi duka la nafaka nimemueleza akae atulie wakati natafakari ni ipi inamfaa ila naona ni yale yale.

Siku tamthilia wakija na biashara hii yeye anahamia huko ikibadilishwa na yeye anabadilisha wakikasilikiana na yeye ananikasilikia nina mashaka tunakoelekea nitapoteza mke 😳😳😳

Wazo langu ni kuacha kulipia kifurushi ila nahofia kwenda kwa majirani maana anaweza kusimulia huyu na hawezi kukosa ata siku moja mimi mwenyewe huwa ananipatia simulizi na nikaja kugundua shida ni huyo de pozi....

Msaada jamani..😥😥😥😥😥."

Nawasilisha...........
 
Back
Top Bottom