Mkapa: Yote yanayosemwa juu yangu namuachia Mungu

Jamani wakuu kuna useme wa wahenga unasema myonge mnyogeni lakini haki yake mpeni,Mh.Rais wa awamu ya tatu amefanya mengi mazuri na ya kuleta tija na maemdeleo kwa wanachi na taifa letu la tanzania kwa ujumla.

Tabia ya sisi viumbe binandamu tunaangalia sana upande mmoja wa maisha ya mwanandamu hasa upande mbaya,na ubaya unaenea haraka kuliko wema hii ndiyo hulka ya wanadamu tangu enzi hizo.

mimi binafsi pamoja na mambo yote yanayoemwa kuhsu rais mstaafu wa awamu ya tatu bado nakubali utendaji kazi wake uliyotukuka kwa maslahi ya nchi yetu changa ya Tanzania

Lazima utakuwa ulikula naye. Ukiwa baba wa familia halafu ukaleta chakula nyumbani kwako huwezi kuanza kutamba kuwa inabidi usifiwe. Hilo ni jukumu lako. Damn it.
 
Kwa wale walio wahi kuona sinema ya Denziil Washington "Man on Fire" wakati anataka kutumia rocket launcher kwa wabaya wake wenye nyumba walimwuliza " are you a Christian? Don't you believe in forgiveness" aliwajibu "forgiveness is between god and man i am just setting the meeting" kisha akawalipua. sisi kumlipua Mkapa ni ku-arange hthe meeting btween him and God.
 
Yule ni mhalifu.Hakuna kiongozi duniani anayesifiwa kwa kujenge uwanja wa mpira.Kwanza uwanja wenyewe hasara tupi wachina wameingiza vifaa kibao karibu 60% ya vitu walivyoingiza nchini wakidanganya wanajengeea uwanja vinauzwa kariakoo wamekwepa kodi huku jamaa akikodoa machoa with his 10% mfukoni
Angejenga shule,vyuo na hospitali then asinge kusanya na kusaidiana narafiki yake sumay kuchota rushwa tusingekea hapa

Mungu alaani
 
mungu anatosha kumuhukum mkapa ameua watu bila ya hatia watu wamebakwa pemba huu unyama alofanya mungu ndio atamlipa hana jema alofanya ila ufisadi na kutumia madaraka kujilimbikizia mali
 
Niambie nchi iliyowahi kumfunga rais wake wa zamani, wote wamejaribu kuwapeleka mahakamani na hamna hata aliewahi kutolewa hukum...in short though law inasema no one is above the law, hawa watu wapo na kinga kubwa...hata wakipelekwa kesi zao haziishi, au ataishia kuchukua assylum.
Peru. Nixon asingepata pardon na kujiuzulu alikuwa anaelekea lupango. At least huko rule of law reigns.
 
tukimfungulia tunamfungulia kwa kosa gani na katika sheria ipi?, je makosa hayo yapo katika criminal law ya Tanzania.

Yaani huyajui makosa ya Mkapa yanayostahili kumfungulia mashtaka? Kwani kuna makosa ambayo hayapo katika criminal law ya Tanzania!?
 
Yaani huyajui makosa ya Mkapa yanayostahili kumfungulia mashtaka? Kwani kuna makosa ambayo hayapo katika criminal law ya Tanzania!?

Mkapa amefanya mema mengi kuliko haya mabaya yanayobeba vichwa vya habari kila leo.Mi cyo mwana ccm ila huyu jamaa hata akigombea kesho nitampa kura yangu hakuna mwingine ndani ccm ninayeweza kumpigia kura yangu.
 
Mkapa amefanya mema mengi kuliko haya mabaya yanayobeba vichwa vya habari kila leo.Mi cyo mwana ccm ila huyu jamaa hata akigombea kesho nitampa kura yangu hakuna mwingine ndani ccm ninayeweza kumpigia kura yangu.

Tatizo binadamu hawaoni mema, unaweza kufanya mazuri 100 lakini ukifanya baya 1 tu ndio litakalooneka.
 
Benjamin Mkapa


Benjamin William Mkapa (born November 12, 1938) is a former [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/List_of_Presidents_of_Tanzania"]President[/ame] of the United Republic of [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Tanzania"]Tanzania[/ame] (1995 - 2005) and former Chairman for the Revolutionary State Party ([ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Chama_Cha_Mapinduzi"]Chama Cha Mapinduzi[/ame], CCM).[1]

Biography

Mkapa is a graduate of [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Makerere_University"]Makerere University[/ame].[1] Previous posts include being the administrative officer in [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Dodoma"]Dodoma[/ame] and the Minister for Science, Technology and Higher Education. He also led the Tanzania mission to the [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/United_States"]United States[/ame] and was the [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Foreign_affairs"]Foreign affairs[/ame] Minister from 1977 to 1980 and from 1984 to 1990.[2]
In 1995, Mkapa was elected president based on a popular anti-corruption campaign and the strong support of former president [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Julius_Nyerere"]Julius Nyerere[/ame].[3] Mkapa's anti-corruption efforts included creation of an open forum called the Presidential Commission on Corruption (Warioba Commission) and increased support for the Prevention of Corruption Bureau.[3]
Mkapa's second 5-year term of office as President ended in December 2005. During this term in office, Mkapa privatized state-owned corporations and instituted free market policies.[4] His supporters argued that attracting foreign investment would promote economic growth. His policies won the support of the [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/World_Bank"]World Bank[/ame] and [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/IMF"]IMF[/ame] and resulted in the cancellation of some of Tanzania's [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Foreign_debt"]foreign debts[/ame].[3]
He has been criticized for some ineffectiveness of his anti-corruption efforts[3] as well as for his lavish spending. He spent £15 million on a private presidential jet, as well as almost £30 million on military aviation equipment which experts deemed beyond the limited needs of the country's armed forces.[5] It was over the latter purchase that then [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/United_Kingdom"]British[/ame] [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Secretary_of_State_for_International_Development"]International Development Secretary[/ame] [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Clare_Short"]Clare Short[/ame] expressed public outrage, resulting in her becoming known as 'Mama Radar' in the Tanzanian press.
Having left office due to a two term limit, Mkapa is dogged by many accusations of corruption among them improperly appropriating himself and his former finance Minister Daniel Yona the lucrative "Kiwira Coal Mine" in the southern highlands of Tanzania without following procedures. By privatizing the kiwira coal mine to himself, he broke the Tanzanian constitution which does not allow a president to do a business at state house.
He was appointed to Aga Khan University Board of Trustees in November 2007.
 
Mahokaaaaaaa!!!! !!!! ha !!! ha !!! ha !!! ha !!!!! iiiii hi !!!! hi hi!!! ha !!! ha !!! a !! khi !!! khi !!!khi !!!khi !!! Mkap!! mka!!! mkappa !!!! hahahaha !!!!!

ah! ah! ah! ah!

Ati anamuachia mungu...... kha !!!!! kha !!!!! uuuwi!!

LAHHHHH!!!!!!!! UH!

Sijui kama atamuachia Mungu anayewaona watanzania hawa wakifa kwa magonjwa yanayoweza kutibika au Mungu mwingine wa wajanja kama yeye mwenyewe Mkapa ambaye anaona kuwa watanzania ni wavivu wa kufikiri hivyo ni haki yao kupata shida walizo nazo sasa huku utajiri wa nchi ukichukuliwa na wageni.

kha!

MBAVU ZINAUMA
 
Mkapa amefanya mema mengi kuliko haya mabaya yanayobeba vichwa vya habari kila leo.Mi cyo mwana ccm ila huyu jamaa hata akigombea kesho nitampa kura yangu hakuna mwingine ndani ccm ninayeweza kumpigia kura yangu.


Baadhi ya Watanzania ndivyo walivyo!!! Unakumbuka kauli ya "Hata majani tutakula lakini rada lazima inunuliwe" habari yote kuja kuanikwa hadharani kumbe ile rada thamani yake ilikuwa ni $28 millioni tu $12 miilioni fedha za walipa kodi mafisadi wameingia nazo mitini. Huyo huyo Vithalani ndiye aliyekuwa wakala wa ununuzi wa ndege ya Rais na helicopters za jeshi hapo lazima kutakuwa na ufisadi ambao hatujaujua lakini iko siku tutakuja kuufahamu.

Siku za mwisho za Mkapa ndiyo papa fisadi Rostam alichota $40 miilioni si ajabu hapa pia Mkapa alihusika kwa namna moja au nyingine. Kakopa shilingi bilioni 7 toka NSSF na hadi hii leo hajarudisha hata senti tano. Huyu alikuwa anazimezea mate nyumba fulani za Serikali akaja na mpango wake wa kuzitapeli nyumba za Serikali kwa kuziuza kwa mawaziri na makatibu wakuu kwa bei poa kabisa. Kufuatilia hili Serikali imeingia hasara ya $200 millioni kwa kuwaweka maofisa wake mahotelini kwa ukosefu wa nyumba. Huyu huyu Mkapa ndiye aliyesaini mikataba ya uchimbaji madini ambayo Tanzania tunapata 3% tu huku wageni wakichukua 97% Wabunge walipokuja juu kama sikosei 2003 au 2004 kutaka kuiona mikataba ile ya madini akawafuata Dodoma na sijui kama aliwatisha au aliwaambia nini maana baada ya kikao kile kelele za Wabunge wa CCM kutaka kuiona mikataba ile na kuijadili Bungeni zikapotea kabisa.

Aliiba Kiwira na kututukana Watanzania kwamba tuna wivu wa kike tukimuona mtu ana vijisenti vyake tu basi tunadhani ni mwizi (kumbe mara nyingi huwa hatukosei). Pamoja na kumlipa mshahara na marupurupu makubwa, hakutosheka akaamua kufanya biashara akiwa Ikulu hadi hii leo hataki kusema alikuwa anafanya biashara gani na alifanya nani. Yote haya huyaoni kama ni kasoro kubwa kwa kiongozi wa nchi ambaye ameaminiwa na Wananchi wake na kumpa madaraka ya kuwaongoza eti unadai akigombea tena utampa KULA (kura) YAKO!!! Kweli Watanzania ndivyo walivyo!!! Wacha nchi yetu igeuzwe kichwa cha mwendawazimu miaka nenda miaka rudi!
 
Baadhi ya Watanzania ndivyo walivyo!!! Unakumbuka kauli ya "Hata majani tutakula lakini rada lazima inunuliwe" habari yote kuja kuanikwa hadharani kumbe ile rada thamani yake ilikuwa ni $28 millioni tu $12 miilioni fedha za walipa kodi mafisadi wameingia nazo mitini. Huyo huyo Vithalani ndiye aliyekuwa wakala wa ununuzi wa ndege ya Rais na helicopters za jeshi hapo lazima kutakuwa na ufisadi ambao hatujaujua lakini iko siku tutakuja kuufahamu.

Siku za mwisho za Mkapa ndiyo papa fisadi Rostam alichota $40 miilioni si ajabu hapa pia Mkapa alihusika kwa namna moja au nyingine. Kakopa shilingi bilioni 7 toka NSSF na hadi hii leo hajarudisha hata senti tano. Huyu alikuwa anazimezea mate nyumba fulani za Serikali akaja na mpango wake wa kuzitapeli nyumba za Serikali kwa kuziuza kwa mawaziri na makatibu wakuu kwa bei poa kabisa. Kufuatilia hili Serikali imeingia hasara ya $200 millioni kwa kuwaweka maofisa wake mahotelini kwa ukosefu wa nyumba. Huyu huyu Mkapa ndiye aliyesaini mikataba ya uchimbaji madini ambayo Tanzania tunapata 3% tu huku wageni wakichukua 97% Wabunge walipokuja juu kama sikosei 2003 au 2004 kutaka kuiona mikataba ile ya madini akawafuata Dodoma na sijui kama aliwatisha au aliwaambia nini maana baada ya kikao kile kelele za Wabunge wa CCM kutaka kuiona mikataba ile na kuijadili Bungeni zikapotea kabisa.

Aliiba Kiwira na kututukana Watanzania kwamba tuna wivu wa kike tukimuona mtu ana vijisenti vyake tu basi tunadhani ni mwizi (kumbe mara nyingi huwa hatukosei). Pamoja na kumlipa mshahara na marupurupu makubwa, hakutosheka akaamua kufanya biashara akiwa Ikulu hadi hii leo hataki kusema alikuwa anafanya biashara gani na alifanya nani. Yote haya huyaoni kama ni kasoro kubwa kwa kiongozi wa nchi ambaye ameaminiwa na Wananchi wake na kumpa madaraka ya kuwaongoza eti unadai akigombea tena utampa KULA (kura) YAKO!!! Kweli Watanzania ndivyo walivyo!!! Wacha nchi yetu igeuzwe kichwa cha mwendawazimu miaka nenda miaka rudi!

Mkuu lazima tukubali kuwa hakuna aliyemtumilifu kwa 100% kuna mambo ambayo nakubaliana na wewe na yapo ambayo nitapingana na wewe na kumuona Mkapa ni kiongozi kwangu mimi binfsi.
Suala la madini ni kweli na ndo kwanza tulikuwa tunaingia kwenye hii biashara lakini mbona hata waliokuja mbele yake wamesaini mikataba fake? Mfano mzuri ni Karamagi au haya unayasahau? Wao baada ya kuona mapungufu ilibidi warekebishe na si kuturudisha nyuma tena.
Na kuna mengine kama Rada, ndege na mgodi ni tamaa tu za waliokuwa nyuma yake kutaka kujilimbikizia mali kwa fedha za walipa kodi cyo kwamba Mkapa ndo aliyepanga na kumaliza haya mambo huenda na yeye kuna mengine alipotoshwa na hawa walafi wachache.
Kafanya mengi mazuri kama kuiweka nchi angalau vizuri kidogo kiuchumi ikiwa ni pamoja na kudhibiti mfumuko wa bei n.k kajenga sana barabara achilia mbali uwanja wa burudani...
 
Mazuri ya kuwaingiza wale makaburu pale TANESCO kwa mtutu wa bunduki na kuwalipa mabilioni ya shilingi huku hawajui chochote kuhusu umeme. Mazuri ya kuwaachia wachukuaji wachukue dhahabu yetu kwa bei ya bure kabisa. Mimi sioni mazuri yoyote ya Mkapa uchumi tulioambia unakuwa sikuona ahueni kwa Watanzania walio wengi. Wengi wao walikuwa wanalalamika kwamba hali ya maisha imezidi kuwa ngumu. Ukiondoa wachache ambao hawakufika hata milioni. Alikuwa mstari wa mbele katika sera za ubinafsishaji kuwazuia Watanzania wasinunu hata moja ya mashirika yaliyouzwa. Sioni uzuri wa hata moja alilolifanya alikuwa FISADI TU!
 
Mkuu lazima tukubali kuwa hakuna aliyemtumilifu kwa 100% kuna mambo ambayo nakubaliana na wewe na yapo ambayo nitapingana na wewe na kumuona Mkapa ni kiongozi kwangu mimi binfsi.
Suala la madini ni kweli na ndo kwanza tulikuwa tunaingia kwenye hii biashara lakini mbona hata waliokuja mbele yake wamesaini mikataba fake? Mfano mzuri ni Karamagi au haya unayasahau? Wao baada ya kuona mapungufu ilibidi warekebishe na si kuturudisha nyuma tena.
Na kuna mengine kama Rada, ndege na mgodi ni tamaa tu za waliokuwa nyuma yake kutaka kujilimbikizia mali kwa fedha za walipa kodi cyo kwamba Mkapa ndo aliyepanga na kumaliza haya mambo huenda na yeye kuna mengine alipotoshwa na hawa walafi wachache.
Kafanya mengi mazuri kama kuiweka nchi angalau vizuri kidogo kiuchumi ikiwa ni pamoja na kudhibiti mfumuko wa bei n.k kajenga sana barabara achilia mbali uwanja wa burudani...

Mvina
Ukimlinganisha Mkapa na mwungwana wa sasa, Mkapa hakamatiki. Lakini kwa vipimo vya kizalendo alivyoviacha Baba wa Taifa, basi Mkapa si lolote kama asemavyo Bubu.
Ubora wa uongozi ni relative. Kwa hali hiyo tusimlinganishe Mkapa na viongozi wachovu kama JK.
 
Mkuu lazima tukubali kuwa hakuna aliyemtumilifu kwa 100% kuna mambo ambayo nakubaliana na wewe na yapo ambayo nitapingana na wewe na kumuona Mkapa ni kiongozi kwangu mimi binfsi.
Suala la madini ni kweli na ndo kwanza tulikuwa tunaingia kwenye hii biashara lakini mbona hata waliokuja mbele yake wamesaini mikataba fake? Mfano mzuri ni Karamagi au haya unayasahau? Wao baada ya kuona mapungufu ilibidi warekebishe na si kuturudisha nyuma tena.
Na kuna mengine kama Rada, ndege na mgodi ni tamaa tu za waliokuwa nyuma yake kutaka kujilimbikizia mali kwa fedha za walipa kodi cyo kwamba Mkapa ndo aliyepanga na kumaliza haya mambo huenda na yeye kuna mengine alipotoshwa na hawa walafi wachache.
Kafanya mengi mazuri kama kuiweka nchi angalau vizuri kidogo kiuchumi ikiwa ni pamoja na kudhibiti mfumuko wa bei n.k kajenga sana barabara achilia mbali uwanja wa burudani...

Haikataliwi kuwa kweli alifanya mazuri...hili halina ubishi na atakayebisha basi atakuwa anabisha tu for the sake of it.
Kinachobishaniwa ni ukweli kuwa linapoharibika, lawama ya kwanza inamwangukia kiongozi.Uongozi ni pamoja na kubeba lawama, kuwa makini zaidi na pia kujua kuwa kuna kupewa sifa na kutupiwa lawama.Mbona zinapotolewa sifa watu hawajali kusema kuwa hizi sifa ziwaendee waliokuwa nyuma yake kwa vile wao ndio watendaji?...TUKIPOKEA SIFA TUPOKEE PIA LAWAMA.
Madhambi aliyoyafanya yeye binafsi nasita kuyazungumzia maana kila mtu ni innocent until proven guilty.
 
Tungeweza kuquantify hasara ambayo tumeipata katika sera za ubinafsishaji ambazo tuliuza mashirika na viwanda vyetu vingi kwa the so called "wawekezaji" na kisha kusaini mikataba ya uchimbaji wa madini na kupata asilimia tatu tu, uchotaji wa mabilioni ya Kagoda, ufisadi wa EPA ambao ulitokea wakati wa Mkapa, uuzwaji wa nyumba za serikali ambao hadi sasa umeingiza hasara ya $200 milioni na mengineyo mengi hayo mnayoyaita "mazuri" yaliyofanywa na Mkapa ambayo mimi siyaoni yanafutika kabisa.

Haiwezekani uchumi wa nchi ukasifiwa na IMF na WB kwamba unakuwa lakini wananchi wa nchi hiyo wasione tofauti yoyote katika hali yao ya maisha ukiondoa kundi la watu wachache. Nendeni Rwanda mkaone mabadiliko makubwa ambayo Wanyarwanda wanayafurahia sana kwa sababu yamewagusa wengi wao lakini haya ya Mkapa tunayoambiwa ni maziuri yaliwagusa wachache tu.

Je, mmesahau ile kauli ya "Mkapa kaleta Ukapa"? Hii ilisababishwa na hali ngumu ya maisha. Sifa za WB na IMF kwa Mkapa ilikuwa ni kutaka kujisifia tu kwamba sera zao za Economic Reforms ambazo Mkapa aliamua kuzifuata kama ibada zilikuwa na mafanikio Tanzania kitu ambacho si cha kweli kabisa. Na hili siyo siri katika nchi zote duniani ambako sera za WB na IMF zilifuatwa katika nchi hizo hakukuwa na ahueni yoyote kiuchumi bali tu kuongezeka hali ngumu ya kimaisha kwa Wananchi walio wengi na ndiyo maana sera hizi za WB na IMF zimekufa kimya kimya maana sasa hivi zinapigwa vita katika nchi nyingi duniani.

Jamaa aliingia na gea kubwa sana ya kuunda tume ya Warioba ili kuchunguza rushwa, Watanzania tukapiga makofi sana. Alipokabidhiwa ripoti akaamua kuikalia kumbe alikuwa anakusanya mali kwa nafasi aliyokabidhiwa ili kujitajirisha yeye na watu wake. Cheo ni dhamana sitakitumia cheo changu kwa manufaa yangu. Na huyu Mkapa hakuona hivyo hivyo mimi nitamuona fisadi tu siku zote, kamwe hawezi kuitwa kiongozi mzuri.
 
Mvina
Ukimlinganisha Mkapa na mwungwana wa sasa, Mkapa hakamatiki. Lakini kwa vipimo vya kizalendo alivyoviacha Baba wa Taifa, basi Mkapa si lolote kama asemavyo Bubu.
Ubora wa uongozi ni relative. Kwa hali hiyo tusimlinganishe Mkapa na viongozi wachovu kama JK.

Mkuu we hapa umenena yote 9 kumi kila mmoja wetu atamalizia..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom