Rais ahusike na misiba maalum tu, bunge litunge muongozo wa Rais kuhusika na misiba

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,261
Nimeona Rais Samia anatangaza msiba wa Mwinyi (akielekeza sehemu ya hotuba yake ifutwe pasipo kujua yuko live, kwa hili kwanza kurugenzi ya mawasiliano ikulu ilitakiwa ivunjiliwe mbali na waajiriwa wote katika hicho kitengo wakiongozwa na Zuhura Yunus watimuliwe kazi).

Pia hivi karibuni Rais alikuwa mstari wa mbele katika mipango ya mazishi ya Edward Lowassa, Hata waziri mkuu Majaliwa alipofika kutoa salamu za rambirambi kwa mara ya kwanza alisema anamwakilisha Rais!

Magufuli alihusika kutangaza kifo cha mkapa na Mkapa pia alitangaza kifo cha Nyerere. Sina uhakika vifo vya makamu wa Rais na mawaziri wakuu waliopita walipofariki vilitangazwa na nani na nani alikuwa mhusika mkuu katika mipango yao ya mazishi.

Kwa maoni yangu Rais aliye madarakani angehusika kutangaza vifo vya baadhi ya viongozi tu vinapotokea tena wale ambao wanakufa wako madarakani/katika nafasi na kuwa muhusika mkuu katika misiba hiyo. Viongozi hao iwe ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mkuu wa majeshi, Jaji mkuu na Spika wa bunge tu.

Matangazo ya vifo na mipango ya misiba mengine yote hususani ya viongozi wastaafu waachiwe Msemaji wa serikali, Makamu wa Rais, Waziri mkuu na familia zao kushughulika nayo na kuwa mstari wa mbele.
 
Unadhani Rais alikuwa hajui yuko live???!! ama ulishawahi kuona taarifa ya msiba wa kiongozi mkuu wa serikali ikitolewa ikiwa recorded??
kama "alijua" yuko live KWANINI AAGIZI KIPANDE KIFUTWE ?!!

Screenshot_20220316-152322_Chrome Beta.jpg
 
Endelea kumtetea ujinga! Hujajua Kuna watu vichwani ni watupu na wanasimamia mambo muhimu yenye kuhitaji umaskini mkubwa.
Inawezekana mara mbili ya utupu wao ndio akili zako kichwani, mnang'ang'ania kujadili vitu petty badala ya mambo ya msingi, bahati nzuri wanaowatawala wanalifahamu hili
 
Nimeona Rais Samia anatangaza msiba wa Mwinyi( akielekeza sehemu ya hotuba yake ifutwe pasipo kujua yuko live, kwa hili kwanza kurugenzi ya mawasiliano ikulu ilitakiwa ivunjiliwe mbali na waajiriwa wote katika hicho kitengo wakiongozwa na Zuhura Yunus watimuliwe kazi),

Pia hivi karibuni Rais alikuwa mstari wa mbele katika mipango ya mazishi ya Edward Lowassa, Hata waziri mkuu Majaliwa alipofika kutoa salamu za rambirambi kwa mara ya kwanza alisema anamwakilisha Rais!

Magufuli alihusika kutangaza kifo cha mkapa na Mkapa pia alitangaza kifo cha Nyerere. Sina uhakika vifo vya makamu wa Rais na mawaziri wakuu waliopita walipofariki vilitangazwa na nani na nani alikuwa mhusika mkuu katika mipango yao ya mazishi.

Kwa maoni yangu Rais aliye madarakani angehusika kutangaza vifo vya baadhi ya viongozi tu vinapotokea tena wale ambao wanakufa wako madarakani/katika nafasi na kuwa muhusika mkuu katika misiba hiyo. Viongozi hao iwe ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mkuu wa majeshi, Jaji mkuu na Spika wa bunge tu.

Matangazo ya vifo na mipango ya misiba mengine yote hususani ya viongozi wastaafu waachiwe Msemaji wa serikali, Makamu wa Rais, Waziri mkuu na familia zao kushughulika nayo na kuwa mstari wa mbele.
Una miaka mingapi..?
Sorry swali liko bias sana..

Unajua sheria ya Mazishi ya Viongozi..
Rais mstaafu bado ni rais Kwahyo hakuna anayeweza kumtangaza zaidi ya Rais aliyeko Madarakani..

VIvo hivyo Waziri Mkuu au waziri Mkuu mstaafu atatangazwa na Makamu wa Rais..

Na Rais aliyeko madarakani atatangazwa na makamu wa Rais ambaye pia atakuwa Rais...

Hiyo ni sheria na sio maamuzi
 
Inawezekana mara mbili ya utupu wao ndio akili zako kichwani, mnang'ang'ania kujadili vitu petty badala ya mambo ya msingi, bahati nzuri wanaowatawala wanalifahamu hili
Umeme ni vitu petty?

Kuna wizi wa mabilioni Tamisemi ni vitu petty?

Kuna mradi upi ulio kamilika au ukioanza bajeti ya 24/25 ni vitu petty?

Boma ya Afya leo hospital binafsi ni vitu petty?

Tunajidanganya wenyewe Kwa wenyewe, 2030 ikifika nchi itakuwa imeoza.
 
Back
Top Bottom