Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

loo bongo imepigwa mnada.sasa tutaishi wapi.maana kodi ya pango itaongezeka tuu kama ilivyoanza kuongezeka garama za internate za ttcl.lakini yote haya tuliyataka wanabingo.Mungu ibariki TZ na madini yake.lakini si watu wake maana wanamzaha na maisha yao kwa kuchagua viongozi bomu
 
Bravoo mzee Butiku. Bila shaka hili ndilo suala pekee lililobaki...kama unajiona uhusiki na hali hii inabidi ujitoe mapema na uuonyeshe umma ni lipi ulilolifanya kuikosoa hali hii kama alivyofanya mzee Butiku.
 
kama aliweza kuuza mashirika ya umma chama kitamshinda kuuza?
This Guy is a businesman.

Kwani ni mchaga? oops!wachaga wenzangu nisameheni, ila jamaa yuko fasta au ndo kichingachinga,unanunua tu kwa bei yoyote bora uongeenaye mpaka mwisho.
 
19.10.2007 0123 EAT



Mkapa ang'aka


*Akataa kuzungumzia tuhuma anazoelekezewa
*Asisitiza kuwa hivi sasa ni muda wa maendeleo
*Asema alikwishastaafu masuala ya siasa nchini


Na Benedict Kaguo, RCT

RAIS mstaafu, Bw. Benjamin Mkapa, amekwepa kuzungumza na waandishi wa habari kwa kusisitiza kuwa huu sasa si wakati wa siasa, bali anaangalia zaidi masuala ya kimaendeleo na kusema alishastaafu siasa.

Bw. Mkapa alitoa kauli hiyo kwenye hoteli ya Kunduchi, Dar es Salaam jana, alikokuwa kufungua mkutano wa mwaka wa taasisi yake ya Mkapa Fellow Programme, unaojadili mafanikio yaliyofikiwa na Mfuko huo kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Waandishi wengi wa habari waliokuwapo eneo hilo, walionekana kuwa na shauku ya kutaka kupata maoni ya kiongozi huyo ambaye amekuwa akituhumiwa kuvunja kanuni za maadili wakati akiwa Ikulu.

Akionekana kufahamu shauku hiyo, Rais mstaafu Mkapa alitoa kauli hiyo wakati akihitimisha hotuba yake na alipomaliza, alisisitiza kuwa hakuwa tayari kuzungumzia masuala ya siasa.

"Tuko hapa kujadili mafanikio yaliyofikiwa na Mfuko wa Benjamin Mkapa, tangu kuanzishwa kwake Julai mwaka jana, ambapo tumejikita zaidi kutoa elimu na dawa kwa wananchi waishio maeneo ya vijijini kukabiliana na UKIMWI na si masuala ya kisiasa," alisema Bw. Mkapa.

Hata hivyo wakati akitoka ukumbini, waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari walisimama mbele yake, ili kumuuliza maswali kadhaa, lakini kiongozi huyo alionesha ishara ya kuomba apishwe apite na kwamba hakuwa tayari kuzungumza.

Juzi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Bw. Joseph Butiku, ambaye ni mmoja wa watu waliokuwa karibu na Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, alizungumza na vyombo vya habari na kushauri kuwa ni vyema Rais mstaafu Mkapa akajitokeza na kujibu tuhuma zinazoelekezwa kwake kuliko kuzinyamazia.

Kitendo cha Bw. Mkapa kukwepa kuzungumza na wanahabari jana kwa kusisitiza kuwa huu si muda wa siasa kwake, kinaweza kufasiriwa kuwa mwendelezo wa kiongozi huyo kupuuzia tuhuma zinazoelekezwa kwake.

Akizungumza awali kuhusu taasisi hiyo, Bw. Mkapa alisema imeanzishwa ili kuona Watanzania wanaoishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI, hususan waishio vijijini, wanapatiwa huduma sawa za matibabu ingawa alisema kuna upungufu mkubwa wa wataalamu wa afya katika maeneo hayo.

Alisema kupitia programu hiyo, walifanikiwa kuwa na wataalamu 99 ambapo 69 kati yao, wako katika wilaya 23 na wanatarajia kupeleka watumishi 30 zaidi katika wilaya 10 ifikapo Novemba 10 mwaka huu.

Programu hiyo imelenga kuendeleza juhudi zinazofanywa na Serikali katika mapambano dhidi ya UKIMWI.

Alisema, mfuko huo peke yake hauwezi kukabiliana na changamoto zilizopo na hivyo kwa kushirikiana na Serikali na Asasi Zisizo za Serikali, mafanikio yanaweza kupatikana.

Aliwasihi wadau wa maendeleo, kutoa nafasi za ubunifu kwa kadri watakavyoweza katika utekelezaji wa programu hiyo.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt. Deo Mtasiwa, alisema lengo la programu hiyo mbali ya kutoa mafunzo, pia ni kuajiri na kuwapeleka wataalamu kazini, kwa lengo la kusaidia jamii.

"Ninawaomba tushirikiane na kuzuia kuingiliana katika kazi moja, ili tuweze kutumia fedha na wataalamu katika kushughulikia janga hili nchini," alisema.

Alisema lengo la programu hiyo ni kutoa mafunzo, kuajiri na kupeleka wataalamu kazini kwa ajili ya kutoa huduma za kitabibu nchini.

Aliongeza kuwa programu hiyo inafadhiliwa na Serikali ya Norwei na kwa sehemu ndogo kutoka katika Mfuko wa Misaada wa Bill Clinton.


Sasa jamani, hivi kweli huyu ndiye rais wetu mstaafu tutakayeendelea kumlipa hadi mwisho wa maisha yake? Yaani akishastaafu tu anasema mabovu yangu yote msinisakame tena? Yaani anasema kuwa ni haki kwa wanasiasa kufanya mambo aliyofanya ila wakishastaafu basi game over?

Sasa itatusaidia nini kuendela kumlipa kama hata yeye mwenyewe hata hatambui nafasi yake katika jamii yetu ?

Mr Clean Huyo
 
Huyu Dawa yake ni Dola kuchukua hatua, kwa kumuweka katika One of the Safe Houses, wakati taratibu zingine zinafuatwa kumfungulia mashtaka katika mahakama kuu kwa uhujumu uchumi au , bunge ku-lift immunity yake kama ipo then kumfungulia mashtaka katika mahakama kuu kwa makosa ya kuhujumu uchumi
 
Mwenye nguvu ya dola alishasema mwacheni mzee wa watu astaafu kwa amani "mimi sina mpango wa kuwacunguza viongozi walionitangulia" Nadhani Muunguna anakwepa naye yasije mkumba yaliyomkubwa Chiluba. Bunge letu nalo halina meno maana wakipingana tuu na serikali wanaitwa kwenye kikao cha waziri mkuu kuwanyamazisha. Kudadeki!!!!!
 
Mkapa up for 6.5bn/- leadership prize

THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

THE Mo Ibrahim Foundation will next week award over $5m (approx. 6.5bn/-) to one former African head of state adjudged to have demonstrated exemplary leadership.

And Tanzania’s immediate former president Benjamin Mkapa is in the running for what organisers of the award call ’the world’s biggest prize’, designed to encourage democracy, transparency and good governance in Africa.

Mkapa - who served as head of state from 1995 to 2005 - is listed along with a dozen other African heads of state or government who left office between 2004 and 2006, and are thus automatically eligible for the cash prize.

The financial backer of the award, Sudanese businessman Mo Ibrahim - the man behind the Celtel International mobile phone network - is awarding $500,000 (650m/-) per year for 10 years, and $200,000 (260m/-) per year thereafter � for life - to the lucky winner to be officially announced at a ceremony in London on Monday.

This brings the actual value of the prize to more than $5m.

A spokesman for Mo Ibrahim said the ’long list’ of candidates in no particular order includes Mathieu Kerekou (Benin), Azali Assoumani (Comoros), Domitien Ndayizeye (Burundi), Henrique Rosa (Guinea Bissau), Maaouya Ould Sid’Ahmed Taya (Mauritania), Joaquim Chissano (Mozambique) and Sam Nujoma (Namibia).

Others also in the running for the prize are Benjamin Mkapa (Tanzania), Abass Bonfoh (Togo), Gnassingbe Eyadema (Togo), Bakili Muluzi (Malawi), France-Albert Rene (Seychelles) and Abdiqassim Salad Hassan (Somalia).

Former United Nations secretary-general Kofi Annan is joined by five other eminent individuals on the committee that will select the winner.

Other members of the committee are former Tanzanian prime minister and OAU secretary general Dr Salim Ahmed Salim; former Finland president Martti Ahtisaari; and Guinea’s former education minister and special advisor to the UNESCO director general, A�cha Bah Diallo.

Also on the panel are Nigeria’s former finance minister and foreign minister Ngozi Okonjo-Iweala; and former Ireland president and UN high commissioner for human rights, Ms Mary Robinson.

The selection committee will pick the winner after assessing every sub-Sahara African leader who has left office in the last three years on their exercise of leadership.

Mkapa is credited with keeping Tanzania on a relatively stable political course despite unrest in neighbouring countries.

He also successfully implemented broad economic reforms, secured financial aid and debt relief for Tanzania, and helped in opening up the country’s economy to foreign direct investment.

Mkapa has recently been back in the media glare in Tanzania, but for all the wrong reasons. New allegations of abuse of office have surfaced against the ex-president, who has so far chosen to remain silent.
 
Huyu Bwana Mkubwa ni Jeuri na Jeuri yake inaongezeka baada ya JK kusema kuwa hawezi kuwachunguza viongozi wastaafu kwani kufanya hivyo kunawafanya viongozi wengi kutaka kubadili katiba ya Nchi ili waendelee kutawala kwa kuogopa kushtakiwa.
Sasa kama mtu kafanya madudu wakati wa utawala wake kwanini asishtakiwe?
Sitaki kuamini kwamba JK naye alijua kuwa atafanya madudu ndio maana akamuwekea kinga Ben. kuhofia naye baadae wembe ambao angeutumia kunyolea Ben ungekuja kumnyoa yeye Pia.
Kulindana kumezidi cha msingi ni wananchi kuungana kwa pamoja na kuwatimulia mbali hawa mafisadi.

"It ain't over till it's over"
 
Huyu Dawa yake ni Dola kuchukua hatua, kwa kumuweka katika One of the Safe Houses, wakati taratibu zingine zinafuatwa kumfungulia mashtaka katika mahakama kuu kwa uhujumu uchumi au , bunge ku-lift immunity yake kama ipo then kumfungulia mashtaka katika mahakama kuu kwa makosa ya kuhujumu uchumi

Kama hataki kujibu tuhuma hizo kistaarabu basi aburuzwe kortini huko mantiki ya kusema,"Niacheni nimesttafu siasa" haina uzito kabisa. Kama alidhani kwamba akishastaafu basi maovu yake yote yatafukiwa amekwenda na maji.
 
Mkapa umekosea, amka useme na taifa
Tanzania Daima

KWA muda sasa kumekuwa na tuhuma dhidi ya rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.
Kwanza zilianza tuhuma za kutumia vibaya madaraka wakati alipokuwa kiongozi wa juu kabisa nchini.

Inadaiwa kuwa wakati akiwa rais, Mkapa alianzisha kampuni binafsi, kuisajili na kuchukua mkopo benki.

Hizi ni shughuli ambazo watu wengi wanazifanya katika maisha ya kila siku. Lakini anapofanya mtu mwenye dhamana ya kuongoza nchi, inaleta shaka, hasa ukizingatia ukubwa wa mkopo uliochukuliwa, na kasi yake ya kulipwa.

Ni vigumu sana katika mazingira ya kibiashara ya kawaida nchini, kwa mfanyabiashara kukopa sh milioni 500, na kuzirudisha katika kipindi cha miezi kadhaa. Inapokuwa shughuli za kampuni iliyotumika kukopa na kulipa hazieleweki vema miongoni mwa wananchi, shaka inaongezeka zaidi.

Imeshaelezwa kuwa si dhambi wala kosa la jinai kuanzisha kampuni na kuitumia kampuni hiyo kukopa benki.

Ni kitu ambacho kinahimizwa kila mara, kwani ndiyo njia kuu ya kuongeza mtaji. Lakini inapofikia hatua ya rais kufanya hivyo akiwa madarakani, inaleta maswali mengi.

Wengine wanamtetea Mkapa kuwa alikuwa anajiandaa atakapostaafu asiwe katika hali mbaya kiuchumi. Lakini tuna sheria ambazo zinahakikisha kuwa viongozi wakuu wastaafu, wanatunzwa vema na serikali baada ya kustaafu.

Hivi karibuni zimeibuliwa tuhuma nyingine dhidi ya Mkapa, safari hii ni kuhusiana na jinsi alivyokiongoza Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwa mwenyekiti wake wa taifa.

Tumeshawahi kusema huko nyuma kuwa kutokana na nafasi yake katika nchi, CCM ina athari kubwa kwa nchi kwa yanayotokea ndani yake. Chenyewe ndicho chama kinachotawala, kinapoharibikiwa, nchi inaharibikiwa, kwa sababu nchi inatawaliwa kutokana na sera za chama hicho.

Tuhuma kuwa uongozi wa Mkapa akiwa mwenyekiti wa CCM ulikuwa na mushkeli kiasi cha kusababisha chama hicho kupoteza dira, ni nzito.

Hili linaweza kuchukuliwa kama siasa, lakini kwa hakika si siasa, kwani kinachozungumzwa kinahusiana na hali ya taifa na mustakabali wake, kwa sababu wengi wa wanaoongoza nchi leo hii, kama si wote, wapo ndani ya CCM.

Kwa maana hiyo, iwapo ni kweli kuwa mfumo ndani ya chama hicho uliachiwa kuzaa viongozi waliopata madaraka kwa kutumia rushwa, hilo ni suala la hatari sana.

Inaweza kuwa suala hilo si sahihi, lakini ukichukulia mjadala unaoendelea sasa hivi kuhusiana na tuhuma za ufisadi, rushwa na ubadhirifu mkubwa wa mali ya taifa, ni vigumu kutoamini kuwa mfumo mbaya wa CCM kupata viongozi ndio umelifikisha taifa hapa lilipo.

Haiyumkiniki basi kwa kiongozi aliyekuwa na dhamana wakati mambo haya yanayodaiwa yakitokea, akae kimya bila kutoa maelezo yatakayowawafanya Watanzania wawe na hakika na kuwa na ufahamu wa uhalisia wa kile kinachozungumzwa hivi sasa.

Wapo baadhi ya watu walioinuka na kumtetea Mkapa, si vibaya, lakini ingekuwa vema zaidi iwapo Mkapa mwenyewe angewaeleza Watanzania, wamsikie kwa kauli yake, akitoa majibu ya tuhuma dhidi yake.

Ni yeye mwenyewe ndiye aliasisi sera ya ukweli na uwazi enzi za uongozi wake. Hatuamini kuwa alianzisha sera hiyo ili aitumie atakapokuwa katika uongozi tu.

Kama mtu aliyewahi kushika madaraka makubwa kabisa nchini, Mkapa ataendelea kuwa kiongozi wa Watanzania hadi mwisho, atake asitake. Hivyo, bado anawajibika kuitekeleza sera yake ya ukweli na uwazi.

Sisi hatutaki kuamini katika tuhuma zinazotolewa dhidi yake, lakini kwa kuangalia mambo yanayotokea na aina ya ushahidi unaotolewa, tunakuwa katika nafasi ngumu sana ya kuamua nini ukweli wa kinachosemwa.

Tunaamini kuwa Watanzania wengi wapo katika kundi hili na mtu pekee atakayewasaidia kuondoka katika hali hiyo ni Mkapa mwenyewe. Tafadhali baba, inuka useme na taifa.
 
Mwacheni mzee BWM apumzike kwa amani.

Kasema kastaafu siasa, nyie mnataka nini?

Kasema hatojibu masuala ya kisiasa, sasa?

Kama alivyosema JK, muacheni apumzike. Nauliza ni nani aliye msafi kati yenu awezaye kumrushia MKapa jiwe?!
 
Hivi mambo yaliyotokea pakistani jana hayawezekani tanzania kwa watu kama hawa??? Msinielewe vibaya ni mtazamo tu.
 
Huyu Bwana Mkubwa ni Jeuri na Jeuri yake inaongezeka baada ya JK kusema kuwa hawezi kuwachunguza viongozi wastaafu kwani kufanya hivyo kunawafanya viongozi wengi kutaka kubadili katiba ya Nchi ili waendelee kutawala kwa kuogopa kushtakiwa.
Sasa kama mtu kafanya madudu wakati wa utawala wake kwanini asishtakiwe?
Sitaki kuamini kwamba JK naye alijua kuwa atafanya madudu ndio maana akamuwekea kinga Ben. kuhofia naye baadae wembe ambao angeutumia kunyolea Ben ungekuja kumnyoa yeye Pia.
Kulindana kumezidi cha msingi ni wananchi kuungana kwa pamoja na kuwatimulia mbali hawa mafisadi.

"It ain't over till it's over"
Zee la shamba,
Kweli kabisa tunahitaji kuungana, lakini kama una hizo mbinu za kuungana au mbinu nyinginezo zile ni bora uzielezee hapa hapa. Kwani ukisema tu 'kuungana' bila kuonyesha mechanism yake ni statement iliyo too general. Basi miye nakuomba kama unaweza kuelezea mechanisms za kufanikisha hili uzitaje pia. Ahsante.

SteveD.
 
Mwacheni mzee BWM apumzike kwa amani.

Kasema kastaafu siasa, nyie mnataka nini?

Kasema hatojibu masuala ya kisiasa, sasa?

Kama alivyosema JK, muacheni apumzike. Nauliza ni nani aliye msafi kati yenu awezaye kumrushia MKapa jiwe?!

Uchafu unatofautiana, na makosa yanatofautiana. Leo hii wewe ukinifinya kwenye mkono je, utaniruhusu miye kukukata bega lako kwa kulinyofoa kwa panga?!

Hata kama hakuna msafi katika jamii, hii haimaanishi kuwa mambo yaende kishagalabagala kwani hakuna aliye msafi. Two wrongs don't make it right. Kama katika jamii kila mmoja ni mchafu basi kila mmoja apokee adhabu yake kulingana na uchafu wake. Yule anaye 'nuka kinyesi' awe flushed na 'treated water za magari ya FFU' na yule mwenye kucha chafu, 'akatwe kucha hizo kwa wembe butu'.

SteveD.
 
Oooh, by the way Kichuguu, nili 'kumiss' kichizi mzee wangu wa busara. Nashukuru Mungu kuwa umerudi tena jamvini na ninakutakia kila kheri na baraka katika familia yako ili usipotee tena 🙂

SteveD.
 
Mwacheni mzee BWM apumzike kwa amani.

Kasema kastaafu siasa, nyie mnataka nini?

Kasema hatojibu masuala ya kisiasa, sasa?

Kama alivyosema JK, muacheni apumzike. Nauliza ni nani aliye msafi kati yenu awezaye kumrushia MKapa jiwe?!

Mwinyi alikuwa head wakati wa kuuza Loriondo, mpaka mwandishi Stan Katabalo akafariki katika kinachohisiwa kuendana na tukio hilo baada ya kuwashikia bango,

Mkapa achunguzwe, Kikwete pia anatakiwa kujibu yale alitoyafanya akiwa waziri wa nishati, Nani atasimamia uchunguzi huu? Nani atasalimika?

MH! Sielewi!
 
Mwacheni mzee BWM apumzike kwa amani.

Kasema kastaafu siasa, nyie mnataka nini?

Kasema hatojibu masuala ya kisiasa, sasa?

Kama alivyosema JK, muacheni apumzike. Nauliza ni nani aliye msafi kati yenu awezaye kumrushia MKapa jiwe?!

Sielewi kwa nini anazichukulia hizi tuhuma kama mambo ya kisiasa wakati yana implications nyingi tu.
 
Oooh, by the way Kichuguu, nili 'kumiss' kichizi mzee wangu wa busara. Nashukuru Mungu kuwa umerudi tena jamvini na ninakutakia kila kheri na baraka katika familia yako ili usipotee tena 🙂

SteveD.

It's friday dude....whatchu got goin' on...?
 
Back
Top Bottom