William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,464
Hmmm! Mtetezi wa mafisadi na wala rushwa! dawa yenu iko jikoni.
Baadaye watapewa wainywe ikiwa imeiva!
Baadaye watapewa wainywe ikiwa imeiva!
Kinachozungumzwa hapa ni kuwa viongozi wa nchi, hawapaswi kujihusisha na biashara. Wana JF, kamwe hawasemi Baregu na Jenerali ni watu safi. Hata kama Baregu na Jenerali wangelikuwemo kwenye serikali na wakati huo huo wanafanya biashara wangepewa vidonge vyao. Hoja ya msingi hapa ni kwamba unapokuwa kiongozi mwenye dhamana kubwa ya kuliongoza taifa hupaswi kujiingiza katika mambo ya biashara. At one time, the conflict of interest would be inevitable. Huwezi kutumikia mabwana wawili na kuwatimizia haja zao kwa wakati mmoja!
Mkuu Mwanamalundi,
Heshima mbele, Salute na sasa you made my day saaa ya kulala nitakuona kesho, I mean hii ndio tunaita,
Where We Dare Kumkoma Nyani Mchana Kweupe Kwa Mwendo Wa Mdundo!
Mkuu Masatu,
Ni ndugu mmoja huko nyuma niliyekuwa ninamjibu aliyemfananisha Clinton na Mkapa, nikasema na ninarudia kuwa ni kweli wanafanana sana waliyoyafanya, meaning maovu kwa mataifa yao, lakini ya Clinton yanavumilika, kuliko ya huyo mwingine,
Anyway, heshima mbele na good debate, keep it up na msimamo imara wa kusimamia hoja, au unachokiamini, maana tunawahatiji sana hapa JF, wenye misimamo kama yako!
Sawa mkuu unajua ktk maisha watu wote ambao hutumia kamusi huwa ndio wenye upeo mdogo kwani kamusi hutumika tu pale unaposhindwa kuelewa maana.
Neno FISADI tunalitumia kila siku ktk maisha yetu hata kama kamusi haipo ndio maana nikasema hata mtoto mdogo asojua kusoma anafahamu maana ya nenoi hili. Ukiwa hujui kusoma ina maana bado unaweza kutoa tafsiri ya neno hili bila kamusi.
Pili, sikuipata tafsiri ya neno hili ktk Taarabu ila nimekupeleka wewe upate kujua matumizi ya neno hili.. kwa sababu ulidai ushahidi.. sasa huo ushahidi niutoe wapi?..ndio maana nikasema hapa nilipo siwezi hata kutoa ushahidi wa jinsia yako kwani hili sii jambo naloweza kuwa nalo mkononi na wala haihusiani kabisa na hoja. Kisha mjomba maana ya neno na matumizi ya neno ni vitu viwili tofauti!.. ijue lugha yako.
Kiswahili lugha nyepesi sana isipokuwa tunaweza kujichanganya sisi wenyewe. Fisadi ni character inayotokana na neno la kiarabu Fasad... na kweli ina maana nyingi lakini maana zote zinahusu mtu mbaya mharibifu na kamwe haiwezi kuhusiana na Kutongoza unless mwandishi alikuwa akizungumzia kuhadi kuwa ni fisadi nayo pia bado haileti matumizi mazuri ya neno hili.
Nimemaliza...
Usiwe na wasiwasi mkuu nachukua maneno yako mwenyewe kama ulivyosema kuwa hapa JF hakuna kutishana ila tunataka issue na kumkomalia nyani giledi!. Ikiwa hilo neno sio tusi nakuomba ulipokee kama ulivyolipamba!
Pili, neno Kiwembe, hapana mjomba Kiwembe tazama tena kamusi itakupa jibu... na kama ktk mipasho kiwembe maana yake ni mtu anayeharibu akikata kama wembe ndivyo ilivyotumika... hilo la totoz ni kiswahili cha bara ama kimepitwa na wakati kama vile tulivyokuwa tukisema chai ya rangi!.
Duh! ama kweli mzee wangu mbishi... hivi unaamini kabisa kuwa kiwembe kimetumika ktk wimbo huo kama mtu wa totoz?..
Mshikaji mwenzako nafunga kati ya 50 kiumri na nimekitumia kiswahili hicho nikiwa shule ya msingi!.. ushahidi gani zaidi unataka!
Hata hivyo kulingana na madai yako, tafsiri ya kiwembe haisemi hivyo ktk kamusi sasa mbona wabishana na wataalam wa kiswahili?.. Anyway nakuacha dogo, mshindi wewe turudi kwa Mkapa!... Field marshal ES anakusubiri kwa hamu.
Pili, neno Kiwembe, hapana mjomba Kiwembe tazama tena kamusi itakupa jibu... na kama ktk mipasho kiwembe maana yake ni mtu anayeharibu akikata kama wembe ndivyo ilivyotumika... hilo la totoz ni kiswahili cha bara ama kimepitwa na wakati kama vile tulivyokuwa tukisema chai ya rangi!.
Sawa wewe endelea na tafsiri yako ambayo haikubaliani na matumizi ya Fisadi ktk kuwataja hawa viongozi wachafu na wahujumu uchumi. Na nadhani hapo upo peke yako Tanzania nzima... wewe mjuzi wa lugha..
Sisi tunaamini kuwa hawa viongozi ni MAFISADI kwa maana yetu sasa kama wewe utaendelea kufikiria kuwa tunasema wao ni malaya na watongozaji endelea kufikiria hivyo na kamusi yako.
Hata mifano unashindwa kuelewa inatumika vipi yaani unachotazama wewe ni kiini macho cha lugha. Mbona usizungumzie LIVE ama KAA si yote lughha safi ya kamusi?. Sikukupa neno moja nimeweka mengi upate picha acha kufahamu lakini ndio badooo..
Imefahamika kwamba hadi mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) na Rais wa Awamu ya tatu Benjamini Mkapa alingatuka Juni 2006, alikuwa ameshindwa kuongoza chama na tayari alikuwa amekibinafsisha kwa matajiri.
habari zilizolifikia Mwanahalisi wiki hii zinasema kushindwa huko kwa Mkapa na ubinafsishaji huo wa CCM kwa matajiri ulikuwa unajulikana kwa wajumbe wote wa Kamati kuu na Halmashauri kuu (NEC) ya chama hicho.
Udhaifu wa Mkapa ktk kukiongoza chama hicho unadaiwa kuanza zamani baada ya kukamata chama hicho mwaka 1996.
Habari zinasema udhaifu huo ulizidi kujibainisha wazi katika mkutano mkuu wa CCM wa mwaka 2002. na kipindi cha kuelekea mchakato wa uteuzi wa mgombea urais kwa kiteti ya chama hicho mei mwaka 2005.
Ktk baru yake ya kurasa 14, ya tarehe 10 Aug 2005 yenye kumbukumbu Na. MNF/AD/37 aliyombwandikia Mkapa na nakala yake kusambazwa kwa wajumbe wa kamati kuu ccm na wenyeviti wote wa mikoa wa ccm katibu mtendaji wa mfuko wa Mwalimu Nyerere (MNF) Joseph Butiku anasema pamoja na mambo mengine " CCM sasa imeanza safari ya kuelekea kwenye kifo chake. imekumbatia jambo ovu, Rushwa, ambayo imeua viongozi wazuri wengi. Vyama vya siasa na serikali makini duniani.
CCM imeanza kushindwa kusema na kutetea haki na ukweli. Imeanza kuvumilia na kutetea ubaguzi. Imeanza kuwa CCM ya viongozi wafanyabiashara wasioonyesha nia thabiti ya kujali maadili ya chama chetu na taifa letu" alisema Batiku.
Hili ni tatizo la mwenyekiti maana yeye ndiye mwenye dhamana ya kutoa na huruhusu matumizi ya ushahidi usiokusanywa na vyombo vya taifa vilivyoteuliwa kufanya kazi hiyo.
Butiku anasema sasa wana CCM wengi na wananchi wengine wanao wasiwasi na nchi kununuliwa na wenye fedha kupita viongozi wa CCM.
Anauliza "Hivi kuna ushahidi fedha nyingi zinazotumika ktk uchaguzi huu zinatoka wapi? Ni za nani? Hao wanaozitoa wanayo malengo gani kwa Tanzania na Watanzanai?