Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

......................Hata kama alileta mabadiliko ya haraka sana, kitu ambacho mimi sikubaliani nacho, Tanzania hatuna sheria inayosema kwamba kiongozi wa nchi anayeleta 'mabadiliko ya haraka sana' atasemehewa maovu yake yote ya kuwafisadi na kuwaibia Watanzania


Sipingani na mawazo yako kwani kila mtu ana wazo na anatakiwa asikilizwe. Lakini nchi haiwezi kuendeshwa dreams za kila mmoja. Haiwezi kuwa nchi. Hata hivyo kurudi kwenye point yako hapo juu ....nadhani ndiyo maana sheria ya kwamba alichotenda Rais akiwa madarakani hakiwezi mpeleka mahakamani. Kipengere nadhani hakitofuatishi issues za kimadaraka, biashara binafsi, kampuni au hata kuua. Ila kinasema akiwa madarakani (I stand to be corrected here with a strong augument). Kwani wewe Bubu unadhani kwanini waliweka hii kipengere?!
 
Hata kama alileta mabadiliko ya haraka sana, kitu ambacho mimi sikubaliani nacho, Tanzania hatuna sheria inayosema kwamba kiongozi wa nchi anayeleta 'mabadiliko ya haraka sana' atasemehewa maovu yake yote ya kuwafisadi na kuwaibia Watanzania

- Strong argument, kipengere kinamlinda rais na maamuzi ya kiserikali sio ya uporaji mali za wananchi.
 
Mkuu Field Marshall ES;

Heshima mbele; Kwa hili la Mh. Mkapa naomba nitofautiane na wewe na Niwe kwenye kambi yakina Gembe etc!!! Kama nilivyosema Katiba haijazuia afunguliwe kesi akiwa amefanya kosa kama yeye binafsi.

Hoja yangu imejikita kwenye Utengamano wa Taifa!


Nchi hii ambayo inasifika kwa utulivu... (yes, nimesema utulivu sijasema amani) ni miongoni mwa nchi ambazo ziko vulnerable sana na mambo fulani fulani... hivyo amani kupotea haraka sana sio jambo la ajabu hapa Tanzania. mifano ya vulnerabilities nyingi za nchi yetu ni issue ya Dini, Siasa etc. Wakati mambo kama Ukabila na Usehemu mtu anapotoka hayana nguvu ya kuporomosha taifa... isipokuwa tu... sehemu kama unaongelea Unguja na Pemba

Mifano ya Mataifa yaliyopata misukosuko kwa kumshitaki Rais mstaafu ni Zambia... etc.

Best Practices:
Majirani zetu walikuwa na uhalali mkubwa sana wa Kumshitaki Mh. Daniel Arap Moi, ambaye alikuwa na kashfa nzito sana tena sana... lakini hawakufanya hivyo kwa ajili ya mstakabali wa Taifa lao.

Kumshitaki Mh. Rais Mstaafu Mkapa... sio jambo rahisi, kumbuka wanadamu wana mioyo... na kumbuka Jamii yetu... inaweza kugeuzwa kimawazo kirahisi sana huenda kuliko jamii nyingi sana... rejea uchaguzi wa 2005(Imani waliyokuwa nayo Wananchi juu ya Mh. Kikwete); 1995(Imani waliyokuwa nayo wananchi juu ya Mzee wa Kiraracha);

Ikumbukwe kwamba Mh. Mkapa alikuwa na Record nzuri ya utendaji... ikumbukwe pia Marais hawa wawili wanatoka Dini tofauti, ikumbukwe akitokea Mchungaji au Sheikh... akapandikiza kwamba hili linafanyika kwa chuki... ya dini, waaumini wataitikia AMEN/AMIN. hapatakalika hapa nchini kwetu.

Mwisho tujadili namna ya kumfanya mtanzania afanye kazi angalau 4hours a day, ili ajitosheleze kwa chakula na aweze kuwa taxable... ana eventually awezekuwa pensionable.

Mwisho:
Ni jambo lililo wazi kwamba at least mlioko hapa kwenye jamvi hili mna uelewa mzuri zaidi kuliko waheshimiwa wengine ambao hata kompyuta hawajawahiiona... of course wapo wachache wazuri zaidi, sasa kama sisi tunataka kutoana macho,,, pamoja na kwamba hatuonani je... kwa watu mitaani itakuwa je? Matusi yaliyoandikwa already hapa kuhusu hili suala... maneno kama mpuuzi,etc... ni miongoni mwa viashiria kwamba hili si jambo rahisi.


Mungu Mbariki Mkapa apumzike vyema Rais Wetu Mstaafu!
Mungu Ibariki Tanzania.
 
- Strong argument, kipengere kinamlinda rais na maamuzi ya kiserikali sio ya uporaji mali za wananchi.

Hapo bado utata. Uporaji ni kufanyeje? Kujiuzia Kiwira kwa bei ya chini? nini comments zako kuhusu TBL, NBC etc? Angekuwa yeye kanunua angekuwa amepora, au siyo! Yeye kama raia wa nchi, kama ulivyo wewe na mwingine, anao uhuru wa kufanya atakacho ikiwemo biashara. Sheria haimzuii kufanya biashara. Na wale wanaosema alifanya akiwa Ikulu, alitakiwa aende wapi ndiyo akafanye?
 
- Mkuu unapoteza muda bure tu na hizi rangi zako nakuona kwenye hii thread unavyojichanganya, huko nyuma ulisema Mama Kilango ndiye mwenye matatizo na Mkapa kwa sababu ya kukosa urais, na since then unabadilika rangi tu maneno yako ni yale yale ukadai hivi ni vita vya kifamilia,

Mkapa hajipendi mwenyewe maana angekua anajipenda asingepora mali za taifa akiwa Ikulu, sheria lazima ifuate mkondo wake kwenye hili hakuna suluhu.


Hayo mengine ya kujichanganya kwangu siyo issue ya kubishana.

Suala ambalo tunakubaliana mimi na wewe ni kwamba sheria lazima ichukue mkondo wake. Lakini kwa nini sheria iende kwa Mkapa peke yake na isiende kwa Kikwete wakati na yeye alitajwa kwenye list of shame?

Hapo ndipo nilipokuja na maoni kwamba kwa sababu katiba yetu ni mbovu na viongozi wana madaraka makubwa tunajenga kautamaduni kakujipendekeza. Fikiria watu wanataka kwenda bungeni kumtungia sheria mtu mmoja yaani Mkapa huoni kama wanasiasa wanatufanya kama sisi hamnazo. Waende bungeni watunge katiba ambayo itaondoa kinga kwa marais wanapovurunda. Mbona Clinton alichunguzwa wakati ni rais. Kwa nini tusubiri mpaka rais asitaafu ndiyo tuanze kujifanya tunataka utawala bora. Utawala bora uwe wakati tunapoongozwa maana hicho ndicho kipindi wanachotuibia. Hawatuibii wanapokuwa wamestaafu. Kwa hiyo badala ya kufikiria kukamata wezi lazima tutunge katiba ambayo itafanya wezi wasiibe.
 
Mimi pia sina mengi ya kuandika mkuu!Lakini niweke angalizo tu.Wakuu nyinyi endeleeni na mchakato wa kumburuza mkapa mahakamani na endeleeni kumshawishi Kikwete ili abadili msimamo wake.Lakini yote hayo yakikamilika basi mjiandae na kusambaratika kwa taifa la tanzania.

Yaleyale ya "Ukimshtaki fisadi nchi itatikisika" taifa lisambaratike yeye nani kwani?? Hamna lolote, hata akishtakiwa na kufungwa bado maisha yatakwenda kama kawaida. Historia tu ndo itabadilika kwa kuongeza kipengele hiki!!

Haya ndio mambo yanayoturudisha nyuma siku zote, hatuna ujasiri wa kuchukua hatua kwa mambo ya kimsingi tunasubiri yaharibike kabisa au tunaacha na kubaki tunalalamika tu chini ya miti
 
Bubu, hizi stories za kumshtaki Mkapa ni porojo tu. Bahati mbaya sana hata wasomi hawagundui kuwa ni porojo. Kwa Rais wa nchi ile yetu, hakuna anayefanana na Mkapa so far. Watu wote wanaangalia kwenye ANBEN, KIWIRA na source ya UFISADI ila hawaangalii kuhusu uchuni ya nchi yetu na mabadiliko ya haraka sana Tanzania kipindi chake.

Binafsi, so far sijamuona rais kama Mkapa kwa Tanzania. Mkapa was the best president of TZ and and will remain so in records for many years. Hakuna kuchekacheka na very serious person. Of course bila kuwa kama vile tusingeweza hata kuc-chat hapa kwenye JF. Ali-open up kila kitu, vingine vinawafanya watu wajichanganye kwa vile wao wanataka. Mimi nashauri kuwa alitakiwa apewa another 10 years watu wajue uchumi imara maana ni nini!.


Zaidi ya hiyo, hizi politics za bei ya vitu kwa investors, by the way sijui kama watu wamewahi kujiuliza watu kama Abrahamovich na na mwenzake mwenye kampuni ya Yukos walinunua kwa bei gani zile kampuni kule Russia na kwanini?! How do we compare with Tanzania? Russia ni mfano mmoja, iko kibao, lakini Russia tunafanana kwa na uchumi wa aina moja (state controlled) kabla ya collapse ya USSR.


Mambo ya mafisadi, hata Kikwete akiondoka tutawaona wengi tu. Mbona enzi za mwinyi kulikuwa kuchafu zaidi lakini kwa kuwa press freedom ilikuwa ndogo hatukuweza kujua na kufanya kama sasa. Unakumbuka ambushi ya Mrema airport na yake majina? Umewahi uliza whose names were they?

Mimi nadhani tusiwe na jazba tu kuwa Mkapa aende mahakamani. Tujumuishe mambo kadhaa ambayo ni mazuri. Vinginevyo tunaweza jikuta tunashangilia tu kama soccer fans ambao kila wakati wanategemea team yao ishinde. Ikishindwa unafukuza coach!

Kuimarisha uchumi ilikuwa ni wajibu wake na vilevile aliomba uongozi kwa kuahidi hivyo!! Ndio kazi aliyoomba. Hiyo haitoshi kumfanya avunje sheria, kuimarisha uchumi haikuwa ndio warranty ya kumfanya afanye mambo atakavyo kama vile uporaji mkubwa wa mali za umma na kufanya bishara ikulu kama ilivyokuwa
 
- Ndio maana nilisema kwamba huyu Shujaa wangu Dr. Slaaa apewe nafasi ya kugombea urais huko Chadema, hata asiposhinda ataaamsha sana wanachi walioko usingizini,

Dr. Slaaa heshima mbelee shujaaa, hapa tupo ukurasa mmoja.


Wasiwasi uliopo ni kuwa anaweza asishinde kutokana na agenda namba moja ya chama tawala na hivyo kupelekea kukosa kiti bungeni na kuua nguvu ya upinzani! Hata hivyo Mh anafaa sana!
 
Enyi watanzania,

Tusiwe wajinga kiasi cha kutumiwa na watu wa manufaa yao,Na nawaomba sana huku nikitumia nguvu za ziada kuonya na kuwaambia tusiwe chujio la kuchuja yale ya wanasiasa wa maji taka.

Kwa kifupi,kuamua kumpeleka Mkapa Mahakamani ni kuangamaiza taifa hili.wananchi wenzangu Ndiyo itakuwa mwanzo wa kuanguka kwa CCM na kuanguka kwa CCM kutapelekea nchi hii kuyumba .

Nasema mie simo na tuendelee kumuombea Dr. Slaa!

Hamna lolote CCM ikianguka maisha yataendelea kama kawaida vyama vingapi vikubwa vilianguka na nchi zinakwenda. Tena ndo tutaanza kijipanga upya na kila atakayepewa madaraka atajua cheo ni dhamana, hayupo juu ya sheria wala uongozi sio mradi wa familia!
 
Enyi watanzania,

Tusiwe wajinga kiasi cha kutumiwa na watu wa manufaa yao,Na nawaomba sana huku nikitumia nguvu za ziada kuonya na kuwaambia tusiwe chujio la kuchuja yale ya wanasiasa wa maji taka.

Kwa kifupi,kuamua kumpeleka Mkapa Mahakamani ni kuangamaiza taifa hili.wananchi wenzangu Ndiyo itakuwa mwanzo wa kuanguka kwa CCM na kuanguka kwa CCM kutapelekea nchi hii kuyumba .

Nasema mie simo na tuendelee kumuombea Dr. Slaa!

Ingependeza kama ungetuweka wazi ili tujue ni kwa vipi Taifa litatetereka! Nafikiri la msingi mheshimiwa asipelekwe kizimbani katika misingi ya kukomoana.Haipendezi kuona viongozi wa aina flani flani ndio wanapelekwa mahakamani wengne wanaachwa.Kama wamefanya makosa wawe awamu ya tatu au ya nne wote wapelekwe.Hapo tutaona haki ndio imelengwa na si kukomoana!
 
Bubu, hizi stories za kumshtaki Mkapa ni porojo tu. Bahati mbaya sana hata wasomi hawagundui kuwa ni porojo. Kwa Rais wa nchi ile yetu, hakuna anayefanana na Mkapa so far. Watu wote wanaangalia kwenye ANBEN, KIWIRA na source ya UFISADI ila hawaangalii kuhusu uchuni ya nchi yetu na mabadiliko ya haraka sana Tanzania kipindi chake.

Binafsi, so far sijamuona rais kama Mkapa kwa Tanzania. Mkapa was the best president of TZ and and will remain so in records for many years. Hakuna kuchekacheka na very serious person. Of course bila kuwa kama vile tusingeweza hata kuc-chat hapa kwenye JF. Ali-open up kila kitu, vingine vinawafanya watu wajichanganye kwa vile wao wanataka. Mimi nashauri kuwa alitakiwa apewa another 10 years watu wajue uchumi imara maana ni nini!.

Bila shaka mwanao alivaa joho wakati wa mahafali ya kindergaten(vidudu)
 
It was the same Nyerere who said CCM siyo baba au mama yake. And for your info CCM madhubuti no longer exists. Ask Makamba.

who is makamba in CCM?he aint nothing to me to you and eveyone who knows properly about this Country.

Furaha ya Wapinzani kushuhudia CCM inaanguka ili japo wapate nafasi ya kutawala




 
You never know,anaweza kuwa pandikizi na yuko kwenye payroll ya jamaa!
Dr. Slaa,
Mkuu kama utasimama imara ktk hili basi kura yangu umeipata..yaani nahitaji nini zaidi kutoka kwako!.hata sioni, labda hilo Azimio la Zanzibar..
-Dr. Slaa for President!
 
Naona tunapoteza mwelekeo hapa... ishu ni huyu mtu Mkapa kwanini asifikishwe kwa pilato kwa makosa yalioainishwa na Rev,,,, hayo ya kafanya kazi ya kujenga shule, sijui kukusanya kodi ni kutimiza wajibu,...kwanza kazi aliiomba mwenyewe. Na nasisi watanzania tulimuhakikishia maisha mazuri for life kwa kutumia kodi yetu, kama malipo ya kutimiza wajibu wake kwa taifa... tuache blah blah hapa, madudu ya Mkapa ni mengi, yame overwhelm mazuri machache(yapo)...kwa walio yasahau, pengine kutokana na kufaidi asali ya hayo madudu yake..... nawawekea tena hapa kwa mujibu wa Rev. kwa uchache ni....

  • Benki Kuu na kashfa zote; Meremeta, Epa, CIS, Tangold, Minara na menginewe.
  • Miundombinu na Nishati: ATC, TRL, Rada, IPTL, Richmond, Kiwira, Ndege ya Rais, Helikopta za Jeshi na mengine.
  • Demokrasia butu: uonevu kwa vyama vya siasa na wafuasi wa vyama ambavyo si CCM, kwa kutumia nguvu ya dola kama kule Pemba, mauaji ya Mwembechai, kufilisi au kutoza ushuru na kodi ya kukomoa kwa mwenye kuipinga CCM na Serikali ya Mkapa na mengineyo.
  • Uwekezaji: Mikataba mibovu, sheria mbovu ambazo zinawapendelea wawekezaji na kulipunguzia Taifa mapato
.

Makosa mauaji ya wananchi Pemba nadhani itakuwa vyema kama yatapelekwa mahakama ya kimataifa The Hugue.
Chini ya utawala wa Ben Tanzania kwa mara ya kwanza ilizalisha wakimbizi
 
Tanzania siku moja itakuwa bila Zitto, Slaa, Mrema, Mkapa, Kikwete, CCM, Chadema, ect kama ambavyo leo Tanzania haina Nyerere na nchi haijalipuka. Wakati wa Nyerere pia tuliambiwa BILA yeye nchi itawaka moto. Tukaimba na ngonjera, mashairi, nyimbo na kucheza ngoma "....bila wewe Tanzania ingalikuwaje?" Ipo.
Mie nilishasema, (kwanza naunga mkono uzawa) wale Wahindi wa EPA waachiwe na waombwe Msamaha. Kamata MIPINGO wote waliosaida au kusababisa ufisadi huo. Hata kama Nchi italipuka, wacha iwake maana NO MOVEMENT, NO FRICTION. Nafikiri hata Kikwete akisoma au akisikia kuwa Mwenzake Mkapa anaweza kushitakiwa, yeye ajue mwaka 2010 (Mwakani???? Ahhh bado siku mbili) tutakuwa na uzoefu wa kupandisha Marais mafisadi kizimbani.

NB: Yes, Slaa for Prezidaaaaa......
 
hata mimi. Wewe uliibuka uchi?

Nilikuwa najua nikivaa nguo za kawaida na siyo Joho ni kuwa SIKO UCHI. Mhhhh, maadamu sijawahi kuvaa JOHO, nimegundua kuwa tangu nizaliwe niko uchi. Nimefurahi kujua, ngoja nikanunue leo nguo (joho) ili nisiwe uchi.
 
Nilikuwa najua nikivaa nguo za kawaida na siyo Joho ni kuwa SIKO UCHI. Mhhhh, maadamu sijawahi kuvaa JOHO, nimegundua kuwa tangu nizaliwe niko uchi. Nimefurahi kujua, ngoja nikanunue leo nguo (joho) ili nisiwe uchi.


Serious matter as this should not be mixed with celibrity; where you can talk UGORO-hapa watu wanakata vitu vya akili mnaleta mizaha; tumerogwa na nani?

Anyway "NO ONE IS ABOVE TH LAW; HUO UTETEZI NI WA MUDA TU ILA SOON LATER SI BEN/JK/ANYBODY LATER WATAPELEKWA LUPANGO KWA MAKOSA"-TUJIPE MUDA na SLAA BIG UP SANA-SONGA MBELE NDIYE MKOMBOZI WA WANYONGE ALIYEBAKI
 
Mbona iko mifano kibao ya nchi marais kupelekwa mahakamani na hakuna kusambaratika kulikotokea. Hapo Zambia tu Chiluba yalimkuta hayo. na bado hakuna tatizo la utaifa. Kwenye makosa hakuna utaifa hata siku moja.

Shauriyako wewe unaeamini kwenye uongozi uliopita. mtu kama kakosea lazima ale adhabu yake.
 
Originally Posted by Sikonge
Nilikuwa najua nikivaa nguo za kawaida na siyo Joho ni kuwa SIKO UCHI. Mhhhh, maadamu sijawahi kuvaa JOHO, nimegundua kuwa tangu nizaliwe niko uchi. Nimefurahi kujua, ngoja nikanunue leo nguo (joho) ili nisiwe uchi.


Serious matter as this should not be mixed with celibrity; where you can talk UGORO-hapa watu wanakata vitu vya akili mnaleta mizaha; tumerogwa na nani?

Umejiroga mwenyewe. Mwenzako anaongea serious issues. Soma kwa makini na elewa points zake.
 
Back
Top Bottom