Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Serious matter as this should not be mixed with celibrity; where you can talk UGORO-hapa watu wanakata vitu vya akili mnaleta mizaha; tumerogwa na nani?

Mawingu-Miguu aka Malunde-malundi,
Mwenye macho haambiwi tazama. The film six sence, the boy say "there are some people they don't know that they are dead..."
 
Originally Posted by Sikonge
Nilikuwa najua nikivaa nguo za kawaida na siyo Joho ni kuwa SIKO UCHI. Mhhhh, maadamu sijawahi kuvaa JOHO, nimegundua kuwa tangu nizaliwe niko uchi. Nimefurahi kujua, ngoja nikanunue leo nguo (joho) ili nisiwe uchi.


Serious matter as this should not be mixed with celibrity; where you can talk UGORO-hapa watu wanakata vitu vya akili mnaleta mizaha; tumerogwa na nani?

Umejiroga mwenyewe. Mwenzako anaongea serious issues. Soma kwa makini na elewa points zake.

Ongea point; dont spin and think of redirecting the issue;Yes serious issue in B-grade celebrity understood;

NO ONE ABOVE THE LAW; NA NCHI HAITATIKISIKA ILA WAO MAFISADI WATATIKISIKA NA KUPATA PRESHA KAMA WAZEE WA VIJISENT YANAYOWATOKEA LAKIN TANZANIA WILL REMAIN; NYERERE KAIACHA ISIWE HAWA MAFISADI-EBO
 
Taifa haliwezi kusambaratika kwa kufuatilia wezi na kurudisha mali walizoiba,wizi kama huu wa mkapa ndio unaosababisha wakati mwingine Jeshi kuchukua Nchi kama Serikali iliopo haifuatilii wezi na wahujumu wa mali za Taifa.Mkapa alidhani baada ya kumzika Mwalimu Nyerere kusingekuwa na kikwazo kwa lolote atakalofanya.Angalia alianza kwa kuweka Lowassa(Kiongozi wa Mafisadi) kwenye baraza la mawaziri wakati Nyerere alikwisha mwambia hafai.Ule uadilifu aliokuwa nao kabla ya Mwalimu akautumia kama kivuli cha kujifichia wakati anaiba,wajanja wote wa ufisadi kama Mramba,Yona,Chenge,Lowassa,Rostam,Megji,Balali,Hosea,Mahita na wengine aliwaweka kwenye nafasi nzuri za kuweza kuiba kivyao ili wasiweze kumfuatilia,lakini Mungu amewafichua wote sasa wasishughulikiwe warudishe mali walizoiba?Lazima warudishe mali walizoiba hatakama siyo sasa lakini siku ipo watakapopatikana Viongozi wenye uchungu hasa na Nchi hii inayofilisiwa mchana kweupe.Wezi hawa mishahara na marupurupu yao wakiwa kazini yanajulikana,sasa je mali walizonazo zinalingana na hivyo vipato vyao?
 
Mkuu Field Marshall ES;

Heshima mbele; Kwa hili la Mh. Mkapa naomba nitofautiane na wewe na Niwe kwenye kambi yakina Gembe etc!!! Kama nilivyosema Katiba haijazuia afunguliwe kesi akiwa amefanya kosa kama yeye binafsi.

Hoja yangu imejikita kwenye Utengamano wa Taifa!


Nchi hii ambayo inasifika kwa utulivu... (yes, nimesema utulivu sijasema amani) ni miongoni mwa nchi ambazo ziko vulnerable sana na mambo fulani fulani... hivyo amani kupotea haraka sana sio jambo la ajabu hapa Tanzania. mifano ya vulnerabilities nyingi za nchi yetu ni issue ya Dini, Siasa etc. Wakati mambo kama Ukabila na Usehemu mtu anapotoka hayana nguvu ya kuporomosha taifa... isipokuwa tu... sehemu kama unaongelea Unguja na Pemba

Mifano ya Mataifa yaliyopata misukosuko kwa kumshitaki Rais mstaafu ni Zambia... etc.

Best Practices:
Majirani zetu walikuwa na uhalali mkubwa sana wa Kumshitaki Mh. Daniel Arap Moi, ambaye alikuwa na kashfa nzito sana tena sana... lakini hawakufanya hivyo kwa ajili ya mstakabali wa Taifa lao.

Kumshitaki Mh. Rais Mstaafu Mkapa... sio jambo rahisi, kumbuka wanadamu wana mioyo... na kumbuka Jamii yetu... inaweza kugeuzwa kimawazo kirahisi sana huenda kuliko jamii nyingi sana... rejea uchaguzi wa 2005(Imani waliyokuwa nayo Wananchi juu ya Mh. Kikwete); 1995(Imani waliyokuwa nayo wananchi juu ya Mzee wa Kiraracha);

Ikumbukwe kwamba Mh. Mkapa alikuwa na Record nzuri ya utendaji... ikumbukwe pia Marais hawa wawili wanatoka Dini tofauti, ikumbukwe akitokea Mchungaji au Sheikh... akapandikiza kwamba hili linafanyika kwa chuki... ya dini, waaumini wataitikia AMEN/AMIN. hapatakalika hapa nchini kwetu.

Mwisho tujadili namna ya kumfanya mtanzania afanye kazi angalau 4hours a day, ili ajitosheleze kwa chakula na aweze kuwa taxable... ana eventually awezekuwa pensionable.

Mwisho:
Ni jambo lililo wazi kwamba at least mlioko hapa kwenye jamvi hili mna uelewa mzuri zaidi kuliko waheshimiwa wengine ambao hata kompyuta hawajawahiiona... of course wapo wachache wazuri zaidi, sasa kama sisi tunataka kutoana macho,,, pamoja na kwamba hatuonani je... kwa watu mitaani itakuwa je? Matusi yaliyoandikwa already hapa kuhusu hili suala... maneno kama mpuuzi,etc... ni miongoni mwa viashiria kwamba hili si jambo rahisi.


Mungu Mbariki Mkapa apumzike vyema Rais Wetu Mstaafu!
Mungu Ibariki Tanzania.


Kama tulikuwa tunawaza pamoja mkuu.Jamani,amani ya tanzania iko delicate sana linapokuja suala la imani.Kumkamata Mkapa siyo sawa na kumkamata Mgonja,Yona au Mramba.Mkapa bado ana influence kubwa sana kuanzia ndani ya ccm na taifa kwa ujumla.Na wakuu mjue kwamba hii kamatakamata tu iliyoanza imeshazua manung'uniko mengi sana ya chinichini.Kuna watu bado wanaona huku si kudeal na ufisadi bali ni kafara inayofanywa kwa watu fulani kwa uonezi pale mtu kama Karamagi anapokingiwa kifua na wakulu ili asiburuzwe mahakamani.
Na hebu tuwe macho wakuu na hawa wanasiasa waliokosa sera wamebaki kuviziavizia tu.
 
Kama tulikuwa tunawaza pamoja mkuu.Jamani,amani ya tanzania iko delicate sana linapokuja suala la imani.Kumkamata Mkapa siyo sawa na kumkamata Mgonja,Yona au Mramba.Mkapa bado ana influence kubwa sana kuanzia ndani ya ccm na taifa kwa ujumla.Na wakuu mjue kwamba hii kamatakamata tu iliyoanza imeshazua manung'uniko mengi sana ya chinichini.Kuna watu bado wanaona huku si kudeal na ufisadi bali ni kafara inayofanywa kwa watu fulani kwa uonezi pale mtu kama Karamagi anapokingiwa kifua na wakulu ili asiburuzwe mahakamani.
Na hebu tuwe macho wakuu na hawa wanasiasa waliokosa sera wamebaki kuviziavizia tu.

Amani yetu haiko delicate, amani yetu utakuwa delicate pindi mafisadi kama Mkapa na wenzake wakiachwa huku wakiwa wametubia mabilioni ya pesa zetu. Tanzania hatuna tabaka katika sheria zetu, mafisadi na wezi wote ndani ya nchi yetu hawana tofauti mbele ya pilato hata kama walikuwa na nyadhifa kubwa kiasi gani. Msilete dhana isiyokuwapo eti amani yetu iko delicate hivyo mafisadi waachwe waendelee kupeta tu. Nchi yetu haipati maendeleo yoyote yale kutokana na waroho wa utajiri wa haraka haraka kama akina Mkapa, halafu mnatafuta visingizio visivyokuwa na vigezo vyovyote vile kwamba amani yetu iko delicate kwa hiyo waachiwe waendelee kula mali waliyotuibia bila kuguswa.

Kamwe amani yetu haitamarika kwa kuwa na matabaka mawili mbele ya sheria ya wale wasiokuwa na nyadhifa zozote na wale tuliowamni na kuwapa nafasi za uongozi lakini wakatumia uaminifu wetu kwao kujitajirisha kwa njia za haramu.
 
Amani yetu haiko delicate, amani yetu utakuwa delicate pindi mafisadi kama Mkapa na wenzake wakiachwa huku wakiwa wametubia mabilioni ya pesa zetu. Tanzania hatuna tabaka katika sheria zetu, mafisadi na wezi wote ndani ya nchi yetu hawana tofauti mbele ya pilato hata kama walikuwa na nyadhifa kubwa kiasi gani. Msilete dhana isiyokuwapo eti amani yetu iko delicate hivyo mafisadi waachwe waendelee kupeta tu. Nchi yetu haipati maendeleo yoyote yale kutokana na waroho wa utajiri wa haraka haraka kama akina Mkapa, halafu mnatafuta visingizio visivyokuwa na vigezo vyovyote vile kwamba amani yetu iko delicate kwa hiyo waachiwe waendelee kula mali waliyotuibia bila kuguswa.

Mkuu,nisome vizuri.Nasema amani iko delicate linapokuja swala la imani.Kama watu wa imani fulani wanadhani wanaonewa katika jambo fulani na wa imani nyingine kupendelewa basi hapo mwisho wa siku hapatakalika kwa vyovyote.
Nilimaanisha hivyo.
 
Date::12/29/2008
Sitta: Nitapokea hoja binafsi dhidi ya Mkapa
Jackson Odoyo
Mwananchi

SPIKA wa Bunge la Muungano, Samwel Sitta ameongeza chachu katika mjadala wa kumuondolea kinga Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, baada ya kueleza kuwa yuko tayari kupokea na kujadili hoja binafsi za wabunge ili ikiwezekana kiongozi huyo wa serikali ya awamu ya tatu apandishwe kizimbani.

Tayari mawaziri wawili wa Mkapa, Basil Mramba na Daniel Yona, pamoja na katibu mkuu wa wizara, Gray Mgonja wameshafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia vibaya ofisi wakati wakiwa mawaziri, lakini bado baadhi ya watu wanataka rais huyo mstaafu apandishwe kizimbani kwa makosa aliyoyafanya akiwa Ikulu.

Mbunge wa Karatu, Dk Wilibrod Slaa ametangaza nia yake ya kuwasilisha hoja binafsi katika kikao kijacho cha Bunge la Muungano, kutaka Mkapa afikishwe mahakamani akidai kuwa suala hilo halihitaji kiongozi huyo wa zamani kuondolewa kinga kama wasomi walivyoshauri, huku kiongozi wa upinzani bungeni, Hamad Rashid akisema ameshaandaa hoja binafsi ya kumuondolea kinga Mkapa.

Na Spika Sitta alikuwa na maneno mazuri kwa wabunge hao wawili na watu wengine wanaoshinikiza kutekelezwa kwa suala hilo.

"Nitatilia maanani hoja yoyote inayomhusu Mkapa itakayofikishwa mezani kwangu na kuiruhusu ijadiliwe ndani ya Bunge," alisema Sitta.

"Bunge bado lina nafasi ya kujadili suala la Rais Mkapa na kulitolea maamuzi kama bunge... na wala mlango haujafungwa kuhusu hoja binafsi itakayotolewa, hivyo kama kuna mbunge yeyote mwenye hoja kuhusu suala hilo anaruhusiwa kuiwasilisha mezani kwangu siwezi kukataa kuipokea."


Lakini Spika Sitta akakumbusha utaratibu wa kuwasilisha hoja bungeni. "Kabla ya hoja hiyo kujadiliwa rasmi bungeni, kuna kamati ya uongozi ambayo hukutana na kuijadili na ikibainika kwamba hoja iliyowasilishwa imejitosheleza na inastahili kujadiliwa, hufikishwa mbele ya wabunge kwa ajili ya mjadala huo," alisema.

Spika Sitta alisema moja ya kanuni za bunge kuhusu hoja yoyote inasema kwamba "hoja lazima ijitosheleze na iwe na uhusiano na suala husika" na kama itajitosheleza kamwe hawezi kufungiwa mlango.

"Kwanza kabla ya mtoa hoja hajawasilisha hoja yake anatakiwa awe na mtandao na wabunge wenzake na wakubaliane ili iwe rahisi kwa hoja yake kuungwa mkono na wenzake bungeni na itakapobainika kwamba, hoja hiyo ina nguvu na imeungwa mkono na wabunge wengi, basi bunge linaweza kubadili katiba na hatimaye Rais huyo Mstaafu akashitakiwa kama raia yeyote ndani ya nchi,"alifafanua Sitta.

Spika Sitta aliongeza kuwa hatua ya pili ambayo mwasilisha hoja anatakiwa kuzingatia ni suala la kanuni za bunge, katiba ya nchi na sheria zilizopo na kwamba hayo yote yakitekelezwa na hoja ikajitosheleza kulishawishi bunge kufanya marekebisho ndani ya katiba yeye kama Spika ama mtu mwingine hawezi kupingana na maamuzi hayo ya bunge.

Alionya kuwa mtoa hoja asipozingatia mambo hayo badala yake akaamua kutoa hoja kwa jitihada zake binafsi huku akijiami kwamba, anaweza kulishawishi bunge kwa kutumia nguvu ya hoja zake, anaweza asifanikiwe hata kama kamati yake ya uongozi itaipitisha hoja hiyo.

Dk Slaa anasema suala la Mkapa kufikishwa mahakamani halihitaji kuondolewa kinga kwa maelezo kuwa tuhuma zinazomkabili za kufanya biashara akiwa Ikulu hazihusiani na nafasi yake kama rais bali mtu binafsi.

Lakini Rashid aliiambia Mwananchi jana kuwa ameshaandaa hoja hiyo na sasa anatafuta kuungwa mkono.

"Kwanza ninampongeza Dk Slaa kwa uamuzi wake wa kujiandaa kuwasilisha hoja hiyo... na mimi natarajia kwamba tutakapokutana na wabunge wenzangu, akiwemo Dk Slaa, tutajadiliana suala hilo ingawa nimeshamaliza kuandika hoja yangu kuhusu marekebisho ya katiba ili Mkapa aweze kushitakiwa pamoja mambo mengine ndani ya nchi kama vile marekebisho ya mikataba feki," alisema Rashid na kuongeza:

"Ili Rais ashtakiwe ama kuondolewa kinga, inabidi katiba ibadilishwe na hivyo ninaamini kwamba, kwa hoja zetu safari hii wabunge watazikubali hasa ikizingatiwa kwamba suala la Mkapa ni kilio cha wananchi cha muda mrefu."


Aliongeza kwamba katiba ina mapungufu mengi na moja ya mapungufu hayo ni kuwapa viongozi nguvu ya kutoshtakiwa na kwamba, katiba hiyo hiyo pia inajipinga yenyewe katika baadhi ya vipengele vyake.
 
Mkuu,nisome vizuri.Nasema amani iko delicate linapokuja swala la imani.Kama watu wa imani fulani wanadhani wanaonewa katika jambo fulani na wa imani nyingine kupendelewa basi hapo mwisho wa siku hapatakalika kwa vyovyote.
Nilimaanisha hivyo.

Ni sawa kabisa Mkuu, kama kutaonekana kuna upendeleo katika kuwachunguza watu mbali mbali ambao kuna tuhuma nzito dhidi yao kutokana na wao kuwa wana mtandao na walimbeba JK kwa namna moja au nyingine kuingia Ikulu basi hapo kutakuwa na mtafaruku mkubwa sana ambao unaweza kuingiza nchi katika matatizo makubwa. Ndiyo maana nimesema kusiwe na matabaka yoyote yale katika hizi kesi dhidi ya mafisadi. Karamagi naye kuna ushahidi tosha kwamba amesaini mikataba ya uchimabji wa dhahabu ambayo imtuingizia Watanzania hasara kubwa sana hivyo na yeye achunguzwe na kufikishwa mahakamani ili sheria ifuate mkondo wake bila upendeleo wowote ule.
 
wandugu,

..nadhani hoja isiwe kumuondolea kinga Mkapa, badala yake hoja iwe kuwaondolea kinga Maraisi wote wastaafu.

..kuna mchangiaji aliwahi kueleza kwamba sheria inapotungwa na Bunge utekelezaji wake huwa ni kwa makosa yaliyofanyika baada ya sheria kutungwa, siyo kabla ya hapo.

..ni kwasababu hiyo hapo juu, na kuondoa manung'uniko ya uonevu wa aina yoyote ile, napendekeza hoja ya kuondoa kinga isiwe dhidi ya Mkapa tu, bali hata Maraisi waliopita, na wa baada yake.

NB:

..kuhusu Karamagi kusaini mkataba wa madini ambao si mzuri, je mkataba huo una tofauti gani na mikataba mingine ya madini? huu mkataba aliosaini Karamagi una kama miaka 2 hivi. kama ni hasara sidhani kama ni kubwa kuliko mikataba ambayo imekuwepo muda mrefu.

..kwa nini ashitakiwa Karamagi peke yake, na siyo mawaziri wengine wa madini na nishati waliopata kusaini mikataba ya madini? kuwakumbusha tu baadhi ya mawaziri waliomtangulia Karamagi na kama ifuatavyo: Jakaya Kikwete, Andrew Shija, Abdalah Kigoda, Maokola Majogo, Daniel Yona, Dr.Msabaha.
 
NB:

..kuhusu Karamagi kusaini mkataba wa madini ambao si mzuri, je mkataba huo una tofauti gani na mikataba mingine ya madini? huu mkataba aliosaini Karamagi una kama miaka 2 hivi. kama ni hasara sidhani kama ni kubwa kuliko mikataba ambayo imekuwepo muda mrefu.

..kwa nini ashitakiwa Karamagi peke yake, na siyo mawaziri wengine wa madini na nishati waliopata kusaini mikataba ya madini? kuwakumbusha tu baadhi ya mawaziri waliomtangulia Karamagi na kama ifuatavyo: Jakaya Kikwete, Andrew Shija, Abdalah Kigoda, Maokola Majogo, Daniel Yona, Dr.Msabaha.

Issue ya Karamagi ni Rahisi sana, watoa hoja walitaka ashitakiwe kesi ya Rushwa ati kisa kusaini mkataba London... lakini kisheria ikaonekana ni upuuzi... kwa kuwa hakuna sheria iliyowahi sema kwamba Mkataba usainiwe Lithuli street au Magogoni street, au ndani ya nchi!!!

Kuhusu ushauri, ilionekana pia amefuata ushauri aliopewa... issue nyingine ni kwamba tatizo lilikuwa sheria iliyoko... sio yeye... in short hajaenda tofauti na sheria ya madini ya 1998... ambayo wabunge wenu wanaolala bungeni muda wote waliipitisha na kusainiwa na mh. Rais wa Jamhuri.


Mkapa asipelekwe maakamani!
 
Issue ya Karamagi ni Rahisi sana, watoa hoja walitaka ashitakiwe kesi ya Rushwa ati kisa kusaini mkataba London... lakini kisheria ikaonekana ni upuuzi... kwa kuwa hakuna sheria iliyowahi sema kwamba Mkataba usainiwe Lithuli street au Magogoni street, au ndani ya nchi!!!

Kuhusu ushauri, ilionekana pia amefuata ushauri aliopewa... issue nyingine ni kwamba tatizo lilikuwa sheria iliyoko... sio yeye... in short hajaenda tofauti na sheria ya madini ya 1998... ambayo wabunge wenu wanaolala bungeni muda wote waliipitisha na kusainiwa na mh. Rais wa Jamhuri.


Mkapa asipelekwe maakamani!

Mkapa aanze kutafuta lawyer tu, kama alifikiri Watanzania tutanyamaza kimya kwa ufisadi mkubwa uliofanyika akiwa madarakani na yeye kuhusika kwa namna moja au nyingine ikiwamo mabilioni ya EPA, Kuuza nyumba za serikali kwa hasara ya $200 millioni, kusaini mikataba ya uchimbaji dhahabu isiyo na maslahi, kuwaleta net group bila idhini ya Watanzania, ununuzi wa ndege ya Rais, rada, magari na helicopters za jeshi, kukwapua mgodi wetu wa Kiwira na kufanya biashara akiwa Ikulu basi ameula wa chuya. Tumechoka na mafisadi wanaojivisha ngozi ya uongozi ili kuifisadi Tanzania mchana kweupe.
 
Mkapa aanze kutafuta lawyer tu, kama alifikiri Watanzania tutanyamaza kimya kwa ufisadi mkubwa uliofanyika akiwa madarakani na yeye kuhusika kwa namna moja au nyingine ikiwamo mabilioni ya EPA, Kuuza nyumba za serikali kwa hasara ya $200 millioni, kusaini mikataba ya uchimbaji dhahabu isiyo na maslahi, kuwaleta net group bila idhini ya Watanzania, ununuzi wa ndege ya Rais, rada, magari na helicopters za jeshi, kukwapua mgodi wetu wa Kiwira na kufanya biashara akiwa Ikulu basi ameula wa chuya. Tumechoka na mafisadi wanaojivisha ngozi ya uongozi ili kuifisadi Tanzania mchana kweupe.


Sasa umeanza kubadilisha mashtaka. Ukibadilisha mashtaka kutoka ANBEN kwenda kwenye hiyo list hapo juu ina maana hata JK anahusika!
 
Hivi kweli Karne hii, bado kuna mtu mwenye AKILI TIMAMU ambaye bado anaamini kwamba mtu mmoja akipelekwa mahakamani nchi itayumba? Really?? Huyu mtu ana nini hasa, amelifanyia nini taifa letu? Please lets be serious, for our own sake. This argument is just to abuse the intellect of majority Tanzanians. YAANI KWELI KUNA MTU ANAAMINI KWAMBA MKAPA AKIPELEKWA MBELE YA SHERIA KUJIBU TUHUMA DHIDI YAKE NCHI ITAYUMBA? NO WONDER HATA WAKENYA WENZETU WANATUDHARAU. Harafu tunataka utawala wa sheria? Au tunakuwa tunamaanisha nini....au sheria ni kwa wanyonge tuu?

Are we aware kwamba Tanzania ina watu zaidi ya million 38? So who is Mkapa? Kwanini watu mnaogopa Mkapa kupelekwa Mahakamani? kama hana hatia si sheria hiyo hiyo itamweka huru?

Mkapa srewed ALL HIS chances of being regarded as a smart elder statesman. The allegations against him are just too much for him to withstand the current scrutiny. By the way, I can assure you, hata Mkapa asipopelekwa na Kikwete mahakamani leo au kesho.... Iko siku atatokea Kiongozi mwenye mapenzi ya kweli na nchi yake...na katika kutafuta muarobaini wa matatizo yetu...atauliza..HOW DID WE GET HERE IN THE FIRST PLACE? And Mkapa will be in the statistics of culprits. Trust me you!

Reality is: Mkapa ana maswali mengi ya kujibu mbele ya watanzania. Mengi yameandikwa humu. Kifupi: HE BETRAYED THE TRUST OF POOR TANZANIANS.

We should all know, Tanzania siyo Mkapa, ilikuwepo kabla yake na itakuwepo long after he is gone. Mimi ni kati ya wale wanaoamini kwamba Tanzania ni ya watanzania wote. Na WATANZANIA WOTE TUNA THAMANI. haiwezekani raia wote tuwe abused na mtu mmoja harafu wanakuja watu wachache kutwambia kwamba Mkapa akipelekwa mahakamani nchi itayumba! Since when did we start politics of personalities. No body is indispensable in our country. Not even Nyerere could EVER claim that, sembuse Mkapa. Kama aliiba apelekwe ajibu mashtaka. Sheria iliyomuweka Yona na Mramba mahabusu, ni sheria hiyo hiyo iliyowaweka huru. So is Mkapa.

By the way hapa hakuna vendetta wala chuki dhidi ya Mkapa. Actions speak loud. Kila siku madudu yanafumuka na yanamlenga yeye. hata mikataba..ambayo ilifichwa...siku hizi yote imeanikwa hata ambao hatukusoma Mlimani tunaona ujinga uliofanywa...Those who want to play vendetta card against Mkapa..I would say..you have run out of options. Tatizo la Tanzania...wananchi tumekuwa gizani mda mrefu..lakini ukweli ni kwamba....

BAADHI ya Viongozi wetu wamekuwa MAJUHA wa siku nyingi..ni wezi wa kutupwa, sema tulikuwa gizani hatujui lolote........na sasa kwa vile tunaanza kuwagundua..hatuna budi kupambana nao. MAPAMBANO NI MAGUMU. NO DOUBT. BUT WE HAVE TO START FROM SOMEWHERE.

Mkapa must account for his actions. If he is innocent, The law will exonerate him. Not otherwise.
 
Ben aondolewe kinga ili iwe fundisho kwa maraisi wengine ata Mwl ALISEMA IKULU NI MAHARI PATAKATIFU sasa Ben AKAPAGEUZA SEHEMU YA BIASHARA.
Keep it up Dr SLAA ktk ilo
 
Yeye kama raia wa nchi, kama ulivyo wewe na mwingine, anao uhuru wa kufanya atakacho ikiwemo biashara. Sheria haimzuii kufanya biashara. Na wale wanaosema alifanya akiwa Ikulu, alitakiwa aende wapi ndiyo akafanye?
Mkuu utakuwa unakosea sana kuhusu suala la muheshimiwa kufanya biashara akiwa Ikulu. Yule bwana hakuchaguliwa kwenda ikulu kuwa CEO wa biashara zake binafsi; biashara aliyotakiwa kwenda kufanya pale ni kuwapatia faida wale waliompeleka ambao ni wananchi. Kama alikuwa na haja sana ya kuwa mjasirimali, basi angeendelea tu na biashara zake bila ya kuja kwetu sisi kutaka kura.
Hatukumuweka pale kama BWM, alikuwa pale kama Rais wa jamhuri ya Muungano wa tanzania, na kama ukipitia katiba ya nchi, inaeleza vizuri tu ni majukumu gani rais wa nchi anatakiwa afanye, biashara binafsi halimo, hivyo kila biashara ya kujinufaisha kama Benjamin Mkapa ilikuwa ni batili....Just a common sense tu hapo.
 
Mkapa angelikuwa kijana tungelimwambia kuwa "Andaa Vaseline ........" te teteteee
 
Kama tulikuwa tunawaza pamoja mkuu.Jamani,amani ya tanzania iko delicate sana linapokuja suala la imani.Kumkamata Mkapa siyo sawa na kumkamata Mgonja,Yona au Mramba.Mkapa bado ana influence kubwa sana kuanzia ndani ya ccm na taifa kwa ujumla.Na wakuu mjue kwamba hii kamatakamata tu iliyoanza imeshazua manung'uniko mengi sana ya chinichini.Kuna watu bado wanaona huku si kudeal na ufisadi bali ni kafara inayofanywa kwa watu fulani kwa uonezi pale mtu kama Karamagi anapokingiwa kifua na wakulu ili asiburuzwe mahakamani.
Na hebu tuwe macho wakuu na hawa wanasiasa waliokosa sera wamebaki kuviziavizia tu.

Influence kwa taifa? Labda ya kifisadi. Ufisadi ambao ndio hasa vita iliyoko mbele yetu. Kushinda vita hii ni muhimu kukata kichwa cha ufisadi: Che Nkapa.

We want Chinga's head in the court (Kisutu) as soon as possible.
 
Mkuu utakuwa unakosea sana kuhusu suala la muheshimiwa kufanya biashara akiwa Ikulu. Yule bwana hakuchaguliwa kwenda ikulu kuwa CEO wa biashara zake binafsi; biashara aliyotakiwa kwenda kufanya pale ni kuwapatia faida wale waliompeleka ambao ni wananchi. Kama alikuwa na haja sana ya kuwa mjasirimali, basi angeendelea tu na biashara zake bila ya kuja kwetu sisi kutaka kura.
Hatukumuweka pale kama BWM, alikuwa pale kama Rais wa jamhuri ya Muungano wa tanzania, na kama ukipitia katiba ya nchi, inaeleza vizuri tu ni majukumu gani rais wa nchi anatakiwa afanye, biashara binafsi halimo, hivyo kila biashara ya kujinufaisha kama Benjamin Mkapa ilikuwa ni batili....Just a common sense tu hapo.



kujibu kauli yako: Hivi wewe unadhania finance and support kubwa ambayo Lowassa and company waliyompatia Jk kwenda ikulu ilikuwa bure bure! Tatizo Lowassa ni kumba kumba na mrafi wa ghafla ghafla. Ile bond tungeishangaa after 10 years.


Juzi juzi Jk and company wamekodisha TRC kwa wahindi kwa mkataba fake. Reason kubwa- ni kuwa wataalamu wa reli waliwadanyanga investors kuhusu halisi halisi ikiwemo uhai wa mabehewa/engines na kwahiyo wahindi hawakuandaa fungu la kutosha kwa kuendeleza hayo (very stupid)!. Matokeo yake Pinda kuepusha aibu anawabeba wahindi wazi wazi kwa kisingizio cha kuwasaidia wafanyakazi ambao ni wajibu wa RITES huku waalimu na wanafunzi vyuo vikuu wanaambia hakuna hela!. Je hizi hela za kuwapa wahindi wanazichukua wapi na kwa mpango upi? Je tunahitaji kumshitaki JK na Pinda wake baada ya dakika 90 kwa huu uhuni?! Bado hatujui hatma ya Richmond, Buzwagi, ATCl etc zote hizi zikiwa ni JK creation. Tutahitaji kuwashitakia hawa after their tenure?

Kwa hiyo, Kuhusu huyu "Serious man, Ben", wabongo ni Jazba na wivu tu kama kawaida yetu. Sheria zote za TZ zinasema kila mtu hana kosa mpaka apatikane nalo. Sasa hili la kusema Ben kaiba nani katoa hukumu na wapi? Halafu ni nani kasema Mramba na Yona wameisababishia serikali hasara? Hakuna hata mmoja mpaka itakapoamuliwa na mahakama kuwa ni hivyo. Inaweza kula kwa serikali tukala hasara zaidi. Until then, let is shut up and work hard for our prosperity!
 
kujibu kauli yako: Hivi wewe unadhania finance and support kubwa ambayo Lowassa and company waliyompatia Jk kwenda ikulu ilikuwa bure bure! Tatizo Lowassa ni kumba kumba na mrafi wa ghafla ghafla. Ile bond tungeishangaa after 10 years.


Juzi juzi Jk and company wamekodisha TRC kwa wahindi kwa mkataba fake. Reason kubwa- ni kuwa wataalamu wa reli waliwadanyanga investors kuhusu halisi halisi ikiwemo uhai wa mabehewa/engines na kwahiyo wahindi hawakuandaa fungu la kutosha kwa kuendeleza hayo (very stupid)!. Matokeo yake Pinda kuepusha aibu anawabeba wahindi wazi wazi kwa kisingizio cha kuwasaidia wafanyakazi ambao ni wajibu wa RITES huku waalimu na wanafunzi vyuo vikuu wanaambia hakuna hela!. Je hizi hela za kuwapa wahindi wanazichukua wapi na kwa mpango upi? Je tunahitaji kumshitaki JK na Pinda wake baada ya dakika 90 kwa huu uhuni?! Bado hatujui hatma ya Richmond, Buzwagi, ATCl etc zote hizi zikiwa ni JK creation. Tutahitaji kuwashitakia hawa after their tenure?

Kwa hiyo, Kuhusu huyu "Serious man, Ben", wabongo ni Jazba na wivu tu kama kawaida yetu. Sheria zote za TZ zinasema kila mtu hana kosa mpaka apatikane nalo. Sasa hili la kusema Ben kaiba nani katoa hukumu na wapi? Halafu ni nani kasema Mramba na Yona wameisababishia serikali hasara? Hakuna hata mmoja mpaka itakapoamuliwa na mahakama kuwa ni hivyo. Inaweza kula kwa serikali tukala hasara zaidi. Until then, let is shut up and work hard for our prosperity!

Duh! ama kweli bado kuna watu wana mawazo ya mwaka 47!!!! Eti wabongo ni wivu na jazba tu!!! Labda ulinufaika kwa namna moja au nyingine na ufisadi wa fisadi Mkapa ndiyo maana unamkingia kifua kwa nguvu zote na hutaki kuona ushahidi chungu nzima uuliokuwepo dhidi ya fisadi Mkapa. Hakuna atakayeshut up, wewe ni nani katika Tanzania mpaka utuamrishe umma wa Watanzania tu shut up!!! Watu wengine bwana!!!! wanapenda kujipa madaraka wasiyokuwa nayo!!! Hajatwambia JK tushut up sembuse wewe!!!!

Na kwa taarifa yako tu ni kwamba Watanzania hatuna wivu wala jazba kwa Mtanzania yeyote yule au hata mgeni aliyejipatia mali zake ndani ya Tanzania kwa njia za halali, lakini tuna usongo wa hali ya juu kwa Watanzania au wageni ambao wanajilimbikizia mali chungu nzima kwa njia za haramu au kwa kutuibia mali zetu au kusaini mikataba mibovu yenye maslahi ya juu kabisa kwa wageni na isiyokuwa na chochote kwa Watanzania. Tumechoka nchi yetu kufanywa shamba la bibi.

Katika nchi yenye utawala bora hakuna yeyote yule ambaye anastahili kuwa juu ya sheria. Kama kafanya madhambi ambayo yameliingizia hasara Taifa kubwa basi ushahidi ukusanywe dhidi yake na kisha kufikishwa kwa pilato na akionekana ana hatia basi asote lupango kwa miaka mingi tu na kufilisiwa pia afilisiwe. Hili litarudisha imani ya Watanzania katika serikali yao. Mwambie fisadi hana pakutorokea maana za mwizi ni arobaini.
 
Back
Top Bottom