Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Nachekelea kwani hoja ya kumuondolea kinga mkapa ikipelekwa bungfeni itapita bila shida.Jamaa alikandamiza wabunge vibaya wakati wake. Vile vikao vya kuwekana sawa kwa wabunge wa CCm enzi zile, alikuwa akiwapa vitisho na ukandmizaji mbaya sana.Ndio maana bunge enzi zake nilikuwa halifai..watu hofu tupu. Usidhani walipenda...jamaa lilikuwa dictator.
U smart wa Mkapa mimi si uoni, akiondlewa kinga ameula wa chuya. Mwalimu angekuwepo angempigia debe asiondolewi kinga, si unajua yy ni wa kubebwa?
Personaly, Rais ambaye alini disappoint ni mkapa...hasa kwenye uwekezaji wa sector ya madini. Hopelessly and intentionaly aliamua kuwapa wageni resouces zetu for free!!! I hate the guy.Angalia anajiuzia mgodi kwa Tsh 700m! kwani alikuwa anunua nyumba buguruni? Halafu kalipa only 10%! (70m). Asipofikishwa mahakamni basi nchi yetu imeoza. he deserves it. Period!
 
Pasco,
Mkuu samahani kidogo kwani ile sahihi ya rais ktk hukumu ya Kifo huja kabla la mahakama ya rufaa!.. Mimi nilidhani rais huwa ndio mtu wa mwisho kabisa kusamehe ama kusaini... akianguka wino ni masaa au dakika tu kwa mtu kunyongwa..naomba ufafanuzi na shria hiyo kusema kweli sifahamu.

Pili, wanabodi wenzangu - Pamoja na maelezo ya kutia nguvu ya Pinda, ningependa kujua hiyo katiba Ibara ya 46(3) ambayo inazuia kumshtaki Rais mstaafu, kulingana na Takukuru inasema exactly kama walivyosema wao:- Kuwa, Isipokuwa kama ataacha, kushika madaraka ya Rais kutokana na masharti ya ibara 46 a (10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.

Kama ndivyo, basi tumeliwa wajomba katiba inatakiwa kufanyiwa marekebisho makubwa na wale wote wanaotetea kutorekebisha kifungu cha katiba kinachomlinda rais na msaafu, wasitokee kabisa kuweka lawama zao kuhusiana na Mkapa au rais yeyote kwa sababu huwezi kupika keki ukataka kula mwenyewe!..
Kwa niko New Dheli, India nikirudi home nitafanya mapitio makabrasha yangu ila la Mkapa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria halihitaji kubadilishwa kwa katika ni suala la ufafanuzi tuu.
Rais ndio mtu wa mwsho kupelekewa hukumu za kifo baada ya taratibu zote za mahakama kukamilika. Nyerere alinyonga 2. Mwamwindi na muuaji wa Karume. Mwinyi alinyonga 16 sina majina. Mkapa hakunyonga hata mmoja na Jk bado hajanyonga. Kuna shinikizo kubwa kufuta adhabu ya kifo retrorespectively ili walioshahukumiwa wasemehewe na kuna wanaotaka hao jamaa wapewe haki yao kwa kunyongwa kuliko kuendelea kusota magerezani.
 
Mama,
Binafsi nimeshindwa kutenganisha vitu ambavyo unaweza kusema ni vya maslahi ya Taifa au maamuzi yake mwenyewe ikiwa matendo yake yanaendana na Maazimio ya taifa ambayo hayamteganishi yeye kama rais na raia wa kawaida..

Haijalishi anaishi humo au ndipo ofisi yake ilipo. Kuchaguliwa kuwa rais ni wajibu alipewa kutumikia wananchi, je inakuwaje akajitumikia mwenyewe badala ya kuwatumikia wananchi i.e kuwa mjasiria mali badala ya kuwawezesha wananchi wake kuwa wajasiria mali?

Kama rais anaruhusiwa kuwa mjasiria mali, je anatakiwa kufuata taratibu za ujasiria mali ? Hilo Azimio la Zanzibar limeelezea vipi kuhusu conflicts of interests kwa viongozi watakaotaka kuwa wajasiria mali ?

Kama rais anaweza kuwa mjasiria mali, kwa nini anapewa incentives za life time ilhali anaweza kubangaiza akiwa ikulu na hata baada ya kuondoka ikulu?

Kwa maana hiyo basi, tutegemee kila rais atakayeingia madarakani kutoka na chake kwa mgongo wa ujasiria mali?

Hapo ndipo mimi nafikiri tumepigwa bao hasa nikizingatia kwamba Azimio la Zanzibar lilimpa ruksa yeye na viongozi wote nchini kuwa Wajasiamali..
This can happen only in Tanzania, pale viongozi wanapoongozwa na tafsiri zao binafsi za sheria husika.
 
Pasco,
Rais ndio mtu wa mwsho kupelekewa hukumu za kifo baada ya taratibu zote za mahakama kukamilika. Nyerere alinyonga 2. Mwamwindi na muuaji wa Karume. Mwinyi alinyonga 16 sina majina. Mkapa hakunyonga hata mmoja na Jk bado hajanyonga. Kuna shinikizo kubwa kufuta adhabu ya kifo retrorespectively ili walioshahukumiwa wasemehewe na kuna wanaotaka hao jamaa wapewe haki yao kwa kunyongwa kuliko kuendelea kusota magerezani.
Duh, mkuu sasa naona umekwenda mbali sana na maswala ya hukumu za kifo..Hivi kweli Mkapa angemyonga nani kisheria wakati yeye ndiye aliyekuwa haramia...Hiyo sinema kweli ingekuwaje!
Kina Nyerere walivyonga kwa sabu hakuna mtu anayetakiwa kuwa above the law!.. Mkapa is above the law.
Mimi nakubalina na TzPride, na Mkapa alini disappoint kwa sababu huyu kwa macho yangu alikuwa na kila sifa ya kiongozi bora.. Nilikuwa wa kwanza kufurahia kuondoka kwa Mwinyi lakini yaliyofuata from 2000 mkuu wangu aibu tupu tena basi kafanya makusudi wala sio mapungufu ama bahati mbaya..
 
Mama,
Nasikitika kusema kwamba Azimio la Zanzibar halikatazi chochote zaidi ya Ruksa kwa viongozi kupora mali. Kuhus Conflict of interest halikutazama wala kufikiria ndio maana umeona wakitumaliza ktk kila sekta..
Hawa ndio watunga sheria, wanaotakiwa kulinda maslahi ya Taifa na ndio wao leo hii wanabishana.. kama ingekuwa amri yangu Mkapa siku nyingi yuko Lupango. Ni katiba na maazimio kama haya ndio yanamweka hata Mugabe kutawala Zimbabwe..
 
Mama,
Nasikitika kusema kwamba Azimio la Zanzibar halikatazi chochote zaidi ya Ruksa kwa viongozi kupora mali. Kuhus Conflict of interest halikutazama wala kufikiria ndio maana umeona wakitumaliza ktk kila sekta..
Hawa ndio watunga sheria, wanaotakiwa kulinda maslahi ya Taifa na ndio wao leo hii wanabishana.. kama ingekuwa amri yangu Mkapa siku nyingi yuko Lupango.

Je masikitiko yako huoni kama hayataleta utatuzi bali kudidimiza Taifa hili siku za mbeleni ? Panapokuwa na tatizo kinachotakiwa ni uamuzi wa kurekebisha hilo tatizo.

Kipi kipo juu ya mwenzie, Katiba ya JMT, au Azimio la Zanzibar ?

Binafsi naona kama Mkapa kavunja katiba, hii ni sawa na dhambi ya shirki. Mkapa have to face the consequences, tusikatishane tamaa mapema hii kwa kusema kuwa jamaa katupiga bao la kisigino. Afikishwe mbele ya sheria huko itajulikana nani atamfunga mwenzie bao, na hilo bao litakuwa la aina gani.

Further more, hilo Azimio la Zanzibar lifutwe haraka na upesi, au liwe rectified asap, ili kuwazuia na marais wengine kutojinyakulia mali za wananchi kwa maslahi yao binafsi. Kikwete naye akichota, tena akaamua kuchota zaidi ya alivyochota Mkapa! akaja Rais Mbowe naye akaamua kuchota zaidi ya atakavyochota Kikwete ITAKUWAJE ? Tutaendelea kulialia ? Tutawaambia nini wanetu na wajukuu zetu?
 

Ofisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kipwani alisema jana kuwa, taasisi yake haina uwezo wa kumchunguza kiongozi huyo kutokana na Katiba ya nchi kutotoa nafasi hiyo katika Ibara ya 46 (3) ya Katiba ya Tanzania. Kapwani alieleza kuwa taasisi yake inaheshimu Katiba na ina wajibu wa kuilinda na kuheshimu matakwa hayo ya Katiba.

Kifungu hicho cha Katiba kinaeleza kuwa "Ni marufuku kumshitaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii."

Wananchi tukakatae hii tafsiri ya serikali kwamba katiba inaruhusu Rais kuvunja sheria.

Kuna siku jaji ya mahakama kuu alikua anaamua kesi ya kikatiba. Swala lilikuwa whether mtu yeyote – hata asiyehusika, ambaye hajaumizwa na sheria fulani inayovunja katiba – anaruhusiwa kuleta pingamizi mahakamani. Serikali ilidai kwamba kikatiba na kisheria haruhusiwi. Kwa kiasi kikubwa, serikali haikuwa mbali sana na ukweli. Katika mifumo ya common law, ili uweze kufungua kesi, ni lazima uonyeshe kwamba unastahili kusimama mbele ya mahakama, locus standi. Uonyesha kwamba, moja la msingi, kuna athari iliyokupata wewe binafsi, au iliyoko usoni kukupata kutokana na sheria ambayo unataka kudai ni kinyume na Katiba. Mantiki ya hii nguzo ya locus standi ya common law ya mwingereza, ambayo na sisi tumerithi, ni kwamba kesi ya Juma akashitaki Juma, sio kila mtu akimbile kushitaki malalamiko ya kaka yake.

Katika kesi hiyo ya mwaka 1993, mlalamikaji alikuja, pamoja na mambo mengine, kupinga uhalali wa sheria iliyompa Waziri nguvu ya kufungia magazeti, Michapo na Cheka. Serikali ikasema wewe ni mwanasiasa, mchungaji, kufungiwa kwa gazeti kunakuuma nini? Huna locus standi ya kushitaki. Kabla ya kuamua yale nyeti yenyewe ya kesi, merits of the case, ikadili jaji kwanza aamua, je, huyu mtu ana locus standi?

Jaji akaamua kwenda kinyume na utamaduni wa locus standi, msingi ambao bado unafatishwa na nchi kubwa, vinara wa common law, kama Marekani. Yeyote mwenye kesi na alete, akasema. Lakini ikabidi atoe sababu, maana katika common law, maamuzi ya jaji inakuwa sheria mpya, kama vile imetoka bungeni, inayobidi kufuatwa na majaji wenzie, decisional law. Akasema:

``First of all, illiteracy is still rampant. We were recently told that Tanzania is second in Africa in wiping out illiteracy but that is statistical juggling which is not reflected on the ground. If we were that literate it would have been unnecessary for Hanang District Council to pass bye-laws for compulsory adult education which were recently published as Government Notice No. 191 of 1994. By reason of this illiteracy a greater part of the population is unaware of their rights, let alone how the same can be realised. Secondly, Tanzanians are massively poor. Our ranking in the world on the basis of per capita income has persistently been the source of embarrassment. Public interest litigation is a sophisticated mechanism which requires professional handling. By reason of limited resources the vast majority of our people cannot afford to engage lawyers even where they were aware of the infringement of their rights an the perversion of the Constitution. Other factors could be listed but perhaps the most painful of all is that over the years since independence Tanzanians have developed a culture of apathy and silence. This, in large measure, is a product of institutionalized mono-party politics which in its repressive dimension, like detention without trial, supped up initiative and guts.``

Lugakingira, Justice; Mtikila v. the Attorney General, Civ Case No. 5 of 1993, High Court of Tanzania

Jaji Lugakingira, Mungu amrehemu, anasema Watanzani hatuna initiative and guts!!

Hakuna wa kwenda mbele ya mahakama kupinga serikali. Hatuna kende!! Anasema ziliyeyuka wakati wa tawala za kikandamizi za nyuma. They used to scare the crap, they scared the guts out of us!! Na huyu sio mpiga kelele wa mtandaoni mwenye chuki na viongozi au aliyesoma historia ya nchi yetu vitabuni na kwenye tovuti tu. Hapana. Huyu ni mtu alikuwepo enzi hizo, aliyepewa uongozi na waasisi wa nchi, u-ujaji mahakama kuu, aliyeona the forces of the power that be kwa karibu, sio kwamba ana hana hiana na fitina na viongozi na waasisi wa nchi. Anasema hakuna Watanzania wenye ujasiri wa ku-face serikali.

Inabidi twende tuka challenge tafsiri ya Tukukuru, tafsiri ya Serikali, kwamba Katiba inasema Mkapa hawezi kushtakiwa. Sidhani tutafanya.

Jaji Lugakingira alishasema Watanzania hatuna initiative and guts!
 
Mama,
Nakuelewa sana isipokuwa hata katiba bado inanichanganya..
Hao Takukuru wanasema hivi:-
Ibara ya 46(3) ambayo inazuia kumshtaki Rais mstaafu, kulingana na Takukuru inasema exactly kama walivyosema wao:- Kuwa, Isipokuwa kama ataacha, kushika madaraka ya Rais kutokana na masharti ya ibara 46 a (10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.

hayo maandishi mekundu mama yanamkinga rais Mkapa na ukija weka Azimio la zanzibar ndio kabisaaa!.. sasa nachoshauri mimi ni kwamba tusiangalie Katiba wala Azimio la Zanzibar. Aliyofanya Mkapa ni kinyume cha Maadili ya Uongozi bora... period.
Tena kayafanya kwa makusudi kabisa kuharibu kama hao kina Mugabe ambao kikatiba wanadai hawana makosa..
Kufikishwa Mkapa mahakamani ndio dua yangu siku zote kukomesha kabisa mchezo wa viongozi na hasa marais kuwa Miungu watu. Washenzi na wabaya kuliko hata Mkoloni kwa sababu ya kinga kama hizi.
 
Mama,

Ibara ya 46(3) ambayo inazuia kumshtaki Rais mstaafu, kulingana na Takukuru inasema exactly kama walivyosema wao:- Kuwa, Isipokuwa kama ataacha, kushika madaraka ya Rais kutokana na masharti ya ibara 46 a (10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.

In relation to allegations zinazomkabili Mkapa, naombeni mnielezee kwa kina hayo maandishi yalikuwa bolded blue yanamaanisha nini hasa kisheria. Labda kuna kitu nina miss hapo.
 
Kwa niko New Dheli, India nikirudi home nitafanya mapitio makabrasha yangu ila la Mkapa kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria halihitaji kubadilishwa kwa katika ni suala la ufafanuzi tuu.
Rais ndio mtu wa mwsho kupelekewa hukumu za kifo baada ya taratibu zote za mahakama kukamilika. Nyerere alinyonga 2. Mwamwindi na muuaji wa Karume. Mwinyi alinyonga 16 sina majina. Mkapa hakunyonga hata mmoja na Jk bado hajanyonga. Kuna shinikizo kubwa kufuta adhabu ya kifo retrorespectively ili walioshahukumiwa wasemehewe na kuna wanaotaka hao jamaa wapewe haki yao kwa kunyongwa kuliko kuendelea kusota magerezani.

samahani natoka nje ya mada. kumbukumbu zangu zinaniambia muuaji wa karume (jamaa aliyefyatua risasi) aliuwawa on the spot na walinzi wa karume. na habari za wakati ule huyu jamaa hakuwa na imani ya kutoka eneo lile hai na alikwishasafirisha familia yake nchini oman kama sikosei.

tuendelee na mada
 
Kafara,
Nilvyosikia mimi enzi hizooo. kuwa aliyemuua Karume ni shemeji yake au mtu katika familia ambaye alikuwa analipa kisasi..Hakuuawa on the spot kama sikosei, na Kisiasa mauaji yale yalifikiriwa yamepangwa na kundi la Umma party kina Abraham babu..ndio maana walikuwa wanted Zanzibar.

Mama,
nafikiri umeshindwa kuelewa maana kwa sababu umeacha maneno yanayotangulia.. yanasema hivi..au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.

sasa soma ya bold nyekundu kisha unganisha...na yale yaliyotangulia yaliyosema kuwa:- Itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote...

Kwa kifupi nikiweka kifungu hicho sawa kitakuwa kinasomeka hivi:- Itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.
 
Baadaya tamko la Waziri mkuu Mh: M Pinda, ambae kiutaratibu ndie kiongozi wa shughuli za serekali naona mwangaza unaanza kuonekana upande wa pili wa mtaro, Juu ya sakata na vuta nikuvute kuhusiana na mh: Mkapa, kuwa iko haki na wajibu wa kumfikisha mahakamani? matamshi ya waziri mkuu yanabainisha kuwa haki na wajibu wa kumsimamisha Mkapa mahakamani upo kinachokosekana sasa hivi ni utaratibu, nao unazoroteshwa na madai ya kinga ya katiba kwa rais mstaafu.
Naamini ibara hiyo inayozungumzia kinga inafasiriwa vibaya au kwa makusudi ya kujaribu kumlinda mtuhumiwa. Iko wazi kuwa Wabunge toka pande zote pamoja CCM wako tayari kuirudisha katiba ubaoni. Nafikri sasa tuache kuzoza tuanze kazi chini ya Wazri mkuu ili zoezi hili la kupambana na Mafisadi lisizoroteshe mambo mengine,tujaribu kulitatua katika miezi sita ijayo.
Ikiwa tunaamini Demokrasia yetu inakua na sheria zinaimarika nilazima wote tuwe sawa mbele ya sheria.
 
Kwa kifupi nikiweka kifungu hicho sawa kitakuwa kinasomeka hivi:- Itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais.

Kwa maana hiyo basi, kwenye suala la Kiwira and the like, Mkapa hajafanya kama Rais. Amefanya kama Mkapa. Vinginevyo, kwenye nyaraka lingekuwepo jina la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...na kwa sasa mmoja wa wamiliki hao angekuwa Rais aliyeko madarakani. Je Rais aliyeko madarakani sasa ana mamlaka yeyote au ni mmoja wa wamiliki wa Kiwira for example ?

If Mkapa alifanya ujasiria mali kama Mkapa na sio kama Rais, basi hapo kifungu hicho cha katiba hakimpi kinga Mkapa ya kutoshitakiwa. Hiyo marufuku hapo ni null and void.
 
Hakika Tanzania ni nchi ya siasa, nilifikiri labda Pinda atatoa the way forward juu ya swala la Mkapa na Katiba lakini nae anazukuka zunguka tuu sijaona clear way forwad nini kifanyike kama onyo kwa rais mstaafu na marais watakaofuata ili kuzuia matumizi mabaya ya madaraka wakiwa viongozi.

Kimsingi kigugumizi hiki kikifanikiwa kutofanya mabadiliko yakatiba ili kuweza kumfikisha Mr. Clean mahakamani then tunaweka mwanya wa rais atakaye kuwa madarakani kufanya atakalo akijiamini kuwa sheria itamlinda. Nadhani huu sii utawala mzuri wa sheria. Sheria ni msumeno unakata pande zote sasa msumenu huu unakata upande mmoja tunapaswa kuangalia vizuri.
 
Kwa maana hiyo basi, kwenye suala la Kiwira and the like, Mkapa hajafanya kama Rais. Amefanya kama Mkapa. Vinginevyo, kwenye nyaraka lingekuwepo jina la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...na kwa sasa mmoja wa miliki hao angekuwa Rais aliyeko madarakani sasa hivi. Je Rais aliyeko madarakani sasa ana mamlaka yeyote na Kiwira kama Mkapa lifanya jambo hili kama Rais ?

If Mkapa alifanya ujasiria mali kama Mkapa na sio kama Rais, basi hapo kifungu hicho cha katiba hakimpi kinga Mkapa ya kutoshitakiwa. Hiyo marufuku hapo ni null and void.

Thank you Mama 🙂
 
Ukweli ni kwamba issue ya Rais Mstaafu haihusiani na ile ile kinga ya kutofikishwa mbele ya sheria. Hapa wanachanganya mambo mawili ya president kama institution na president kama person.

Bwana Pasco,
hakuna President kama institution duniani hapa.Tuna President kama person tuu full stop.NA KAMWE HUWEZI KUTOFAUTISHA MKAPA KAMA RAIA MWINGINE NA MKAPA KAMA RAIS KUANZIA November 1995 hadi November 2005.Kitu unachotakiwa kujua tu ni kuwa Rais Mkapa ni mtanzania na siyo watanzania wote ni Rais.

Nawapa Tahadhali nyie wenye hulka na silka kama ya huyo Pinda.Msifikiri Mkapa ni mjinga.Kukaa kwake kimya msifikiri anawaogopa sana ninyi wavivu wa kufikiri.Mkitaka mjue Tanzania mawe na marungu yananunuliwa wapi mkamateni Mkapa muone.Na msifikiri mimi napenda mnavyomdharirisha rais wetu mstaafu.Mngejua ni haki rais kushitakiwa mngebadili ako ka katiba kenu siku nyingi.Wewe Pinda na jamii ya watu mnaofanana nakushauri HUSIKURUPUKE eti kisa unataka kumridhisha balozi wa kijiji.Hata mbinguni kuna malaika wateule ije kuwa Tanzania?????

-Mangapi Nyerere kafanya ya ajabu na hakushtakiwa???
-Mangapi Mwinyi kafanya ya AJABU zaidi ya Mkapa na hakushtakiwa???
-Kwa nini awe Mkapa???

Wewe pinda si ni Usalama wa taifa wewe??unafikiri hakuna wanaomtii Mkapa 100%,unafikiri jeshini na Polisi mkapa yupo yupo tu??Acheni hizo nyie.Kama mmemaliza kahawa na kashata semeni.Unajua sometimes amani nayo ikizidi inakuwa karaha.Haya ngoja tujaribu na machafuko kidogo ili tuheshimiane.
Majita
MIMI NADHANI WATU WANAICHANGANYA SHERIA HII.SIDHANI KAMA SHERIA HII INAMLINDA RAIS KUTOSHTAKIWA AKIFANYA KOSA LA JINAI KAMA MTU BINAFSI.NAAMINI SHERIA HII INAMLINDA KWA KOSA LA MAAMUZI KAMA RAIS.mIMI NAAMINI TUKIANZA MFUMO HUU ILE KASI YA KUNG'ANG'ANIA KILA MTU KUTAKA KWENDA IKULU ITAPUNGUA.TUSIPOITEKELEZA HATA WAUZA MADAWA YA KULEVYA WATATAKA KUWA MARAIS.hAPO ITAKUWA HATARI KWA NCHI YETU.
 
Amani iwe Nanyi, nawapeni mkono wa Krismas!

Mkandara nashukuru sana kwa kuongezea uhai kwenye hii mada, pamoja na wachangiaji wengine wote.

Nafikiri kinachowashina wengi kuelewa ni kwa nini Mkapa aonekane ni Rais mbovu pamoja na kujitutumua kwake kulipa madeni (ambayo tuliishia kusamehewa wala si kuyalipa), kuongezeka wa wawekezaji(walianza nyakati za Mwinyi, Mkapa akafanya urahisi kwa kulegeza kodi na ushuru ulioruhusu utapeli na uhujumu) kujenga shule na barabara( ambazo hazikuwa na msingi imara) na uafanisi serikalini.

Ukiangalia kosa la kwanza la uhujumu BOT, jiulize je huoni kuwa uhujumu wote uliotokea BOT huku Mramba, Yona, Ballali na Mgonja wakiwa vinara unatokana na uzembe wake ikiwa yeye kama Rais hakukagua mahesabu ya mwaka ya BOT?

Ikiwa ni yeye aliidhinisha Jeshi lianzishe mradi wa Meremeta, na kuruhusu usiri wa kukopa nje ya nchi na wala si ndani ya nchi kutumia mabenki yetu na kisha kushurtisha BOT na serikali ilipe deni hamuoni kuwa kuna kasoro na matumizi mabaya ya uongozi na dhamana ya madaraka? je uaminifu alioapia katika katiba ulikwenda wapi kwa kuhakikisha kuwa JWTZ linafungua kampuni na kuisajili nje ya nchi kisha ije kufanya kazi nchini?

Je nia hii ilikuwa ni kuhakikisha Meremeta inapata huduma kama Barrick, misamaha ya kodi na ushuru, upendeleo kutoka Serikaini na usiri kusema hii ni kampuni ya kigeni tuwape zulia jekundu?

BOT walipoendelea kutumbua kujenga majengo yao huku kwa kutumia pesa zaidi ya mtaji mzima wa kuendesha BOT, je ni nani aliidhinisha hizo pesa bila kuwa mwangalifu kujua kuwa gharama ya ujenzi wa majengo ni zaidi ya mtaji wa BOT?Jek ama BOT ndio wadhibiti wa sarafu yetu ikiwa ni pamoja na kutuliza mfumuko wa bei, kupanda na kushuka kwa thamani ya shilingi, iweje walitumia pesa nyingi zaidi ya mtaji wao kwa matumizi ambayo hayakuwa ya ulazima?

Mimi si mchumi, lakini kama wale wafanyabiashara wa Tandale au mtu mwingine, inapofika hatua kuwa gunia la mchele kutoka Shinyanga linapata tabu kuja Dar kuuzwa lakini gunia kutoka Kampuchea linafika kwa uharaka na hata kupunguziwa kodi, hiyo ni dalili tosha kuwa uchumi si mzuri na kuna udhaifu ndani ya uongozi na mipango. Leo bidhaa tunazozalisha hakuna Mtanzania anayeweza kununua na mzalishaji huishia kuingia hasara. Waulizeni watu wa Kilimanjaro na Arusha kuhusu kahawa yao na kwa nini wanakimbilia kulima maharage au ulezi.

Sasa kama BOT walitumia pesa ambazo zinazidi mtaji na hivyo kushusha thamani ya fedha yetu, je Mkapa alikuwa wapi kudhibiti matumizi haya holela na si kujenga barabara kutoka Shinyanga au kuboresha kilimo cha kahawa na hata usindikaji ili pato letu kama Taifa lisitegemee kodi na wawekezaji pekee bali lishamiri kutokana na uuzaji wa mali asili nje ya nchi?

Leo hii nimesoma kuwa vita vya Kagera vilitugarimu dola za Marekani $500 milioni, hivyo ni wazi kuwa Mwinyi alipokuja kazi yake ilikuwa ni kusisimua uchumi.

Lakini Mwinyi, hata kama alikuwa ndiyo Mzee Ruksa au mkewe alikamatwa na dhahabu (je tuna ushahidi kuwa alikuwa ameiba hiyo dhahabu?) hakufanya maamuzi mabaya ama binafsi au kwa uzembe. Cha kumlaumu Mwinyi si kinachojadiliwa hapa, bali ni alichofanya Mkapa kuruhusu mianya ya kuhuju uchumi.

Ningetegemea kuwa Mwinyi na Mkapa wangeleta mapinduzi ya uzalishaji mali kutumia mfumo wa Kibepari na miundo mbinu yake na si kukimbilia soko huria kama mfumo wa uzalishaji ambao umeendeleza utegemezi.

Nyerere ana makosa yake ya kiutendaji. Azimio la Arusha halikuwa kosa lake binafsi wala hakuamua pekee,vijiji vya ujamaa, elimu ya UPe na mengineyo yalikuwa ni maamuzi ya Chama na Serikali na si Nyerere pekee.

Ndiyo maana hata Azimio la Zanzibar, simnyooshei Mwinyi au Malecela kidole kwa kuwa yalikuwa maamuzi ya jumla na si mtu mmoja au wawili.

Lakini maamuzi mengi ya Mkapa ambayo ndiyo chimbuko la kesi hii yalikuwa ni yake binafsi bila hata kuhusisha Chama au Serikali.

Jee hii inatokana na kiburi cha kuwa Rais wa nchi na kuamini ana madaraka ya kufanya kila anachotaka kwa kuwa yeye ni Rais?

Ikiwa Katiba yetu inasema hivi katika kifungu cha 27

27​
.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya Jamhuri
ya Muungano, mali ya Mamlaka ya Nchi na mali yote
inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia kuiheshimu mali
ya mtu mwingine.
(2) Watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali ya
mamlaka ya nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za uharibifu
na ubadhilifu, na kuendesha uchumi wa taifa kwa makini kama

watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya taifa lao.
iweje leo tutetee kinga kwa Mkapa kwa kushindwa kulinda mali asili ya jamhuri au kutunza mali za jamhuri kwa kudai ana kinga?
 
Ama waandishi wetu ni vihiyo kweli kweli au basi tunaongozwa na mazuga.

Katiba hiyo hiyo kifungu 46.a kinatoa upenyo wa kumshitaki Rais kupitia bunge...


46​
.-(1) Wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika
madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii, itakuwa ni marufuku
kumshitaki au kuendesha mashataka ya aina yoyote juu yake
mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.
(2) Wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka
yake kwa mujibu wa Katiba hii, haitaruhusiwa kufungua
mahakamani shauri kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosa
kulitenda yeye binafsi kama raia wa kawaida ama kabla au
baada ya kushika madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku
thelathini kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais
atapewa au ametumiwa kwamba taarifa ya madai kwa maandishi
kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria
iliyotungwa na Bunge, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo
kuhusu chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai yenyewe, jina
lake na anwani ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa
analodai.
(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais
kutokana na masharti ya ibara ya 46A(10), itakuwa ni marufuku
kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la
kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya
kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye
kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais
kwa mujibu wa Katiba hii.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
_________________________________________________________________​
37​
Bunge laweza
kumshtaki Rais
Sheria ya 1992
Na.20 ib.8
Sheria ya 1995
Na.12 ib.4​
46A​
.-(1) Bila ya kujali masharti ya ibara ya 46 ya Katiba hii,
Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani
endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa
mujibu wa masharti ya ibara hii.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja
yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama
inadaiwa kwamba Rais-

Sheria ya ….​
(a) ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja
Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;
(b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili
yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa
yaliyotajwa katika ibara ya 20(2) ya Katiba, au
(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha kiti cha Rais
wa Jamhuri ya Muungano, na haitatolewa hoja ya
namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili tangu hoja
kama hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.
(3) Bunge halitapitisha hoja ya kumshtaki Rais isipokuwa tu
kama-
(a) taarifa ya maandishi, iliyotiwa sahihi na kuungwa
mkono na Wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya
Wabunge wote itawasilishwa kwa Spika siku
thelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyo
inakusudiwa kutolewa Bungeni, ikifafanua makosa
aliyoyatenda Rais, na ikipendekezwa kuwa Kamati
Maalum ya Uchunguzi iundwe ili ichunguze
mashataka yaliyowasilishwa dhidi ya Rais;
(b) wakati wowote baada ya Spika kupokea taarifa
iliyotiwa sahihi na Wabunge na kujiridhisha kuwa
masharti ya Katiba kwa ajili ya kuleta hoja
yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja
kuiwasilisha hoja hiyo, na kisha Spika atalitaka
Bunge, bila ya kufanya majadiliano, lipige kura juu ya
hoja ya kuunda Kamati Maalum ya Uchunguzi na
kama ikiungwa mkono na Wabunge waiopungua
theluthi mbili ya Wabunge wote atatangaza majina ya
wajumbe wa Kamati Maalum ya Uchunguzi.
(4) Kamati Maalum ya Uchunguzi, kwa madhumuni ya ibara
hii, itakuwa na wajumbe wafuatao, yaani-
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye
atakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati;
(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar na

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
_________________________________________________________________​
38​
(c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwa mujibu wa
Kanuni za Bunge na kwa kuzingatia uwiano wa
uwakilishi baina ya vyama vya siasa
vinavyowakilishwa Bungeni.
(5) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamati Maalum
ya Uchunguzi, Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, kisha kazi
na madaraka ya Rais yatatekelezwa kwa mujibu wa masharti ya
ibara ya 37(3) ya Katiba hii hadi Spika atakapomfahamisha Rais
juu ya azimio la Bunge kuhusiana na mashataka yaliyotolewa
dhidi yake.
(6) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalum ya Uchuguzi
kuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashataka dhidi ya
Rais, pamoja na kumpatia Rais fursa ya kujieleza, kwa kufuata
utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge.
(7) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile katika muda
usiozidi siku tisini, Kamati Maalum ya Uchunguzi itatoa taarifa
yake kwa Spika.
(8) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalum ya
Uchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata
utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge.
(9) Baada ya taarifa ya Kamati Maalum ya Uchunguzi
kuwasilishwa kwa mujibu wa ibara ndogo ya (8), Bunge litaijadili
taarifa hiyo na litampa Rais fursa ya kujieleza, na kisha, kwa kura
za Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote,
Bunge litapitisha azimio ama kuwa mashtaka dhidi ya Rais
yamethibitika, na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha
Rais, au kuwa mashtaka hayo hayakuthibitika.
(10) Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya
Rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti
cha Rais, Spika atawafahamisha Rais na Mwenyekiti wa Tume
ya Uchaguzi juu ya azimio la Bunge, na hapo Rais atawajibika
kujiuzulu kabla ya kuisha kwa siku ya tatu tangu Bunge
lilipopitisha azimio hilo.
(11) Endapo Rais ataacha kushika kiti cha Rais kutokana na
mashataka dhidi yake kuthibitika, hatakuwa na haki ya kupata
malipo yoyote ya pensheni wala kupata haki au nafuu nyinginezo
alizo nazo kwa mujibu wa Katiba au Sheria yoyote iliyotungwa na
Bunge.​
Katiba
 
Tukumbuke wakati wote kwamba taifa letu lina Katiba ya Nchi ambayo imeweka misingi mikuu ya kuendesha nchi yetu, haki na wajibu wa kila Mtanzania. Katiba kama sheria mama imeweka pia mipaka katika kushughulikia mambo mbalimbali ya nchi na kwa mantiki hii, haina budi kuheshimiwa wakati wote.”

Kifungu hicho cha Katiba kinaeleza kuwa “Ni marufuku kumshitaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii.”

- Yale yale ya Hosea, aliyetuambia kua amechunguza Richimonduli na kuona hakuna makosa yanayo-amount into a crime kwa katiba yetu, sasa huyu tena na maneno yake yale yale ya kitoto na kusadikika as if wabongo wote tumelala usingizi, you wonder hawa Takukuru's mission ni nini hasa kuteteta mafisadi kwa visingizio vya limitations za sheria au kulilinda taifa kwa kudai bunge litengue sheria batili kwa taifa kama hii,

- Yes, huu sio wakati wa Takukuru kutudanganya na maneno ya sheria, walitakiwa at this point wawe mstari wa mbele kutafuta public support ya kubadilishwa kwa baadhi ya vipengele vya katiba kama hiki kinachomlinda Mkapa, ili atinge mapema Kisutu ili kutupunguzia wananchi the wait na long legal rumblings ambazo eventually zitaruhusu tu Mkapa kwenda Kisutu, lakini at the wrong time maana the time is now, anatakiwa aongoze wenziwe Kisutu, kama alivyokuwa akiwaongoza kwenye kupora mali za wananchi wakiwa kwenye power.

- Hawa Takukuru wasitupandishe mkenge, kinachotakiwa ni simply 2/3 ya wabunge kuunga mkono muswaaada kama hiyo sheria ipo kweli, iondolewe haraka sana ili tuendelee na safari za Kisutu na Taukukuru wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kwenye kilio cha kubadilishwa katiba sio kujificha nyuma ya ufisadi. Huyu Hosea it is about time sasa naye akatinga Kisutu kwa kulidanganya taifa kwenye uchunguzi wa Richimonduli, sasa kama alisema uongo then inakuwaje eti leo anasema ukweli?

- Hivi karibuni nilimwambia waziri wetu wa sheria na akakubaliana na mimi kwamba wakati umefika wa Tanzania, kubadilisha katiba kwenye kipengele kitakacho wabana wasaidizi wote wanaoteulwia na rais, kupitishwa na bunge au special kamati yake ili wawe responsible kwa wananchi na sio rais na excecutive branch kama ilivyo sasa, ndio the only way hawa kina Hosea na Taukukuru wanaweza kuimba a different song badala ya hizi nyimbo za kusadikika. Haiwezekani Yona mbia wa Mkapa Kiwira, akatinga Kisutu halafu wakatuambia eti Mkapa analindwa na sheria, hawa viongozi wetu sometimes wawe na huruma na sisi wananchi na hili taifa hata kidogo tu!

Off course wanaudhi, lakini hatuwezi kukata tamaa.

Mungu Aibariki Tanzania.
 
Kama kuna mtu yoyote anasikiliza wanayosema TAKUKURU basi itakuwa ni ajabu. Kama Bunge lisilo na professional expertise na resources za kuchunguza ufisadi liliweza kugungua kuwa Richmonduli ni ufisadi waziwazi na wenye ushahidi wa kutosha kufikisha watu mahakamani, na TAKUKURU yenye "professionals" na resources ilishindwa, leo utaisikiliza TAKUKURU kwa nini? utakuwa ni ujinga, na tunajua kuwa wanachosema ni uongo mtupu.
 
Back
Top Bottom