BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
- Hivi karibuni kumekuwa na kauli nyingi za kukingana kati ya Pinda na Muungwana, hapa Muungwana alisema Mkapa aachwe apumzike, lakini Pinda anasema haogopwi.
- Wanaoyajua vizuri ya huko ndani wananiambia niogope Pinda maana huwa hasemi bila matendo na kwamba hii ya Kisutu ni operation yake, sasa anaposema hamuogopi Mkapa, ninapata faraja sana kwamba hii ngoma ya Kisutu inogile eh! he! he! he! inogile mwananagu! Tanzania inogile ooh! ooh! inogile!!!!
Na mimi nilikuwa nalifikiria hili. Kama tujuavyo JK alishatoa kauli kwamba, "Mwacheni Mzee wetu apumzike kwa amani." Je, JK ataweza kutoa kauli kama hii ya Pinda kwamba "Tunatakiwa kuafiki juu ya utawala wa sheria. Sheria kwa urahisi kabisa inasema hakuna mtu aliye juu yake. Hivyo kama utafanya kosa, hasa la jinai, sheria inakutaka ufikishwe kwenye chombo kinachohusika ambacho ni mahakama," alisema Pinda.
Bado JK ana kazi nzito maana swala la Mkapa halikwepeki na atajisafishia njia zaidi na kujiweka kwenye nafasi nzuri katika kinyang'anyiro cha 2010 kama akiamua kulishughulikia mapema na kuacha sheria ifuate mkondo wake na wakati huo huo kurudisha miliki ya Kiwira kwa Watanzania.