Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Ni wakati muafaka bunge likamuondolea kinga ben ili awajibishwe.
Mwalimu alisema ikulu ni patakatifu na sio sehemu ya kufanya biashara
 
Niliwahi kusihi hapa ndani, kuwa ni vema tukawasoma baadhi ya wazamivu amba o walipingana na ufisadi tangu huko nyuma, nchi haikufika hapa kwa bahati mbaya hata kidogo, matokeo haya ya rushwa, mmomonyoko wa maadili na kunyosheana vidole huku.

Tukubali tu kuwa mwalimu hakuwa mtoa rushwa wala mpokeaji rushwa bali hatuwezi kumuondoa ktk dhambi ya mmomonyoko wa maadili yetu, ni maono yake ya uchumi kuhudumia siasa yaliyoipeleka nchi hapa tulipo,mwinyi yeye hatuwezi kusema kuwa si mla rushwa wala mpokea rushwa bali tunathubutu kusema kuwa yeye ni chanzo cha mageuzi ya kifikra kwa kizazi kipya ambacho mostly hakikuwa na experience ya mfumo wa kibepari zaidi ya ule wa kijamaa (unafiki). Watu wakaanza kuuona ukweli wa dunia na ni hapo alipochelea ktk udhibiti wa mageuzi, mambo yakawa holela na heshima ya dola ikapotea, ilikuwa ni zama hizi tulipowasikia akina noushad , raza, gulamali, dewji na wengi wa namna hii wakiwa ndio main speakers wa issue za sirikali!!!!! Kimsingi hapa ndipo lilipoanza taifa lenye uchumi wa black market. Hapa ndipo muungano ulipoyumba sana, hapa ndipo nyara na madini ziliporwa kinyemela, hapa ndipo udini uliposhamiri lakini hapa ndipo shamrashamra za kula nguruwe zikaanza, siasa za kushutimiana zikaanza, wana ccm waandamizi wakaamini ccm ina wenyewe.
Mwinyi alirithi idadi kubwa ya wajamaa wanafiki walio na njaa, alipowapa fursa ikawa balaa mwisho akajikuta naye anahusishwa nao moja kwa moja.

Mkapa mtu asiye mvuto, aliyepewa nchi na jkn, aliapa kuli shape taifa, nathubutu kusema kuwa aliianza kazi hiyo kwa ujasiri mkubwa lakini shughuli ni pale alipowagusa wazee, kuna ushahidi kuwa mwalimu ndiye aliyemtaka kuacha kuwafuata wazee na kusaka wachawi na ajikite kujenga nchi aliyopewa, alifanya kazi yake kimyakimya akiwagusa mmoja baada ya mwingine huku akirejea maagizo ya mzee jkn, baadaye akaamua sasa afanye kazi ya ku-shape utawala wa nchi, serikali na idara zake, ajira serikalini,elimu kwa vyuo vya elimu ya juu na baadae msingi na mwisho sekondari,ujenzi wa barabara na madaraja,usambazaji wa umeme,ufutaji wa kodi za maendeleo, kupunguza ada za elimu ya sekondari,kuruhusu mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu visivyo vya serikali, akaamua kama noma na iwe noma pale alipoyaswaga makampuni ya umma psrc kwa kasi ya sunami, akaingia ktk maliasili ya madini hapa kwa kutumia tic ya samwel sitta shughuli ikaanza kwa kasi, taratibu serikali ikajirejeshea ile sifa ya kuwa mteja mkubwa ktk biashara na sekta binafsi kwa kununua na kulipa kwa wakati, taratibu heshima ya mfanyakazi ikarejea serikalini kwa japo hata mabenki kuanza kuwakopesha ingawaje kwa riba kubwa, akaajiri watendaji ndani na nje ya nchi.

Ktk harakati hizi ni lazima mambo kama kiwira,ndege ya rais, radar, meremeta hazikwepeki, ni katika mambo haya ndipo ninaposema kuwa nchi hii bado haina uchumi ulio wazi, kosa ambalo mkapa amelifanya na kumfanya atuhumiwe ni ileile dhambi ya kuacha uchumi uendelee kuhudumia siasa. Pengine kuhusiana na anben hapo nina jibu moja fasaha "mzee alikuwa anajindaa kustaafu hivyo ilimpasa kuanzisha ile kampuni ktk siku zake za mwisho mamlakani"

benjamin william mkapa anadumu kuwa rais wa awamu ya tatu yenye kauli mbiu "hii ni zama ya uwazi na ukweli"

huo ndio ukweli wenyewe tutake tusitake, he did his presidency and now is resting time after a job well done.
 
Niliwahi kusihi hapa ndani, kuwa ni vema tukawasoma baadhi ya wazamivu amba o walipingana na ufisadi tangu huko nyuma, nchi haikufika hapa kwa bahati mbaya hata kidogo, matokeo haya ya rushwa, mmomonyoko wa maadili na kunyosheana vidole huku.

Tukubali tu kuwa mwalimu hakuwa mtoa rushwa wala mpokeaji rushwa bali hatuwezi kumuondoa ktk dhambi ya mmomonyoko wa maadili yetu, ni maono yake ya uchumi kuhudumia siasa yaliyoipeleka nchi hapa tulipo,mwinyi yeye hatuwezi kusema kuwa si mla rushwa wala mpokea rushwa bali tunathubutu kusema kuwa yeye ni chanzo cha mageuzi ya kifikra kwa kizazi kipya ambacho mostly hakikuwa na experience ya mfumo wa kibepari zaidi ya ule wa kijamaa (unafiki). Watu wakaanza kuuona ukweli wa dunia na ni hapo alipochelea ktk udhibiti wa mageuzi, mambo yakawa holela na heshima ya dola ikapotea, ilikuwa ni zama hizi tulipowasikia akina noushad , raza, gulamali, dewji na wengi wa namna hii wakiwa ndio main speakers wa issue za sirikali!!!!! Kimsingi hapa ndipo lilipoanza taifa lenye uchumi wa black market. Hapa ndipo muungano ulipoyumba sana, hapa ndipo nyara na madini ziliporwa kinyemela, hapa ndipo udini uliposhamiri lakini hapa ndipo shamrashamra za kula nguruwe zikaanza, siasa za kushutimiana zikaanza, wana ccm waandamizi wakaamini ccm ina wenyewe.
Mwinyi alirithi idadi kubwa ya wajamaa wanafiki walio na njaa, alipowapa fursa ikawa balaa mwisho akajikuta naye anahusishwa nao moja kwa moja.

Mkapa mtu asiye mvuto, aliyepewa nchi na jkn, aliapa kuli shape taifa, nathubutu kusema kuwa aliianza kazi hiyo kwa ujasiri mkubwa lakini shughuli ni pale alipowagusa wazee, kuna ushahidi kuwa mwalimu ndiye aliyemtaka kuacha kuwafuata wazee na kusaka wachawi na ajikite kujenga nchi aliyopewa, alifanya kazi yake kimyakimya akiwagusa mmoja baada ya mwingine huku akirejea maagizo ya mzee jkn, baadaye akaamua sasa afanye kazi ya ku-shape utawala wa nchi, serikali na idara zake, ajira serikalini,elimu kwa vyuo vya elimu ya juu na baadae msingi na mwisho sekondari,ujenzi wa barabara na madaraja,usambazaji wa umeme,ufutaji wa kodi za maendeleo, kupunguza ada za elimu ya sekondari,kuruhusu mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu visivyo vya serikali, akaamua kama noma na iwe noma pale alipoyaswaga makampuni ya umma psrc kwa kasi ya sunami, akaingia ktk maliasili ya madini hapa kwa kutumia tic ya samwel sitta shughuli ikaanza kwa kasi, taratibu serikali ikajirejeshea ile sifa ya kuwa mteja mkubwa ktk biashara na sekta binafsi kwa kununua na kulipa kwa wakati, taratibu heshima ya mfanyakazi ikarejea serikalini kwa japo hata mabenki kuanza kuwakopesha ingawaje kwa riba kubwa, akaajiri watendaji ndani na nje ya nchi.

Ktk harakati hizi ni lazima mambo kama kiwira,ndege ya rais, radar, meremeta hazikwepeki, ni katika mambo haya ndipo ninaposema kuwa nchi hii bado haina uchumi ulio wazi, kosa ambalo mkapa amelifanya na kumfanya atuhumiwe ni ileile dhambi ya kuacha uchumi uendelee kuhudumia siasa. Pengine kuhusiana na anben hapo nina jibu moja fasaha "mzee alikuwa anajindaa kustaafu hivyo ilimpasa kuanzisha ile kampuni ktk siku zake za mwisho mamlakani"

benjamin william mkapa anadumu kuwa rais wa awamu ya tatu yenye kauli mbiu "hii ni zama ya uwazi na ukweli"

huo ndio ukweli wenyewe tutake tusitake, he did his presidency and now is resting time after a job well done.
 
Kwa nini usianzishe thread yako ukawajadili Mwinyi na Mama Sitti? au ukaanzisha thread kusifu aliyofanya Mkapa? kwa nini utulazimishe kuongea unalotaka na usilianzishie hoja?

Ushauri mzuri sana... Mchungaji nafikiri umkumbushe huyo kondoo ya kuwa Daktari hasifiwi kwa kutibu'ni wajibu' vivyo hivyo hakuna mema aliyofanya Mkapa isipokuwa akitimiza wajibu wake,kinyume na hapo ndo habari yenyewe hii inayojadiliwa.

Ni kupoteza muda kusifia Mambo aliyoyafanya wakati alikuwa anawajibika kufanya,lakini lazima asemwe kwa yale aliyoyafanya ambayo ni kinyume na yale yaliyotarajiwa na wanajamii na hayo ndo tunataka akatueleze mahakamani...
 
rev. Kishoka,

Swala la kumuondolea kinga Mkapa na kumpeleka mahakamani ni hoja finyu na hatari. Kama Mkapa alifanya makosa akiwa rais, basi rais aliyeko madarakani atengue maamuzi hayo na kuyarekebisha. Tuchukue mfano rahisi, wamarekani wamemchagua Obama kuwa rais wao katika kipindi kigumu kabisa. Rais Bush amefanya maamuzi mengi mabaya ambayo yameitumbukiza Marekani na dunia katika msukosuko mkubwa sana, lakini kamwe hautasikia wamarekani wakisema Bush aburuzwe mahakamani kama ambavyo wengi wetu hapa tunavyomshupalia Mkapa aburuzwe kisutu! na hautasikia kamwe Obama akisema 'amerithi' matatizo ya nchi kutoka kwa Bush, wamerekani watampima kwa uwezo wake wa kutatua matatizo yao na sio kwa kisingizio cho chote kile. Vile vile JK hatakiwi kutoa lawama zozote kwamba amerithi matatizo kwa Mkapa. kama kuna maamuzi yeyote mabaya aliyofanya Mkapa, basi atengue (reverse) na abadilishe.
Kumpeleka Mkapa mahakamani kuta -set precedence, ambapo baada ya Mkapa atafuata mzee ruksa, na wakati huo huo JK akijitayarisha kutia nywele zake maji maana baada tu ya kumaliza kipindi chake naye ataburuzwa mahakamani!
kinachotakiwa kufanyika kama nilivyosema ni kutengua maamuzi yote mabaya aliyofanya Mkapa akiwa madarakani tu!

nawasilisha.

Mmmh mtazamo na utetezi wa aina hii ni hatari sana kwa maendeleo yetu na utatutukanisha waafrika kama si watanzania,Makosa ya Bush ni makosa ya 'policy' na si makosa ya kushiriki au kufumbia macho uhalifu dhidi ya mali ya umma kwa faida ya viongozi na wafanyabiashara wachache. Sasa unataka awamu ya nne atengue ????!!!! una maanisha auze rada, abomoe majengo pacha ya BOT awarudishe netgroup solution walete fedha walizochukua na kuifilisi TANESCO au awape ATCL ndege ya Rais hayo ni machache kwa mfano tu. naomba ufafanue namna ya ulunganifu uliopo kwa Bush Marekani na Mkapa Tanzania hasa juu ya makosa waliyoyatenda dhindi ya nchi zao.
 
Mmmh mtazamo na utetezi wa aina hii ni hatari sana kwa maendeleo yetu na utatutukanisha waafrika kama si watanzania,Makosa ya Bush ni makosa ya 'policy' na si makosa ya kushiriki au kufumbia macho uhalifu dhidi ya mali ya umma kwa faida ya viongozi na wafanyabiashara wachache.

Makosa ya Bush ni makosa ya policy? are you sure? unakumbuka kampuni ya Enron? fuatilia kidogo. haya na vita ya Iraq? is that policy au wendawazimu? kwa namna ye yote ile, Wamarekani wana sababu nyingi nzito za kumburuza bwana kichaka mahakamani, lakini hawafanyi hivyo! sasa jiulize ni kwa nini hawafanyi hivyo?

Sasa unataka awamu ya nne atengue ????!!!! una maanisha auze rada, abomoe majengo pacha ya BOT awarudishe netgroup solution walete fedha walizochukua na kuifilisi TANESCO au awape ATCL ndege ya Rais hayo ni machache kwa mfano tu. naomba ufafanue namna ya ulunganifu uliopo kwa Bush Marekani na Mkapa Tanzania hasa juu ya makosa waliyoyatenda dhindi ya nchi zao.

Katika hutuba ya kwanza ya rais JK bungeni, alisema watapitia upya mikataba yote iliyosainiwa hasa ya sekta ya madini. kauli hiyo ilinipa moyo kwamba mikataba yote mibovu itatenguliwa na serikali ya awamu ya nne. Badala yake, walisaini mikataba mengine tena nje ya nchi! Nilimaanisha kwamba mikataba yote ingepititwa upya na yale yasiyokuwa na tija na nchi yetu yatupiliwe mbali.
swala la kuuza rada au kubomoa majengo pacha ya BOT ni yako mkuu, waliofanya ubadhirifu katika ununuzi wa rada na katika ujenzi wa majengo pacha, wapelekwe mahakamani.
 
FDR.jr,
Mkapa mtu asiye mvuto, aliyepewa nchi na jkn, aliapa kuli shape taifa, nathubutu kusema kuwa aliianza kazi hiyo kwa ujasiri mkubwa lakini shughuli ni pale alipowagusa wazee, kuna ushahidi kuwa mwalimu ndiye aliyemtaka kuacha kuwafuata wazee na kusaka wachawi na ajikite kujenga nchi aliyopewa, alifanya kazi yake kimyakimya akiwagusa mmoja baada ya mwingine huku akirejea maagizo ya mzee jkn, baadaye akaamua sasa afanye kazi ya ku-shape utawala wa nchi, serikali na idara zake, ajira serikalini,elimu kwa vyuo vya elimu ya juu na baadae msingi na mwisho sekondari,ujenzi wa barabara na madaraja,usambazaji wa umeme,ufutaji wa kodi za maendeleo, kupunguza ada za elimu ya sekondari,kuruhusu mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu visivyo vya serikali, akaamua kama noma na iwe noma pale alipoyaswaga makampuni ya umma psrc kwa kasi ya sunami, akaingia ktk maliasili ya madini hapa kwa kutumia tic ya samwel sitta shughuli ikaanza kwa kasi, taratibu serikali ikajirejeshea ile sifa ya kuwa mteja mkubwa ktk biashara na sekta binafsi kwa kununua na kulipa kwa wakati, taratibu heshima ya mfanyakazi ikarejea serikalini kwa japo hata mabenki kuanza kuwakopesha ingawaje kwa riba kubwa, akaajiri watendaji ndani na nje ya nchi.
Mkuu hivi umeandika habari hii kwa kusimuliwa ama!.. inashangaza sana kuona Mtanzania akisifia vitu ambavyo viko wazi na kila Mtanzania anafahamu kwamba Utawala wa Mkapa umetufikisha hapa tulipo leo..
Mkapa kama kiongozi alianza vizuri sana 1995 -2000 na kila mtu, ikiwa ni pamoja na wachumi wasomi wote walikubaliana na mwelekeo wa nchi yetu. Mipango yote ya IMF ilipangwa wakati huo ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa kodi.. bado serikali ilikuwa ikisomesha watoto wetu bure na huduma muhimu kama Afya na maji vilikuwepo..

Hakuna ushahidi wowote unaoweza kusema mwalimu alimzuia Mkapa kuwafuata WAZEE na kusaka wachawi..Ni ajabu kwa Mkapa kuanza kusaka wachawi wakati inajulikana kabisa alikuwa mwadilifu wakati mwalimu akiwa hai..
Baada ya kifo cha Nyerere ambacho nina mashaka sana kama Mkapa hahusiki kwa kumpandisha pressure mzee wetu (Mungu anisamehe), ndipo Mkapa alipoanza kututoa Kapa..Huwezi kabisa kujenga uchumi wa nchi kama Infrastructure (miundombinu) mibovu na wala hakuna strategy ya ujenzi wa infrastucture kuwezesha nchi kujiendeleza..
Nimeuliza watu kibao ambao wanamsifia Mkapa wanambie ni miundombinu ipi ya KITAIFA ambayo Mkapa alijenga wanambie hata Mmoja wapo!....HAKUNA..
Alichofanya Mkapa ni sawa na watu waliorithi nyumba za Kariakoo... kweli walikuwa maskini enzi za mwalimu lakini leo hii wameuza nyumba hizo ili kupata mtaji wa biashara na biashara zenyewe ni kwenda China kuleta nguo na madawa feki!..
It's exactly what Mkapa did!..badala ya kuijenga nchi katuuzia madawa feki ya uchumi na wananchi tuna hesabu na kusifia kuuza nyumba ya Kariakoo iliyojengwa kwa thamani ya Dollar 2,000 imeuzwa kwa dollar 400,000 kwa mhindi ambaye kesho atawapangisha Apt. kwa gharama ya dollar 1000 kwa mwezi with downpayment ya mwaka mzima na contract ya miaka mitatu..Huyo muhindi kajenga ghrofa yenye apartment 20, hivyo ataingiza 720,000 within 3 years..Akili yetu inashindwa kuona 720,00 kwa miaka mitatu na umiliki wa ardhi against 400,000 tulizopokea.
Kwa ujinga na umaskini wetu sisi tunatazama kilichopo mezani na individual, Akili yetu finyu inatutuma kuamini kuwa what is 36,000 kwa miaka mitatu kama utaweza kupata 400,000 kwa mkupuo!
Ndivyo hata serikali yake ilijisifiwa kwa ongezeko la pato la taifa kwa sababu madini yetu kama dhahabu yalikuwa hayana thamani chini ya ardhi sawa na nyumba ya Kariakoo, hivyo katutoa toka zero hadi kukusanya mamillioni Wadanganyika tuliona Mkapa ndiye mwenye akili sana..
Kisha basi, iweje leo tunafurahia kufikishwa kwa mafisadi mahakamani ikiwa kweli Mkapa alifanya kazi nzuri?
 
Wazalendo, habari za hapa Jamvini

Kwa maoni yangu binafsi, nadhani Rais Mstaafu Mkapa alijitahidi kufanya mengi mazuri. Matatizo mengi ambayo Rev. ameyanyambulisha yanatokana na loopholes ya baadhi ya sheria zetu, usimamizi na uwajibikaji.

Hebu tuangalie USA wakati Bill Clinton alipokuwa na Sex Scandal na Monica, kwa sababu ya sheria, usimamizi na uwajibikaji uliokuwepo wa watu na Institutions mbalimbali bado tunaona ni namna gani suala lake lilishughulikiwa. Jiulize kama ingekuwa Tanzania lililofanyika kule lingewezekana?

Yawezekana Mkapa alishindwa kusimamia mambo yote au kulikuwa na loopholes ambazo si vema zikaachwa tena.

Natoa hoja ni vema sheria zetu nyingi ziangaliwe na kupitiwa upya, pia kuwe na machanism ya kuwafanya watu wawajibike kuliko ilivyo sasa ambapo watu wakipata loopholes wanazitumia.

Swali langu kwa wote ambalo ni kuhusiana na Utashi na Uzalendo ni hasa katika suala zima la UFISADI: Je, ikiwa kuna loop hole ya wazi ya kujinufaisha binafsi na ambayo at that time umeiona na unadhani kuwa hakuna mtu wa kukuzuia au kukushika au kukushitaki, Je utaitumia au utaiacha? Kama jibu lako ni UTAIACHA basi Una Utashi Mwema na Pia ni Mzalendo, lakini kama jibu lako ni UTAITUMIA basi wewe ni POTENTIAL FISADI kama mafisadi wengine ila tu hujapata opportunity ya kuonyesha ufisadi wako.
 
rev. Kishoka,

Swala la kumuondolea kinga Mkapa na kumpeleka mahakamani ni hoja finyu na hatari. Kama Mkapa alifanya makosa akiwa rais, basi rais aliyeko madarakani atengue maamuzi hayo na kuyarekebisha. Tuchukue mfano rahisi, wamarekani wamemchagua Obama kuwa rais wao katika kipindi kigumu kabisa. Rais Bush amefanya maamuzi mengi mabaya ambayo yameitumbukiza Marekani na dunia katika msukosuko mkubwa sana, lakini kamwe hautasikia wamarekani wakisema Bush aburuzwe mahakamani kama ambavyo wengi wetu hapa tunavyomshupalia Mkapa aburuzwe kisutu! na hautasikia kamwe Obama akisema 'amerithi' matatizo ya nchi kutoka kwa Bush, wamerekani watampima kwa uwezo wake wa kutatua matatizo yao na sio kwa kisingizio cho chote kile. Vile vile JK hatakiwi kutoa lawama zozote kwamba amerithi matatizo kwa Mkapa. kama kuna maamuzi yeyote mabaya aliyofanya Mkapa, basi atengue (reverse) na abadilishe.
Kumpeleka Mkapa mahakamani kuta -set precedence, ambapo baada ya Mkapa atafuata mzee ruksa, na wakati huo huo JK akijitayarisha kutia nywele zake maji maana baada tu ya kumaliza kipindi chake naye ataburuzwa mahakamani!
kinachotakiwa kufanyika kama nilivyosema ni kutengua maamuzi yote mabaya aliyofanya Mkapa akiwa madarakani tu!

nawasilisha.

Mrefu,

Sisi ni Tanzania si Marekani. Ikiwa raia wa Marekani wameazimia kuwa Rais wao alifanya mambo na wao wanayaona ni sawa, basi hilo ni lao. Zaidi ni kuwa Marekani unayoisifia imejijenga kwa kutumia mihimili yote mitatu ya Serikali (Executive, Judiciary and Legislative) ambayo ina uwezo sawa na kila mmoja ina uwezo wa kuhakiki chombo kingine.

Nikukumbushe jinsi gani Marekani ilivyoendelea, Nixon aliondolowa madarakani na Bunge na akakimbilia kujiuzulu. Clinton alipigiwa kura ya kutokuwa na imani na bunge (impeach) alipotoa kiapo na kudanganya aikiwa chini ya kiapo kuhusiana na mahusiano yake na Monica Lewinsky.

Kwa mtaji huo basi, kama Bush ameharibu, ruhusa alipewa na bunge na mahakama nayo ingeridhia kama kungekuwa na kesi imepelekwa dhidi yake.

Kwa tanzania, mfumo wetu hauruhusu hata Bunge kuihakiki Serikali kuu sembuse Rais. hivyo mfano wako ni BUTU.

Kama Tanzania ingekuwa na mfumo mzuri unaofanya kazi ambao unatoa madaraka sawa na kuwajibishana kati ya Serikali Kuu, Bunge na Mahakama, upotevu huu wa fedha uiliofanywa Benki Kuu, mikataba mibovu ya madini na hata Jeshi kujiingiza katika biashara ya dhahabu kusingetokea.

Namlaumu Mkapa kwa kuruhusu mianya hiyo ya udhaifu wa Katiba na Sheria itumike na wachache waliojinufaisha na kulihujumu Taifa. Mbaya zaidi ni vile Mkapa alivyodinda na kukataa ushauri wa kisheria na kitaalamu wa kubadili katiba na kusema Katiba an Sheria hazina kasoro yoyote!

Hivyo basi, huwezi kusema kuwa hatuwezi mfikisha Mkapa mahakamani huku yeye ndiye aliyekuwa Alpha na Omega wa kila kitu Tanzania hata kulidhibiti Bunge. Hii ina maana kuwa madaraka ya urais yana nguvu nyingi bila kuwajibishwa na anapotokea mzembe au mtu ambaye si mwajibikaji, kila siku Raia na Taifa la tanzania litaendelea kusota kutokana na kinga tunayompa Rais huku tukimpa madaraka makubwa bila kuwa na chombo cha kumwajibisha.
 
mchungaji tafadhari linda heshima yako kwa kuwa mwepesi wa kupokea hoja zinazopingana nawe.

FDR,

Mtarajiwa hakuleta hoja kujibu hoja, kaleta madai bila kujibu hoja na kushurtisha madai yake kama hoja mpya, ndiyo maana hata nimejinukuu tena kumuonyesha ni nini nilikidhamiria katika hoja hii.
 
FDR,

Mtarajiwa hakuleta hoja kujibu hoja, kaleta madai bila kujibu hoja na kushurtisha madai yake kama hoja mpya, ndiyo maana hata nimejinukuu tena kumuonyesha ni nini nilikidhamiria katika hoja hii.


Naomba nikuulize mchungaji, hivi JK hakuwahi kuwa waziri katika serikali ya Mkapa? Kama Mkapa aliendesha serikali corrupt JK ni msafi kiasi gani kuweza kumfikisha Mkapa mahakamani?

Nakubalina na wewe kwa kitu kimoja tu kuwa Mkapa alifanya makosa. Na hapa nakupa angalizo siyo Mkapa peke yake viongozi wetu wengi (wakiwemo marais wamekuwa wakifanya makosa na wanaendelea kufanya makosa). Kwa hiyo kumpa JK kisingizio kuwa mambo mengi yameharibika kwa sababu ya Mkapa ni ukosefu wa kufikiri. Ni jukumu lake kurekebisha hayo makosa na kufanya kazi yake sawa sawa. Lakini biashara ya kumwondoa JK katika serikali ya Mkapa ni unafiki usiovumilika kati ya watu wenye kufikiri.

Tumpe hadidu za rejea JK za kufanya kazi, na siyo kazi ya kukamata kamata (bila kujenga mfumo wa utawala bora) wakati Dar inakosa maji, wanafunzi wanafukuzwa na kuteua mawaziri ambao hata hawajui majukumu yao ni nini.
 
Naomba nikuulize mchungaji, hivi JK hakuwahi kuwa waziri katika serikali ya Mkapa? Kama Mkapa aliendesha serikali corrupt JK ni msafi kiasi gani kuweza kumfikisha Mkapa mahakamani?

Nakubalina na wewe kwa kitu kimoja tu kuwa Mkapa alifanya makosa. Na hapa nakupa angalizo siyo Mkapa peke yake viongozi wetu wengi (wakiwemo marais wamekuwa wakifanya makosa na wanaendelea kufanya makosa). Kwa hiyo kumpa JK kisingizio kuwa mambo mengi yameharibika kwa sababu ya Mkapa ni ukosefu wa kufikiri. Ni jukumu lake kurekebisha hayo makosa na kufanya kazi yake sawa sawa. Lakini biashara ya kumwondoa JK katika serikali ya Mkapa ni unafiki usiovumilika kati ya watu wenye kufikiri.

Tumpe hadidu za rejea JK za kufanya kazi, na siyo kazi ya kukamata kamata (bila kujenga mfumo wa utawala bora) wakati Dar inakosa maji, wanafunzi wanafukuzwa na kuteua mawaziri ambao hata hawajui majukumu yao ni nini.



Hivi kuna matatizo gani kujenga hoja kwa kutumia facts? Rev. Anajenga hoja zake kwa Mkapa na makosa aliyoyafanya.

Kwa mfano: kama Rev anatoa hoja kuwa Mkapa alijiuzia Kiwira. Unachotakiwa ni kusema kuwa Mkapa hakununua Kiwira, au anayo haki kama mtu mwingine kununua Kiwira. Na baadaye weka facts ku-support hoja zako.

Pili rais sio mwendesha mashitaka wa serikali. Anayewatia watu ndani ni DPP.

Mfumo wa utawala bora ni mzuri kama watendaji wanaoutumia. Hivyo hakuna sababu ya watanzania kufikiri kuwa na mfumo wa utawala mzuri wakati watendaji wenyewe ndio wanaonunua mitambo mibovu ya umeme. Kuiba kutoka katika akaunti za serikali n.k.
 
Ni kwelikuwa mbegu za rushwa zilipandwa na Mwinyi, lakini mimi nadhani hana haja ya kulaumiwa kwani alijaribu alichoweza na huend hapo palikuwa ukomo wa uwezo wake kimaono na kiutendaji.

Mkapa sivyo, alifanya uhujumu huu kwa makusudi na tene kwa kujua na kupanga vema. Ninaamini kabisa kuwa alikuwa bikira kwa suala la rushwa katika madaraka yake kabla ya uraisi na hata katika miaka mitano ya kwanza. Lakini huyu jamaa akageuka, akawa dictetor, akatishia vyombo vya habari, akajinyakulia rasilimali za nchi hii kuanzia nyumba za serikali na kuwaacha wngine wanyanganyane mali ya nchi hii kama ya marehemu. Mifano mingi imeelezwa.

Kwa hivi, nivema kabisa akaondolewa kinga akapelekwa na kama ni mimi awe mpangaji wa kudumu keko. Kwanza kwa kuvunja kiapo chake amejiondolea kinga kwasababu hakufanya kama alivyoapa.

Je kama ka mchezo ni kuhujumu nji hii katika kipindi cha pili je JK atafanya nini? Au ndo maana hataki kuwapeleka hawa?
 
Kwa nini usianzishe thread yako ukawajadili Mwinyi na Mama Sitti? au ukaanzisha thread kusifu aliyofanya Mkapa? kwa nini utulazimishe kuongea unalotaka na usilianzishie hoja?

Kwanini unamtaka Mtarajiwa aanzishe thread wakati wewe umeshaianzisha. Anachofanya hapo ni kukujibu shutuma zako, kwa maoni yake. Kama wewe hukubaliani nayo, si umjibu tu?

Kushtakiwa Mkapa ni ndoto za alinacha. Ni afadhali kutumia muda wenu kufikiria mambo mengine, maana hilo halitatokea. Mnajaribu kumfanya Rais wetu kuwa hajui analofanya. Mnakosea sana. Na wengine mnajua kabisa kuwa akifuata ushauri wenu, nini kitakachotokea. Mnataka kujenga wanasiasa wasiojengeka na kutoa fursa za vyama vya upinzani kujikweza. Taifa gani manalolitaka kwa kuliteketeza?
 
Kwanini unamtaka Mtarajiwa aanzishe thread wakati wewe umeshaianzisha. Anachofanya hapo ni kukujibu shutuma zako, kwa maoni yake. Kama wewe hukubaliani nayo, si umjibu tu?

Kushtakiwa Mkapa ni ndoto za alinacha. Ni afadhali kutumia muda wenu kufikiria mambo mengine, maana hilo halitatokea. Mnajaribu kumfanya Rais wetu kuwa hajui analofanya. Mnakosea sana. Na wengine mnajua kabisa kuwa akifuata ushauri wenu, nini kitakachotokea. Mnataka kujenga wanasiasa wasiojengeka na kutoa fursa za vyama vya upinzani kujikweza. Taifa gani manalolitaka kwa kuliteketeza?


Rectu,

Hivi ukienda mahakamani ukafunguliwa mashitaka ya ugoni huanza utetezi kwa kusema wewe ni meneja?
 
Mazee Ni kweli kabisa Mukapa aliteleza kama mwanadamu wa kawaida.

Lakini nguvu na ushabiki wa kishindo namuma hii kutaka mukapa awajibishwe unatoka wapi?kuna walaikini,yeah,kuna uwalakini....kwani inaboa kupita kiasi kumwandama Mkapa kwa degree hii,hasa ukizingatia amejitahidi kutuletea maendeleo ya uhakiaka ukilinganisha na marais waliopita na hata aliyeko sasa madarakani ni kilza tuuuuuuuu.

1.Mwinyi alitupeleka kubaya kuliko,nchi ilijaa matatizo ya kila aina.Mfano ulio hai,ni kitendo cha mkewe kuwa kinara wa kuuza madawa ya kulevya hapa nchini,haingii akilini kuona kila kiumbe kinafoka juu ya MKAPA wakati kuna uozo wa karne umefanya na viongozi wengi tuuu hapa nchini.
2.Kero na migogoro ya kidini,iliota mizizi ndani ya kipindi cha Mwinyi na sasa tunashuhudia JK akiiendeleza kwa style yake.why Mukapa mazeee?...udini au?
3.Mwinyi huyu huyu ndie alietaka kuibadilisha TZ kuwa the united islamic republic of TZ,leo hatuhoji,...tunamfokea Mukapa mukapa...why?
Mizizi hii ya mwinyi imedumu hadi sasa na JK anataka kutusilimisha nchi nzima bila aibu tujiunge na OIC,bt we don't see..tumebaki mukapa mubaya mubaya....
4.JK mwenyewe ana mabaya yake kupitiliza,laikini hatuyapi msukumo tunaouumia zidi ya nkapa...

$$$$mukapa ana mabaya yake,hao wachache nao wana maovu yao,hivyo iko haja ya kuhoji kila pande,si jambo jema kumwandama MUKapa.

fair game mazeee
 
Mazee Ni kweli kabisa Mukapa aliteleza kama mwanadamu wa kawaida.

Lakini nguvu na ushabiki wa kishindo namuma hii kutaka mukapa awajibishwe unatoka wapi?kuna walaikini,yeah,kuna uwalakini....kwani inaboa kupita kiasi kumwandama Mkapa kwa degree hii,hasa ukizingatia amejitahidi kutuletea maendeleo ya uhakiaka ukilinganisha na marais waliopita na hata aliyeko sasa madarakani ni kilza tuuuuuuuu.

1.Mwinyi alitupeleka kubaya kuliko,nchi ilijaa matatizo ya kila aina.Mfano ulio hai,ni kitendo cha mkewe kuwa kinara wa kuuza madawa ya kulevya hapa nchini,haingii akilini kuona kila kiumbe kinafoka juu ya MKAPA wakati kuna uozo wa karne umefanya na viongozi wengi tuuu hapa nchini.
2.Kero na migogoro ya kidini,iliota mizizi ndani ya kipindi cha Mwinyi na sasa tunashuhudia JK akiiendeleza kwa style yake.why Mukapa mazeee?...udini au?
3.Mwinyi huyu huyu ndie alietaka kuibadilisha TZ kuwa the united islamic republic of TZ,leo hatuhoji,...tunamfokea Mukapa mukapa...why?
Mizizi hii ya mwinyi imedumu hadi sasa na JK anataka kutusilimisha nchi nzima bila aibu tujiunge na OIC,bt we don't see..tumebaki mukapa mubaya mubaya....
4.JK mwenyewe ana mabaya yake kupitiliza,laikini hatuyapi msukumo tunaouumia zidi ya nkapa...

$$$$mukapa ana mabaya yake,hao wachache nao wana maovu yao,hivyo iko haja ya kuhoji kila pande,si jambo jema kumwandama MUKapa.

fair game mazeee

Kesi ya Panya mahakamani inasema Panya amekula mahindi na kumwaga maziwa mchangani. Wewe unadai mbona fisi na kunguru nao walikojoa? Huo ni utetezi au ni kutoelewa kesi?

Kama una ushahidi kuwa Panya hakula mahindi au kumwaga maziwa, toa ushahidi si kusingizia fisi na kunguru kukojoa barabarani!
 
Na Emmanuel Lengwa, Jijini

Baada ya Rais Mstaafu Benjamin Mkapa kutuhumiwa sana kuwa yeye na aliyekuwa Waziri wake wa Nishati na Madini Bw. Daniel Yona walijiuzia kwa bei poa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira, hatimaye suala hilo limefikia arobaini yake kwani sasa litaanikwa hadharani na kujadiliwa kipengele kimoja baada ya kingine.

Aidha, wabunge kibao wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanadaiwa kuwa wameshajipanga katika kulijadili kwa undani suala hilo, ambalo linadaiwa kuwa limejaa utata na kuna wakati lilizusha mjadala wa aina yake bungeni.

Kufikia kwa arobaini ya sakata hilo linalodaiwa kumhusisha zaidi Mkapa na Yona, kunatokana na taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini Bw. William Ngeleja, aliyesema kuwa ripoti kamili juu ya suala la Kiwira iko tayari na kilichobaki ni kuiwasilisha bungeni.

Lakini, baada ya Waziri Ngeleja kusema hayo na kisha Spika wa Bunge kukaririwa vilevile akisema kuwa Bunge linaisubiri kwa hamu ripoti hiyo na nyingine kadhaa, baadhi ya wabunge wamedaiwa kuwa tayari wamejipanga vilivyo katika kumlipua Mkapa na wengine wanaodaiwa kushiriki katika kuuza kwa bei poa mgodi huo wa Kiwira.

Chanzo chetu kimoja kimedai kuwa bila woga wala kumuonea haya mtu yeyote, baadhi ya wabunge wamepania kulijadili kwa kina suala hilo na hatimaye kutetea raslimali za taifa.

``Kuna mambo mengi yanayotia shaka juu ya uuzwaji wa raslimali za taifa... sasa kuna wabunge kibao waliojipanga katika kuhakikisha kuwa suala hili linajadiliwa bila kufunikwafunikwa,`` kikadai chanzo hicho.

Hatahivyo, akizungumza na Alasiri leo asubuhi, Mbunge aliyeliibua sakata hilo bungeni na kuwatuhumu wazi Mkapa na Yona, Mhe. Aloyce Kimaro wa Jimbo la Vunjo (CCM), amedai kuwa taarifa hiyo ya Mgodi wa Kiwira anaisubiri kwa hamu bungeni na kwa sababu kila kitu kiko wazi, anaamini kuwa Serikali haitaficha kitu.

Mheshimiwa Kimaro amesema kuwa suala hilo litakapotua bungeni, yeye binafsi atahakikisha kuwa, kama walivyo wabunge wengine, atapigania kwa kila namna kuona kuwa sasa mgodi huo unamilikiwa kihalali.

Akasema hivi sasa, suala sio mmiliki wa mgodi ni nani, bali ni kuona mgodi huo unamilikiwa kihalali na unafanya kazi iliyokusudiwa ili kutimiza malengo ya kuanzishwa kwake.

Akaongeza kuwa kipindi hiki ni cha kusafisha uchafu wote wa ufisadi ili baada ya hapo, nchi ianze kuzungumzia namna ya kujiletea maendeleo.

``Hiki ni kipindi cha kusafisha uchafu. Tuweke mambo yote kwenye mstari, uchafu ufike mwisho na kisha tuanze kupigania zaidi maendeleo yetu,`` akasema Bw. Kimaro.

Akasema lengo ni mgodi huo ufanye kazi ya uzalishaji kama ilivyokusudiwa na kuwa wale wote waliokuwa wakiuchezea kwa madai ya kujiuzia kwa bei poa, sasa wavune walichopanda.

Naye Mbunge wa Viti maalum kupitia CHADEMA, Mheshimiwa Halima Mdee, amedai kuwa ikiwa taarifa hiyo ya Mgodi wa Kiwira itakuwa na maudhui kama watu wengi wanavyolifahamu sakata la mgodi wa Kiwira, inabidi wahusika wake wachukuliwe hatua kama walivyoanza kuchukuliwa watuhumiwa wa wizi wa fedha za Akauti ya Malipo ya Madeni ya Nje, EPA.

``Tunaisubiri kwa hamu taarifa hiyo. Na kama kweli itafanana na taarifa tuliyonayo kuhusu mgodi huo, sioni kama `treatment` yao itatofautiana na ile ya watuhumiwa wa EPA,`` akasema Mheshimiwa Halima.

Akadai kuwa ikiwa sheria za nchi zitafuatwa, ni dhahiri kuwa wahusika kwa kujimilikisha mgodi kinyume cha taratibu ni kosa la jinai na kuwa hawafai kuendelea kuumiliki.

``Kama walinunua kinyume cha utaratibu, hawana uhalali wa kumiliki mgodi huo,`` akasema.

Akaongeza Mheshimiwa Halima kuwa yeye anatarajia kuona wabunge wote wakipitisha maazimio ya kuwanyang`anya wahusika mgodi huo na kuurejesha Serikalini, ili taratibu na sheria zifuatwe.

Kwa taarifa zilizowahi kutolewa na Mheshimiwa Kimaro Bungeni, ni kwamba Mgodi huo uliuzwa kwa bei poa ya shilingi milioni 700 kwa kampuni ambayo wamiliki wake ni pamoja na Mkapa na Yona.

Cha kusikitisha zaidi, ilidaiwa kuwa licha ya kampuni husika kuuziwa kwa bei hiyo poa, bado ililipa Sh. Bilioni 70 pekee.

Hata hivyo, madai hayo yatakuja kubainika kuwa ni ya kweli au la baada ya ripoti kamili kuhusu Mgodi wa Kiwira kutolewa bungeni kama alivyoahidi Waziri Ngeleja.
* SOURCE: Alasiri
😉

Huu mchele, una mawe!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom