Ngoja turudi nyuma:
(a) Mwishoni mwa utawala wa Mwinyi, wahisani waliitishia kusitisha misaada kutokana na misamaha ya kodi. Ndipo wakati huo wakaisimamia serikali kuimarisha ukusanyaji wa kodi. Hiyo iliendana na kumwondoa Professor malima kutoka kwenye Wizara ya fedha, na kuanza tartibu za kuundwa kwa TRA kama tasis inyojitegemea isiyoingiliwa na wanasiasa.
(b) kwenye mkutano wa viongozi wa G7 ( baadaye G8) uliokaa June 1995 huko ,
Halifax, Canada, pamoja na mambo mengine waliongelea jinsi ya kuzisaidia nchi maskini kiuchumi, na mojawapo ya makubaliano yao ilikuwa ni kusamehe madeni kwa nchi maskini sana ikiwemo Tanzania. Makubaliano hayo ya G7 kuhusu kusamehewa madeni hayakuwa na uhusiano wowote na utawala wa Mkapa; wakati huo Mkapa alikuwa bado ni Waziri wa Elimu ya Juu. Taarifa kamili iliyotolewa baadaye na mawaziri wa fedha wa nchi hizo kuhusiana na utaratibu wa kusamehe madeni kwa nchi fukara nimeimabatanisha hapa chini.
(c) Mkapa alipoingia madarakani, alikuta taratibu zote za uundwaji wa TRA kwa ajili kuthibiti ukusanyaji kodi na zile za G8 kuhusu kusamehe madeni na kutoa misaada zaidi kwa kwa nchi maskini zikiwa zimekamilika. Ni kutokana na mazingira hayo ndipo wahisani walipoanza kutoa fedha tena kwa utawala wa Mkapa hata wakiwa hawajui kama atakuwa ni kiongozi wa namna gani.
(d) Pamoja na kusamehewa madeni, kupewa misaada zaidi, na kuboreka kwa ukusanyaji wa kodi, Mkapa alijikita tena katika uuzaji wa mashirika ya umma hata yale ambayo yalikuwa yanafanya kazi kwa faida na nyumba za serikali kwa kisingizio cha kuwekeza na kuindoa serikali kwenye biashara. Yote haya yalichangia kwa kiasi kikubwa sana kujaza fedha kwenye sefu za serikali kuliko ilivyokuwa kwenye serikali zilizopita. Kabla sijaongelea hilo la fedha, labda nikumbushe kuwa swala la uuzwaji wa mashirika halikuwa jambo baya; ubaya wa Mkapa ni jinsi uuzwaji huu ulivyofanyika, kwani sasa kuna ushahidi kuwa kuwa rushwa ilikuwa inatumika sana kiasi kuwa maslahi ya taifa hayakuangaliwa. Mkapa akiwa na kama rais wa nchi, ilikuwa ni wajibu wake kulinda maslahi ya nchi kwa gharama yoyote ile, lakini hakufanya hivyo.
(f) Baada ya serikali kuwa inapata pesa nyingi sana kuliko serikali zote zilizoitangulia kama nilivyoeleza hapo (d), serikali ya Mkapa ilikuwa na uwezo wa kufanya mambo mengi sana ya kuindeleza nchi lakini hawakufanya hivyo. Fedha zilzotumika kwa maendelo zilikuwa ni kidogo sana kuliko zile zililotumika kwa mambo ya kuwanufaisha viongozi. Kwa mfano, kwenye bajeti ya mwaka 2001, matumizi halisi kwa ajili ya maendeleo ilikuwa ni asilimia 13 tu, nyingine zote zikiishia kwenye recurrent expenditure;
data zote ziko hapa. Mpangilio huu ni tofauti sana na bajeti ya mwaka 1970 ambapo sehemu ya maendeleo ilikuwa ni zaidi ya asilimia 30.
(g) Sasa ngoja tuliangalie hili la uchumi kukua chini ya serikali ya Mkapa. Kipimo kikubwa kinachotumika kupima ukuaji wa uchumi ni GDP. Formula itumikayo katika kukokota GDP ni hii:
GDP = Matumizi ya ndani + Uwekezaji ndani ya nchi + matumizi ya Serikali + (mauzo ya Nje − manunuzi kutoka nje)
Baada ya serikali kuwa ina pesa nyingi, matumizi ya serikali yalipanda,, na hivyo kuchangia kukua kwa GDP. Vile vile kwa vile serikali ya Mkapa iliuza ardhi yote ya madini na viwanda vyote, waliouziwa walileta vifaa vya kuwawezesha kufanya bishara zao. Hiyo iliongeza kiwango cha uwekezaji wa ndani ya nchi na hivyo kukua kwa GDP zaidi. Inawezekana pia matumizi ya ndani yaliongezeka kwa kiasi fulani lakini siyo significant sana kiasi cha kuweka dent kweny GDP kwa vile idadi kubwa ya wanachi wamebaki katika maisha ya kimaskini huku wengine wakiwa hawamudu kula milo miwili.
Mauzo yetu ya nje yaliendelea kubaki ya chini ingawa manunuzi ya nje yalikuwa makubwa lakini yakwa offset na mehsabu ya uwekezaji ndani ya nchi.