Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

Lowasa akija UKAWA mimi natoka , amechafuka , hana na wala hajawahi kuwa na fikra mpya , ndio maana hadi leo anaamini kwamba rushwa itampeleka ikulu .

Mkuu hivi Lowassa ameshakuwa na mawazo mapya tokea amehamia?
 
Mkuu upo? Hebu tupe taarifa zaidi .. hivi Dr Slaa pia alihusishwa?

LOWASSA AKWAMA AAHIRISHA KAMPENI.

Juzi kwenye mitandao ya kijamii ilisambaa taarifa kuwa MGOMBEA WA UKAWA, Ndg LOWASSA ameanguka ghafla nyumbani kwake. Taarifa hiyo ambayo haikukanushwa na familia ya LOWASSA wala Uongozi wa juu wa CHADEMA naUKAWA kwa ujumla wake bali walikuwepo wafuasi wa CHADEMA ambao walihaha (kwa maelekezo) kukanusha taarifa hiyo.

UKWELI umedhihiri, gazeti la kila siku la NIPASHE limeandika LOWASSA AKWAMA AAHIRISHA KAMPENI lakini mwandishi amepindisha ukweli katika habari hiyo, baada ya kutaja sababu halisi ya SINTOFAHAMU ya shughuli ya Uzinduzi wa Kampeni ambayo ni HALI YA AFYA YA MGOMBEA ambayo bado haijakaa sawa mpaka sasa, mwandishi anasema sababu ya SINTOFAHAMU kuwa ni kukosa eneo la mkutano.

Tanzania ina eneo la kilometa za mraba LAKI TISA NA ELFU AROBAINI NA TANO MIA MBILI NA TATU 945, 203. Ni UJUHA kudhani kuwa pamoja na eneo lote hilo UKAWA wanaweza kukosa sehemu ya kufanyia MKUTANO WA UZINDUZI wa kampeni.

DAR peke yake ina maeneo ya wazi 87, kuanzia jangwani, kidongo chekundu, mbagala, mwembeyanga, hapa haujazungumzia Kirumba, Furahisha, Nyamagana kule MWANZA. Sheikh Amri Abeid, Ngarenaro na Tindinagi kule ARUSHA yanatosha kabisa..viwanja vya Uhasibu jijini Mbeya havina kazi, na UKAWA wanadhani wataweza kuwaahadaa watanzania kwa uongo wa dhahiri kiasi hiki.

TAHADHARI kwa UKAWA, leo wameghairisha shughuli za uzinduzi wa Kampeni, ila tunakoelekea mtailazimisha Tume ya Uchaguzi (NEC) kughairisha zoezi la upigaji kura ama UCHAGUZI MKUU kabisa..
 
Japo ambalo si la siri kwamba kambi zote za wagombea uraisi CCM zinamuogopa sana Lowassa, hivyo kuna kila aina ya jitihada ya kuhakikisha jina la Lowassa halipitishwi kugombea nafasi ya uraisi.

Huku wapinzani wakijipanga kukata jina lake lakini Lowassa yeye anaendelea na mikakati yake ikiwa ni pamoja na kugawa fedha kama njugu kwani anaamini yeye ni raisi wa Tanzania 2015-2025 "PIGA UA"

Lowassa anatishia kukiua chama (CCM) endapo hata pitishwa kugombea uraisi.

Wakati huo huo, endapo jina la Lowassa halitapitishwa CCM wanyetishaji wetu wanasema mkakati wa Lowassa kugombea kupitia UKAWA kwakuwa tayari ana mtaji wa wanaCCM wengi hivyo ni rahisi kwake kushinda nafasi ya uraisi.

Inasemekana kuwa tayari Lowassa ameshaanza mazungumzo ya chini chini na viongozi wa UKAWA lakini bado hawajafikia makubaliano rasmi.

Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)

Mchunguzi Huru bado upo humu?
JF kiboko! Uliandika short and clear na ndicho kilichotokea.
 
Swali mazungumzk ya chini kwa chini yalikuwa yanafanyika baina ya nani na nani...jibu lake jwa tunaojua limetushua.
 
Swali mazungumzk ya chini kwa chini yalikuwa yanafanyika baina ya nani na nani...jibu lake jwa tunaojua limetushua.
"Ni dk Willibroad Slaa ndiye aliyewasiliana na Josephat Gwajima kuhusu Lowassa kuja chadema.Ni dk Willibrod Slaa ndiye aliyemwambia mwenyekiti kuwa lowassa akikatwa tumchukue kwakuwa ana mtaji wa wapiga kura'.Tundu Antipas Lissu
 
"Ni dk Willibroad Slaa ndiye aliyewasiliana na Josephat Gwajima kuhusu Lowassa kuja chadema.Ni dk Willibrod Slaa ndiye aliyemwambia mwenyekiti kuwa lowassa akikatwa tumchukue kwakuwa ana mtaji wa wapiga kura'.Tundu Antipas Lissu

Umeangalia tarehe ya thread hii?

Wengine huwa si rahisi kudanganywa kirahisi; mipango ilianza zamani, kikwazo walikijua wakarusha kamba ili mtu ajinyonge mwenyewe bila kujua
Wanayemrushia anaakili zaidi ya wakufunzi wake.

Mafisadi ni wajanja sana, ila Mungu ni full stop yao.... Mwaka huu wamekula matango pori.... Subiri uone wanavyodondoka kwa kosa dogo ambalo mpaka sasa hawajaligundua.
 
Natamani kuona wachingiaji wa hii thread wakichangia tena baada ya unabii kutimia
 
kapige mswaki kaka maana inaonekana ulikuwa usingizi..

unadhani ukawa ni kwepesi kivile?..
akijiloga akaingia tu ataambiwa akagombee udiwani ili wampime imani km kweli ni kamanda
rugemaa maneno yako hukuweka expire date nadhani..
 
Last edited by a moderator:
Piga ua Rais Ajaye Wa Tanzania Ni Kati Ya Watu Hawa :

1. Sospeter Muhongo.....15%
2.Stephen Wassira.....20%
3. Jaji Augustino Ramadhani.....5%
4. John Magufuli.........60%

Makamu Wa Rais Iwe Isiwe Amepangwa Kuwa Mzee Samuel Sitta



NB. Endapo Hii Itabadilika Basi Mjue 100% UKAWA Wanashika Hatamu Na Padre Wangu Wilbroad Slaa Kuwa Rais Wangu Mpya.
Hii sikuiona
 
Back
Top Bottom