Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

Mkakati: Lowassa kuhamia UKAWA

Wengine tulikuwa na msimamo huo miaka yote na tunasema Ukawa wametusaliti! Wamegeuka kuwa wasaka tonge! Wazalendo kama akina Dr Slaa wamekaa pembeni, wale wa maslahi ndo wamejaa tele humo kwa sasa.
 



Tumeamua kuungana na maamuzi ya viongozi wetu wa UKAWA kumsapoti Lowasa kama mgombea uraisi kwetu ambalo tuliona haliwezekeni sasa limewezekana kumbe kwenye siasa hakuna urafiki wala uadui wa kudumu lakini bado lengo ni kuitoa ccm madarakani naamini tutafanikiwa huo ndo msimamo wangu




Mkuu Mzee Mwanakijiji, nakubaliana na wewe, hata mimi ningependa kuwasikia, kwanza waliosema hili haliezekani, baada ya kuwezekana leo wanasemaje?!. Kuna waliosema hili likitokea watahama, limetokea lakini hadi leo hawajahama, jee bado wanasubiri nini?!, ila pia kuna waliosusa na kuamua kujinyamazia kimya, tungependa kuwasikia leo wanasimama wapi?!.

Pasco
[/QUOTE]

Hahahaa kuleni matapishi yenu!
Tutafukua makaburi kuonyesha kuwa hamna msimamo ni wasaka tonge! Mtazidi kupata aibu.
Wenye misimamo ya dhati tunaendelea kusema hatuwezi kumpokea fisadi papa na kumsafisha!
Hamuwezi kusema lengo ni kuitoa CCM bila kueleza WHAT DO YOU STAND FOR?
Mkishika nchi labda mtakuwa WORSE than CCM hata hiyo ni change? Hapana mme-fail big time!
 
Mtoa mada umeongelea Lowassa 'kugawa pesa kama njugu' ili awe rais. Nakukumbusha kuwa UKAWA haihitaji mgombea mwenye sifa kama hiyo! Na siyo mgombea tu, bali haihitaji hata mwanachama wa kawaida tu kuwa na hiyo sifa ya kutoa rushwa.
Kamanda hapa ulikuwa unaongea kama nani?
 
Japo ambalo si la siri kwamba kambi zote za wagombea uraisi CCM zinamuogopa sana Lowassa, hivyo kuna kila aina ya jitihada ya kuhakikisha jina la Lowassa halipitishwi kugombea nafasi ya uraisi.

Huku wapinzani wakijipanga kukata jina lake lakini Lowassa yeye anaendelea na mikakati yake ikiwa ni pamoja na kugawa fedha kama njugu kwani anaamini yeye ni raisi wa Tanzania 2015-2025 "PIGA UA"

Lowassa anatishia kukiua chama (CCM) endapo hata pitishwa kugombea uraisi.

Wakati huo huo, endapo jina la Lowassa halitapitisBhwa CCM wanyetishaji wetu wanasema mkakati wa Lowassa kugombea kupitia UKAWA kwakuwa tayari ana mtaji wa wanaCCM wengi hivyo ni rahisi kwake kushinda nafasi ya uraisi.

Inasemekana kuwa tayari Lowassa ameshaanza mazungumzo ya chini chini na viongozi wa UKAWA lakini bado hawajafikia makubaliano rasmi.

Posted by: MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)

Hongera mkuu kwa andiko lako. Ulichosema kimetimia. Intelligensia yao ipo juu sana
 
ukiona mtu anamsifu mtu mchafu kama Lowassa ujue yeye ni mchafu zaidi raisi ajaye chaguo la watanzania ni DR Slaa pekee yake hana skendo za wizi kama ccm
Wewe Mbowe akikijua utajuta.
 
Back
Top Bottom