Uncle Rukus
JF-Expert Member
- Jun 16, 2010
- 2,415
- 398
Wachetani ni wachetani tu.Maggid lini uliuza roho yako kwa shetani?
Wachetani ni wachetani tu.Maggid lini uliuza roho yako kwa shetani?
Tatizo la Mjengwa ni shule.Anajitahidi sana kujitambulisha kama mwandishi wa makala mwenye upeo mkubwa ilhali ametawaliwa na na udini na mapenzi yaliyokubuhu kwa Kikwete.Laiti angekuwa na upeo stahili,asingekurupuka na takwimu outdated.Yeye na JK wake wanatufanya Watanzania wajinga,wanaamini chochote watakachosema kitakuwa hivyo.
Ni mlevi pekee anayeweza kudai eti CUF itashika nafasi ya pili bara....unless huo ndio mkakati wa Usalama wa Taifa,kuiba kura za Chadema ziiwezesha CCM kushinda na zitakazosalia wapewe CUF.
Dawa ya wababaishaji kama Mjengwa ni kuwapuuza tu.Huyu hana tofauti na Sheikh Yahya
Ama hawa wachadema bado wamelala ,hivi wanasahau kuwa CUF ni kinara wa siasa hapa Tanzania ,CUF imeikomalia Zanzibar ,chadema mnapoambiwa kuwa badu nyinyi ni watawaliwa basi mkubali tu hamna na hamuwezi kufanya siasa angalau kuikaribia CUF ,maggid amewagusa na amewapopoa vibaya sana pale alipowambia kuwa hata nafasi ya tatu hamuipati, waulizeni CUF itawambia vipi wanakutoa kapa ?
Na Maggid Mjengwa,
Mwalimu Nyerere alipata kusimulia kisa cha mbwa wa Manzese. Nilikuwa bado kijana mdogo sana niliposikia kisa kile. Ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 80. Ni kwenye kilele cha Sherehe za Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi. Sherehe zile zilifanyika pale Uwanja wa Taifa. Nilibahatika kuwapo uwanjani.
Baadhi ya mabango ya wafanyakazi yaliyopita mbele ya Mwalimu siku ile yaliwakilisha ujumbe juu ya hali ngumu ya kimaisha iliyokuwa ikiwakabili wafanyakazi; mishahara midogo na mengineyo.
Wakati huo, Serikali ya Mwalimu ilikataa masharti ya Shirika la Fedha Duniani na Benki ya Dunia pia. Hii ni kwa sababu, licha ya athari nyingine mbaya kwa masharti hayo kwa nchi yetu, uhuru wetu wa kujiamulia mambo yetu nao ulikuwa hatarini.
Ilipofika wakati wa kutoa hotuba yake, Mwalimu Nyerere alisema;
" Ndugu zangu watu wa Dari Salama ebu nisikilizeni; kulikuwa na mbwa wawili, mmoja wa Manzese na mwingine wa Oysterbay. Ikatokea siku moja mbwa wa Manzese akatembea hata akafika Oysterbay.
Kwenye moja ya nyumba za huko Oysterbay akamwona mbwa mwenzake aliye ndani ya geti. Mbwa yule wa Manzese akasogea getini huku akimshangaa mbwa wa Oysterbay. Mbwa yule wa Oysterbay alinenepeana huku manyoya yake yakiwa yameteremka hadi machoni. Mbwa wa Oysterbay naye alimshangaa mwenzake wa Manzese. Mbwa yule wa Manzese alionekana kukondeana huku masikio yake yakiwa yameteremka hadi shingoni. Mbwa wa Oysterbay kwa mshangao akamwuliza mwenzake wa Manzese; " Hivi nawe ni mbwa kama mimi?!
"Naam, miye ni mbwa kama wewe." Alijibu mbwa wa Manzese.
" Sasa mbona umekondeana hivyo, njoo humu ndani kwa bwana wangu nawe uwe kama mimi."
Mbwa wa Manzese akajibu;
" Lakini wewe umefungiwa, mwenzio niko huru!"
Sitakisahau kamwe kisa kile alichosimulia Mwalimu Nyerere pale Uwanja wa Taifa. Naamini katika alichokisema Mwalimu. Nitaendelea kuamini hivyo hata katika muda wangu uliobaki humu duniani. Mwalimu alizungumzia dhana ya uhuru. Ingawa ni neno fupi sana, lakini neno uhuru lina maana kubwa. Asiye na uhuru ni mtumwa.
Mimi ni mtu huru. Na siku zote nimepigania nibaki kuwa mtu huru. Kwa uhuru kabisa nakutana na kuongea na watu wengi; vijijini na mijini. Nakutana na kuongea na wasomi na wasio wasomi, matajiri na masikini. Sijapata maishani mwangu kulazimishwa au hata kulipwa ujira ili niongee au niandike mawazo yasiyo yangu au nisiyokubaliana nayo.
Ni bahati mbaya pia, katika jamii yetu, kila anayeandika makala magazetini kama nifanyavyo, basi, atasemwa kuwa ni mwandishi wa habari. Wengi hawatofautishi baina ya mwandishi wa habari na mwandishi wa makala.
Napenda sana kuandika fikra zangu huru kwa azma ya kuchochea mijadala. Jana niliandika fikra zangu kwenye Jamii Forums. Nimefanya hivyo huko nyuma. Lakini jana nimepata watu wengi walioshiriki mjadala. Wametoa fikra zao, kuna walionitukana pia. Nimeshazoea. Nayasoma matusi hayo, nikiamini, hata kwenye matusi hayo kuna cha kujifunza. Kufahamu fikra za watoa matusi hayo.
Na hakika, kuna wanaofikiri wananifahamu. Wamenipa majina, wamenihusisha na huyu na yule. Kimsingi hawanijui. Wamekuwa ni wakandamizaji wa fikra huru na wanaamini kila anayeandika mawazo yasiyofanana na yao, basi, amenunuliwa. Huu ni udhaifu, ni unyonge wetu pia. Hatujiamini.
Nitaendelea kuandika fikra zangu huru, napenda sana kuandika mawazo yangu. Nimefanya hivyo tangu nikiwa Sekondari pale Tambaza, tena kwa kuazisha kijarida cha shule. Niliandika mwenyewe kwa mkono, nilikuwa na wasomaji wangu pia. Tuliokuwa nao Tambaza miaka ile ya 80 ni mashahidi wa hilo.
Najua kuwa wakati mwingine kuna wanaokerwa na niandikayo. Hao wapo siku zote. Hatuwezi kufanana kimitazamo. Na tumekuwa wepesi sana, kila tusomapo mawazo ya mtu, kutafuta droo ya kabati la kumpachika. Siku hizi kuna droo za CCM, CHADEMA, CUF, Uislamu, Ukristo, Uchaga, Usukumuma na kadhalika.
Na ni bahati mbaya sana, kuwa wengi tumeisahau "Droo ya Tanzania". Hii ni droo muhimu sana na ilipaswa iwe ya kwanza. Kwa kila tutendalo liwe kwa MASLAHI YA TANZANIA KWANZA. Maslahi ya Taifa. Na Hilo Ni Neno La Leo.
Maggid,
Iringa,
mjengwa
Na Maggid Mjengwa,
Mwalimu Nyerere alipata kusimulia kisa cha mbwa wa Manzese. Nilikuwa bado kijana mdogo sana niliposikia kisa kile. Ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 80. Ni kwenye kilele cha Sherehe za Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi. Sherehe zile zilifanyika pale Uwanja wa Taifa. Nilibahatika kuwapo uwanjani.
Baadhi ya mabango ya wafanyakazi yaliyopita mbele ya Mwalimu siku ile yaliwakilisha ujumbe juu ya hali ngumu ya kimaisha iliyokuwa ikiwakabili wafanyakazi; mishahara midogo na mengineyo.
Wakati huo, Serikali ya Mwalimu ilikataa masharti ya Shirika la Fedha Duniani na Benki ya Dunia pia. Hii ni kwa sababu, licha ya athari nyingine mbaya kwa masharti hayo kwa nchi yetu, uhuru wetu wa kujiamulia mambo yetu nao ulikuwa hatarini.
Ilipofika wakati wa kutoa hotuba yake, Mwalimu Nyerere alisema;
" Ndugu zangu watu wa Dari Salama ebu nisikilizeni; kulikuwa na mbwa wawili, mmoja wa Manzese na mwingine wa Oysterbay. Ikatokea siku moja mbwa wa Manzese akatembea hata akafika Oysterbay.
Kwenye moja ya nyumba za huko Oysterbay akamwona mbwa mwenzake aliye ndani ya geti. Mbwa yule wa Manzese akasogea getini huku akimshangaa mbwa wa Oysterbay. Mbwa yule wa Oysterbay alinenepeana huku manyoya yake yakiwa yameteremka hadi machoni. Mbwa wa Oysterbay naye alimshangaa mwenzake wa Manzese. Mbwa yule wa Manzese alionekana kukondeana huku masikio yake yakiwa yameteremka hadi shingoni. Mbwa wa Oysterbay kwa mshangao akamwuliza mwenzake wa Manzese; " Hivi nawe ni mbwa kama mimi?!
"Naam, miye ni mbwa kama wewe." Alijibu mbwa wa Manzese.
" Sasa mbona umekondeana hivyo, njoo humu ndani kwa bwana wangu nawe uwe kama mimi."
Mbwa wa Manzese akajibu;
" Lakini wewe umefungiwa, mwenzio niko huru!"
Sitakisahau kamwe kisa kile alichosimulia Mwalimu Nyerere pale Uwanja wa Taifa. Naamini katika alichokisema Mwalimu. Nitaendelea kuamini hivyo hata katika muda wangu uliobaki humu duniani. Mwalimu alizungumzia dhana ya uhuru. Ingawa ni neno fupi sana, lakini neno uhuru lina maana kubwa. Asiye na uhuru ni mtumwa.
Mimi ni mtu huru. Na siku zote nimepigania nibaki kuwa mtu huru. Kwa uhuru kabisa nakutana na kuongea na watu wengi; vijijini na mijini. Nakutana na kuongea na wasomi na wasio wasomi, matajiri na masikini. Sijapata maishani mwangu kulazimishwa au hata kulipwa ujira ili niongee au niandike mawazo yasiyo yangu au nisiyokubaliana nayo.
Ni bahati mbaya pia, katika jamii yetu, kila anayeandika makala magazetini kama nifanyavyo, basi, atasemwa kuwa ni mwandishi wa habari. Wengi hawatofautishi baina ya mwandishi wa habari na mwandishi wa makala.
Napenda sana kuandika fikra zangu huru kwa azma ya kuchochea mijadala. Jana niliandika fikra zangu kwenye Jamii Forums. Nimefanya hivyo huko nyuma. Lakini jana nimepata watu wengi walioshiriki mjadala. Wametoa fikra zao, kuna walionitukana pia. Nimeshazoea. Nayasoma matusi hayo, nikiamini, hata kwenye matusi hayo kuna cha kujifunza. Kufahamu fikra za watoa matusi hayo.
Na hakika, kuna wanaofikiri wananifahamu. Wamenipa majina, wamenihusisha na huyu na yule. Kimsingi hawanijui. Wamekuwa ni wakandamizaji wa fikra huru na wanaamini kila anayeandika mawazo yasiyofanana na yao, basi, amenunuliwa. Huu ni udhaifu, ni unyonge wetu pia. Hatujiamini.
Nitaendelea kuandika fikra zangu huru, napenda sana kuandika mawazo yangu. Nimefanya hivyo tangu nikiwa Sekondari pale Tambaza, tena kwa kuazisha kijarida cha shule. Niliandika mwenyewe kwa mkono, nilikuwa na wasomaji wangu pia. Tuliokuwa nao Tambaza miaka ile ya 80 ni mashahidi wa hilo.
Najua kuwa wakati mwingine kuna wanaokerwa na niandikayo. Hao wapo siku zote. Hatuwezi kufanana kimitazamo. Na tumekuwa wepesi sana, kila tusomapo mawazo ya mtu, kutafuta droo ya kabati la kumpachika. Siku hizi kuna droo za CCM, CHADEMA, CUF, Uislamu, Ukristo, Uchaga, Usukumuma na kadhalika.
Na ni bahati mbaya sana, kuwa wengi tumeisahau "Droo ya Tanzania". Hii ni droo muhimu sana na ilipaswa iwe ya kwanza. Kwa kila tutendalo liwe kwa MASLAHI YA TANZANIA KWANZA. Maslahi ya Taifa. Na Hilo Ni Neno La Leo.
Maggid,
Iringa,
mjengwa
Na Maggid Mjengwa,
Mwalimu Nyerere alipata kusimulia kisa cha mbwa wa Manzese. Nilikuwa bado kijana mdogo sana niliposikia kisa kile. Ilikuwa mwanzoni mwa miaka ya 80. Ni kwenye kilele cha Sherehe za Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi. Sherehe zile zilifanyika pale Uwanja wa Taifa. Nilibahatika kuwapo uwanjani.
Baadhi ya mabango ya wafanyakazi yaliyopita mbele ya Mwalimu siku ile yaliwakilisha ujumbe juu ya hali ngumu ya kimaisha iliyokuwa ikiwakabili wafanyakazi; mishahara midogo na mengineyo.
Wakati huo, Serikali ya Mwalimu ilikataa masharti ya Shirika la Fedha Duniani na Benki ya Dunia pia. Hii ni kwa sababu, licha ya athari nyingine mbaya kwa masharti hayo kwa nchi yetu, uhuru wetu wa kujiamulia mambo yetu nao ulikuwa hatarini.
Ilipofika wakati wa kutoa hotuba yake, Mwalimu Nyerere alisema;
" Ndugu zangu watu wa Dari Salama ebu nisikilizeni; kulikuwa na mbwa wawili, mmoja wa Manzese na mwingine wa Oysterbay. Ikatokea siku moja mbwa wa Manzese akatembea hata akafika Oysterbay.
Kwenye moja ya nyumba za huko Oysterbay akamwona mbwa mwenzake aliye ndani ya geti. Mbwa yule wa Manzese akasogea getini huku akimshangaa mbwa wa Oysterbay. Mbwa yule wa Oysterbay alinenepeana huku manyoya yake yakiwa yameteremka hadi machoni. Mbwa wa Oysterbay naye alimshangaa mwenzake wa Manzese. Mbwa yule wa Manzese alionekana kukondeana huku masikio yake yakiwa yameteremka hadi shingoni. Mbwa wa Oysterbay kwa mshangao akamwuliza mwenzake wa Manzese; " Hivi nawe ni mbwa kama mimi?!
"Naam, miye ni mbwa kama wewe." Alijibu mbwa wa Manzese.
" Sasa mbona umekondeana hivyo, njoo humu ndani kwa bwana wangu nawe uwe kama mimi."
Mbwa wa Manzese akajibu;
" Lakini wewe umefungiwa, mwenzio niko huru!"
Sitakisahau kamwe kisa kile alichosimulia Mwalimu Nyerere pale Uwanja wa Taifa. Naamini katika alichokisema Mwalimu. Nitaendelea kuamini hivyo hata katika muda wangu uliobaki humu duniani. Mwalimu alizungumzia dhana ya uhuru. Ingawa ni neno fupi sana, lakini neno uhuru lina maana kubwa. Asiye na uhuru ni mtumwa.
Mimi ni mtu huru. Na siku zote nimepigania nibaki kuwa mtu huru. Kwa uhuru kabisa nakutana na kuongea na watu wengi; vijijini na mijini. Nakutana na kuongea na wasomi na wasio wasomi, matajiri na masikini. Sijapata maishani mwangu kulazimishwa au hata kulipwa ujira ili niongee au niandike mawazo yasiyo yangu au nisiyokubaliana nayo.
Ni bahati mbaya pia, katika jamii yetu, kila anayeandika makala magazetini kama nifanyavyo, basi, atasemwa kuwa ni mwandishi wa habari. Wengi hawatofautishi baina ya mwandishi wa habari na mwandishi wa makala.
Napenda sana kuandika fikra zangu huru kwa azma ya kuchochea mijadala. Jana niliandika fikra zangu kwenye Jamii Forums. Nimefanya hivyo huko nyuma. Lakini jana nimepata watu wengi walioshiriki mjadala. Wametoa fikra zao, kuna walionitukana pia. Nimeshazoea. Nayasoma matusi hayo, nikiamini, hata kwenye matusi hayo kuna cha kujifunza. Kufahamu fikra za watoa matusi hayo.
Na hakika, kuna wanaofikiri wananifahamu. Wamenipa majina, wamenihusisha na huyu na yule. Kimsingi hawanijui. Wamekuwa ni wakandamizaji wa fikra huru na wanaamini kila anayeandika mawazo yasiyofanana na yao, basi, amenunuliwa. Huu ni udhaifu, ni unyonge wetu pia. Hatujiamini.
Nitaendelea kuandika fikra zangu huru, napenda sana kuandika mawazo yangu. Nimefanya hivyo tangu nikiwa Sekondari pale Tambaza, tena kwa kuazisha kijarida cha shule. Niliandika mwenyewe kwa mkono, nilikuwa na wasomaji wangu pia. Tuliokuwa nao Tambaza miaka ile ya 80 ni mashahidi wa hilo.
Najua kuwa wakati mwingine kuna wanaokerwa na niandikayo. Hao wapo siku zote. Hatuwezi kufanana kimitazamo. Na tumekuwa wepesi sana, kila tusomapo mawazo ya mtu, kutafuta droo ya kabati la kumpachika. Siku hizi kuna droo za CCM, CHADEMA, CUF, Uislamu, Ukristo, Uchaga, Usukumuma na kadhalika.
Na ni bahati mbaya sana, kuwa wengi tumeisahau "Droo ya Tanzania". Hii ni droo muhimu sana na ilipaswa iwe ya kwanza. Kwa kila tutendalo liwe kwa MASLAHI YA TANZANIA KWANZA. Maslahi ya Taifa. Na Hilo Ni Neno La Leo.
Maggid,
Iringa,
mjengwa
crapAma hawa wachadema bado wamelala ,hivi wanasahau kuwa CUF ni kinara wa siasa hapa Tanzania ,CUF imeikomalia Zanzibar ,chadema mnapoambiwa kuwa badu nyinyi ni watawaliwa basi mkubali tu hamna na hamuwezi kufanya siasa angalau kuikaribia CUF ,maggid amewagusa na amewapopoa vibaya sana pale alipowambia kuwa hata nafasi ya tatu hamuipati, waulizeni CUF itawambia vipi wanakutoa kapa ?
Kamanda Mjengwa.Na Maggid Mjengwa,
............Napenda sana kuandika fikra zangu huru kwa azma ya kuchochea mijadala. Jana niliandika fikra zangu kwenye Jamii Forums. Nimefanya hivyo huko nyuma. Lakini jana nimepata watu wengi walioshiriki mjadala. Wametoa fikra zao, kuna walionitukana pia. Nimeshazoea. Nayasoma matusi hayo, nikiamini, hata kwenye matusi hayo kuna cha kujifunza. Kufahamu fikra za watoa matusi hayo.
Na hakika, kuna wanaofikiri wananifahamu. Wamenipa majina, wamenihusisha na huyu na yule. Kimsingi hawanijui. Wamekuwa ni wakandamizaji wa fikra huru na wanaamini kila anayeandika mawazo yasiyofanana na yao, basi, amenunuliwa. Huu ni udhaifu, ni unyonge wetu pia. Hatujiamini.
.........MASLAHI YA TANZANIA KWANZA. Maslahi ya Taifa. Na Hilo Ni Neno La Leo.
Maggid,
Iringa,
mjengwa
Maggid;Nauona mjadala umepamba moto. Nasoma kila kinachoandikwa. Na matusi ninayotukanwa nayasoma pia. Kuna siku pale Kariakoo nilimkanyaga jamaa kwa bahati mbaya. Basi, acha anitolee matusi, mengine ya nguoni. Alipomaliza kunitukana nikwambia; " Ahsante sana!". Nikajiendea zangu.
Ni wale ambao, wameambiwa ukifika mjini lazima uwe ngangari. Mwenzio akikusukuma au kukukanyaga usimnyamazie. Mpe vipande vyake na zaidi mtukane.
Wengine tumefundishwa, kuwa ' Mwungwana' ni kauli na matendo, na si kauli za matusi, tena hadharani. Ahsanteni sana mliochangia na mnaoendelea kuchangia mada hii. Ahsanteni sana, hata mnaonitukana.
Kamanda Mjengwa.
kwanza pole sana kwa ujasiri wa kusoma hoja na matusi tele baada ya kuweka post yako humu. Ama kwa hakika umekutana na gari moshi ambalo halikukusubiri upite bali likakuburuza mpaka umeumia sasa.
Nafahamu kwamba unajua kuwa hivi sasa kuna vuguvugu la mabadiliko na hii yote inatokana na ujinga wa watanzania wachache ambao wanadhani kwa kuwa wao wanaifaudu keki ya taifa basi wanafanya hivyo kwa niaba ya taifa zima. na bila shaka unafahamu kuwa waandishi wa tanzania wananunulika bei chee hasa ktk kipindi hiki cha uchaguzi. Naamini unafahamu pia kwamba asilimia kubwa ya watanzania include waandishi hawana huruma na mafukara wa tanzania. Uongo unaozalishwa kila siku na waandishi walionunuliwa ndio ambao umesaidia kuweka watawala WABAYA madarakani. na watawala hawa wabaya wanawanufaisha waandishi commodities kwa kuwapa hela na nini cha kuandika.
Makala yako ile kwa ukweli imekera wengi na ni haki yao kukerwa kwa kuwa wewe mwandishi huru umeandika hoja huru ambazo kina anayezisoma ana uhuru wa kuziafiki au kutoziafiki. Amini nakwambia kaka yangu, hata nyerere alisema kwamba hakufanya mema peke yake seuse wewe na mimi? Kuna watu humu siyo waandishi kama ulivyo lakini ni wasomaji wazuri wa maandishi ya wenzao na kuyachambua kwa manufaa ya wengine, kuna ambao ukishaandika ndipo wao hupata cha kuandika pia, kuna wale kama mimi ambao tunasubiri uandike kisha tuyasome hayo maandiko yako. Mimi nilishaacha kukusoma loong ago ila huwa nasoma posts zako humu JF pekee.
Bandiko lako (huru) lilinipa uhuru wa kukunanga na kukusuta kama walivyofanya wengine.
ni kweli ana uhuru wa kutoa mawazo,lakini kipindi hiki walio wengi wanataka nini? Watu wana hali mbaya kaka,ila wanashindwa wafanye nini ili kuuondoa utawala mbovu. Kama hajui wengi wanataka nini basi si kosa la waliom-crush. Pole ndio demokrasia hiyo (lazima gharama ziwepo).