Mjengwa katika kampeni za Kikwete 2010?

Mjengwa katika kampeni za Kikwete 2010?

Kweli njaa haina BAUNSA.

Nilikuwa najiuliza mara kwa mara huyu Mjengwa anapata wapi pesa za kusafiri huku na kule?, anakipato gani cha kumuwezesha kuzunguka huku na kule (VASCO DA GAMA). Sasa napata jawabu kwamba anatumwa na mashetani ya CCM ili kuwaua Watanzania. Lakini ningependa kumwambia Mjengwa kwamba pesa si kila kitu, bali utu ni kitu cha maana. Ni mwenda wazimu tu ndiye haoni machafu na mabaya ya CCM, na Mjengwa ni moja kati ya hao wenda wazimu.
 
Mimi nadhani huyu ametumwa na serikali kuweka hisia miongoni mwa jamii kwamba Slaa atakuja Na 3 kwa Lipumba ili kurahisishia kazi NEC kutangaza hivyo baada ya uchaguzi. You know, CCM ina mikakati mingi sana! Hizi kura za maoni katika mitandao zinazomuonyesha Slaa kuwa ni top zinawauma CCM kwelikweli.
 
Huyu mjengwa wa kuurumia, tena nimegundua ni kibaraka wa CCM hana lolote, yaani watu kama hawa natamani niwameze maana naona kama hawaoni watu tunavyoteseka kwenye nchi yetu yenye raslimali kibao, timua huko
 
hi majid!
kwanza sikatai kwamba ccm itashinda ila naomba upanue ubongo wako kidogo

1. Kwanini ukazanie tathmini ya lipumba mikoa ya pwani huku ukiacha tathmini ya slaa mikoa ya kaskazini?

2. Kwa nini huongelei tathmini ya chadema kuongoza halmashauri nne na unang'ang'ania nafasi ya pili ya lipumba uchaguzi uliopita?

3. Kwa nini huangalii mvuto kwa wananchi kati ya lipumba na slaa?

kuna mambo umeyasema ya ukweli kuhusu mtandao mpana wa ccm lakini hujagusia mtandao wa wapuuzi kama tendwa na usalama wa taifa ambao kwa aibu zao wenyewe wameamua kuwa makada wa ccm?

4. Umeongelea uchumi wa vyama pinzani ni sawa, lakini si unajua ccm wana nafasi ya kuchukua wanachotaka kwa wakati wanaotaka na mahali wanapotaka?
mimi naamini ushindi huwa unaanza moyoni.

Uchaguzi utakapoisha nina ujasiri wa kuwauliza ccm kama wangeachia uwanja sawa kwa wote je wangeshinda? Lakini pia hujadokeza juu ya rais mtarajiwa kutokuwa na uoga wa kuwa mnafiki na muongo mbele ya watanzania, kwamba leo nawashtaki mafisadi na kesho mafisadi walionewa!!! Kwa hakika jk atashinda ila kwa mara ya kwanza tutakuwa na rais aliyelaaaniwa!!!


U nailed it my dear..................bravooo!
 
Maggid soma alama za wakati fumbua macho uweze kuona ya kuwa
wahenga walisema mavi ya jana hayanuki

Michanganuo ya miaka ile ya zamani sijui 2005 na kadhalika haitakusaidia kuwa uchaguzi huu ni "referendum on state sponsored graft" na wala siyo wapigakura kujipigia tu kama mwaka arobaini na saba.

Wake-up and grow........... It is written in the scriptures:-

PROVERBS:12:23 A prudent man conceals his ignorance but the hearts of a fool proclaims his foolishness

Vilevile imeandikwa
PROVERBS 13:15: Poverty and shame will come to him who disdains correction but he who regards a rebuke will be honoured

Jirekebishe na kiri ya kuwa upeo wako ni mdogo sana kwenye taaluma hii ya upembuzi yakinifu.
 
Nilitamani sana kujua umri wako...shida yako ni kuwa bado unaongozwa na siasa za mapokeo....ungekuwa na umri wa makamba nisingekulaumu..ukweli ni kuwa mtanzania wa 2005 ana tofauti kubwa sana na wa 2010,mi mwenyewe mmojawapo..nimejua sababu ya umaskini wa nchi hii ni ccm sababu ccm ni kichaka cha watu wachache wanaojinufaisha wenyewe kupitia rasilimali za nchi hii.....
 
.Huu ni mtizamo wangu nilioupata kwa uzoefu wa kuwasoma waandishi mbalimbali wa kitanzania. Maghdi ni mwandishi mwenye fikra za kizamani za wakati ule wa magazeti yaliyokuwa yakiitwa mzalendo na mfanyakazi. Ni mwandishi anayelazimisha mazingira yamfuate sio yeye kubadilika kulingana nayo. Ana ndoto za kudumisha fikra sahihi za bwana wake dhidi ya uhalisia ndio maana makala yake katika gazeti lolote utakaloyakuta hayana mvuto kulingana na waandishi wengine kwenye gazeti hilo hilo. Ameachwa nyuma kwa kila jambo huku akijivunia hali hiyo. Ana dalili za kujitokeza na huenda ndicho kitu kilichomziba asiweze kuwa mkweli. Ana kawaida ya ku-propageti dhidi ya taaluma na atajitutumua kujaribu kuthibitisha vinginevyo. Huyo ndie mgendwa anaeomba radhi kwa makala itakayowachukiza wengine kana kwamba anayo makala ambayo ilishawahi wafurahisha.
MAJIDI KAWAAMBIE WALIOKUTUMA WAMECHELEWA, KWANI UMEWAKUTA RAIA WASHAJIANDAA KUMPIGIA SLAA KURA YA NDIO, NA HATA HIVYO HAWADANGANYIKI TEEEENA!!
PIA MTU MZIMA HATISHIWI NYAUUU... ETI DOLA HUAGA NDIO INAYOPANGA MATOKEO, IPANGE TENA SASA IONE KILICHOMTOA NYOKA PANGONI.
 
Magid Mjengwa,
Pole kaka na kazi.
Makala yako ni nzuri kutegemea ni nani anasoma, wala huna sababu ya kusema utaudhi wengi, hii ni jamiiforums.
Mimi nashindwa kukuelewa baada ya kusoma na kuona ni makala zile zile za siku zote. Nilitegemea wewe kama mwandishi wa habari kama sijakosea, ungekuja na tathimini yakinifu ya uchaguzi wa 2010 badala ya kutumia takwimu za zamani ambazo zinaweza zisifanyekazi mwaka huu. Dr Slaa alishinda ubunge Karatu 1995 bila ya kuwa na madiwani kama sio mmoja vilevile Dr walid amani kaburu, Lyatonga mrema Temeke, Makongoro nyerere Arusha nk.

Nilitegemea kwa kuwa wewe unabahati ya kukutana na wapiga kura katika pita pita zako ungeleta takwimu hata kama sio rasmi. Mfano ungewauliza wapiga kura kila unapopita usingekosa kumi au ishirini kwa jimbo moja na kuweka viswali virahisi angalau mmbunge na raisi ukaweka vyama, ungeweza kuja na picha ambayo tusingeweza kuweka walakini na kazi yako ya uandishi.

Nikijaribu kufuatilia makala zako, naona kama vile unaogopa kitu fulani kwahiyo huna jinsi ila kuna wakati unakuwa wewe kuna wakati inabidi uridhishe upande. Inaniwia vigumu kama Synavote wameminya matokeo ya utafiti ulioonyesha Dr.Slaa anashinda. Vilevile matokeao ya maoni kwenye majimbo mbali mbali yanaonyesha jinsi wapinzani wanavyokubalika sio Chadema pekee kuna baadhi Chadema, CUF. Kizazi hiki tunatakiwa kuwa tofauti kidogo badala ya kuandika ukiwa chumbani twendeni kwenye maeneo ya tukio na tuandike habari inayotokea.

Sina chanzo za habari zako, ila nanona umetumia uchaguzi wa mwaka 2005. Mapinduzi ya demokrasia duniani huwa yanashangaza wengi, watawala wengi wanashtukizwa ndio maana wengi wanaishia kuleta vita, kama Mugabe, nk. Wamarekani waliamini Obama hawezi kuwa Raisi kwani ni mweusi na kazaliwa na baba mwafrika. Walishangaa sana walipomkuta Ikulu, mpaka hivi leo wapo amabao hawaamini.

Sikulazimishi uandike habari ambayo unaona si ya kweli, lakini habari yako haina mshiko wowote. Tukiangalia mwamko wa wananchi mwaka huu tunaona uko juu, elimu ya uraia na uchaguzi na watu kujua haki zao imepanda, watu wa kada mbali mbali wameanza kuamini kuwa wapinzani nao wanaweza kuleta mabadiliko. Majimbo mengi wamesimama wagombea ambao wanaeleweka na wananchi tofauti na miaka mingi, wachangiaji wamaeongezeka wanakisaidia chama hii ikiwa ishara ya kukubalika.

Ni wabunge wangapi Chadema inaweza kupata, Tendwa alisema 80-100, wewe mjengwa unasema wachache kuliko wa CUF, Chadema wanasema zaidi ya 100. Na sisi tunasema tutawapata wengi kwani mori upo juu. Sisi tuliopo kwenye uhamasishaji kuanzia ngazi za matawi tunapata matumaini makubwa, tunaona tofauti yawananchi wa leo na 1995.

Ndugu Mjengwa Duniani hakuna kampuni ya poll ya chumbani, zote zinakwenda kufanya kazi na kuuliza wapiga kura waliojindikisha, na sayansi hiyo inafanya kampuni hizo zisitofautiane kwenye majibu yao kwa asilimia nyingi. Mara nyingi wanasema ukweli kutokana na hali halisi. Sasa wewe kuja na takwimu za chumbani sio za kisayansi kwenye dunia ya leo ukiwa mwandishi unakuwa umeshindwa kazi yako. Takwimu za ukweli hakuna wa kuziogopa wala kuchukia labda mwehu kama wananchi watasema tunamchagua Mjengwa huwezi kataa. Ila kutumia kalamu kuwa mtabiri kama shekhe Yahaya ni usaliti wa elimu ya uandishi wa habari. Kazi kubwa ya waandishi ni kuelimisha umma kwa kutumia vyanzo vya ukweli na habri zilizotafitiwa.

Unapima mwendo wa uchaguzi kwa kuuliza wapiga kura kwa wakati huo. Siasa za Tanzania zinabadilishwa na nani anagombea wakati huo, bado hatuna siasa za kichama sana, watu wanaswing na mgombea na rushwa wakati mwingine inahamisha wapiga kura. Sasa badala ya kutuletea matokeo ya maruhani anza kujadili jimbo kwa jimbo au mgombea kwa mgombea.

I salute you Monsieur.........asante sana kwa maelezo hayo, nimeyapenda.
 
Wacha kujifanya kipofu wakati macho unayo, makala za juma na roza zimetuchosha ile mbaya and to tell you the truth my bro.......this time we mean business. Mimi nikikutafakari nakuona unaishi kwenye denial tu wakati ukweli wewe na wenzio mnaujua. Tunataka mabadiliko ya kweli, enough is enough.
 
Nauona mjadala umepamba moto. Nasoma kila kinachoandikwa. Na matusi ninayotukanwa nayasoma pia. Kuna siku pale Kariakoo nilimkanyaga jamaa kwa bahati mbaya. Basi, acha anitolee matusi, mengine ya nguoni. Alipomaliza kunitukana nikwambia; " Ahsante sana!". Nikajiendea zangu.

Ni wale ambao, wameambiwa ukifika mjini lazima uwe ngangari. Mwenzio akikusukuma au kukukanyaga usimnyamazie. Mpe vipande vyake na zaidi mtukane.
Wengine tumefundishwa, kuwa ' Mwungwana' ni kauli na matendo, na si kauli za matusi, tena hadharani. Ahsanteni sana mliochangia na mnaoendelea kuchangia mada hii. Ahsanteni sana, hata mnaonitukana.
 
Na lengo la hizi polls za JF zinatolewa offline kwa ajili ya matengenezo halafu baada ya matokeo kuchongwa zinarudishwa je ni kwa ajili ya kujitayarisha kisaikolojia?

Synovate wenyewe wamekataa kuwa hawajawahi kufanya hiyo kura ya maoni, sasa kama siyo kuathirika kisaikolojia basi kulazimisha kitu ambacho hakipo sijui ni maradhi ya aina gani. :tonguez:

Kwa nini Synovate "wamekataa" kufanya polls kipindi hiki? Kuna sababu yoyote ya msingi kwa organization ambayo kazi yake ni kufanya polls wakatae kufanya poll kwenye kitu muhimu kama uchaguzi wa raisi wa Tanzania?
 
Nauona mjadala umepamba moto. Nasoma kila kinachoandikwa. Na matusi ninayotukanwa nayasoma pia. Kuna siku pale Kariakoo nilimkanyaga jamaa kwa bahati mbaya. Basi, acha anitolee matusi, mengine ya nguoni. Alipomaliza kunitukana nikwambia; " Ahsante sana!". Nikajiendea zangu.

Ni wale ambao, wameambiwa ukifika mjini lazima uwe ngangari. Mwenzio akikusukuma au kukukanyaga usimnyamazie. Mpe vipande vyake na zaidi mtukane.
Wengine tumefundishwa, kuwa ' Mwungwana' ni kauli na matendo, na si kauli za matusi, tena hadharani. Ahsanteni sana mliochangia na mnaoendelea kuchangia mada hii. Ahsanteni sana, hata mnaonitukana.

Maggid lini uliuza roho yako kwa shetani?
 
Maggid Mjengwa,
Mkuu wangu nadhani sasa hivi umeonyesha wazi rangi yako halisi kama walivyoeleza waliotangulia. Sii vibaya kabisa kwa mwandishi kuandika na kuorodhesha mapungufu au makosa ya chama chochote lakini unapoweka maoni yako kuhusiana na Ushindi wa Uchaguzi huu ni vizuri zaidi ukaelezea sababu ambazo zitamfanya mgombea fulani ashinde au ashindwe. Na wala sii haramu mwandishi kuonyesha yeye ni mshabiki wa itikadi na sera gani (chama gani) kwani hapo utakuwa unapimwa maelezo yako vizuri zaidi.

Ni tabia mbovu ya waandishi wa Kitanzania wanaofikiria kwamba waandishi wa habari hawatakiwi kuwa wanachama au washabikia chama na sera zake..Na upotofu huo ndio mara zote hupelekea mabandiko yenu mengi yanakosa sura kwa sababu mnachanganya vitu kwa kutoelewa unapendekeza kitu gani na kwa sababu gani. Ukiwa na msimamo ni rahisi kujieleza kinagaubaga kuliko kuwa kati kwani kuwa kati ni sawa na kutokufahamu jibu..

Kwa mfano sikuona mahala ulipozungumzia sababu ambazo zitampa ushindi JK, sikuona sifa ya aina yeyote inayomwezesha yeye kumshinda Dr.Slaa ambaye umempa sifa zote ili hali wananchi huko kijijini watakipigia kura chama cha CCM isipokuwa watawachagua viongozi wao. Hivyo huwezi kutompa sifa yeyote kiongozi fulani kisha ukampa ushindi wa juu hali nguvu kubwa ipo Upinzani na kama kweli wananchi wa vijijini wangekuwa hawakijui chama kingine basi mwaka 1995 NCCR na Mrema wasingepata ushindi dhidi ya Mkapa na CCM au pasingekuwepo na shift ya kura za wananchi kwenda CUF, Chadema, TLP na NCCR mwaka 2000 na kisha kurudi tena CCM mwaka 2005. Hivyo mpaka sasa hujatwambia kwa nini JK atashinda mwaka huu.

Na ukitazama utafiti ulofanyika mwaka kabla ya uchaguzi wa mwaka 2005, Kikwete alipewa nafasi kubwa ya Ushindi kwa sababu zilizohusiana na dhana ya Ubora wake ingawa haukuwepo..Wananchi wengi na hata hao wa Vijijini walimchagua JK wakidhani kwamba yeye ni mkombozi wao toka utawala wa Mkapa na kwamba Upinzani ulitoka ndani ya CCM dhidi ya Mafisadi kwani hakuna Mtanzania mpiga kura ambaye hakufahamu Ufisadi wa Utawala wa Mkapa ambao uliwatajirisha zaidi viongozi ukawaacha wananchi maskini. Fikra za Upinzani utatoka CCM ndio hali halisi iliyokuwepo mwaka 2005 na mtandao waliweza kuitumia nafasi hiyo vizuri.

Wengi walisema JK amechaguliwa kutokana na sura au Ujana wake, lakini ukweli utabakia kwamba JK na kundi lake la Mtandao waliweza kupenyeza fedha kuonyesha jijnsi serikali yake itakavyoweza kumwaga mifedha na utajiri kwao, na kama ujuavyo akili ya maskini haina tofauti na mwendawazimu. Zile fedha na ahadi ambazo haziwezi kutekelezeka ndizo ziliwavutia wananchi na kuingia kiherehere cha umalaya wa kujitakia kumchagua Kikwete na CCM...Matokeo yake ndio haya matusi, tuyaonayo tumebeba mimba na HIV kama JK alivyowatukana wanafunzi na wagonjwa wa Ukimwi.

Kwa hiyo mkuu wangu ningekuomba ungezungumzia kidogo sifa ambazo zitampa ushindi JK kulingana na utafiti wako, kama umewauliza wananchi wa vijijini nadhani itakuwa vizuri ukituelezea kwa nini wanazidi kumchagua JK pamoja na kwamba utawala wake umefanya mengi kinyume cha CCM wanayoifahamu. Haya ya Zimwi likujualo, hayahusiani kabisa na kumchagua JK badala ya Dr.Slaa kwani wananchi wengi vijijini hawamjui JK kihivyo ila wanakifahamu chama cha CCM chini ya mwalimu Nyerere. Sasa iweje wananchi wakifahamu chama cha CCM lakini unapokuja kwa Chadema huzungumzii chama isipokuwa kwamba wananchi hawamfahamu Dr.Slaa...

Hivi kweli unataka tuamini kwamba huko vijijini wananchi hawafahamu kabisa kwamba kuna chama kiitwacho Chadema pamoja na kwamba wameweka wagombea wao...Pamoja na ukweli kwamba CCM wamejikita hadi ktk mashina, kata, matawi ya wilaya kuwa ndio sababu kubwa unayowapa ushindi basi nilitegemea kwamba umefanya utafiti mkubwa na kutambua kwamba wananchi huko vijijini hawatamchagua Dr.Slaa kwa sababu Chadema hawana uwakilishi wa kutosha katika sehemu hizo. Je ni sababu hii tu ambayo itawanyima Chadema na Dr.Slaa ushindi lakini sababu hiyo hiyo inawapa CUF ushindi wa pili ktk sehemu ambazo nao hawana wawakilishi kama Chadema.

Kuhusiana na swala la Zitto, mkuu wangu awe kasema au hakusema lakini swala kubwa ni sisi wenyewe kujiuliza kwa nini tunahofia Zitto kugombea mwaka 2015 ikiwa sisi wenyewe ndio tulipinga mila na desturi za CCM ambazo zilimpitisha JK kugombea mwaka huu pasipo upinzani toka ndani ya chama?. Iweje leo kwa CCM inakubalika lakini haitakubalika kwa Chadema kama sio sisi wenyewe kushindwa ku practice demokrasia ila pale penye mapenzi na maono yetu.

Binafsi hainipi shida Zitto kugombea Urais mwaka 2015 kwani Chadema hawana utaratibu sawa na CCM, na hakika hii inawapa nguvu zaidi Chadema kuonyesha demokrasia ya kweli na sio mila na desturi za Upambe kama wa CCM. Inatupa mwanya wa kutomchagua Dr.Slaa mwaka 2015 akivurunda na wananchi hawataridhika naye lakini bado wanakubaliana na sera za Chadema.

Hivyo Zitto anaweza pambana na Dr.Slaa ktk uchaguzi ndani ya chama na Dr.Slaa kama atakuwa amefanya vizuri ataendelea kwa miaka mingine mitano lakini akivurunda kama JK upinzani utatoka ndani ktk uchaguzi.. tatizo liko wapi hapa kama sio kuwasifia Chadema kwa utaratibu mzuri wa Kiutawala!..

Mwisho mkuu wangu sikuona mahala popote ulipozungumzia mapungufu ya CUF ila sifa tupu kwa Lipumba ambaye mkuu wangu hakika amebakia pumba..CUF ingekuwa na mvuto mkubwa sana mwaka huu kama ingeweza kubadilisha viongozi wa juu hasa nafasi hiyo ya kugombea Urais..Mimi naamini kabisa kwamba kiongozi anaposhindwa uchaguzi mkuu mara mbili basi umaarufu wake hushuka zaidi kwa kila mwaka anapojaribu kugombea.. Inajulikana wazi kwamba CUF itapata viti vingi kutoka visiwani kinyume cha hapo huko kusini mkuu wangu bado ni jinamizi kwani wanakubalika mijini (uswahilini) lakini vijijini bado CCM imechukua nafasi kubwa.
 
Nauona mjadala umepamba moto. Nasoma kila kinachoandikwa. Na matusi ninayotukanwa nayasoma pia. Kuna siku pale Kariakoo nilimkanyaga jamaa kwa bahati mbaya. Basi, acha anitolee matusi, mengine ya nguoni. Alipomaliza kunitukana nikwambia; " Ahsante sana!". Nikajiendea zangu.

Ni wale ambao, wameambiwa ukifika mjini lazima uwe ngangari. Mwenzio akikusukuma au kukukanyaga usimnyamazie. Mpe vipande vyake na zaidi mtukane.
Wengine tumefundishwa, kuwa ' Mwungwana' ni kauli na matendo, na si kauli za matusi, tena hadharani. Ahsanteni sana mliochangia na mnaoendelea kuchangia mada hii. Ahsanteni sana, hata mnaonitukana.

Hilo bomba unaloteka maji lifungulie mpaka mwisho ili uweke akiba maana maji yatakatika muda si mrefu!!!!
 
Na sababu ya Dr Slaa kuondoka nafasi ya Pili kufikia ya Tatu ni nini?

Chakachua yani hadi hapo nawe unategemea majibu.

The whole system NEC is blacklisted what do u expect

Hapa tulipaswa kukubali ile Computerized system kama waliopewa wa Kenya juzi kupitisha katiba yao mpya na kama hatutojirekebisha hata 2015 yawezekana ikawa ndio yale yale chakachuaaaa na Royal Family kuchukua nafasi kiraiiiiiiini kama wana nawa vileeeee
 
hee! nimepata shoku ya ghafla, si na mchango labda nikipata nguvu.
 
Ama hawa wachadema bado wamelala ,hivi wanasahau kuwa CUF ni kinara wa siasa hapa Tanzania ,CUF imeikomalia Zanzibar ,chadema mnapoambiwa kuwa badu nyinyi ni watawaliwa basi mkubali tu hamna na hamuwezi kufanya siasa angalau kuikaribia CUF ,maggid amewagusa na amewapopoa vibaya sana pale alipowambia kuwa hata nafasi ya tatu hamuipati, waulizeni CUF itawambia vipi wanakutoa kapa ?
 
Maggid, Uchambuzi wako nimeupenda na umelenga pande zote muhimu.... Hakika huo ndio ukweli wenyewe ni kwamba Chadema hawana hawafiki popote na mbio zao za miti....Ni vizuri sana watu wakakubali ukweli na kuacha ubishi.... Saa sita usiku, unabisha unasema ni mchana mbona jua linawaka.
Nadhani hujawahi kukaa maeneo ambapo usiku na mchana hautafsiriwi kwa jua au kiza.Endelezeni harakati za TBC1,Uhuru na Mzelendo,Habari Leo na mafisadi wa habari corporation.
 
Tatizo la Mjengwa ni shule.Anajitahidi sana kujitambulisha kama mwandishi wa makala mwenye upeo mkubwa ilhali ametawaliwa na na udini na mapenzi yaliyokubuhu kwa Kikwete.Laiti angekuwa na upeo stahili,asingekurupuka na takwimu outdated.Yeye na JK wake wanatufanya Watanzania wajinga,wanaamini chochote watakachosema kitakuwa hivyo.

Ni mlevi pekee anayeweza kudai eti CUF itashika nafasi ya pili bara....unless huo ndio mkakati wa Usalama wa Taifa,kuiba kura za Chadema ziiwezesha CCM kushinda na zitakazosalia wapewe CUF.

Dawa ya wababaishaji kama Mjengwa ni kuwapuuza tu.Huyu hana tofauti na Sheikh Yahya
 
Back
Top Bottom