Magid Mjengwa,
Pole kaka na kazi.
Makala yako ni nzuri kutegemea ni nani anasoma, wala huna sababu ya kusema utaudhi wengi, hii ni jamiiforums.
Mimi nashindwa kukuelewa baada ya kusoma na kuona ni makala zile zile za siku zote. Nilitegemea wewe kama mwandishi wa habari kama sijakosea, ungekuja na tathimini yakinifu ya uchaguzi wa 2010 badala ya kutumia takwimu za zamani ambazo zinaweza zisifanyekazi mwaka huu. Dr Slaa alishinda ubunge Karatu 1995 bila ya kuwa na madiwani kama sio mmoja vilevile Dr walid amani kaburu, Lyatonga mrema Temeke, Makongoro nyerere Arusha nk.
Nilitegemea kwa kuwa wewe unabahati ya kukutana na wapiga kura katika pita pita zako ungeleta takwimu hata kama sio rasmi. Mfano ungewauliza wapiga kura kila unapopita usingekosa kumi au ishirini kwa jimbo moja na kuweka viswali virahisi angalau mmbunge na raisi ukaweka vyama, ungeweza kuja na picha ambayo tusingeweza kuweka walakini na kazi yako ya uandishi.
Nikijaribu kufuatilia makala zako, naona kama vile unaogopa kitu fulani kwahiyo huna jinsi ila kuna wakati unakuwa wewe kuna wakati inabidi uridhishe upande. Inaniwia vigumu kama Synavote wameminya matokeo ya utafiti ulioonyesha Dr.Slaa anashinda. Vilevile matokeao ya maoni kwenye majimbo mbali mbali yanaonyesha jinsi wapinzani wanavyokubalika sio Chadema pekee kuna baadhi Chadema, CUF. Kizazi hiki tunatakiwa kuwa tofauti kidogo badala ya kuandika ukiwa chumbani twendeni kwenye maeneo ya tukio na tuandike habari inayotokea.
Sina chanzo za habari zako, ila nanona umetumia uchaguzi wa mwaka 2005. Mapinduzi ya demokrasia duniani huwa yanashangaza wengi, watawala wengi wanashtukizwa ndio maana wengi wanaishia kuleta vita, kama Mugabe, nk. Wamarekani waliamini Obama hawezi kuwa Raisi kwani ni mweusi na kazaliwa na baba mwafrika. Walishangaa sana walipomkuta Ikulu, mpaka hivi leo wapo amabao hawaamini.
Sikulazimishi uandike habari ambayo unaona si ya kweli, lakini habari yako haina mshiko wowote. Tukiangalia mwamko wa wananchi mwaka huu tunaona uko juu, elimu ya uraia na uchaguzi na watu kujua haki zao imepanda, watu wa kada mbali mbali wameanza kuamini kuwa wapinzani nao wanaweza kuleta mabadiliko. Majimbo mengi wamesimama wagombea ambao wanaeleweka na wananchi tofauti na miaka mingi, wachangiaji wamaeongezeka wanakisaidia chama hii ikiwa ishara ya kukubalika.
Ni wabunge wangapi Chadema inaweza kupata, Tendwa alisema 80-100, wewe mjengwa unasema wachache kuliko wa CUF, Chadema wanasema zaidi ya 100. Na sisi tunasema tutawapata wengi kwani mori upo juu. Sisi tuliopo kwenye uhamasishaji kuanzia ngazi za matawi tunapata matumaini makubwa, tunaona tofauti yawananchi wa leo na 1995.
Ndugu Mjengwa Duniani hakuna kampuni ya poll ya chumbani, zote zinakwenda kufanya kazi na kuuliza wapiga kura waliojindikisha, na sayansi hiyo inafanya kampuni hizo zisitofautiane kwenye majibu yao kwa asilimia nyingi. Mara nyingi wanasema ukweli kutokana na hali halisi. Sasa wewe kuja na takwimu za chumbani sio za kisayansi kwenye dunia ya leo ukiwa mwandishi unakuwa umeshindwa kazi yako. Takwimu za ukweli hakuna wa kuziogopa wala kuchukia labda mwehu kama wananchi watasema tunamchagua Mjengwa huwezi kataa. Ila kutumia kalamu kuwa mtabiri kama shekhe Yahaya ni usaliti wa elimu ya uandishi wa habari. Kazi kubwa ya waandishi ni kuelimisha umma kwa kutumia vyanzo vya ukweli na habri zilizotafitiwa.
Unapima mwendo wa uchaguzi kwa kuuliza wapiga kura kwa wakati huo. Siasa za Tanzania zinabadilishwa na nani anagombea wakati huo, bado hatuna siasa za kichama sana, watu wanaswing na mgombea na rushwa wakati mwingine inahamisha wapiga kura. Sasa badala ya kutuletea matokeo ya maruhani anza kujadili jimbo kwa jimbo au mgombea kwa mgombea.