Duh, Mpenzi Faiza, ni vile tuu hunijui vizuri,
Mimi ni Msukuma niliyezaliwa Ocean Road
Baba na mama watumishi wa umma wa ile Idara!.
Nimesoma O'Bay-Tambaza-Ilboru-TSJ. Mimi ni wa 60s, Ephraim Kibonde ni wa 70s, Kibonde sio tuu ni mdogo wangu sana!, mimi na Kibonde tuna 5-year age gap!, na amini usiamini mimi nimemfundisha kazi Kibonde, japo wote ni watangazaji, kwenye hizi fani za vipaji, Mwalimu anakuja kuwa cha mtoto mbele ya mwanafunzi. Hata katika Muziki, Mwalimu Guromo wa Nuta Jazz, Juwata Jazz, Ottu Jazz na mwisho Msondo Ngoma, baada ya kuimba kwa miaka 40, bila kuwa na uwezo wa kununua motokari, ni Diamond Platinumz amekuja kumnunulia gari lake la kwanza katika maisha yake, hivyo Ephraim Kibonde alikuja kupata umaarufu kuliko waalimu wake na kaka zake!. Mimi niliingia kwenye fani ya utangazaji kwa kusomea na kwenda shule, Kibonde aliingia direct kutoka kwenye u MC na sijui kama alikujaga kwenda shule zile za brush up!.
Wakati mimi nasoma Primary O-Bay, Kibonde (RIP) yuko Chekechea, wanakaa mtaa wa Uganda Evenue. Mimi niko darasa la 6, Kibonde anaanza darasa la kwanza!. Wakati mimi niko sekondari Tambaza, naanza form 1, Kibonde (RIP), alikuwa primary Muhimbili darasa la 3!, we share the same compound. Mimi namaliza Tambaza form 4 nakwenda kuanza A level Ilboru hadi namaliza, Kibonde hajamaliza hata primary!.
Mimi nimemaliza shule, nimeenda chuo nimemaliza, nimeanza kazi ya utangazaji RTD mwaka 1990
Kibonde anaaza sekondari ya Shaaban Robert.
Mwaka 1994 TV zinaanzishwa Kibonde hajamaliza sekondari!.
Nimefanya kazi miaka 5 RTD, nikafatwa
Na mhindi wa DTV Shabbir Dewji, na baada ya miaka miwili DTV ndio Ephraim anachukuliwa na Shabbir Abji CTN, Wakati wote wa Kiti Moto, Kibonde alikuwa bado, CTN ime merge na DTV kuanzisha Channel Ten 1997 nimemfundisha kazi Kibonde for 2 years hadi 1999 mimi nikarudi serikalini kuanzisha TVT!.
Kitu ambacho sii kweli, usidhani Masai Studio waliniokota, nilikuwa nafanya Kiti Moto nikiwa na kazi yangu DTV tena kwa taarifa yako sikuanzia na Kiti Moto, kipaji changu cha Talk Show Host kilivumbuliwa na mama mmoja wa Kihaya, Beatrix Mugishwage na Mjerumani mmoja, Wolfgang Baraniek kupitia kipindi cha "Mada Moto Uchaguzi 95", ndipo Masai Studio wakaniona baada ya uchaguzi wakaanzisha Kiti Moto.
Kitu ambacho Masai Studio walinisaidia sana ni mwaka 1997, Tajiri Reginald Mengi alikinunua Kiti Moto toka DTV kikahamia ITV, mimi ikanibidi kuacha kazi DTV ili niajiriwe ITV, kilichotokea naomba nisikiseme ila nikajikuta jobless, Jove Consalves wa Masai Studio akaokoa jahazi, hadi kipindi kilipo kufa, akanipele mimi na familia yangu tukahamia UK, then US, nimekuja kurudi Bongo 1999 kuanzisha TVT na hadi leo familia inaishi US!.
Katika kujifagilia ili kukubaliwa na Faiza Mwaka 2003 niliachishwa kazi TVT kwa summary dismissal kwa kosa la insubordination, and it was a
blessing in disguise maana ndio niliabzisha PPR, na mimi kwenda UDSM sheria kwa miaka 4 ya LL.B tena ni with honours, hadi 2007, 2008 nikajiunga JF na kuanza kumzimia FF kwa hoja zake na ile avatar yake yenye hijab na wanja, sura kama Siti Binti Saad au Um Kuluthum, mimi huniambii kitu!.
Kwa Kiti Moto, nawashukuru sana wote kuanzia Ali Oki, Jove Conslves, Eric Fernandez, Babu Joshua Mwaituka, Agnelo, Farid Jabir, Islam Barafaa, Sheikh Jabir, Mzee Shaffi Adam Shafii, Fresh Nzowa, Silvia Mndala, Nuri, etc.
Panapo majaaliwa mwaka huu ndio mwaka wangu wa mwisho kwenye fani, nimetumikia miaka 30, hivyo najipanga kufanya farewell.
Ukinikubalia, wewe sasa ndio unakuwa wa kiutu uzima wa kufa na kuzikana.
P