Habari wakubwa kwa wadogo!
Kwa niaba ya
charminglady JF Miss Chit-chat 2012, napenda kuchukua fursa hii kuelekeza shukrani zangu za dhati kwa Mungu kwa kutuvusha mwaka 2012 na kuuona mwaka 2013 zaidi sana kwa kumuwezesha
charminglady kuchukua taji la JF Miss Chit-chat 2012.
Zaidi napenda kuelekeza shukrani kwa mkuu
Ruhazwe JR, kaka Mungu aendelee kukupa uzima na siha njema. Shukrani pia ziwaendee wale wote walitumia muda wao kupiga kura iwe kwa kutumia kompyuta au simu zao, napenda kuwa taarifu kuwa kura zenu hazikupotea bure.
Kiukweli ni ngumu kumshukuru mtu mmoja mmoja maana waliotoa "support" ni wengi mno, ila wengi wao walitokea Jukwaa la MMU, Siasa, Photo, Hoja Mchanganyiko na Chitchat.
Pili shukrani za pekee ziende kwa familia yangu ya Mr.
watu8 na Mrs.
measkron,watoto
WiseLady,
charminglady,
sweetlady,
beibe nasty na
Davie S.M. Pia sina budi kumshukuru mkwe wangu
C6 na marafikize
Nicas Mtei na
Erickb52.
Tatu kwa wadau ambao waliweza kufanikisha suala zima la udhamini na ufadhili ambao kwa asilimia kubwa umemwangukia mshindi wa taji hili, ambao nilikutana nao katika harakati za kampeni na ndugu hao kwa moyo mkunjufu wakaweza kutunisha kapu la zawadi, nao ni kaka yangu
masopakyindi na mkuu
Samaritan
watu8
Charminglady's Campaign Manager