Mishahara ya SUMATRA kufuru

ME NADHAN BASIC SALARY KWENYE SLIP YA MLETA MADA INASOMA 432,000.kwa hyo sio kosa lake,ila hajawah kuona salary slip nyingne zaid ya za watumish wenzie wa kada yake na ya huyo jamaa yake.

Sio vyema sana kumshambulia mtoa mada, hayo ni mawazo yake ambayo probably yametokana na exposure aliyonayo hivyo ni vyema kumuelimisha tukianzia na salary wewe unayopata maana sio kukazania huyu analipwa hivi mara yule mbona hatusemi mimi! Nafikiri kwa point of view 1.53 M pesa ya kuanzia kwa graduate sio mbaya tena kwa taasisi ya Serikali. Ni mtizamo tu na hili suala lingekuwa la manufaa sana kama tungelijadili vizuri lingekuwa na msaada hasa kwa wenzetu graduates na ambao wako un employed. Nawasilisha
 
Ukifuatilia sana serikalini mambo ya mishahara, utapata presha. Kuna ukiritimba wa hali ya juu mno
 
MKUU kachek tanapa na ngorongoro ndo utajua ka watu wanaish dunian au pepon...we unashangaa 1.5
 
Dah mi nilijua analipwa pesa miiiingggiii kumbe 1.5mil tu.We jamaa ajira zinakufanya uwe na akili za kimasikini sana.Mwache alipwe tu hyo pesa ndogo sana.
 

Jamaa kaniacha hoi sana huyu.Mi nilivyoona kufuru nikajua labda analipwa milioni 40 au 80 kwa mwezi ambapo kibongobongo ni mshahara mkubwa sana.
 

Pole sana wewe na huo mshahara wako wa kwa muhindi ndo unaleta huku?!
 
hapo bold sasa umeanza matusi,
una uhakika gani kwamba mtoa mada ni mwanamke??
je wewe mama yako alikuwa baba?? na dada yako ni kaka??
mwanao wa kike ni mvulana na mkeo ni mume??

Na akujibu
 
ndugu yangu husishangae sana meli itakuacha......by the way wakala wengi wa serikali mishahara yao si haba kabisa. lakini pia kama unamuona huyo anafaidi basi kaangalie mishahara ya hawa jamaa TANROADS, TRA, BoT, TPA, EWURA, TBS, TANTRADE, hapo bado haujaenda PCCB etc.

1.53 ni mshahara wa kawaida sanaaa, na hapo am sure makato bado anaweza kuwa anaondoka na 900,000 na kitu.....TPA ukifikia ngazi ya umeneja tu kwenda juu ujue unakula above 9mil, sasa jiulize wakurugenzi watakua wanalamba ngapi...? kwahiyo huyo jamaa wa SUMATRA ujue anatakiwa alalamike mshahara mdogo
 

Hiyo ndo kubwa? Ukiwa mtu wa majungu kwenye ujana ujue uzeeni utakuwa tu mchawi
 
Ukitoa makato na kodi inabaki kama laki 8 take home. Mbona kawaida!!
 
Mi naona huo ni mshahara mdog sana na kulingana na maisha yalivyo bado haumtoshi. Pia nafaham watu wenye elimu ya kawIda tu ya digrii moja wanalipwa zaid ya huo na masafari na masemina kubao.
 

9 million a month kibongo bongo sio mbaya mkuu
 
unashangaa muhasibu kulipwa hivyo,wakati kuna taasisi za serikali dereva tu analipwa 3.5.:heh:
 
hiyo ni hela ndogo sana....wenzio 10m ni ya kununulia kabichi tu(Tibaijuka)
 
Ukweli ni kwamba mishahara ya watumishi wa serikali na watumishi wa taasisi za serikali inatofautiana kwa kiwango kikubwa, hapa namaanisha kwa mtu mwenye degree:
Mtu anayefanya kazi halmashauri mshahara wake huwezi kulinganisha na NSSF, PSPF,LAPF,GEPF,TRA,BOT...Wao hubebwa sana na allowances, but vinginevyo daah majanga.

hiyo millioni 20 au 40m inawezekana lakini labda Vilabu vya Mpira, NGO za Kimarekani au mashirika ya kimataifa....


Maneno yangu siyo sheria mpaka yafuatwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…